Pages

KAPIPI TV

Wednesday, November 16, 2016

SERIKALI KUBORESHA MITAMBO YA KUCHAPISHA NYARAKA YA KIWANDA CHA UHAMIAJI KIJICHI JIJINI DAR ES SALAAM

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akizungumza na baadhi ya wananchi waliokuja kupata huduma Makao Makuu ya Idaya ya Uhamiaji wakati wa ziara yake ya siku moja aliyoifanya leo Kurasini jijini Dar es Salaam.

THBUB YASHUKURU UN KWA KUSAIDIA PROGRAMU ZA SHERIA

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeshukuru Umoja wa Mataifa kwa msaada wake mkubwa inaotoa kwa taasisi zisizo za kiserikali za kujengea uwezo wa kuweza kutetea haki za binadamu nchini Tanzania.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa THBUB, Mary Massay wakati wajumbe wa nchi za Nordic ambao ni wafadhili wakubwa wa programu za Umoja wa Mataifa zinazotekelezwa nchini Tanzania walipozuru katika ofisi hizo kwa mazungumzo.

“Kuna ongezeko kubwa la ufahamu kuhusu haki za binadamu, upatikanaji wa haki kwa makundi maalumu, uandishi wa habari kuhusu haki za binadamu na kuboreshwa kwa huduma za kisheria na ukaribu wa serikali wa kufanyakazi na wadau wa haki za binadamu,” alisema Massay akifafanua zaidi kuhusu manufaa ya ufadhili wa Umoja wa Mataifa katika kuboresha haki za binadamu nchini.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga (wa pili kushoto) akitoa neno la ukaribisho kwa wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa (hawapo pichani) ulipotembelea tume hiyo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto), Katibu Mtendaji wa THBUB, Mary Massay (wa pili kulia), Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Awa Dabo (kulia).(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Katika mazungumzo yao na ujumbe wa nchi za Nordic ambazo ni Sweden, Denmark, Norway Finland na Iceland kulikuwepo pia asasi mbalimbali zisizo za kiserikali kama Women’s Legal Aid Center, Tanzania Women Lawyers Association, Tanzania Women Judges Association, Legal Aid and Human Rights Center, Human Rights Defenders Coalition, na Tanganyika Law Society.

Katika mazungumzo hayo asasi hizo zilielezea ufanyaji kazi wao mafanikio na changamoto wanazokumbana nazo na umuhimu wa ufadhili wa mashirika ya Umoja wa Mataifa.

Akizungumzia changamoto zinazokabili Umoja wa Mataifa, serikali na asasi Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez alisema ipo haja ya kuwa na muono wa muda mrefu wa kuratibu shughuli zinazohusiana na maendeleo endelevu.

Katibu Mtendaji wa THBUB, Mary Massay akizungumzia shughuli mbalimbali zinazofanywa na tume hiyo kwa ujumbe kutoka nchi za Nordic ulioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa (hawapo pichani) ulipotembelea tume hiyo.

Alisema kwamba mabadiliko ya kitabia kwa binadamu huchukua muda mrefu kukubalika hivyo ni wajibu wa kila mmoja kufanya bidii ya kuhakikisha kwamba maisha yanabadilika na watu wanakumbatia mambo ya kisasa yanayochochea maendeleo yao na jamii

Akizungumza kwa niaba ya wajumbe kutoka nchi hizo za Nordic, Anders Rönquist, ambaye ni kiongozi wa ushirikiano wa kimataifa wa Shirika la Misaada la Sweden (SIDA), alisema pamoja na changamoto zilizopo kitaasisi, kisiasa, kifedha na kitamaduni maendeleo yaliyopo katika sheria na haki za binadamu nchini Tanzania yanatia moyo sana.

Alisema ipo haja ya serikali kuendelea kuhimiza mabadiliko na kwamba wao wapo tayari kusaidia mkakati wa kuboresha masuala ya sheria na haki za binadamu.

Kiongozi wa ushirikiano wa kimataifa wa Shirika la Misaada la Sweden (SIDA), Anders Rönquist (kulia) akizungumza kwa niaba ya wajumbe kutoka nchi hizo za Nordic ulipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Awa Dabo (kulia), akizungumza katika mkutano huo ambapo alishukuru mataifa hayo kwa kuendelea kusaidia programu za haki a binadamu nchini Tanzania. Alisema kwamba haki za binadamu ni kitu cha msingi katika maendeleo kwa kuwa hakuna maendeleo ya kweli bila kuwapo na haki za binadamu. Alisema kwamba maendeleo na haki za binadamu ni mambo yanayoshabihiana na kuimarika kwake kunasaidia kuimarisha ustawi wa jamii. Alishukuru pia serikali ya Tanzania kwa kuhakikisha kwamna masuala ya utawala bora na haki za binadamu yamo katika mpango wa miaka mitano wa maendeleo ambao unasaidiwa pia na UNDAP ll.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga akisisitiza jambo kwenye mkutano na wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake na Watoto (WLAC), Theodosia Muhulo akielezea shughuli mbalimbali zinazofanywa na kituo chake katika kuhakikishwa wanawake na watoto wapata msaada wa kisheria wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mwansheria kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Benedict Ishabakaki akizungumzia shughuli mbalimbali wanazofanya za msaada wa kisheria wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Jaji wa Mahakama Kuu na Makamu Mwenyekiti wa TAWLA, Sophia Wambura aki-'share' uzoefu wake katika masuala ya sheria wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitoa neno la shukrani kwa Mwenyekiti wa THBUB wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Jaji wa Mahakama Kuu na Makamu Mwenyekiti wa TAWLA, Sophia Wambura akikabidhi zawadi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kulia) baada ya kumalizika mkutano wa wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufaa, Eusebia Munuo akikabidhi zawadi kwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga wakati wa ziara ya wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipokutana na uongozi wa ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.
Picha juu na chini ni wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB).



Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga katika picha ya pamoja na wajumbe kutoka nchi za Nordic walioambatana na wataalam kutoka mashirika ya Umoja wa Mataifa walipotembelea ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) jijini Dar es Salaam.

Tuesday, November 8, 2016

DKT. POSSI AIPONGEZA UNESCO KUPUNGUA KWA UKATILI DHIDI YA ALBINO


Naibu Waziri (Ofisi ya Waziri Mkuu), Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Dkt. Abdallah Possi amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) kwa kusaidia kutoa elimu kwa wananchi kuhusu watu wenye ualbino pamoja na kufanya tathmini jinsi wananchi walivyo na uelewa kuhusu watu hao.

Dk. Possi ameyasema hayo katika mkutano wa kuelezea tathmini ambayo imefanywa na UNESCO kwa wananchi wa wilaya nne ambazo tathmini ilifanyika na kusema kuwa ni jambo zuri ambalo limesaidia kuonyesha hali jinsi ilivyo na ni njia gani ambayo serikali inaweza kutumia ili kumaliza vitendo vya ukatili kwa watu wenye ualbino.

"Watu wenye ualbino wamekuwa wakiteseka kwa kipindi kirefu, wanakosa nafasi ya kusoma, kufanya biashara na mambo mengi yanawakabili, watu wa mashirika sio suluhisho ni jamii yenyewe, watu wengi bado hawana elimu ya kutosha kuhusu ualbino,

"Inabidi ifike hatua watu wenye ualbino waishi sawa na watu wengine na serikali imekuwa ikifanya jitihada kumaliza vitendo hivyo lakini inabidi jamii itambue hili sio jukumu la serikali peke yake ni muhimu kila mmoja akashiriki kuvitokomeza vitendo vya ukatili, UNESCO imetuonyesha njia ya kuiwezesha serikali kufanikisha nia yake," alisema Dkt. Possi.

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt Abdallah Possi kutoa hotuba kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. (Habari picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Kwa upande wa UNESCO kupitia Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues alisema UNESCO imnatambua kila mwanadamu ana haki ya kuishi kama binadamu wengine na kupitia utafiti wao ambao uliambatana na kutoa elimu wanaamini kuwa ni muda wa jamii kushirikiana ili kutokomeza vitendo vya kikatili kwa maalbino.

