Mkuu
 wa wilaya ya Singida Mwalimu Queen Mlozi akizungumza na wananchi wa 
kata ya Utemini manispaa ya Singida ahamasisha maadili mema kwa 
watoto.
(Picha  na Nathaniel Limu). 
Na Nathaniel Limu
Baadhi
 ya ya wakazi wa manispaa ya Singida wamelalamikia mavazi yanayovaliwa 
na wanafunzi wa vyuo vya uhazili na uhasibu, kwa madai kwamba 
yanachangia kuharibu maadili ya watoto wao.
Malalamiko
 hayo yametolewa na wakazi  hao kwenye viwanja vya shule ya sekondari ya
 Utemini mjini Singida katika mkutano ulioitishwa kwa ajili ya mkuu wa 
wilaya ya Singida, Mwalimu Queen Mlozi kuhamasisha ujenzi wa maabara 
katika shule za sekondari za kata.
Wakifafanua,
 wamesema wanafunzi wa vyuo hivyo na hsasa wa kike, wanavaa nguo ambazo 
ni kinyume na maadili ya kitanzania na zinachochea vitendo vya ngono 
zembe.
“Mheshimiwa
 mkuu wa wilaya, nguo zinazovaliwa na hawa wanafunzi wa kike, zinaacha 
nusu ya mwili ubaki kama alivyozaliwa na mbaya zaidi zinawabana 
kupindukia, na Kwa upande wa wanafunzi wa kiume, wao suruali zao 
wanazivaa chini kabisa ya makalio” almeema Ntandu Jumbe.
Wamesema
 uvaaji wa nguo unaofanywa na wanafunzi wa vyuo hivyo, unachochea kasi 
ya mmomonyoko wa maadili kwa vijana na atoto wao kuongezeka mara dufu.
Kwa
 upande wake Mkuu wa Wilaya Queen Mlozi amesema tatizo hilo na yeye 
amelibaini lakini hata hivyo, akadai kuwa hayo ni matunda ya utandawazi.
Amesema
 tatizo la kuharibika kwa watoto kwa maana ya kutokuwa na maadili mema 
ni la karibu kila familia na hivi sasa ni kubwa mno.
Queen
 Mlozi amesema kwa kweli dawa pekee hivi sasa ya kupambana na janga hili
 la watoto kuharibika, ni sisi sote wazazi, walezi, viongozi wa serikali
 na wa madhehebu ya dini, kuunganisha nguvu zetu pamoja na kuimba wimbo 
mmoja, nao ni wa malezi bora kwa watoto wetu.
Aidha,
 mkuu huyo wa wilaya ameagiza kwamba kuanzia sasa kila vikao vya maamuzi
 vya ngazi mbalimbali, ajenda yao kuu iwe ni mkakati wa kudhibiti kasi 
ya mmomonyoko wa maadili kwa watoto.



No comments:
Post a Comment