Pages

KAPIPI TV

Friday, June 10, 2016

WATOTO WALIOZALIWA NA MAMBUKIZI YA VVU MATUMAINI DODOMA, WAITAKA JAMII KUWAKUMBUKA

Imeelezwa ili kuwawezesha watoto yatima ambao walizaliwa wakiwa na Virusi vya UKIMWI ambao wanapatikana katika Kituo cha Matumaini kilichopo Manispaa ya Dodoma, Watanzania wametakiwa kuungana kwa pamoja na kuwasaidia watoto hao ambao wanaishi katika kituo hicho ili kuwawezesha kuishi mazingira bora pamoja na kupata huduma za bora za afya.

Hayo yalisemwa na Msimamizi wa Kituo cha Matumaini, Sister Maria Rosaria Gargiulo, alisema kituo hicho chenye watoto 151 wakati kimeanzishwa kilikuwa kikipokea msaada kutoka Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na TACAIDS lakini kwa sasa msaada umesimama na hivyo kuwafanya kwa sasa kuishi katika mazingira magumu.

Sister Maria alisema kuwa hali ya maisha kwa watoto hao ni ngumu na hivyo kuwataka Watanzania kuwakumbuka watoto hao ambao walizaliwa wakiwa na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ili waweze kupata huduma bora ambazo zitawawezesha kuishi katika mazingira bora, kupata elimu na kupata dawa ambazo zitaimarisha afya zao.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu (kushoto) na mfanyakazi mwenzake Beatrice Mkiramweni wakiongozwa na Msimamizi wa Kijiji cha Matumaini, Sista Rosaria Gargiulo mara baada ya kuwasili katika kituo hicho kilichopo katika manispaa ya Dodoma karibu na Hoteli ya Mtakatifu Gasper.(Imeandaliwa na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

“Hapa wanakuja tu watu wa hapa Dodoma mara nyingi siku za Jumamosi na Jumapili ila tofauti na hivyo hatuna msaada mwingine, watoto hawa wanahitaji faraja kutoka kwa watu wengine inapendeza kuona watu wanakuja kuwaona na kuwasaidia nao wanafurahi,

“Ukiangalia hali ya kimaisha inazidi kupanda tunafanya jitihada kujisimamia sisi wenyewe lakini tunashindwa bado tunahitaji msaada sisi tumejitoa kuwasaidia hawa watoto hata hatulipwi lakini tunahitaji sana msaada wa Watanzania,” alisema Sister Maria.

Nae Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999 na Mtalaam wa Mawasiliano wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN), Hoyce Temu ambaye alifika kituoni hapo kwa ajili ya kutoa msaada ambapo alituma ujumbe kwa Watanzania wengine ambao wamekuwa hawana utaratibu wa kutoa misaada kwa wahitaji na kuwataka kubadilika.

Bi. Temu alisema kuwa mazingira ambayo wanaishi watoto hao ni magumu na hawana wazazi kutokana na wazazi wao kuwa wamefariki hivyo kuwataka Watanzania kujitoa kwa pamoja na kuwasaidia watoto hao kwa chochote ambacho kinaweza kuwasaidia kuimarisha maisha yao ili waishi mazingira bora.

“Jamani kama watu wanasema tunapoishi kuna shida basi hakuna, shida zipo huku, ukiangalia kuna watoto wengine wana wiki moja na hawana wazazi wametupwa wanahitaji kupata misaada ya Watanzania,

Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akimsikiliza kwa makini mmoja wa watoto wanaoishi kituoni hapo aliyewahi kumuona mara ya kwanza alipofika kituoni hapo.

“Nitoe rai kwa Watanzania wenzangu kama una pesa au nguo au chochote ambacho kinaweza kuwasaidia tutoe kwa watoto hawa mazingira yao ni magumu sana, hawana makosa hawa hata mbele za Mungu naomba tuwasaidie,” alisema Bi. Temu.

Kwa yoyote atakayeguswa na angependa kufika kituoni hapo kusaidia anaweza kupiga simu kwa Msimamizi wa Kituo cha Matumaini, Sister Maria Rosaria Gargiulo +255754272707
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu (kulia) na mfanyakazi mwenzake Beatrice Mkiramweni wakiwa wamewabeba watoto yatima wanaoishi kituoni hapo.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akifurahia jambo mara tu baada ya kuwasili katika kijiji cha Matumaini kilichopo mkoani Dodoma kinacholea watoto yatima ambao 98% wanaishi na Virusi vya Ukimwi.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akiwa kwenye wodi ya watoto wachanga ambao ni yatima wanaoishi waliozaliwa na maambuki ya Virusi vya Ukimwi.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu na mfanyakazi mwenzake Beatrice Mkiramweni pamoja na Msimamizi wa Kijiji cha Matumaini, Sista Rosaria Gargiulo (kulia) walipotembelea wodi ya watoto wachanga waliozaliwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akifurahi na watoto wachanga ambao ni yatima waliozaliwa na maaumbikizi ya Virusi vya Ukimwi waliolazwa katika wodi ya watoto kijiji cha Matumaini kilichopo mkoani Dodoma.
Wewe acheka afurahi kumuona Aunty....Jiji jiji jiji.....jamani acheka....Ni maneno ya Mlimbwende Hoyce Temu akicheza na mmoja wa watoto hao katika wodi hiyo.
Meneja Mwendeshaji wa mtandao wa Habari wa Modewjiblog, Zainul Mzige akimbeleza mmoja wa watoto waliozaliwa na maambukizi ya Virusi vya Ukimwi wanaolelewa katika kijiji cha Matumaini kilichopo mkoani Dodoma.
Eweee Mwenyezi Mungu, mwingi wa Rehema, tunakuomba wajaalie Malaika wako hawa afya njema, maisha marefu, wape uponyaji viumbe hawa wasiokuwa na hatia, Amen!
Msimamizi wa Kijiji cha Matumaini, Sista Rosaria Gargiulo akimsimulia Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu historia ya mtoto Richard aliyeshikwa mikono na mlimbwende huyo.
Mmoja wa Masista wanaohudumia watoto hao Sista Mary Shayo akifurahi jambo wodini mbele ya kamera ya Modewjiblog.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akicheza kwaya ya wimbo maalum aliokuwa akiimbiwa na bendi ya kijiji cha Matumaini kabla ya kukabidhi msaada wa vitu mbalimbali.
Hoyce Temu akigawa zawadi kwa watoto wanaolelewa kwenye kijiji cha Matumaini mkoani Dodoma.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akikabidhi 'Pampers' kwa mmoja wafanyakazi wanaohudumia (jina lake halikuweza kupatikana) watoto kituoni hapo.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akikabidhi mfuko wa sukari.
Mlimbwende wa Taji la Miss Tanzania 1999, Hoyce Temu akikabidhi makopo ya maziwa. (Picha zaidi ingia hapa)

Wednesday, June 8, 2016

MSASA WA SDGS WAENDELEA UDOM, VITIVO VYAKAMILIKA

Ninajisikia kuelimika na kuelewa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu kiasi ya kwamba ninaweza sasa kuwaelimisha marafiki, vijana wenzangu na familia. Elimu hii hapo awali sikuwa nayo, sikuwa naelewa vyema malengo haya. Ukomo wa mpango huu wa dunia ni mwaka 2030 wakati ambapo mimi nitakuwa na umri wa miaka 40. Nataka kuwa sehemu ya mashuhuda wa mafanikio katika utekelezaji wake na ndio maana nataka kutimiza wajibu wangu kwa kupeleka elimu hii kwa wengine.” anasema Jane, mmoja wa washiriki wa semina.

VIJANA 1000 na wanazuoni 200 wa Chuo Kikuu Dodoma (UDOM) wamepatiwa mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu Duniani kwa nia ya kuwawezesha kutumia maarifa yake kusukuma mbele maendeleo ya mkoa wa Dodoma.
Kazi ya kufunza malengo hayo ilifanywa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo hapa nchini kwa kushirikiana na Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mafunzo hayo ni sehemu ya juhudi ya Umoja wa Mataifa (UN) kuwezesha uelewa kwa tumaini kuwafanya wananchi hasa vijana kutambua wajibu wao katika kutekeleza malengo hayo.
Mafunzo hayo katika Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) ni mwendelezo wa mafunzo yaliyozinduliwa Arusha wiki iliyopita na Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Bw. Alvaro Rodriguez.
Mtaalamu wa mawasiliano katika Ofisi ya Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu akiendesha mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu Duniani (SDGs) kwa nia ya kuwawezesha kutumia maarifa yake kusukuma mbele maendeleo ya mkoa wa Dodoma kwa wanafunzi wa vitivo mbalimbali na walimu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yaliyomalizika jana chuoni hapo.(Picha na Modewjiblog)

Mafunzo hayo yalifanywa kwa kundi la vijana 50 kutoka maeneo mbalimbali nchini Tanzania ili waende kusambaza uelewa wa malengo hayo kwa vijana wenzao nchini kote.

Inatarajiwa kuwa zaidi ya vijana elfu 20 watakuwa wamepatiwa mafunzo katika kipindi cha mwaka mmoja ujao.

Akizungumza katika kampasi ya UDOM Bw. Rodriguez alisema kwamba Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) yanahitaji ushirikiano wa watu wote ili kuyafanikisha kama ilivyokusudiwa. Malengo ya Maendeleo Endelevu ukomo wake ni mwaka 2030.

Aliwapongeza wanachuo na wanazuoni kwa kujikita kwao kuelewa Malengo ya Maendeleo Endelevu ambayo ndiyo malengo ya dunia ili kuweza kuyasimamia na kuyatekeleza.

Pia alizungumzia umuhimu wa vijana kushiriki katika masuala ya maendeleo hasa kwa kuzingatia kwamba asilimia 60 ya wananchi wa Tanzania ni vijana.

“Mna wajibu mkubwa kwa vijana wenzenu” alisema Bw. Rodriguez na kueleza kwamba amefurahishwa kuona kwamba vijana na wanazuoni 1,200 wameahidi kuwa walimu na mabalozi wa malengo ya maendeleo endelevu majumbani kwao, katika taasisi zao na katika jamii inayowazunguka.



Pichani juu na chini ni Sehemu ya wanafunzi na walimu wa UDOM wakimsikiliza mkufunzi Hoyce Temu (hayupo pichani) kwa makini wakati wa mafunzo ya siku mbili yaliyomalizika jana chuoni hapo.

Alisema katika hilo Umoja wa Mataifa utaendelea kusaidia kuhakikisha kwamba wake kwa waume na vijana wanatekeleza wajibu wao kwa kushiriki vyema katika mipango ya maendeleo yenye kulenga kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu duniani.
Alisema wajibu wa kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu duniani kunategemea watu wote na hasa vijana.

Akipongeza juhudi za kuelimisha za Umoja wa Mataifa, Profesa Flora Fabian kutoka UDOM, alisema chuo hicho kimefurahishwa kuwa moja ya vituo vya kufunza mabalozi vijana wa kusambaza elimu na wajibu katika kufanikisha Malengo ya Maendeleo Endelevu.

Alisema malengo hayo ya Dunia ni lazima yajulikane kwa kila mmoja; huku akiwataka wanazuoni kuyazungumza katika kazi zao za kila siku, katika tafiti na ripoti kama ilivyo kwa wanafunzi ambao wanastahili kupikwa kuwa katika nafasi ya kuweza kuchambua malengo hayo kwa kuwa na takwimu na taarifa sahihi.

Alipongeza uamuzi wa utoaji elimu wa Umoja wa Mataifa na kuamini kwamba watasambaza elimu hiyo kwa vyuo vikuu vyote nchini Tanzania.

Septemba 2015, viongozi kutoka nchi 193 duniani walitia saini Malengo ya Maendeleo Endelevu duniani. Malengo hayo mapya yanatarajiwa kufanyiwa kazi katika kipindi cha miaka 15 huku ikiweka pamoja shughuli za maendeleo ya kijamii, kiuchumi yanayojali mazingira kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.