"UNESCO imeamua kujihusisha sana na hili jambo na kujitahidi kutoa elimu kwa jamii, tumeanza kulifanyia kazi jambo hili la kikatili kwa maalbino na mashambulizi ambayo wamekuwa wanakutana nayo sababu ya imani za kishirikina ambazo ni kinyume na haki za kibinadamu,

"Utafiti huu utaweza kusidia kumaliza vitendo vya kikatili kwa watu wenye ualbino, kila mtu ana haki za kimsingi na hilo ndilo ambalo UNESCO inalisimamia, na katika kufanikisha hili kila mtu katika jamii kwa nafasi yake ana wajibu wa kushiriki kumaliza vitendo hivi, ni lazima kushirikiana kumaliza jambo hili," alisema Rodrigues.

Tathmini hiyo imefanyika katika wilaya nne ambazo ni Misungwi na Sengerema kwa Mwanza, Msalala iliyopo Shinyanga na Bariadi mkoani Simiyu.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt Abdallah Possi akizungumza katika mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wenye Alibinism Tanzania (TAS) Nemes Temba akitoa neno kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kiongozi mkuu wa tathmini hiyo, Dkt. Nandera Mhando akiainisha mambo muhimu yaliyobainika kwenye tathmini wakati mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Sweden nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnitt akitoa maoni kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. Kulia ni Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp.
Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp akizungumza jambo kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini, Dr. Qasim Sufi akifafanua jambo wakati wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi akifafanua jambo kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Picha juu na chini ni Sehemu ya washiriki wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) wakiwemo wadau kutoka mashirika na taasisi mbalimbali uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.



Mshehereshaji wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism), Mathias Herman akiendesha mjadala kwa washiriki katika mkutano huo uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi akibadilishana mawazo na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnitt (wa pili kushoto), Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp (wa pili kulia) pamoja na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini, Dr. Qasim Sufi wakati wakijiandaa na zoezi la picha ya pamoja.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
-- Zainul A. Mzige, Operation Manager, MO BLOG, www.modewjiblog.com +255714940992.

KUTOKA VOA Swahili: ZULIA JEKUNDU

Zulia Jekundu ni kipindi cha televisheni cha kila wiki ambacho hukuletea habari mbalimbali za burudani zinazotamba. Humu utapata kujua juu ya habari za mastaa zinazogonga vichwa vya habari, kujua baadhi ya wanaosherehekea siku zao za kuzaliwa wiki husika na hata filamu 5 zilizoongoza kwa mauzo katika wiki hiyo.
KARIBU

WANAFUNZI WA NELSON MANDELA WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUSAIDIA KUTATUA MATATIZO YA MAZINGIRA,MAJI

Pichani juu na chini ni Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya EU kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akihutubia wanafunzi wa vyuo mbalimbali katika ukumbi Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela ambapo alifanya ziara ya kutembelea Chuo jijini Arusha.(Picha na Ferdinand Shayo).

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau akifafanua jambo katika ziara ya Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer alipotembelea chuo hicho.
Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akisalimiana na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau, wakati wa ziara ya balozi huyo chuoni hapo.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela wakiwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela jijini Arusha.

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu (wa pili kushoto) na Amon Manyama (kushoto).
-- Zainul A. Mzige, Operation Manager, MO BLOG, www.modewjiblog.com +255714940992.

TEKNOLOJIA INAVYOBADILI MIENDENDO YA WASAFIRI

Na Jumia Travel Tanzania

Miaka kadhaa iliyopita kabla ya matumizi ya tekinolojia kuingia na kushika kasi mtu ulikuwa ukitaka kusafiri itakubidi kuulizia kwa watu ambao tayari wameshawahi kuwepo kwenye eneo unalolitarajia kwenda.

Baadae kidogo simu zilivyoanza kuingia zilirahisisha mambo watu wakawa wanapigiana simu na kuulizana hali na mazingira kwa ujumla ya eneo wanalotaka kwenda ili kujiandaa vema.

Lakini sasa hivi kwa msaada wa tekinolojia ni wewe tu aidha na simu au kompyuta yako iliyounganishwa vizuri na mtandao wa intaneti ambapo unaweza kupata taarifa lukuki bila ya kumuhusisha mtu yeyote yule. 

Kadiri ya maendeleo ya tekinolojia yanavyokua sehemu mbalimbali duniani na ndivyo huduma mbalimbali zinavyosogezwa na kurahisishwa zaidi kumzunguka binadamu.

Leo hii mtu huna haja ya kupata shida ya kuanza kusumbuka kutembea umbali mrefu au kumuuliza jirani, ndugu au jamaa kuhusu huduma kama vile za usafiri, malazi, bidhaa, na bei zake kwani kila kitu kimo na kinaweza kupatikana kwa njia ya mtandao wa intaneti.

Vivyo hivyo kwa upande wa huduma za usafiri na utalii zilivyorahisishwa na mitandao ya huduma za hoteli kama vile Jumia Travel, Expedia, Airbnb, TripAdvisor, Booking.com na kadhalika.

Wasafiri na watalii wengi wa siku hizi kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi wanapenda kupata huduma wazitakazo kwa urahisi zaidi na uhakika wakiwa mahali popote.

Wanataka kwamba wakiingia kwenye mtandao aweze kupata taarifa zote juu ya sehemu anayotaka kwenda kama vile atafika kwa njia gani pamoja na sehemu atakayofikia.

Kwa upande wa malazi mitandao iliyotajwa hapo juu imekuwa na nafasi kubwa sana katika kuhakikisha msafiri anapata sehemu ya uhakika anayoihitaji, gharama na hadhi yake.

Mitandao hii inatoa uwanja mpana wa kuweza kupata huduma zote sehemu moja, za uhakika tena ndani ya muda anaoutaka msafiri.

Tofauti na kipindi cha nyuma kidogo ambapo ilimbidi mtu afanye taratibu za malazi kwa sehemu anayokwenda mpaka atakapofika.

Kwa namna moja ama nyingine mitandao hii ya huduma za hoteli kwa mtandao na tekinolojia kwa ujumla imeleta msaada mkubwa na mapinduzi ya hali ya juu kwa watoa huduma nchini na sehemu zingine duniani.

Licha ya maendeleo hayo na madhumuni mazuri ya tekinolojia katika kuboresha maisha ya binadamu lakini bado kuna changamoto kubwa kwa watumiaji hususani wasafiri kuiamini na kuitumia mara kwa mara lakini pia hata kwa wenye hoteli na sehemu zingine zinazotoa huduma za malazi kwa ujumla.

Bado wasafiri wengi wanaamini kuwa huduma za kweli na uhakika utazipata mara utakapofika eneo husika licha ya kuwa kwenye mitandao hii kuna picha, huduma, gharama na mawasiliano ya wahusika.

Na kwa upande wa wamiliki wa sehemu za malazi kama vile hoteli bado nao hawana imani kubwa na wamiliki wa hii mitandao. Wao wanadhani kwamba wanaweza kutumia hoteli zao kuwatapeli wateja na kunufaika wao binafsi, dhana ambayo si kweli.

Ukweli wa mambo ni kwamba kwa watumiaji wa huduma hizi, wateja na wamiliki wa hoteli ambao huitumia mara kwa mara wamethibitisha imekuwa na msaada mkubwa sana.

Kwa mfano, hoteli nyingi hutegemea umaarufu wa sehemu husika ndio mteja aende na kutumia huduma zao kitu ambacho kwa dunia tuliyopo na tunayokwenda nayo kinapitwa na wakati.

Kupitia mitandao hii wamiliki wa hoteli na sehemu zingine za malazi wana wigo mpana wa kuwapata wateja kutoka maeneo mbalimbali kwani huduma zao zinakuwa tayari kwenye mitandao hiyo.

