Pages

KAPIPI TV

Sunday, August 17, 2014

CHADEMA YAKUBALI KUSHIRIKIANA NA ACT-KIGOMA

Na Magreth Magosso,Kigoma

CHAMA  cha  Demokrasia  na  Maendeleo (Chadema) mkoani hapa,kimekubali kushirikiana na vyama vya upinzani kikiwemo chama kipya cha ACT  kwa lengo la kukiondoa madarakani  chama Tawala ambacho ni chachu ya kudumaza huduma za jamii zishio vijijini.
 
Kauli hiyo ni moja ya harakati ya uongozi mpya wa chama hicho kukiri mabadiliko ya mfumo wa vyama vya upinzani  vinahitaji dhati ya mshikamano,uwazi,uwajibikaji  na utoaji wa elimu sahihi ya uraia kwa tija ya umma kubaini uhalisia wa mambo hatimaye kukiondoa chama tawala madarakani 2015.
 
Mwenyekiti wa chadema Mkoa huo  Ally Kisala alisema kukaidi kuviunga mkono vyama vipya ni moja ya mapungufu ya vyama kutokukubali alama za nyakati  ambazo huchangia baadhi ya viongozi wa vyama husika kutumia muda mwingi  kuponda uongozi wa chama kingine ambapo wote wana nia ya kushika dola kwa mujibu wa katiba zao.
 
Kisala alitoa kauli hiyo jana kwenye mkutano wa hadhara katika viwanja vya mwanga center kigoma ujiji,uliokuwa ukitambulisha safu ya uongozi mpya wa chadema na kuelezea wananchi uhai wa chama mkoani hapo na  lengo la  vyama vya upinzani ni kukiondoa ccm kwenye mfumo wa utawala wa miaka kenda usiorasimisha mabadiliko ya  utawala mpya kwa kushindwa  kuwajibikaji kwa viongozi wazembe.
 
“hatunahaja  ya kulumbana,tunataka tuungane ili kukitoa ccm katika madaraka,waliotoka chadema tufanye kazi pamoja ya kuelimisha umma,ili wakati wa uchaguzi mkuu vyama vya upinzani tushike majimbo yote na si kubomoana wenyewe” alianisha Kisala.
 
Katibu wa Chadema wa hapa Shaban Madede aliwataka wakazi wa hapo watumie fursa kwa kuchukua  fomu za  chama hicho kwa  kuomba  nafasi ya kada mbalimbali za uongozi kuanzia ngazi ya kitongozi hadi taifa kwa maslai ya kukijenga chama ili kufanikisha ndoto za kuingia ikulu mwakani.
 
Mkurugenzi  wa  Mipango Taifa  Benson  Kigaila alisema chadema taifa  inathamini nguvu za wakazi wa kigoma kwa kujitolea mali na jasho lao katika kukiimarisha chama tangu kuanzishwa kwake ndio maana inatoa nafasi nyingi  kwa wazawa wa hapo kwenye safu ya uongozi taifa na kuwasihi wanachama wazingatie maadili na falsafa ya katiba yao.
 
Pia ,imependekeza kuwa suala la kujadili rasimu ya katiba ifutwe kwa sasa ili fedha mtambukwa zisaidie huhudumia  jamii na kushawishi wananchi ifikapo 2015 wakipe kura chadema ili ishike dola na rasimu ya katiba ifanyike katika mfumo wa utawala wao.
 
Jamboleo liliwahoji  Katibu mwenezi  wilaya ACT wa hapa Anzoluni Kibela    na Katibu wa NRA Taifa Hamis Kiswaga ni kweli wapo tayari kushirikiana kukiondoa madarakani ccm 2015 na kuacha kudoboana majukwaani  kwa nyakati tofauti walisema  ni ndoto  kwa vyama hivyo ,kutokana na sera,itikadi ,utashi na ubinafsi uliopo miongoni mwa  viongozi wa vyama vilivyopo.
 
Walisema baadhi ya viongozi katika vyama wanautashi binafsi na kushawishi jambo Fulani kwa wakati maalum na linapokuja suala la umoja,mshikamano wa kusimika mgombea mmoja katika kiti cha urais ili kukiondoa ccm madarakani huibuka hisia za utashi na  ubinafsi kwa kusalitiana hatimaye ccm inaendelea kuhodhi madaraka  na kushauri wasafiane nia na uwazi wa malengo ili kutimiza hilo.
 
Kwa upande wa Katibu mwenezi CCM wa hapa Kalembe Masudi alisema vyama vya upinzani hawana dhati ya umoja,mshikamano ,kutokana na kushindwa kuwa  na uwazi wa uwajibikaji kwa wanachama wake kwa mujibu wa katiba zao na kudai  ccm itaendela kutawala kutokana na vyama hivyo kuwa na umoja wa mashaka kwa kutawaliwa na ubinafsi na si tija kwa wananchi.

No comments: