Pages

KAPIPI TV

Monday, March 24, 2014

WAJAWAZITO HATARINI MKOANI KIGOMA

Mkoa wa Kigoma Wastani wa wanawake wajawazito 48 hufariki Kila Mwaka wilayani  kasulu ,kutokana na tatizo la uzazi pingamizi wakati wa kujifungua.
 
Akithibitisha  hilo Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali ya wilaya ya Kasulu Mageni Mpondamali alisema sababu hiyo inachangiwa na ukosefu wa vifaa na dawa za kutosha katika vituo vya Afya na hospitali zilizopo wilayani humo.
 
“ pamoja na baadhi ya akina mama wajawazito kuchelewa kufika katika vituo vya afya na hosptali jambo ambalo linasababisha wanawake hao wanapofika katika vituo hivyo kuwa na hali mbaya ambayo inahatarisha usalama wa maisha yao” alisema Mpondamali.
 
Aidha amesema kuwa licha ya kuwahimizi kufika maeneo ya kupatia huduma muhimu pamoja na kujifungua bado jamii imekuwa na tabia ya kuendekeza mila na desturi na hivyo wengine kujifungulia kwa wakungawa Jadi.
 
 
Alisema kuwa tatizo hilo katika wilaya ya kasulu imekuwa ikiongezeka kila kukicha licha ya kuwapatia elimu mbalimbali akinamama hao pamoja na wakunga wanaowazalisha kuwapatia elimu ili wakipata mama mjamzito wamfikishe katika vituo vya afya na hospitali.
 
 
Akipokea msaada kutoka katika kikundi cha pretty mother cha akinamama wilaya ya Kasulu Afisa Muuguzi katika hosptali ya wilaya ya Kasulu Bi Janet Gabriel   ametoa shukrani kwa kikundi hicho ambapo ameeleza kuwa itasaidia kupunguza matatizo mbalimbali yanayojitokeza katika hospitali hiyo.
 
Amesema kuwa sambamba na hilo bado kunatatizo la  elimu ya uzazi salama kwa akinamama wajawazito na wenzawao kutohudhuria kliniki pamoja na wengine kuamini tiba mbadala za asili ambapo ni miongoni mwa sababu zinazochangia kuongezeka kwa vifo hivyo.
 
Akikabidhi msaada huo mwenyekiti wa kikundi hicho bi Edita Nsila amesema kuwa lengo la kikundi ni kuisaidia jamii iliyopo katika Makundi maalumu yakiwemo ya walemavu, wagonjwa, na watu wengine wenye mahitaji maalum.

No comments: