Pages

KAPIPI TV

Friday, February 12, 2016

WADAU WA UFUGAJI,KILIMO NA UVUVI WAKUTANA NA KUTOA MAONI YA UCHAMBUZI

Wakulima wadogo wadogo zaidi ya 45  katika harakati za maendeleo nchini na  sekta za uvuvi, na ufugaji kutoka mikoa mbalimbali nchini wamekutana jijini Dar es salaam katika kujadili mwongozo wa kuandaa mpango na bajeti ya serikali 2016/2017.


Warsha hiyo ambayo imeandaliwa  na ushirikino wa mashirika matano ambayo ni  Oxfam, Policy Forum, ANASAF, Action Aid na TGNP zaidi ikiwa ni kuwaleta pamoja wakulima hao wadogowadogo  katika kupitia mwongozo na kuujadili kwa ukaribu pamoja na kuuchambua kwa kina zaidi.


Wakati akitoa majumuisho kutoka ukurasa wa 14-20 Bi Flora Mathias Kutoka Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkulima mdogo ameomba Mkulima ameiunga mkono hoja ya mwanamke kuthaminiwa na kupata nafasi ya kuuza Bidhaa zake, kupewa nafasi ya kujitambua na kumiliki Ardhi, huku akiulalamikia mwongozo huo wa bajeti elekezi kutoweka wazi kuhusu mfuko wa wanawake katika kusaidia uzalishaji na kuomba bajeti inayokuja izingatie hilo.


Mzee Namagono Hassan kutoka kundi la wakulima ametoa  maelezo kutoka ukurasa wa 6-9  kuhusu mambo muhimu katika mwongozo wa Bajeti 2016/17, kuwa pamoja na kuanzishwa kwa Benki ya wanawake, isitazame tuu wanawake wa mjini bali na  vijijini kwani wao ndio wazalishaji zaidi wa Chakula kuliko waishio mijini.



Kwa upande wake Datius Pastory Inshansha Mwanaharakati na Mkulima mdogo ukurasa wa 20-23 amepitia ukurasa 23-24 unaotoa maelekezo mahsusi kwa sekretarieti za mikoa na mamlaka ya serikali za mitaa na kushauri kuwepo uwazi wa mapato na matumizi ya Serikali za Mitaa, pia Bajeti ielekezwe zaidi vijijini kulipo mjini na kudhibiti fedha za uvuvi,kilimo na ufugaji zisiishie kwa watu wachache bali wahusika kwa ujumla.


Maelezo mengine yametolewa na Bwana Adam Simwinga kuhusu ukurasa wa 9-15 kipengele cha Maelekezo ya Maandalizi ya bajeti kwamba amegundua hakuna mkakati wa kuongeza mapato kupitia simu, mkakati wa msamaha wa kodi, hivyo wameshauri kilimo kiwe ni sehemu ya eneo wezeshi na malighali katika viwanda nchini Tanzania na katika mpango wa maendeleo na kuongeza kuwa asilimia 30% hazijitoshelezi kukuza sekta ya kilimo nchini.


Wanaharakati hao wameishauri serikali kutowasahau katika kuwawezesha mikopo ili kukuza sekta zao kimaendeleo huku wakilalamika wakulima  kutoshirikishwa kikamilifu.


“Tunaomba mkopo wa Magari ya wabunge upungue kutoka Mil 90 hadi Mil 20 ili zile mil 70 zitumike katika shughuli zingine za maendeleo ikiwemo na kilimo na pia kuwe na viwanda vidogo vidogo katika mikoa mbalimbali mfano kiwanda cha Machungwa” aliongeza Bi. Kidani Mhenga wanajadili ukurasa wa 3-5 mapitio ya uchumi na utekelezaji wa Bajeti

 Bi. Kidani Mhenga kutoka kikundi namba tatu ambao walikuwa wanajadili ukurasa wa 3-5 mapitio ya uchumi na utekelezaji wa Bajeti za Serikali kuoka katika mpango wa bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2016/2017 
Mzee Namagono Hassan Kutoka kikundi namba moja akitoa maelezo kutoka katika mwongozo wa kuandaa mpango wa bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2016/2017 kutoka ukurasa wa 6-9  unaoelezea mambo muhimu katika mwongozo wa Bajeti 2016/17 
 Bi Flora Mathias Kutoka Mkoa wa Mbeya ambaye pia ni Mkulima mdogo akitoa majumuisho kutoka kipengele cha namna ya kudhibiti Bajeti za Serikali kutoka katika mwongozo wa kuandaa mpango wa bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2016/2017 ukurasa wa 14-20, picha ya juu ni wanakundi wakiwa wanajadili swala hilo. Picha ya juu ni baadhi ya mama Shujaa wa chakula ambao wanatoka katika Kampeni ya Grow inayoendeshwa na Oxfam Tanzania pamoja na wadai wengine wa kilimo
Bwana Adam Simwinga akitoa maelezo kutoka kundi namba mbili ambao walikuwa wachambua mpango wa bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2016/2017 ukurasa wa 9-15 kipengele cha Maelekezo ya Maandalizi ya bajeti
 Datius Pastory Inshansha ambaye ni Mwanaharakati na Mkulima mdogo mdogo akiwasilisha kundi lake la Tano ambao walikuwa wanajadili ukurasa wa 20-23 kutoka katika mwongozo wa kuandaa mpango wa bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2016/2017 inayozungumzia maelekezo mahsusi kwa sekretarieti za mikoa na mamlaka ya serikali za mitaa.
Baadhi ya wakulima, wafugaji na wavuvi wakiendelea namjadala 

Picha na Fredy Njeje/Blogs za Mikoa



TIGO YATOA MSAADA WA MADAWATI 400 KWA SHULE ZA MSINGI MKOANI MOROGORO

Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani Goodluck Charles akiongea na wananchi na wanafunzi waliohudhuria hafla ya kukabidhi msaada wa madawati 400 katika shula za wilaya ya Morogoro vijijini.
Mwanafunzi wa darasa la sita kutoka shule ya msingi kibangile Radia Hamis akishukuru kwa msaada wa madawati  kwa niaba ya wanafunzi wa shule hiyo kwa Mkurugenzi wa Tigo kanda ya pwani Goodluck Charles katika hafla ya kukabidhi madawati 400 kwa shula 10 za wilaya ya Morogoro vijijini.

Mbunge wa jimbo la Morogoro kusini Prosper Mbena akimshukuru Mkurugenzi wa tigo kanda ya pwani  Goodluck Charles baada ya hafla ya kukabidhi  msaada wa madawati 400 yaliyotolewa na kampuni ya Tigo Tanzania kwa  shule 10 za jimbo la morogoro kusini.



Mkurugenzi wa tigo kanda ya pwani Goodluck Charles akimkabidhi Afisa wa Elimu wilaya ya Morogoro vijijini Donald Pambe msaada wa madawati 400 katika shule 10 za wilaya hiyo hafla iliyofanyika katika shule ya msingi  Kibangile



Mkurugenzi wa Tigo, kanda ya Pwani Goodluck Charles(wa nyuma kushoto) na Afisa  Uhusiano wa Tigo Halima Okash (mbele kushoto) wakikabidhi madawati 400 yaliyotolea na kampuni ya tigo Tanzania kwa shule kumi za wilaya ya Morogoro vijijini kwa mbunge wa jimbo la Morogoro Kusini Mh Prosper Mbena (nyuma kulia) na Afisa Elimu wilaya hiyo Donald Pambe katika shule ya msingi Kibangile iliyopo kata ya Matombo.




Februari 11 2016 Morogoro: Kampuni ya Tigo Tanzania imetoa msaada wa madawati 400 yenye thamani ya shilingi milioni 60 kwenye shule 10 za msingi katika mkoa wa Morogoro ikiwa ni mchango wa kampuni hiyo katika kuisaidia serikali kukabiliana na upungufu wa madawati katika shule za msingi nchini.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika katika Shule ya Msingi Kibangile iliyopo Kitemu katika kata ya Matambo, Morogoro Kusini, Mkurugenzi wa Tigo wa Kanda ya Pwani Goodluck Charles mchango huo ni sehemu ya utekelzaji dhamira ya kampuni hiyo ya kuunga mkono shughuli mbalimbali za maendeleo nchini.

“Mchango huu ni sehemu ya jitihada mbalimbali zinazofanywa na Tigo katika kusaidia utekelezaji wa miradi yenye tija kubwa kwa jamii. Tunaamini kwamba kupitia msaada huu, Tigo inatoa mchango wake katika kujenga viongozi wa baadaye wa taifa hili na wanataluuma mbalimbali wakiwamo madaktari, wahandisi na wengineo, "alisema Charles.

Charles alisema mwaka jana Tigo ilikabidhi msaada kama huo wa madawati katika shule za msingi katika mikoa ya Shinyanga, Mbeya na Iringa na kuongeza kwamba kampuni hiyo itaendelea kutoa madawati zaidi sehemu mbalimbali nchini siku za zijazo.

Makabidhiano yalihudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dr Rajabu Rutengwe ambaye alisema madawati hayo 400 yataboresha mazingira ya kujifunzia kwa watoto katika Mkoa wa Mporogoro na kutoa wito kwa wadahu wengine kuunga mkono zoezi hilo.


“Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa kampuni ya Tigo kwa kuwa mdau muhimu kwetu katika jitihada zinazoendelea za kujaribu kupunguza tatizo la ukosefu wa madawati ya kutosha katika shule za msingi za mkoa wetu wa Morogoro. Ni Dhahiri kwamba msaada huu wa madawati 400 yatawawezesha mamia ya wanafunzi wetu kupata sehemu za kukaa na hivyo kujipatia elimu zao katika mazingira bora Zaidi,” alisema Dr Rutengwe. 



UFISADI WA SHILINGI MILIONI 20 WAZUA TAFRANI MSIKITINI JIJINI DAR ES SALAAM

Waumini wa dini ya Kiislam wakizozana nje ya Msikiti wa Masjidi Pelapela uliopo eneo la Mtakuja Vingunguti jijini Dar es Salaam katika swala ya Ijumaa leo mchana, baada ya kutokea tafrani ya waumini hao dhidi ya viongozi wao ambao wanatuhumiwa kutafuna fedha zaidi ya sh.milioni 20 walizochanga kwa ajili ya ujenzi wa msikiti mpya.
Muumini wa Msikiti huo, Mbarouk Mohamed Makame (kushoto), akizungumza kuhusu fedha hizo zinazodaiwa kutumiwa vibaya na viongozi wao. Kulia ni mmoja wa wazee wa msikiti huo, Mzee Selasela.
 Mzee Selasela akionesha dari la msikiti huo lililochakaa ambapo fedha hizo zinazodaiwa kutumiwa vibaya na viongozi wao zingesaidia kuufanyia ukarabati.
Hapa mzee Selasela akionesha uchakavu wa kapeti.
Hapa akionesha vyoo vilivyo chakaa vya msikiti huo.
Mwonekano wa vyoo vya msikiti huo vinavyotumika.
Waumini wakiwa nje ya msikiti huo wengine wakiswali.
Waumini wakiwa mbele ya vibanda vya biashara vilivyopo nje ya msikiti huo.
Watoto wa shule ya awali katika msikiti huo wakiwa na mwalimu wao (kulia)

Na Dotto Mwaibale

TAFRANI kubwa imezuka katika Msikiti wa Masjidi Pelapela uliopo eneo la Mtakuja Vingunguti jijini Dar es Salaam baada ya viongozi wa msikiti huo kudaiwa kutafuna zaidi ya sh.milioni 20.

Fedha hizo imeelezwa kuwa  zilichangwa na waumini wa msikiti huo kwa ajili ya ujenzi wa msikiti mpya baada ya unaotumika kuchakaa.

Imamu mkuu wa msikiti huo aliyetajwa kwa jina la Hamidu Mitanga alilazimika kutoweka ndani ya msikiti huo baada ya kuendesha swala ya Ijumaa iliyofanyika jana mchana kutokana na waumini kuwa na jaziba kufuatia imamu huyo kutamuka kuwa hakuhitaji kuulizwa maswali yoyote kuhusu upotevu wa fedha hizo na kuwa uongozi uliopo utaendelea kuwepo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi msikitini hapo Dar es Salaam leo mchana wakati wa swala ya Ijumaa mmoja wa waumini wa msikiti huo Mbarouk Mohamed Makame alikiri kuwepo kwa ubadhilifu wa fedha za waumini zilizochangwa kwa ajili ya ujenzi wa msikiti mpya.

"Suala la upotevu wa fedha hizo lipo na limeleta changamoto kubwa kwa waumini na kusababisha kuwepo kwa makundi mawili moja likiwa lile linalolalamikiwa kutafuna fedha hizo na lile linalotaka fedha hizo zitolewe maelezo zilipo" alisema Mzee Makame.

Mzee wa msikiti huo na Mwenyekiti wa Kamati ya watu 10 Saidi Ngubi alisema fedha zinazoshindwa kutolewa maelezo ya matumizi yake na viongozi wa msikiti huo zilitokana na mradi wa maji na michango ya waumini.

"Mimi ndiye niliyeanza kuuliza matumizi ya fedha hizo lakini viongozi hao wakawa hawana majibu na badala yake waliivunja kamati yetu na kuchagua nyingine jambo lililoleta sintofahamu" alisema Ngubi.

Imamu mkuu wa msikiti huo Hamidu Mitanda alisema fedha hizo zilitumika kwa ajili ya mchakato mzima wa kupata umiliki wa kiwanja ulipo msikiti huo na michoro ya ujenzi wa msikiti mpya na kuwa yeye ndiye aliyeanzisha mpango wa kupata msikiti ulio bora na si bora msikiti.

