Pages

KAPIPI TV

Sunday, June 15, 2014

"FICHUENI WATUMISHI WANAOUZA DAMU HOSPITALINI"-SALMA KIKWETE

Mwenyekiti wa taasisi ya Wanawake na Maendeleo nchini WAMA Mama Salma Kikwete,Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Bw.Steven Kebwe pamoja na Mbunge wa vitimaalum Bibi Magreth Sitta wakati wa Maadhimisho ya Kilele cha Uchangiaji damu mkoani Kigoma

Mama Salma Kikwete akiwa na kikundi cha ngoma ya asili inayofahamika kwa jina la Mapigo tisa mkoani Kigoma wakati wa Maadhimisho ya Uchangiaji damu.

Na Magreth Magosso,Kigoma
Mwenyekiti  wa  WAMA  Mama  Salma Kikwete amewataka wananchi  wawafichue watumishi wanaouza Damu Salama  katika hospitali mbalimbali  nchini hapa ,kwa lengo la kuongeza hamasa ya uchangiji damu   na kuokoa maisha ya  wahitaji hasa mama mjamzito  na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.
Akifafanua hilo kwenye kilele cha uchangiaji wa Damu salama ambapo kitaifa ilifanyika mkoani  hapa,   katika  uwanja wa Lake Tanganyika  ambapo  pia  alikuwa  Mgeni rasmi katika kilele hicho alisema, watumishi wasio na maadili mema ni chanzo cha jamii kusuasua  kushiriki katika suala la uchangiaji Damu  salama.
“wananchi, shirikianeni kuwaumbua watumishi wasio na madili ,wanaotumia fursa ya wahanga ili wajipatie kipato haramu,damu haiuzwi na mkigundua mtumishi wa hivyo jamani mfichueni ili apate haki yake” alibainisha Mama Salma.
Pia alisema wananchi  waliowengi wanaogopa kujitokeza kuchangia damu kwa hofu ya kukutwa na maradhi mbalimbali  ya mambukizo kitendo ambacho kinachangia wananchi kuishi maisha mafupi ,kutokana na kuishi na maradhi ambapo wakibadilika kwenda kupima kila wakati ni rahisi kupata tiba ya ugonjwa husika .
Kwa upande wa Mkurugenzi wa  Evidence  For  Action  Craig Ferla alisema asasi za kiraia na serikali walipe uzito changamoto ya vifo vya kinamama wajawazito ambapo  kina mama 8,000 hupoteza maisha kila mwaka  wakati wa kujifungua kutokana na kutokwa na damu nyingi ambao unachangiwa na ukosefu  wa damu ya akiba kwa ajili ya kuepusha vifo hivyo.
Alisema Kigoma imeonyesha njia ya kuokoa maisha ya mama na mtoto kwa kufanikisha  lengo la kimkoa katika uchangiaji damu,ambapo  chupa 3620 zimepatika katika wilaya sita mkoani humo, licha ya mkoa huo kutakiwa kutoa chupa 3000 za damu  hiyo.
Naye Mwakilishi wa Tasisi ya CDC Dr.Regina Kutaga alisema  changamoto ya ukosefu  wa damu salama katika benki ya damu katika sekta ya afya inachangia vifo vya uzazi kwa 80% sanjari na kukwamisha malengo  husika kuwa, ifikapo 2020 kila nchi ifanikishe kuwa na damu salama kwa 100%.
 Kwa upande wa Meneja wa Damu salama  Taifa Dr.Abdul  Juma  na Meneja Damu salama kanda Magharibi Ipyan Kaganuka kwa nyakati tofauti  walisema wameanzisha mfumo rasmi wa kuweka  kumbukumbu za majina ya  wathubutu wa uchangiaji damu ambapo itasaidia  kupata idadi ya uchangiaji wao sanjari na kupatiwa motisha.
Walisema lengo ni kuwawekea utaratibu wa  uchangiaji  wao wa kuchangia damu salama kila ifikapo wakati wa kufanya hivyo.huku wakiri  kufikia lengo la kitaifa ambapo zilihitajika chupa 6500, ambapo jana  katika  sherehe za kilele cha shughuli hizo  walipata chupa 7,000 ambazo bado hazijakaguliwa kitaalamu zaidi kama zipo salama.

No comments: