Pages

KAPIPI TV

Wednesday, June 11, 2014

BIMA YA AFYA YATOA MSAADA WA SHUKA 100 HOSPITALI YA UJIJI KIGOMA


Na Magreth Magosso,Kigoma.

Wajawazito wanaolazwa katika hospitali ya Ujiji wamepunguziwa  adha ya kutumia khanga  kutandika vitanda vyao, pindi  walazwapo katika hospitali  hiyo,  baada ya kituo hicho  kukabidhiwa mashuka 100kutoka  Mfuko wa Taifa Bima ya Afya  kwa lengo la kuboresha afya ya mama na mtoto.
 
Akikabidhi mashuka hayo  hospitalini hapo  Ally  Mchumo ambaye ni Mwenyekiti wa bodi ya mfuko huo(NHIF) alisema msaada huo umelenga madhimisho ya siku ya wadau wa mfuko huo ambao hufanyika kila mwaka ,hawana budi kutumia fursa hiyo kama sehemu ya mchango wao kwa jamii husika.
 
      
Balozi Mchumo alisema kiasi cha sh.milioni 294 zimetumika katika mashuka hayo ambayo ni tija kwa wadau ,Huku akiwataka wakuu wa idara ya afya watumie fursa ya huduma ya Mikopo ya ghalama nafuu ya mfuko huo  ili kusaidia kupunguza adha ya vifaa tiba .
 

Kwa upande wa Mganga Mkuu wa Manispaa hiyo John Magiga  alisema  wadau wa afya wanawajibu wa kutambua adha na kupunguza changamoto katika vituo vya afya, zahanati katika mikoa iliyopo pembezoni mwa  nchi ambayo ipo nyuma kimaendeleo.
 
Baadhi ya wagonjwa Latifa Omari na Neema Joshua kwa nyakati tofauti walisema wajawazito wamekuwa wakitumia khanga kutandika vitanda,kutokana na uhaba wa mashuka hivyo kuwa na wakati mgumu wakati wa kujifungua kwa wale wasio na nguo za kutosha .
 
Naye Muguzi wa kituo hicho Siwazuri Mwinyiomvua amekiri msaada huo utapunguza adha hiyo,ambapo ilikuwa ikiwathiri  kisaikolojia wajawazito walio na kipato cha chini hasa wanapokosa mashuka ya kutandika vitanda .
 
Muuguzi Mkuu wa Wilaya hiyo Joyce  Malekela alisema hospitali hiyo  inakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo ukosefu wa maji,watumishi pamoja na vitendea kazi hali inayowalazimu watumishi kufanya kazi katika mazingira magumu.
 
 
 Naye Meneja Mfuko  (NHIF) Mkoa wa Kigoma Elias Odhiambo aliwataka viongozi wa Mkoa huo na wanasiasa waongeze  uhamasishaji kwa  jamii wajiunge na mifuko ya afya NHIF na CHF ili  waondokane na gharama kubwa za matibabu ya papo kwa papo.
 
Aidha  mfuko unalenga kutoa huduma kwa wakazi wote ambapo kwa mwaka 2013 mfuko umefikia asilimia 15% ya wanachama kwa Mkoa wa Kigoma na wanatarajia wanachama waongezeka kwa 30% ,kama kauli mbiu ya serikali inavyotaka umma ujiunge na mfuko huo.

No comments: