Pages

KAPIPI TV

Saturday, July 23, 2016

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII,MHANDISI RAMO MAKANI ATEMBELEA HIFADHI YA TAIFA YA KISIWA CHA RUBONDO

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Rubondo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akipokelewa na Mbunge wa Geita Vijijini Joseph Kasheku (Msukuma) mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ,Herman Kapufi mara baada ya kuwasili katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha  Rubondo. 
 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Utalii katika Shirika la Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ,Missana Mwishawa muda mfupi baada ya kuwasili katika hifadhi hiyo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisalimiana na baadhi ya watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo.
  Mkurugenzi wa Idara ya Utaliii wa Shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) Ibrahimu Musa akiteta jambo na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani kabla ya kuanza kikao na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Mkurugenzi wa Idara ya Utaliii wa Shirika la Hifadhi za Taifa,(TANAPA) Ibrahimu Musa akizungumza wakati wa kikao cha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo.
Baadhi ya Madiwani wa mkoa wa Geita wakiwa katika kikao hicho.
Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ,Missana Mwishawa akisoma taarifa ya hifadhi hiyo kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani.
Mkuuu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo,Missana Mwishawa akimkabidhi Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani taarifa ya Hifadhi hiyo.
Kaimu Mkuu wa mkoa wa Geita ,Herman Kapufi akizungumza katika mkutano wa Naibu Waziri wa  Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani (kulia kwake) alipotembelea Hifadhi ya Taifa ya kisiwa cha Rubondo.kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Utalii wa Shirika a Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa.
Baadhi ya watumishi katika Hifadhi ya taifa ya kisiwa cha Rubondo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo alipofanya ziara ya siku moja katika Hifadhi hiyo.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo pamoja na viongozi wengine wa serikali wa mkoa wa Geita mara baada ya kumalizika kwa kikao na watumishi wa hifadhi hiyo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhandisi Ramo Makani akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa wa Geita mara baada ya kumaliza kikao na watumishi wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo. 

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog kanda ya Kaskazini.

Friday, July 22, 2016

WANACHAMA WA CUF KUPIGA HODI KWA IGP MANGU ENDAPO ATAENDELEA KUKIFUATILIA CHAMA HICHO

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, Shaweji Mketo, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam , wakati wa kutoa msimamo wa chama hicho kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi dhidi ya vyama vya siasa hasa cha Cuf. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Ulinzi Taifa, Mustafa Wandu na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul (wa nne kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, wakati akitoa msimamo wa chama hicho kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi dhidi ya vyama vya siasa hasa cha Cuf. Wengine ni maofisa mbalimbali wa chama hicho.

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, Shaweji Mketo, akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

MKURUGENZI wa Uchaguzi wa Chama cha Wananchi (CUF) Shaweji Mketo amesema iwapo Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, IGP Ernest Mangu ataendelea kukifuatilia chama hicho wanachama wa chama hicho watekwenda ofisini kwake kumsalimia.

Mketo ameyasema hayo Makao Makuu ya Chama hicho Buguruni leo Dar es Salaam leo wakati Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul alipo kuwa  akizungumza na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa chama hicho kuhusu mikakati ya Jeshi la Polisi dhidi ya vyama vya siasa hasa cha Cuf.

"Tunasema sisi Cuf hatumuogopi IGP na kama ataendelea kutufuatafuata haita pita wiki mbili tutamfuata kwenda kumsalimia ofisi kwake" alisema Mketo.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrul
alisema chama hicho kimesikitishwa na kauli ya IGP aliyoitoa hivi karibuni wakati akihojiwa Tido Mhando wa Kituo cha Televisheni cha Azzam kuwa jeshi hilo wakati wowote litamkamata  Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad kwa kuwachochea  wafuasi wake ili waichukie serikali iliyopo madarakani.

Alisema baada ya kuitafakari kauli hiyo ya IGP wamebaini kwamba hivi sasa IGP  Mangu ameamua kuwathibitishia watanzania kuwa jeshi la polisi ni idara maalumu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mazrul  alisema kwa muda mrefu IGP Mangu amekuwa akilitumia jeshi la polisi kushiriki katika matukio mbalimbali ya kuhujumu demokrasia na kukiuka haki za binadamu kwa lengo la kukinusuru Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutokana na anguko kubwa la kukataliwa na wananchi kama ilivyothibitika kabnla na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana.

Alisema jeshi la polisi limekuwa na utaratibu wa kukamata raia, kuwapiga kuwabambikia kesi, kuwashikilia na kuwatesa katika vituo vya polisi bila ya kuwafikisha mahakamani.

Mazrul alisema  hadi sasa zaidi ya wananchi 400 wameathiriwa kutokana na hujuma za jeshi la polisi kwa kuwabambikia kesi.









DKT. REGINALD MENGI AMTUMIA UJUMBE MZITO WAZIRI MKUU, KASSIM MAJALIWA

Katika kufikia malengo ya Tanzania kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025, Mwenyekiti wa Taasisi za Sekta Binafsi (TPSF), Dkt. Reginald Mengi amemtumia Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa ujumbe kupitia kwa Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana, Wazee na Wenye Ulemavu Mh. Jenista Mhagama, ujumbe ambao anaamini kama ukifanyiwa kazi Tanzania itaweza kufikia malengo yake kwa haraka zaidi.
Dkt. Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti wa makampuni ya IPP alituma ujumbe huo kwa Waziri Mkuu wakati ufunguzi wa Kongamano la Mashauriano ya Ushiriki wa Watanzania katika Uwekezaji ambalo linafanyika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam, kongamano lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC).

Alisema kuwa pamoja na serikali kufanya jitihada nyingi ili kuwashirikisha wananchi wake katika uwekezaji kwa ajili ya kukuza uchumi wa nchi lakini bado kuna changamoto nyingi ambazo zimekuwa zikijitokeza na zinahitaji kufanyiwa kazi.

Mwenyekiti wa Taasisi za Sekta Binafsi (TPSF), Dkt. Reginald Mengi akizungumza katika Kongamano la Mashauriano ya Ushiriki wa Watanzania katika Uwekezaji kwa niaba ya TPSF ambapo alitumia fursa hiyo kuishauri serikali mambo ambayo anaamini serikali ikiyafanyia kazi uchumi wa Tanzania utakua kwa kasi tofauti na sasa.(Picha na Modewjiblog)

"Serikali imekuwa ikitumia pesa kuwapeleka vijana kusoma nje lakini nikakutana na kijana mmoja akaniambia kasoma nje lakini bado hana ajira na alipelekwa kusomea digrii ya mambo ya mafuta na gesi,

"Nadhani ni vyema serikali ikabidili mwenendo wake na kuhakikisha vijana wote ambao wanapelekwa kusoma nje wakirudi nchini wapewe nafasi za kazi ili kulisaidia taifa kwa hiyo naomba utufikishie ujumbe kwa Waziri Mkuu ukienda Dodoma katika mkutano mkuu wa chama," alisema Dkt. Mengi.

Pia alisema nchi yetu imekuwa ikitegemea zaidi kilimo hivyo iwekeze katika kilimo na iache kuagiza nje bidhaa ambazo zinatengenezwa na vyakula ambavyo vinapatikana nchini lakini pia kuwapa vipaumbele wawekezaji wazawa na hata wanapokuja wageni ihakikishe na watanzania wanashiriki kikamilifu katika kuwekeza.

Mwenyekiti wa Taasisi za Sekta Binafsi (TPSF), Dkt. Reginald Mengi akizungumza katika Kongamano la Mashauriano ya Ushiriki wa Watanzania katika Uwekezaji lililoandaliwa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi.

"Nchi yetu kwa miaka mingi tunajulikana kuwa tunafanya zaidi kilimo na nadhani hapa kunahitaji ushirikishwaji mkubwa wa watanzania na tuache kulima nanasi na hapo hapo tunaagiza juisi ya nanasi nje ni muhimu watanzania watambue kuwa nchi yao ni tajiri na wakishiriki kikamilifu itafika mbali," alisema Dk. Mengi.

Kwa upande wa Waziri Mhagama ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi alikiri kuwepo kwa baadhi ya changamoto ambazo zimekuwa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi lakini serikali inalifahamu hilo na wameanza kufanya mabadiliko ya sheria na sera wanazozitumia kwa sasa.

Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri mkuu Kazi, Ajira, Vijana, Wazee na Wenye Ulemavu Mh. Jenista Mhagama akitoa hotuba katika kongamano hilo pamoja na kujibu baadhi ya hoja alizotoa Dkt. Mengi.

"Serikali inalifahamu jambo hilo kama kuna umuhimu wa kufanya mabadiliko ili kuwasaidia Watanzania kukuza uchumi wao na wa taifa, kwa sasa tumeanza kufanya mabadiliko kwa baadhi ya sheria na sera na tutaendelea kuangalia ni wapi kunahitajika mabadiliko ili kila jambo lifanyike kwa faida ya watanzania wote," alisema Waziri Mhagama.

Akielezea kongamano hilo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng`i Issa alisema malengo ya kongamano ni kubadilishana mawazo na wadau mbalimbali wa serikali na sekta binafsi lakini pia kushirikisha mashirika ya nje ya nchi ili kuweza kupata njia bora ambayo itakwenda kutumika katika kuwashikirikisha watanzania wote ili kila mmoja ashiriki kukuza uchumi wa taifa.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng`i Issa akielezea malengo ya kongamano hilo la siku mbili.

Baadhi ya wageni waalikwa ambao wamehudhuria kongamano hilo la siku mbili.



Wageni rasmi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa kongamano.

KUELEKEA MKUTANO MKUU MAALUMU WA CCM MJINI DODOMA, WAJUMBE KUTOKA MKOANI MWANZA WAELEZEA IMANI YAO

Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM mkoani Mwanza, Simon Mangelepa, akizungumzia maandalizi ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho kutoka mkoani Mwanza, ambao tayari wameanza kuwasili mkoani Dodoma kwa ajili ya Mkutano huo ambao unatarajiwa kufanyika Jumamosi Julai 23,2016 ambapo pamoja na mambo mengine pia Mkutano huo ni maalumu kwa ajili ya uchaguzi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa.

Katika Mkutano huo, Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa Chama cha Mapinduzi CCM wanatarajiwa kumpitisha kwa kura za ndiyo Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.John Pombe Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho, akipokea Uongozi kutoka kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa Chama cha Mapinduzi CCM kutoka mkoani Mwanza, wamesema wana imani kubwa na Rais Dkt.John Pombe Magufuli ambaye anatarajiwa kukabidhiwa uenyekiti wa Chama hicho ngazi ya Taifa.

Katibu Mwenezi wa CCM mkoani Mwanza, Simon Mangelepa, ameyasema hayo hii leo, wakati akizungumzia maandalizi ya wajumbe hao ambao baadhi yao tayari wamewasili mkoani Dodoma kwa ajili ya Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM unaotarajiwa kufanyika Jumamosi ya Julai 23 mwaka huu.

“Sisi wajumbe tunaotoka Mkoa wa Mwanza tunaamini kwamba anatosha (JPM) na yuko makini na chama chetu kitaendelea kuimarika zaidi akikabidhiwa uongozi. Amesema Mangelepa na kuwasihi viongozi wengine wa CCM kuanzia ngazi ya Mashina, Matawi, Kata, Wilaya na Mkoa, kuendelea kukiimarisha chama, ikiwemo kusimamia vizuri Ilani ya uchaguzi katika kuwaletea maendeleo wananchi hususani wanyonge kama Rais Magufuli anavyosisitiza.

Ametanabaisha kwamba wananchi wakiwemo wanaccm, wanayo matumaini makubwa kwa Rais Magufuli katika utendaji wake wa kazi, na kwamba wapenda amani na maendeleo wanaochukia rushwa pamoja na ubadhirifu wanampenda sana.

Katika hatua nyingine Mangelepa amepuuzilia mbali madai yanayotolewa na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani wanaobeza utendaji kazi wa Rais Magufuli na kwamba hiyo inaashiria hofu waliyo nayo baada ya kukabidhiwa uongozi wa CCM kwa kuwa watakosa hoja za kuzungumza kisiasa.
Bonyeza HAPA Kusikiliza. Au Bonyeza Play Hapo Chini.

MAN UTD DORTMUND KUFUNGUA PAZIA LA MICHUANO YA ICC ITAKAYOONEKANA KUPITIA STARTIMES




 Na Dotto Mwaibale

 IKIWA chini ya kocha wake mpya Mreno, Jose Mourinho, Manchester United wanatarajia kushuka dimbani jijini Shanghai, China kuwakabili Borrusia Dortmund siku ya Ijumaa Julai 22, 2016 mechi itakayopigwa saa tisa za alasiri kwa saa za hapa nyumbani kupitia ving’amuzi vya StarTimes.

Akizungumzia juu ya habari hiyo njema kwa wapenda soka nchini Makamu wa Rais wa StarTimes Tanzania, Bi. Zuhura Hanif amebainisha kuwa michuano hiyo itakuwa ni ya kusisimua kutokana na orodha ndefu ya timu kubwa zitakazoshiriki kama vile Real Madrid, Barcelona, Manchester United, Manchester City, Paris Saint-Germain, Juventus, Liverpool, Chelsea na Bayern Munich kwa uchache.

“Tunayofuraha kuwatangazia wateja wetu na watanzania kwa ujumla kuwa watapata fursa ya kutazama timu zao katika mechi za awali kabla ya kuanza kwa ligi kuu mbalimbali duniani kupitia ving’amuzi vya StarTimes pekee. Mechi zote za michuano ya ICC itaonekana moja kwa moja kupitia chaneli ya World Football inayopatikana katika kifurushi cha Mambo kwa malipo ya shilingi 12000/- tu kwa mwezi. Michezo yote itakuwa ni yenye msisimko mkubwa kwani timu zinazoshiriki ni kubwa, nyingi zikiwa ni mabingwa katika ligi kuu zao, zina wachezaji nyota na kikubwa zaidi zingine hazikuwahi kukutana kabla.” Alisema Bi. Hanif

“Hii ni fursa ya pekee kwa watanzania kwani tunafahamu ya kuwa ni wapenzi wakubwa wa mchezo huu na siku zote StarTimes tunajitahidi kuwapatia kile wanachokipenda. Hii ni mara ya pili tunaonyesha moja kwa moja michuano hii kwani mwaka jana tulifanya hivyo ambapo timu ya Real Madrid waliibuka mabingwa. Hivyo basi mashabiki watakuwa na shauku kubwa ya kujua ni timu gani itakayoibuka mabingwa au kama utarudi kwa Real Madrid,” alisema na kumalizia Bi. Hanif kuwa, “Ni wajibu wetu kuhakikisha wanafikiwa na matangazo ya vipindi vizuri na kusisimua kama hivi kwa ubora wa hali ya juu na gharama nafuu ambazo kila mtu atazimudu.”

Mchezo huo ni sehemu ya ufunguzi wa michuano ya kombe la mabingwa wa kimataifa almaarufu kama International Champions Cup au ICC itakayoanza kutimua vumbi Julai 22 na kumalizika Agosti 13, 2016 katika viwanja mbalimbali nchini Marekani, Ulaya, Australia na China.

Katika michuano hii wapenzi wa soka duniani watapat fursa kujionea kwa mara kwanza mechi ya watani wa jadi kutoka jiji la Manchester au unavyojulikana kama ‘Machester Derby’ miongoni mwa mashabiki wengi. Mechi hiyo itapigwa siku ya Jumatatu ya Julai 25 jijini Beijing, China.

Mchezo huo utanogeshwa si tu na ushindani baina ya wachezaji au mashabiki bali safari hii ni makocha waliopewa vibarua vya kunoa vikosi hivyo, Jose Mourinho wa Manchester United na Pep Guardiola wa Manchester City.

Ukiachana na mechi hiyo, pia macho ya mashabiki wengi yatakuwa yakisubiria kwa hamu kutazama mechi kali zitakazozikutanisha timu za, Real Madrid na  PSG,  Chelsea na Liverpool, Real Madrid na Chelsea, Bayern Munich na Real Madrid pamoja na Liverpool na Barcelona.

Kwa ujumla timu zitazoshiriki  michuano hii ni pamoja na Real Madrid, Barcelona, Manchester United, Manchester City, Paris Saint-Germain (PSG), Juventus, Liverpool, Chelsea, Bayern Munich, Liverpool, Tottenham Hotspurs, AC Millan, Inter Millan, Leicester City FC, Celtic FC, Atletico Madrid, Melbourne Victoria na South China.

Thursday, July 21, 2016

“NAVY KENZO KUMSINDIKIZA MISS TANGA 2016”


                      

                NA, MWANDISHI WETU TANGA
MSANII wa Mziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania Navy Kenzo anatarajiwa kutumbuiza kwenye shindano la kumtafuta malkia wa Mkoa wa Tanga Miss Tanga 2016 litakalofanyika Julai 29 mwaka huu kwenye ukumbi wa Hotel ya Tanga Beach Resort.

Licha ya Navy Kenzo wasanii wengine ambao watasindikiza onyesho hilo kwa kutoa burudani ni kundi la mziki wa kizazi kipya mkoani Tanga,Wazenji Classic pamoja na Dances.


Akizungumza jana,Mratibu wa Onyesho hilo, alisema kuwa maandalizi ya kuelekea shindano hilo yanaendelea vizuri ambapo tayari warembo watakaoshiriki wameanza kuingia kambini .


Shindano hilo ambalo limeandaliwa na kituo cha Radio cha TK FM 88.5 kilichopo mjini Tanga kwa kushirikiana na Hotel ya Tanga Beach Resort wameelezea namna walivyo jipanga kuhakikisha onyesho hilo linakuwa na ushindani mkubwa kutokana na aina ya warembo waliopo .

   
“Nisema tu tumejiandaa vizuri kuhakikisha shindano hilo linafanyika kwa umakini mkubwa ili kuwawezesha wadau wa tasnia ya urembo mkoani hapa kuweza kupata ladha halisi ya onyesho hilo kwani licha ya kuwaona warembo wakali wakini pia mzee wa kamatia chini atakuwepo kuwapagawisha “Alisema.


Hata hivyo alisema kuwa mazoezi ya warembo watanaoshiriki onyesho hilo yanaendelea kwenye ukumbi wa New Hotel uliopo mjini hapa kuanzia saa kumi jioni.

Aidha alisema kuwa kabla ya kufanyika shindano hilo warembo hao watapata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii mkoani hapa ikiwemo Mapango ya Amboni na Hifadhi ya Taifa ya Saadani.
Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

CHAMA CHA NCCR- MAGEUZI CHABAINI NCHI KUONGOZWA KWA MATAMKO YA RAIS BADALA YA KATIBA



Mkuu wa Idara ya Kampeni na Uchaguzi wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Faustine Sungura (kulia), akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho, Ilala jijini Dar es Salaam leo asubuhi wakati akimkaribisha Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia (katikati), kuzungumza kuhusu maazimio yaliyofikiwa  na Kikao cha Halmshauri Kuu ya Taifa cha kawaida kilichoketi Julai 16 mwaka huu. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambabe.
 Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu maazimio mbalimbali yaliyopendekezwa katika kikao cha Halmshauri Kuu ya Taifa ya chama hicho cha kawaida  kilichoketi Julai 16 mwaka huu. Kushoto Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambabe.


 wanahabari wakiwa kwenye mkutano huo.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

CHAMA cha NCCR Mageuzi kupitia Halmshauri yake Kuu ya Taifa kimesema kinasikitishwa na hali ya nchi hivi sasa ambayo inaongozwa kwa matamko ya Rais badala ya kufuata katiba jambo ambalo ni hatari kwa taifa.


Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi Taifa, James Mbatia wakati akizungumza na wanahabari makao makuu ya chama hicho, Ilala jijini Dar es Salaam leo, kuhusu mapendekezo yaliyofikiwa na kikao hicho.

"Hivi sasa nchi inaongozwa kwa matamko mbalimbali ya Rai badala ya kufuata katiba ya nchi" alisema Mbatia.

Mbatia alisema Rais Dk.John Magufuli amekuwa akiongoza nchi kwa kutoa matamko badala ya kuongozwa kwa kufuata katiba, sheria na kanuni za nchi.

"Mfano siku akiongea na majaji aliwaamuru watoe hukumu haraka dhidi ya waliokuwa na makontena ambayo yalikuwa hayajalipiwa kodi na kuahidi kama wakilipa atawapa sehemu ya fedha hizo wakati bunge ndiyo lenye mamlaka yakuidhinisha matumizi ya pesa za serikali,"alisema Mbatia.

Alisema kutokana na tamko hilo kwa majaji ilikuwa ni kuingilia mamlaka ya Mahakama na Bunge kitu ambacho ni kinyume cha kanuni, taratibu na katiba ya nchi.

Alisema hali hiyo imesababisha demokrasia kukiukwa huku uhuru wa kujieleza (Freedom of Exptression) ukiendelea kudidimia siku hadi siku. 

Alisema kumekuwa na matumizi ya nguvu za dola kupitia jeshi la polisi kwa kuzuia mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa kwa kuwakamata na kuwaweka rumande viongozi wa kisiasa na kuwashtaki kwa  makosa mbali mbali.

"Viongozi wakisiasa wamekuwa wakikamatwa na Jeshi la Polisi kwa makosa mbali mbali lakini kinachofanyika ni ukiukwaji wa uhuru na hazi za vyama vya siasa katika kufanya kazi zao ambazo zipo kikatiba pamoja na sheria za vyama vya siasa,"alisema.

Kwa upande mwingine chama hicho kupitia maazimio ya kikao cha Halmashauri Kuu ya chama kimetangaza kumsimamisha uongozi wa Umakamu Mwenyekiti (Bara) na kumvua uanachama Leticia Ghate Mosore kwa makosa mbali mbali aliyoyafanya ndani ya chama.

Mbatia alisema wameamua kumsimamisha uongozi na kumvua uanachama kwa kukiuka kanuni na katiba ya chama hicho ikiwa ni pamoja na usaliti alioufanya kipindi cha uchaguzi mkuu wa mwaka jana.

"Kwa jumla makosa aliyoyafanya ni pamoja kujihusisha na migogoro ndani ya chama, kutoa tuhuma dhidi ya kiongozi wa cham au mwanachama nje ya utaratibu, kukashifu kiongozi wa chama au mwanachama, kuhujumu chama katika uchaguzi na wakati mwingine wowote na kutoa na kupokea rushwa," alisema Mbatia.

Alisema milango iko wazi kwa Leticia kukata rufaa kama atakuwa hajaridhika na maamuzi hayo na rufaa yake itasikilizwa na kama ataonekana hana hatia juu ya makosa hayo atarudisha kundini.

Aidha kuhusu chama chake kushiriki katika muungano wa Umojka wa kaiba ya wananchi (Ukawa), alisema chama hicho kitaendelea kushirikiana na vyama hivyo kwa nguvu zote.

Alisema kupitia umoja huo chama chake kipo pamoja na wanachi katika kupambana na kupigania kuhakikisha katiba mpya inapatikana kama matakwa yao wananchi wenyewe.

Alisema ikiwa Jaji Lubuva ataleta katiba ile iliyopitishwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) watapiga kampeni za kuipinga kwa nguvu zote mpaka itakapopatikana katiba inayokidhi mahitaji ya wananchi.




SBL YAZINDUA BOMBA LA MIL.470/= KUDHIBITI MAJITAKA.



Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina (katikati) akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Helene Weesie  wakiongozana kuelekea kwenye  bomba la kudhibiti wa majitaka  ambalo linalenga  kuhakikisha kiwango cha juu kiafya kwa kampuni, mazingira  na wakazi wa maeneo yaliyo karibu.





Mkurugenzi wa Mahusiano wa kampuni ya bia ya Serengeti, John Wanyancha akifafanua jambo kwa wageni waalikwa katika hafla   ya uzinduzi wa bomba la majitaka  ambalo lilizinduliwa na  Mhe. Luhaga Mpina Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira mapema leo katika kiwandani hapo mapema leo.









Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina , Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Helene Weesie na waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini jinsi mtambo wa kusafirisha majitaka unavyofanya kazi kutoka kwa mmoja wa wasimamizi wa mradi huo.





Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina (katikati) akifurahi jambo  na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Helene Weesie mara baada ya kukata utepe katika mtambo kusafirisha majitaka katika hafla iliyofanyika mapema leo kiwandani hapo,


Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina akiwasha mtambo wa kusafirisha majitaka  kiwandani hapo mara baada ya kuzindua rasmi katika hafla iliyofanyika katika kiwanda hicho Temeke Jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa bomba la kudhibiti majitaka katika kiwanda cha bia cha serengeti wakifuatilia kwa makini

Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Raisi Mazingira Mheshimiwa Luhaga Mpina akiongea na wafanyakazi wa kiwanda cha bia ya serengeti mara baada ya uzinduzi wa bomba la kudhibiti majitaka katika kiwanda hicho Jijini Dar es salaam.

Dar es Salaam, Kampuni ya Bia ya Serengeti leo imezindua  bomba la kudhibiti wa majitaka  ambalo linalenga  kuhakikisha kiwango cha juu kiafya kwa kampuni, mazingira  na wakazi wa maeneo yaliyo karibu.


Bomba hilo  limejengwa chini ya usimamizi wa Kampuni ya Maji Safi na Taka  ya Dar es Salaam (Dawasco), Mamlaka ya Barabara (Tanroads) na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke  likihusisha takribani  kilometa mbili kuanzia katika kiwanda cha bia cha Serengeti kilichpo Temeke  hadi Kurasini ambako ndip ulipo mfumo wa majitaka wa Dawasco.


Akizungumza wakati wa uzinduzi, huo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti Helene Weesie, alisema kwamba  mradi huo wa aina yake na wa kwanza nchini unadhihirisha juhudi zisizo na ukomo za kampuni hiyo katika kuhifadhi mazingira.


“Ubora wa maji ni jambo lililo mstari wa mbele katika utengenezaji wa bia  lakini suala la usafi kutokana na kuzalishwa kwa majitaka ni sehemu kubwa inayotujengea hisia za kimazingira katika shughuli za kutengeneza bia. Kwa hiyo uzinduzi wa bomba hili ni moja ya hatua ya kusonga mbele  katika kuhakikisha yanakuwepo mazingira safi kiafya,” alisema Weesie.


Mkurugenzi Mtendaji huyo alibainisha kwamba majitaka yanayotolewa na bomba hilo yatakuwa yanafanyiwa tiba kwanza ili kuondoa aina yoyote ya sumu kabla ya kuachiwa ili kuingia katika mfumo wa majitaka wa Dawasco.


 Alisema kuwa uzinduzi huyo uko katika mkondo  mmoja na sera ya Kampuni ya Serengeti ya kujikita katika ustawi wa jamii ambayo imeainishwa katika maeneo manne ya vipaumbele ambavyo vinajumuisha, Utoaji wa Stadi za Maisha, Uendelevu wa Mazingira na Kuboresha Unywaji wa Kistaarabu.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Masuala ya Muungano na Mazingira, Mh. Luhanga Mpina aliipongeza Serengeti kwa kuzindua bomba hilo  akibainisha kwamba  ujenzi  unaendana na ajenda ya serikali  ya uhifadhi wa mazingira.

Mpina alibainisha kwamba uchafuzi wa mazingira katika miji na maeneo ya pembezoni unaathiri afya za watu wengi na kupunguza tija inayotokana na mazingira na kutoa wito kwa makampuni mengine kuiga  kazi nzuri ya Kampuni ya Bia ya Serengeti katika kuhifadhi mazingira.