Mmoja wa wanafunzi wa UDOM akipitia makabrasha ya SDGs wakati wa mafunzo hayo.
Mhadhiri Msaidizi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Muya Said akitoa maoni wakati wa mafunzo ya siku mbili ya Malengo ya Maendeleo Endelevu Duniani (SDGs) kwa wanafunzi na walimu wa UDOM yenye nia ya kuwawezesha kutumia maarifa yake kusukuma mbele maendeleo ya mkoa wa Dodoma yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini na kumalizika jana chuoni hapo.
Mwanafunzi wa Digrii ya kwanza ya Mifumo ya Biashara katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Janeth Dutu akiuliza swali kwa mkufunzi wa mafunzo hayo (hayupo pichani) wakati wa mafunzo ya siku mbili ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) kwa wanafunzi na walimu wa UDOM yenye nia ya kuwawezesha kutumia maarifa yake kusukuma mbele maendeleo ya mkoa wa Dodoma ambayo yameandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini na kumalizika jana chuoni hapo.
Mkufunzi wa mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs), Hoyce Temu akifafanua jambo kwa washiriki wa mafunzo hayo wakati zoezi la maswali na majibu.
Mhadhiri Msaidizi wa Maendelelo ya Jamii katika Chuo cha Sayansi za Jamii, Sanaa na Lugha (CHSS) katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), Angelo Shimbi akitoa maoni wakati wa mafunzo ya siku mbili ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) kwa wanafunzi na walimu wa UDOM yenye nia ya kuwawezesha kutumia maarifa yake kusukuma mbele maendeleo ya mkoa wa Dodoma yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini na kumalizika jana chuoni hapo.
Beatrice Mkiramweni kutoka Ofisi ya Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, akipitia makabrasha ya SDGs wakati wa mafunzo ya siku mbili ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) kwa wanafunzi na walimu wa UDOM yenye nia ya kuwawezesha kutumia maarifa yake kusukuma mbele maendeleo ya mkoa wa Dodoma yaliyoandaliwa na Ofisi ya Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini na kumalizika jana chuoni hapo.
Mafunzo ya Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Dunia (SDGs) kwa wanafunzi na walimu wa UDOM yakiendelea chuoni hapo.
Kutoka kushoto ni Mhadhiri Msaidizi wa Idara ya Development Studies -UDOM, Edson Baradyana, Ofisa wa Mawasiliano na Ushirikiano NUNV kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Didi Nafisa, Mtaalamu wa Upangaji na Usimamizi wa Miradi -PRO UDOM, Radhia Rajabu, Mhitimu wa kidato cha sita, Aisha Msantu wa Asasi ya Vijana wa Umoja Taifa Tanzania (YUNA) katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez.
Kutoka kushoto ni Mtaalamu wa mawasiliano katika Ofisi ya Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Hoyce Temu, Mhitimu wa kidato cha sita, Aisha Msantu wa Asasi ya Vijana wa Umoja Taifa Tanzania (YUNA) pamoja na Ofisa wa Mawasiliano na Ushirikiano NUNV kutoka Ofisi ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Didi Nafisa katika picha ya ukumbusho mara baada ya kuhitimisha mafunzo.
Picha ya pamoja ya baadhi ya wanafunzi wa UDOM walioshiriki kwenye mafunzo ya SDGs yaliyomalizika jana chuoni hapo. (Picha zaidi ingia hapa)

HIFADHI YA TAIFA YA RUAHA KINARA KWA UJANGILI WA TEMBO NCHINI

Mwalimu wa Uchumi na Utalii Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM),  Profesa Wineaster Anderson (kulia), akitoa mada kuhusu uchumi na Utalii katika mkutano wa mwaka wa Hifadhi za Taifa Tanzania na wanahabari waandamizi kutoka vyombo mbalimbali mjini Morogoro leo.
Mkurugenzi wa Utalii na Masoko wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA), Ibrahim Mussa (kulia), akitoa mada katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI), Dk. Felician Kilahama (kulia), akitoa mada kuhusu misitu katika mkutano huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA), Dk.Allan Kijazi, akizungumza jana katika mkutano huo.
Wanahabari Khadija Khalili (kushoto) na Beatrice wakiwa kwenye mkutano huo.
Wahariri, Bakari Kimwaga (kushoto) na Anicetus Mwesa wakifuatilia mkutano huo.

Mwanahabari Lazaro kulia akijiandikisha katika kitabu cha mahudhurio
Wanahabari na wahariri wakiwa kwenye mkutano huo.
Mwenyekiti wa Chama cha wamiliki wa Blogu Tanzania (TBN), Joachim Mushi akiwa kazini katika mkutano huo ulihudhuriwa na baadhi ya bloger.
Mhariri wa Nipashe, Jesey Kwayu akiuliza maswali.
Mwanahabari na mpiga picha wa gazeti la mtanzania, Humphrey Shao akiuliza maswali.
'Hapa ni kazi tu' wanahabari wakichukua taarifa mbalimbali za mkutano huo.

Na Dotto Mwaibale

MKURUGENZI Mkuu wa Hifadhi za Taifa (Tanapa), Dk. Allain Kijazi amesema Hifadhi ya Taifa ya Ruaha ni kinara wa ujangili wa Tembo ukilinganisha na hifanyi nyingine

Dk. Kijazi ameyasema hayo leo mkoani Morogoro katika siku ya pili ya Mkutano wa Mwaka wa Hifadhi za Taifa Tanzania ulioandaliwa kwa kwa ajili ya wahariri na wanahabari waandamizi wa vyombo mbalimbali vya habari.

"Hali hii ya  ujangili inatokana na kuwepo kwa tembo wengi ambapo majangili wamekuwa wakiingia katika hifadhi hiyo na kufanya uharifu" alisema Kijazi.

Aliongeza kuwa kutokana na hali hiyo jitihada kubwa zinafanya kwa kutumia mfumo wa kiokorojia kwa lengo la kuhakikisha udhibiti wa ujangili unafanikiwa na kunusuru ujangili huo unaotishia katika hifanyi hiyo.


Katika hatua nyingine Dk.Kijazi ametoa mwito kwa Serikali kutengeneza miundo mbinu ya barabara na Wawekezaji kujenga mahoteli katika mikoa ya Kusini na Magharibi mwa Tanzania ili kukuza utalii katika maeneo hayo jambo litakalo inua uchumi wa maeneo hayo na Taifa kwa ujumla.

Aliongeza kuwa baadhi ya mikoa ya Kusini na Magharibi mbayo inavivutio vya utalii lakini imeshindwa kufanya vizuri katika kuingiza watalii wengi kutokana na miondo mbinu yake ya barabara kutokuwa rafiki.

"Ninaamini waandishi wa habari mkitupigia debe na Serikali ikasikilia kilio hiki na kutengeneza barabara kwa kiwango kizuri na Wawekezaji wakajenga mahoteli hakika itasaidia kuvutia watalii kama ilivyo kwa mikoa ya Kaskazini," alisema.

Alifafanua kuwa mikoa ya Kaskazini ambayo inavivutio imekuwa ikipata watalii wengi kutokana na urahisi wake kufikika kwa maana watalii wanahitaji kutumia muda mfupi kufika mbugani ili atumie muda mrefu kuona wanyama.

Aliongeza kuwa hali hiyo ni tofauti na mikoa ya Kusini na Magharibi ambako mtalii atatumia murefu barabarani na kutumia muda mfupi katika kuangalia wanyama na vivutio vingine jambo ambalo si lengo lake.

Alisema licha miundo mbinu ya barabara za Kusini kutokuwa rafiki kufika katika vivutio, pia hata malazi kwa watalii si ya kuvutia na pengine hakuna kabisa hivyo ni changamoto kwa wawekezaji kuhakikisha wanajenga mahoteli ya kisasa.

Aliweka wazi kuwa ikiwa jambo hilo litafanikiwa kwa kuwa na miundombinu mizuri ya barabara na hoteli zenye viwango hakika watalii katika mikoa ya Kusini wataongezeka.


Wakati huo huo, Mkurugenzi wa Masoko Tanapa, Ibrahimu Mussa alisema kuwa ili kuinua mapato yanayotokana na utalii nchini malipo ya watalii yanafanyika kwa kadi za kibenki.

"Tumeamua kuondokana na upokeaji wa fedha kwa 'Cash' ili kuondoa upotevu wa mapato jambo litakalosaidia kuinua kiwango cha ukusanyaji wa mapato tofauti na ilivyokuwa awali,"alisema.

Akizungumzia suala baadhi ya watalii kulipia gharama viingilio wakiwa nchini kwao, alisema fedha wanazolipa zinafika Tanzania na lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha watalii wanakuwa salama katika mali zao.

Aliongeza kuwa hata mtalii akiumia akiwa hapa nchini akiwa kwenye utalii analipwa bima kupitia nchi yake jambo ambalo linamfanya kuwa salama zaidi.

Pia alisema Tanzania imeshuka katika viwango vya vivutio vya asili ikitoka namba mbili nyuma ya Brazil hadi na namba saba na katika viwango vya jumla inashika nafasi ya 93 kati ya nchi 114 zenye ushindani.

Alifafanua kuwa sababu ya kushuka katika viwango hivyo vya dunia ni kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uvamizi wa maeneo ya vivutio hivyo na miundo mbinu ya barabara na changamoto zingine zilizopo.


Tuesday, June 7, 2016

NAIBU SPIKA WA BUNGE ALIVYOTINGA KWENYE SHOW YA LADY JAY DEE MJINI DODOMA

Mwanamuziki Nyota wa Kike nchini Judith Wambura a.k.a Lady Jay Dee anayetamba na kibao chake cha #NdiNdiNdi amefanya onyesho alilolipa jina la #NaamkaTenaTour katika viwanja vya Royal Village, onyesho lililohudhuriwa na watu na watu mbalimbali akiwemo Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson, Waheshimiwa Wabunge, Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez pamoja mashabiki wake mkoani Dodoma.
Mratibu wa show ya Lady Jay Dee ya Naamka Tena Tour ya mjini Dodoma, Mh. Catherine Magige akizungumza machache na kutambua uwepo wa Naibu Spika wa Bunge na waheshimiwa wabunge wenzake katika viwanja vya Royal Village mjini humo.
Malkia wa Bongo Flava, Lady Jay Dee katika ubora wake.

Mwanamuziki Lady Jay Dee na The Band wakitoa burudani kwa wakazi wa Dodoma na vitongoji vyake katika harakati za kuwafikia mashabiki wake wote nchini nzima kwa show aliyoi' brand' kama Naamka Tena Tour.

Mkali wa R & B kwenye Band ya Lady Jay Dee, John Music akitoa burudani kwa wakazi wa Dodoma.
Vijana watanashati wa bendi Lady Jay Dee wakitoa burudani kwa mashabiki wa Dodoma.
Hoyce Temu, Esther Bulaya, Shyrose Bhanji na Hamisi Kigwangalla wakipiga shwangwe kwa Lady Jay Dee alipokuwa jukwaani.

Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson kwenye viwanja vya Royal Village ilipofanyika show ya mwanamuziki Lady Jay Dee mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Alvaro Rodriguez (kulia) akiteta jambo na Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA), Mh. Shyrose Bhanji kwenye show ya Lady Jay Dee iliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
Mh. Esther Bulaya akiserebuka na Hoyce Temu katika show ya Lady Jay Dee iliyofanyika mwishoni mwa juma mjini Dodoma.
Mh. Halima Mdee, Mh. Catherine Magige, Mh. Esther Bulaya pamoja na Hoyce Temu wakiserebuka.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) Alvaro Rodriguez akisalimiana na Mbunge wa jimbo la Kawe, Mh. Halima Mdee walipokutana kwenye show ya Lady Jay Dee.
Mwanamuziki Lady Jay Dee na Band yake wakishambulia jukwaa.
Mashabiki wa Lady Jay Dee wakiserebuka kwa raha zao.
Pichani juu na chini ni Umati wa wakazi wa mjini Dodoma eneo la VIP wakiwemo waheshemiwa wabunge wakisakata muziki wa Lady Jay Dee.
Upendo waliounyesha watu wa Dodoma kwa mwanamuziki Lady Jay Dee.
Mh. Halima Mdee akipata Ukodak na wananchi wa Dodoma wanaomkubali. PICHA ZAIDI INGIA HAPA