JAMHURI YA
MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI
TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 19/05/2014.
Ndugu
waandishi wa habari, Jeshi la Polisi mkoa wa Tabora linaendelea na Operesheni katika
wilaya zote za mkoa wa Tabora. Ambapo kufuatia operesheni hiyo tumefanikiwa kukamata
watuhumiwa wa makosa mbali mbali kama ifuatavyo:-
KUPATIKANA
NA RISASI: Mnamo tarehe 18/05/2014 huko eneo la barabara ya
Sikonge kata ya Ng’ambo Manispaa ya Tabora alikamatwa BARANABA s/o JOSEPH,
36yrs, Mkonongo, mkazi wa Inyonga wilaya ya Mlele mkoa a Katavi akiwa na risasi 307 za SMG/SAR,
mtuhumiwa amekiri kujihusisha uchuuzi wa risasi na matukio mbalimbali ya
unyanga’anyi wa kutumia silaha. Baada ya mahojiano alieleza kuwa risasi hizo
ameuziwa na CHRISTINA D/O PILIPILI, 42YRS,
muha, mkazi wa mataa wa Hali ya hewa, kigoma mjini ambaye naye amekiri kuwa ni
muuzaji wa risasi na huzitoa maeneo ya kigoma na kuja kuuzia hapa mkoani Tabora
na mikoa mingine ya jirani . Watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara baada
baada ya upelelezi kukamilika.
KUPATIKANA
NA SARE ZA JESHI:
tarehe 18/05/2014 huko eneo la Isike
jirani na NBC Bank manispaa ya Tabora alikamatwa KARIMU S/O ALLY, 25yrs,
Muhurudu mkazi wa Mirambo, akiwa na sare za Jeshi la Wananchi wa Tanzania.
Mtuhumiwa amekuwa akitishia na -kulaghai wanachi kuwa ni askari wa jeshi hilo
kwa nia ya kujipatia fedha na huduma mbalimbali. Mtuhumiwa atafikishwa
mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.
KUPATIKANA
NA SILAHA:
katika eneo la Ndono wilaya ya Uyui alikamatwa, RAJABU
S/O HUSSEIN, 65yrs, Mnyamwezi, mkulima mkazi wa Kidatu manispaa ya Tabora akiwa
na silaha aina ya Shortgun iliyotengenezwa kienyeji kinyume na sheria, kisu
kimoja kikiwa ndani ya ala, tochi moja na Risasi tatu za Short gun. Mtuhumiwa
baada ya kukamatwa aliwataja watu wawili wanaomuuzia risasi ambao ni:- NOEL S/O
VITALI, 40yrs, mkulima, na ADREA S/O JOSEPH, 50yrs, Mnyamwezi, wote ni wakazi
wa Ukumbisiganga wilaya ya Kaliua, wameshakamatwa tarehe 15/05/2014.upelelezi
unaendelea na watuhumiwa watafikishwa mahakamani.
Pia huko eneo la usoke
mjini kata na Tarafa ya usoke wilaya ya urambo walikamatwa HIRALY
S/O RASHIDI @ BAKARI 40YRS ABDALAH S/O RASHID @BAKARI 35YRS, MOSHI S/O RASHID
@BAKARI 38YRS NA ALADIN S/O RASHIDI @BAKARI 22YRS wote wakazi wa
Usoke mjini wakiwa na bunduki aina ya RIFFLE
na
risasi tano ambayo
wanamiliki kinyume na sheria. Upelelezi unaendelea na watuhumiwa watafikishwa
mahakamani.
huko kijiji cha Bulyang’ombe barabara kuu ya Igunga –Nzega gari lenye namba za
usajili T.677 AGJ Scania bus mali ya ZUGA s/o AUGOSTINO @RICHARD wa Mwanza
ikiendeshwa na PIUS s/o? iligonga gari T.968 AJX Iveco iliyokuwa imeegeshwa
pembeni mwa barabara na dereva JUMA s/o BUNDALA, 41yrs, msukuma, mkazi wa
Shinyanga na kusababisha vifo vya watu 2 na majeruhiwa 14 wamelazwa katika hospitali
ya (w) Igunga . chanzo ni uzembe wa dereva.
Jeshi
la Polisi (M) Tabora linatoa shukurani kwa wote wanaolipatia taaarifa tunazidi
wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Jeshi lao ili kukomesha na
kutokomeza vitendo vyote vya uhalifu na kuwafichua wahalifu, pia watumiaji wa barabara wafuate sheria za usalama barabarani ili kupunguza
matukio ya ajali Operesheni za kukamata
wahalifu na makosaya baarabarani zinaendelea ili kuhakikisha mkoa unakuwa na
amani,utulivu na usalama wa raia na mali zao.
Imetolewa
na :-
KAMANDA WA POLISI
MKOA WA TABORA.
No comments:
Post a Comment