Na Magreth Magosso,Kigoma
IMEFAHAMIKA kuwa,Kamanda Mwandamizi msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kigoma,Frasser Kashai amedaiwa kukataa kupokea kiasi cha Shilingi laki moja kwa ajili ya kuhamasisha ujenzi wa choo cha askari polisi kituo cha Mwandiga, zilizotolewa na Chama cha NRA kigoma .
Akifafanua tukio hilo katibu wa chama hicho Rashid Tanganyika alisema awali waligundua changamoto ya ukosefu wa choo kwenye ziara ya katibu wa Taifa NRA 2012-2013 alipotembelea idara mbalimbali wilayani kigoma na kubaini kituo cha polisi cha mwandiga hakina choo zaidi ya miongo kumi. ,hali inayowafanya askari husika kujisaidia kwenye vyoo vya wananchi.
Alisema kutokana na mazingira hayo tete ,katibu Taifa wa chama hicho Hamis Kiswaga aliahidi kwa RCO wa hapa Dismas Kisusi kuwa atachangia fedha hiyo ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha idara ya polisi ikamilishe ujenzi wa choo cha mwandiga ili kulinda heshima na hadhi ya walengwa.
Naye Katibu Taifa wa chama hicho Kiswaga alisema alitoa fedha hizo ,baada ya kubaini baadhi ya wananchi kuwashusha thamani askari wa kituo hicho ambapo inachangia askari husika kutowajibika kikamilifu ,kutokana na baadhi ya washukiwa wa uhalifu wanawasaidia kujisitiri kwenye vyoo vyao.
Alidai kitendo cha Kamanda huyo, kukataa kupokea fedha hizo ni udhaifu wa uwajibikaji kwa jamii na kupelekea wadau wengine washindwe kusaidia idara hiyo na kushauri aweke mpango mkakati wa kuondoa dhana hasi penye changamoto .
Akijibu shutuma hiyo Kamanda Frassser Kashai amekiri kukataa kupokea kwa sababu ya gharama kubwa ya lengo husika,hivyo amehofu fedha hiyo kutumika sivyo ndivyo kutokana na changaoto ya fedha za ziada katika ujenzi wa choo hicho.
Alisema endapo angepokea fedha hizo na kutokamilika kwa ujenzi huo 2013 ,angesemwa kwenye jukwaa la wanasiasa huku akimpa jukumu hilo OCD Medrad Singano afanyie tathimini wa ujenzi huo na atoe mrejesho wa tathimini kwa wadau ili kuondoa dhana ya kukataa kwakwe .
Baadhi ya wananchi walipohojiwa dhana ya usafi na magonjwa ya mlipuko Mariam Issa na Judith Emmanuel kwa nyakati tofauti walisema , serikali inahamasisha umma namna ya kusafisha mazingira hasa usafi wa nyumba na vyoo bora ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko ukiwemo ugonjwa wa Dengue.
Gazeti hili limebaini Jeshi la polisi la hapa lipo njia panda kubuni njia mbadala wa kuhakikisha vituo vyake vina vyoo bora na vya kisasa ,ambapo mbali ya kituo cha Mwandiga pia changamoto hiyo ipo kituo cha polisi cha Ujiji kutokana na choo chake kujaa kinyesi na askari husika kujisaidia vivyo hivyo.
IMEFAHAMIKA kuwa,Kamanda Mwandamizi msaidizi wa Polisi Mkoa wa Kigoma,Frasser Kashai amedaiwa kukataa kupokea kiasi cha Shilingi laki moja kwa ajili ya kuhamasisha ujenzi wa choo cha askari polisi kituo cha Mwandiga, zilizotolewa na Chama cha NRA kigoma .
Akifafanua tukio hilo katibu wa chama hicho Rashid Tanganyika alisema awali waligundua changamoto ya ukosefu wa choo kwenye ziara ya katibu wa Taifa NRA 2012-2013 alipotembelea idara mbalimbali wilayani kigoma na kubaini kituo cha polisi cha mwandiga hakina choo zaidi ya miongo kumi. ,hali inayowafanya askari husika kujisaidia kwenye vyoo vya wananchi.
Alisema kutokana na mazingira hayo tete ,katibu Taifa wa chama hicho Hamis Kiswaga aliahidi kwa RCO wa hapa Dismas Kisusi kuwa atachangia fedha hiyo ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha idara ya polisi ikamilishe ujenzi wa choo cha mwandiga ili kulinda heshima na hadhi ya walengwa.
Naye Katibu Taifa wa chama hicho Kiswaga alisema alitoa fedha hizo ,baada ya kubaini baadhi ya wananchi kuwashusha thamani askari wa kituo hicho ambapo inachangia askari husika kutowajibika kikamilifu ,kutokana na baadhi ya washukiwa wa uhalifu wanawasaidia kujisitiri kwenye vyoo vyao.
Alidai kitendo cha Kamanda huyo, kukataa kupokea fedha hizo ni udhaifu wa uwajibikaji kwa jamii na kupelekea wadau wengine washindwe kusaidia idara hiyo na kushauri aweke mpango mkakati wa kuondoa dhana hasi penye changamoto .
Akijibu shutuma hiyo Kamanda Frassser Kashai amekiri kukataa kupokea kwa sababu ya gharama kubwa ya lengo husika,hivyo amehofu fedha hiyo kutumika sivyo ndivyo kutokana na changaoto ya fedha za ziada katika ujenzi wa choo hicho.
Alisema endapo angepokea fedha hizo na kutokamilika kwa ujenzi huo 2013 ,angesemwa kwenye jukwaa la wanasiasa huku akimpa jukumu hilo OCD Medrad Singano afanyie tathimini wa ujenzi huo na atoe mrejesho wa tathimini kwa wadau ili kuondoa dhana ya kukataa kwakwe .
Baadhi ya wananchi walipohojiwa dhana ya usafi na magonjwa ya mlipuko Mariam Issa na Judith Emmanuel kwa nyakati tofauti walisema , serikali inahamasisha umma namna ya kusafisha mazingira hasa usafi wa nyumba na vyoo bora ili kuepukana na magonjwa ya mlipuko ukiwemo ugonjwa wa Dengue.
Gazeti hili limebaini Jeshi la polisi la hapa lipo njia panda kubuni njia mbadala wa kuhakikisha vituo vyake vina vyoo bora na vya kisasa ,ambapo mbali ya kituo cha Mwandiga pia changamoto hiyo ipo kituo cha polisi cha Ujiji kutokana na choo chake kujaa kinyesi na askari husika kujisaidia vivyo hivyo.


No comments:
Post a Comment