Jumia Travel ni miongoni mwa mitandao hiyo ambayo inayo orodha ndefu ya hoteli takribani 1,500 za nchini Tanzania bara na visiwani ambazo zinaweza kufikiwa na watu wa ndani na nje ya nchi.

Hii ni fursa kwa wamiliki wa hoteli kuweza kutambua wateja wao ni watu wa aina gani na wanatarajia vitu gani kutoka kwao. Wateja wa sasa wanategemea kwa kiasi kikubwa kukuta taarifa zote kuhusu huduma za hoteli husika kuwepo kwenye mtandao na kupatikana mara moja pale wanapozihitaji.

Kwa bahati mbaya si hoteli na sehemu za malazi zote ambazo taarifa zake unaweza kuzikuta mtandaoni na hapo ndipo mitandao hii inapokuja kuziba hilo pengo.

Mitandao ya huduma za hoteli imekuja kuziba pengo lililokuwepo kwa muda mrefu baina ya watoa huduma hizo na wateja ambapo athari zilikuwa kwa pande zote mbili.

Wamiliki kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakikosa wateja wengi ambao wangeweza kuwafikia kwa njia ya mtandao kwa kutegemea ambao wanakwenda moja kwa moja na hivyo kupoteza mapato mengi. Na pia kwa wateja ambao walikuwa na shauku ya kujua sehemu husika kabla ya kwenda walikuwa wanakosa fursa hiyo kwa sababu hakukuwa na mbadala wa huduma hiyo. 

Kuhusu Jumia Travel
Jumia Travel (travel.jumia.com) ni mtandao nambari moja unaongoza wa huduma za hoteli kwa njia ya mtandao wenye orodha ya hoteli zaidi ya 25,000 kwa nchi za Afrika na zaidi ya hoteli 200,000 duniani kote.

Dhumuni letu ni kuleta kila aina ya huduma za malazi kwenye mfumo wa mtandao na kutengeneza njia rahisi na nafuu zaidi kwa wateja kuzilipia.

Hapa Jumia Travel, tunao mamia ya wataalamu katika masuala ya utalii ambao huwasiliana na wateja wetu. Ofisi zetu zinapatikana katika miji na nchi zifuatazo Lagos (Naijeria), Accra (Ghana), Dakar (Senegali), Abidjan (Ivory Coast), Algiers (Algeria), Douala (Cameroon), Kampala (Uganda), Dar Es Salaam (Tanzania), Nairobi (Kenya), Addis Ababa (Ethiopia), Porto (Ureno) na Paris (Ufaransa).

Kabla ya mwezi Juni mwaka 2016, Jumia Travel ilikuwa ikijulikana kama Jovago. Ilianzishwa mwaka 2013 na Jumia ambayo inaendeshwa kwa kushirikiana na MTN, Rocket Internet, Millicom, Orange na Axas kama washirika wao katika masuala ya kifedha. 

Tuesday, October 4, 2016

MRADI WA GREEN VOICES UMEONYESHA MAFANIKIO, UTAWAKOMBOA WANAWAKE TANZANIA


Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, akisalimiana na maofisa wa ulinzi na usalama mara baada ya kuwasili katika bandari ya Nansio, Ukerewe hivi karibuni kuzindua mradi wa kilimo cha viazi lishe unaofadhiliwa na taasisi yake ya inayoshughulikia maendeleo ya Wanawake wa Afrika.
Mama Getrude Mongella (waliosimama katikati mwenye blauzi nyekundu) akifafanua jambo kwa Mkamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, wakati walipotembelea mradi wa kilimo cha viazi lishe wilayani Ukerewe. Kushoto kwa Mama Mongella ni Bi. Leocadia Vedastus, ambaye ni mshiriki kiongozi wa mradi huo.
Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, akiangalia bidhaa zilizo mbele yake ambazo zinatokana na viazi lishe katika kuongeza mnyororo wa thamani. Hii ni wakati alipokwenda kuuzindua mradi huo wilayani Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza.

MRATIBU wa mradi wa akinamama wapambanao na mazingira wa Green Voices, Alicia Cebada, amesema kwamba wamefarijika na mradi huo kwa kuwa umeonyesha mafanikio makubwa nchini Tanzania.

WAFADHILI WAFURAHISHWA NA UKAUSHAJI WA MBOGA MBOGA WA WANAWAKE MOROGORO



Mkurugenzi wa mawasiliano wa taasisi ya Mfuko wa Wanawake Afrika, Anna Salado (kulia), akipakua mboga zilizopikwa kiasili na kuungwa kwa nazi wakati yeye na ujumbe wake walipotembelea mradi wa ukaushaji wa mboga na matunda wa wanawake wa Kata ya Mzinga mkoani Morogoro hivi karibuni. Kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro, Milikieli Mansweat Mahiku.

Mratibu wa mradi wa Green Voices kutoka taasisi ya Mfuko wa Wanawake Afrika ya Hispania, Alicia Cebada, akiwa ameshikilia pakiti ya kisamvu kilichokaushwa na kufungashwa huku akiwapongeza wanawake wa kikundi cha Mzinga katika Kata ya Mzinga, Manispaa ya Morogoro kwamba wamefanya kazi nzuri sana. Mwenye fulana nyeupe ni Bi. Esther Muffui, mshiriki kiongozi wa mradi huo.

SIYO tu mapishi ya asili ya kisamvu kikavu kilichoungwa kwa nazi, lakini mafanikio makubwa katika ukaushaji na usindikaji wa mboga na matunda katika mradi wa wanawake wa Kata ya Mzinga, Manispaa ya Morogoro yamewavutia wahisani wa taasisi ya Women for Africa Foundation kutoka Hispania.
Hali hiyo imewafanya wanawake hao wawe katika nafasi kubwa zaidi ya kusonga mbele ikiwa wafadhili hao watatoa tena fedha katika awamu ya pili ya mradi wa Green Voices unaotekelezwa nchini Tanzania.

NHC YAKABIDHI MARARASA SHULE YA MSINGI SAKU WILAYA YA TEMEKE

1
Meya wa Halmashauri ya Temeke Abdallah Chaurembo akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa madarasa ya shule ya msingi Saku wilayani Temeke wakati wa makabidhiano yaliyofanyika shuleni hapo jana, Madarasa hayo yamejengwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC kwa gharama ya shilingi milioni 32 , makabidhiano hayo yamefanyika shuleni hapo mwishoni mwa wiki kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Nassib Mmbaga , Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari na Mkuu wa wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaviva.
2
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akifungua mlango mara baada ya makabidhiano hayo kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw. Nassib Mmbaga na kushoto ni Meya wa Halmashauri ya Temeke Abdallah Chaurembo.
3
Haya ndiyo madarasa yaliyojengwa na Shirika la Nyumba NHC kwa gharama ya shilingi Milioni 32 katika shule ya msingi Saku.
5
Baadhi ya wanafunzi wakikokotoa hesabu walizopewa na Mh. Meya wa Manispaa ya Temeke Halmashauri ya wilaya ya Mh. Temeke Abdallah Chaurembo.
6
Mh. Meya wa Halmashauri ya wilaya ya Temeke Abdallah Chaurembo akiwafundisha hesabu wanafunzi wa darasa la sita katika shule ya ya msingi Saku.
7
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi wenzake mara baada ya makabidhiano ya madarasa hayo.
8
Mh. Meya wa Manispaa ya Temeke Halmashauri ya wilaya ya Mh. Temeke Abdallah Chaurembo akikabidhi vitabu kwa mwanafunzi Leokadia Projestus wa darasa la sita shule ya msingi Saku katikati ni Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari
9
Mkuu wa wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaviva. akizungumza na wanafunzi.
10 11
mwanafunzi Leokadia Projestus wa darasa la sita shule ya msingi Saku akitoa hotuba kwa niaba ya wanafuzni wenzake.
12
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akizungumza neno katika makabidhiano hayo.
13
Wanafunzi wakiimba kwaya wakati wa makabidhiano hao