Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (Kulia),
akimkabidhi jezi za timu sita za mpira wa miguu Afisa Mtendaji wa Kata
ya Nditi, Patrick Mwasambungu kwa ajili ya kuzikabidhi timu hizo
zilizopo katika Kata hiyo katika Jimbo la Nachingwea mkoani Lindi.
Waziri Chikawe pia alitoa mabati 100 kwa ajili ya ujenzi ya Ofisi Kuu ya
CCM katika Kata hiyo ya Nditi. Mbunge huyo wa Nachingwea yupo jimboni
mwake kwa ajili ya kufanya ziara ya kuzungumza na viongozi wa CCM katika
ngazi mbalimbali. Picha na Felix Mwagara.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (Kushoto),
akikiangalia kifusi cha mchanga kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata
ya Mnerongongo ambayo ipo katika hatua ya mwisho kukamilika ujenzi
wake. Katika ujenzi wa ofisi hiyo, Waziri Chikawe alitoa mabati 100
ambayo tayari yameezekwa. Mbunge huyo wa Nachingwea yupo jimboni mwake
kwa ajili ya kufanya ziara ya kuzungumza na viongozi wa CCM katika ngazi
mbalimbali. Picha na Felix Mwagara.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Nachingwea, Mathias Chikawe (Kushoto),
akikagua ujenzi wa Ofisi ya CCM Kata ya Mnerongongo ambayo ipo katika
hatua ya mwisho kukamilika ujenzi wake. Katika ujenzi wa ofisi hiyo,
Waziri Chikawe alitoa mabati 100 ambayo tayari yameezekwa. Mbunge huyo
wa Nachingwea yupo jimboni akifanya ziara ya kuzungumza na viongozi wa
CCM katika Kata za Wilaya za Nachingwea mkoani Lindi. Picha zote na
Felix Mwagara.
No comments:
Post a Comment