Pages

KAPIPI TV

Tuesday, July 22, 2014

NHIF KIGOMA YAWAFUNDA WANDISHI WA HABARI

Na Magreth Magosso,Kigoma


CHAMA cha wandishi wa habari Mkoa wa Kigoma,wametakiwa watumie chama chao  kujiunga na mfuko wa Afya (Nhif)  kwa  lengo  la  kupunguza  changamoto ya kipato inayochangiwa na kutokuwa na mikataba ya ajira husika.


Hayo yalisema  na Meneja wa mfuko huo mkoani hapa Elias Odhiambo alipokuwa akizungumza na wanachama hao  kigoma Ujiji ,katika ofisi za  KGPC kwa tija ya kutaka watumie fursa ya huduma ya vikundi ili kunufaika na mafao ya matibabu yatolewayo na mfuko huo.


“ changamoto kubwa ni uhakika wa kipato,ambapo kupitia huduma mpya ya vikundi rasmi vya uzalishaji mali ni nafuu kwenu, kujiunga na bima ya afya na kila mwanachama atachangia sh.76,800 tu kwa mwaka” alibainisha Odhiambo.


Alianisha huduma ya vikundi ni chachu kwa kila mtanzania kuwa na uwezo wa kuchangia kiasi hicho kwa mwaka na endapo atahitaji kuongeza hitaji la mtegemezi anapaswa amchangie kiasi hichohicho,kwa dhati ya kuondoka na adha ya kulipa  matibabu ya papo kwa papo.

Alisema wananchi wote waliopo katika vikundi vidogo na vikubwa ambavyo vipo kihalali ni wakati wao kutumia fursa hiyo. ambayo inakidhi hali halisi ya maisha ya mtanzania na kusisitiza wananchi wathubutu hilo kwa faida ya leo na siku za usoni.


Mwenyekiti wa Kgpc Deogratius Nsokolo aliunga mkono huduma hiyo ,ambayo ni fursa kwa wanachama wake,ambao asilimia 99 hawana mikataba ya ajira ,hali inayochangia washindwe kwenda kupima afya zao kwa wakati .


Alisema  wataweka  utaratibu,kanuni na sheria  kwa kuhakiki  kila mchango wa  mwandishi kuingia katika mfuko huo kwa  wakati, ili kuwajengea uwezo wa kulipia huduma hiyo ambayo ni tija katika uwajibikaji wao.

No comments: