Pages

KAPIPI TV

Wednesday, September 21, 2016

JESHI LA POLISI KILIMANJARO LAWATUNUKU ZAWADI ASAKARI WAKE 34

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akipokea salamu za heshima kutoka kwa askari wakati wa gwaride maalum lililoandaliwa wakati wa hafla fupi ya kutunuku zawadi kwa askari 34 wa vyeo mbalimbali waliotekeleza vyema majukumu yao.kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro ,Wilbroad Mutafungwa.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Saidiq akikagua gwaride la heshima baada ya kuwasili katika viwanja vya kikosi cha kutuliza ghasia mjini Moshi kwa ajili ya hafla ya kuwapongeza na kutunuku zawadi kwa asakari 34 waliotekeleza vyema majukumu yao.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Saidiq akihitimisha ukaguzi wakati wa gwaride maalumu lililoandaliwa kwa ajili ya kuwapongeza asakari walitekeleza vyema majukumu yao.
Gwaride likitoka kwa mwendo wa haraka mara baada ya kumalizika kwa ukaguzi.
Ofisa Mnadhimu wa jeshi la Polisi  mkoa wa Kilimanjaro,Koka Moita akizungumza wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutunuku zawadi kwa asakari 34 wa jeshi hilo waliotekeleza vyema majukumu yao.
Baadhi ya maofisa wa jeshi la Polisi wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi kwa askari 34  waliotekeleza vyema majukumu yao.
Baadhi ya wageni waalikwa katika hafla hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ,Said Mecky Sadiq akizungumza wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutunuku zawadi kwa asakari 34 waliotekeleza vyema majukumu yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro,Wilbroad Mutafungwa akimuoneesha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq baadhi ya silaha zilizokamatwa hivi karibuni zikidaiwa kutumika katika vitendo vya uharifu.
Mkuu wa Kitengo cha dawa za kulevya cha jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Mkaguzi wa Polisi,Ezekiel Midala akimuonesha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro sehemu ya dawa za kulevya zilizokamatwa na jeshi hilo.
Baadhi ya askari waliotunukuwa zawadi kwa utendaji kazi mzuri wakisonga mbele kwa ajili ya kutunukiwa zawadi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akitunuku zawadi kwa baadhi ya askari waliofanya vizuri katika kutekeleza majukumu yao.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Asante Tours ,Cuthbert Swai akizungumza wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutoa zawadi kwa asakari waliofanya vizuri wakati wa kutekeleza majukumu yao.
Pikipiki mbili aina ya Fekon zilizotolewa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Utalii ya Asante Tours ,Cuthbert Swai kusaidia jeshi la Polisi katika kutekeleza majukumu yake ya kila siku.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akiwa ameketi juu ya pikipiki na kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro,Kamishana Mwandamizi Msaidizi wa Polisi,Wilbroad Mutafungwa wakati wa hafla ya kuwapongeza na kutoa zawadi kwa askari  34 wa jeshi hilo mjini Moshi.
Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Said Mecky Sadiq akitoa cheti kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Ibraline ,Ibrahim Shayo akitambua mchango wa wadau kwa jeshi la Polisi. 

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.

Tuesday, August 30, 2016

MKURUGENZI WA FULLSHANGWEBLOG AKABIDHIWA TAARIFA YA UCHAGUZI MKUU 2015

1
Bw . Mohamed Seif Ofisa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa niaba ya Mkurugenzi wa Tume hiyo akikabidhi kwa Bw. John Bukuku Mkurugenzi wa Mtandao wa Fullshangweblog Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2015, Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye mgahawa wa Mokka City Mtaa wa Samora jijini Dar es salaam.
2
Bw. John Bukuku Mkurugenzi wa Mtandao wa Fullshangweblog Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2015 mara baada ya kukabidhiwa rasmi.
3
Bw. John Bukuku Mkurugenzi wa Mtandao wa Fullshangweblog Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2015

MAHOJIANO NA PROF.JULIUS NYANG'ORO KATIKA KIPINDI CHA JUKWAA LANGU

Profesa Julius Nyang'oro ni Mwalimu, mtaalam wa sayansi ya siasa na mwanasheria.
Amekuwa mwalimu tangu mwaka 1977 nchini Tanzania na hapa nchini Marekani.

Ni mwandishi wa vitabu zaidi ya 14, vingi vikiigusia Tanzania kwa namna moja ama nyingine. Moja ya vitabu alivyoandika, na ambavyo vilimtambulisha zaidi kwa jamii ya waTanznia, ni kumhusu Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete. Ambapo ameandika vitabu viwili kumhusu.

Prof Nyang'oro alikuwa mkarimu sana kuungana nasi kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU Jumatatu ya Agosti 29, 2016 kuzungumzia mambo mbalimbali kuihusu Tanzania akiwa mwandishi, mwalimu, mtaalamu wa mausala ya siasa na mwanasheria
KARIBU

RC SINGIDA AKABIDHI MADAWATI 630 KWA WAKURUGENZI WA WILAYA NA MANISPAA

Na Mathias Canal, Singida


Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri za Mkoa wa Singida wamekabidhiwa jumla ya madawati 90 kwa kila Halmashauri ili kuondoa adha waliyokuwa wanakumbana nayo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Mkoani humo ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kampeni ya kuchangia madawati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipowaagiza wakuu wa mikoa yote nchini wakati akiwaapisha Ikulu, jijini Dar es Salaam Machi 15, 2016.




Wakurugenzi hao wametakiwa kuyachukua haraka madawati hayo na kuyapeleka Katika shule zenye kadhia hiyo ikiwa ni ishara ya kuamsha taswira ya elimu kwa wanafunzi mchini kuondokana na mateso ya kukaa chini wakiwa darasani.


 Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Mathew J. Mtigumwe wakati wa makabidhiano hayo katika Ukumbi wa Ofisi za Mkoa huo huku akisifu wadau na Taasisi mbalimbali kujitolea kuunga mkono uchangiaji wa madawati ambao awali ulianza kwa ngazi ya Halmashauri kabla ya kuhusisha taasisi mbalimba sambamba na wadau wa maendeleo Mkoani humo.
Mtigumwe amesema kuwa Hali ya Madawati katika Mkoa ilikuwa chini ya asilimia 40% lakini chini ya uongozi wake kwa kushirikiana na wadau 67 wa Maendeleo wameweza kuchangia jumla ya shilingi milioni 42,626,500 hivyo kufanikisha lengo la utengenezaji wa madawati kufikia asilimia 98% ambapo hata hivyo upungufu Mkubwa ulikuwa zaidi katika Halmashauri za Singida na Manyoni.

WATANZANIA WARAHISISHIWA UPATIKANAJI WA HUDUMA ZA TEKNOLOJIA


Pamoja na kuwepo kwa maendeleo ya kasi katika nyanja mbalimbali lakini sekta ya teknolojia inabaki kuwa moja ya njia ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa mafanikio hayo kwa kurahisisha kazi nyingi kufanyika kwa haraka.

Kwa kutambua hilo, kampuni inayohusika na utoaji wa huduma zinazohusiana na teknolojia ya EnGenius imeingia katika makubaliano na kampuni ya usambazaji wa vifaa vya kiteknolojia ya Red Dot ili iweze kusambaziwa vifaa na huduma mbalimbali ambazo zinafanywa na Red Dot katika nchi za Afrika Mashariki.
Mkuu wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao akizungumzia kazi ambazo wanazifanya na mipango ya kutoa bidhaa bora kwa nchi za Afrika Mashariki.

Kampuni ya EnGenius ambayo inatoa huduma kama za internet wireless, radio frequency (RF) technology na kusambaza bidhaa mbalimbali kama kompyuta imesema kuwa imefanya maamuzi ya kuingi katika makubaliano na Red Dot ikiamini kuwa ni moja ya njia sahihi ambayo itawawezesha kuwafikia wateja kwa karibu zaidi.

Akizungumzia makubaliano hayo, Mkuu wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao alisema kampuni ao kwa sasa inahitaji kujitanua katika nchi za Afrika Mashariki kama Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia hivyo wameungana na Red Dot ili waweze kukuza biashara yao zaidi.

"Tumeingia makubaliano na moja ya wasambazaji wakubwa wa Red Dot na tunaamini watatusaidia EnGenius kufikia malengo yetu ya kuwa wauzaji wakubwa wa bidhaa za kiteknolojia kwa Afrika Mashariki, tunafahamu kuwa ni wasambazaji wakubwa na atatusaidia kukuza biashara yetu," alisema Hsiao.


Na Rabi Hume, modewjiblog.com
Mkurugenzi Mtendaji wa Red Dot Distribution akielezea jinsi ambavyo wamejipanga kufanya kazi na EnGenius. (Picha zote na Na Rabi Hume, modewjiblog.com)

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Red Dot Distribution, Munir Bharwani alisema kuwa ni ushirikiano mzuri ambao wameanza kuufanya na EnGenious na wana mipango mingi kuhakikisha malengo ambayo yamewekwa yanafikiwa.

"Tuna taraji mafanikio makubwa, Red Dot ni kampuni ya kitanzania ambayo inafanya kazi katika nchi za Afrika Mashariki kwahiyo tunatazamia ushirikiano huu utakuwa na faida," alisema Bharwani.
Meneja Mkuu wa Red Dot Distribution Tanzania, Rajesh Adiani akifungua halfa ya uzinduzi wa makubaliano kati ya Red Dot na EnGenius kwa kuelezea shughuli ambazo wanazifanya.
Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa EnGenius, Alishan Zaidi akilelezea huduma ambazo wanazitoa za kiteknolojia na usambazaji wa vifaa vya kiteknolojia kama kompyuta na kamera za usalama.
Mkurugenzi Mtendaji wa Red Dot Distribution, Munir Bharwani na Mkuu wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao wakipongezana baada ya kuingia rasmi katika makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja.

Baadhi ya wageni waalikwa wakiangalia bidhaa ambazo zinatolewa na EnGenius.
Baadhi ya wageni waaliakwa waliohudhuria halfa ya makubaliano ya Red Dot Distribution na EnGenius.

Wednesday, August 17, 2016

BLACKFOX MODELS AFRICA WAFANIKISHA ZOEZI YA KUSAJILI VIJANA WA ARUSHA

Jumapili ilikuwa siku ya furaha kwa wanamitindo wa Arusha, kwani timu ya Blackfox Models ilitua jijini humo kusajili vijana wenye fani hiyo.

Zoezi hili lilifanyika katika hoteli ya Tulia Boutique Hotel and SPA iliyopo Sakina.
Miss Aj Mynah, alisema " nimefurahi sana kwa sisi kufanikisha jambo hili, kwani, lengo letu kubwa ni kuendeleza vipaji vya vijana hawa hasa kwenye uanamitindo na hata kwenye mambo ya Arts Vililevile.

Tumeona Arusha ina vipaji vingi sana, na tumekuta kijana mmoja utakuta ana kipaji cha kuimba, uanamitindo, acrobatics na hata kucheza. Kwakweli tumefurahishwa na tutafanya vilivyo kuhakikisha tunakuza vipaji hivi - alisema AJ.
Blackfox wamesajili vijana 12 kutoka Arusha, na wameahidi kutembea kwenye miji mingine kusajili.

Blackfox Models Africa, ni Agency ambayo inajihusisha kwenye kusajili vijana na kuwapa mazoezi kwenye uanamitindo, pia kuwatafutia kazi za kwenye uanamitindo nchini. Ofisi yao iko Karibu na ubalozi wa Marekani. Kwa wale vijana ambao wanataka kuingia Blackfox wanaweza kwenda kwenye tovuti yao www .blackfoxmodelsafrica.com< /div>

KAIMU KAMISHNA MSAIDIZI WA SHIRIKA LA MAENDELEO YA PETROLI KUTOKA WIZARA YA NISHATI NA MADINI ATUA TANGA KUANGALIA ENEO LITAKAPOJENGWA GATI KWA AJILI YA KUSHUSHIA MAFUTA GHAFI


 Greda likisafisha eneo ambalo linatarajiwa kujengwa gati kwa ajili ya kushushia mafuta ghafi
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kulia akiwa na viongozi kutoka Wizara ya Nishati na Madini walipotembelea sehemu  ambayo litajengwa gati mpya eneo la Chongoleani jijini Tanga kushushia mafuta ghafi kulia ni Kaimu Kamishna Msaidizi wa Petroli kutoka Wizara ya Nishati na Madini ,Mwanamani Kidaya kushoto ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kushoto akisisitiza jambo wakati walipotembelea eneo la Chongoleani ambapo kutajengwa gati ya kushushia mafuta ghafi



Kaimu Kamishna Msaidizi wa Petroli kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Mwanamani Kidaya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kulitembelea eneo hilo leo
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akizungumzia namna mkoa huo ulivyojipanga na fursa hiyo mara baada ya kulitembelea eneo hilo

Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika kulia akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa tatu kutoka kushoto namna walivyojipanga kutokana na fursa hiyo
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Petroli kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Mwanamani Kidaya kushoto akimuonyesha kiti Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella mara baada ya kutembelea eneo hilo






Muonekano wa eneo ambalo kutajengwa gati mpya kwa ajili ya kushushia mafuta ghafi
Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.