"Binafsi sina shida na cheo hiki cha Uimamu kwani nina shughuli zangu nyingi mkitaka kuniondoa fuateni taratibu kama zili zilizoniweka madarakani na sisi kama viongozi dhamira yetu ni kuwa na msikiti uliobora wa ghorofa na si bora msikiti" alisema Mitanga.

Mitanga alisema chokochoko hizo zilianza tangu mwaka 2007 ambapo tulikubaliana kila muumini kati ya waumini 205 achangie sh.5000 za ujenzi lakini waliochangia walikuwa ni waumini wachache ambapo zilipatikana sh.milioni moja tu.

Imamu huyo alisema uongozi unaoendesha msikiti huo hauko tayari kuachia madaraka kwa tuhuma hizo ambazo hazina ukweli alizodai zinachochewa na baadhi ya waumini.

WAZIRI UMMY MWALIMU AONGOZA MKUTANO WA WADAU WA SEKTA YA AFYA WA MWAKA UNAOFANYIKA KARIMJEE

1
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza katika mkutano wa mwaka wa mapitio ya sekta ya afya unaofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, wadau hao wa Sekta ya afya wanajadiliana mambo mbalimbali na baada ya kumalizika kwa mkutano huo kutakuwa na kusaini makubaliano yaliyofikiwa kwa utekelezaji katika sekta ya afya hapa nchini , Katika picha kulia ni Carol Hannon Mshauri wa Afya katika ubalozi wa Ireland nchini Tanzania.PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE
2
Carol Hannon Mshauri wa Afya katika ubalozi wa Ireland nchini Tanzania akizungumza katika mkutano huo Kushoto ni Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu.
3
Dk.Ulisubisya Mpoki Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto akichangia hoja katika mkutano huo unaofanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.
4
Dk. Deo Mtasiwa Naibu Katibu Mkuu wa Afya TAMISEMI akizungumza katika mkutano huo ambao umekutanisha wadau wa afya na kujadili changamoto mbalimbali zinazokabili sekta ya afya.
5
Baadhi ya wadau wakiwa katika mkutano huo
6
7
8
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu katikati na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mh. Suleman Jafo wa tatu kutoka kulia wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa sekta ya afya kwenye mkutano unaofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.
9
Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu katikati na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mh. Suleman Jafo wa tatu kutoka kulia wakiwa katika picha ya pamoja na wadau wa sekta ya afya kwenye mkutano unaofanyika katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam.
10
........................................................................................................................
TAMKO LA PAMOJA KUHUSU VIPAUMBELE VYA SEKTA YA AFYA KWA MWAKA 2016/2017
  1. KINGA NA AFYA YA JAMII
Mwaka 2015 Serikali ya Tanzania ilikamilisha Mpango wa Afya katika Jamii na kuanzisha mafunzo kwa kada mpya za Wahudumu wa Afya ya Jamii (Community Health Workers). Wafanyakazi hawa wana jukumu kubwa kuifikishia jamii huduma za afya za msingi.
Mwaka 2016, Serikali ya Tanzania itaendelea kutekeleza agenda ya huduma za Afya katika jamii kwa kuhakikisha ubora wa mafunzo kwa wahudumu wa Afya ya Jamii, kuendelea kuajiri wahudumu wa Afya ya Jamii na kufikisha huduma za Afya za Kinga na tiba karibu zaidi na jamii.
  1. UWIANO
Mpango Mkakati wa Nne wa Sekta ya Afya (HSSP IV) umejielekeza zaidi katika uwiano na kusaidia maboresho katika Sekta ya Afya katika maeneo ya pembezoni ambayo huduma za Afya hazifiki kwa urahisi. Jambo muhimu katika hili ni kuendelea kusambaza kwa uwiano rasilimali zote za kifedha zilizopo kutoka vyanzo vya ndani na nje.
Ili kuhakikisha uwiano katika mgawanyo wa rasilimali, ni muhimu kuwa na takwimu sahihi kuhusu uwepo wa rasilimali kutoka vyanzo vya nje hususan wadau wa maendeleo, sekta binafsi, mashirika ya dini na mashirika yasiyo ya kiserikali katika ngazi ya wilaya.
Serikali itahakikisha kwamba takwimu zilizopo zinaboreshwa kwa kukamilisha Mpango Kabambe wa kutambua vyanzo vya nje vya mapato kwa mwaka 2016.
  1. UGHARAMIAJI WA HUDUMA ZA AFYA
Mpango wa Afya kwa wote ni kipaumbele cha Serikali ya Tanzania. Mkakati mpya wa ugharamiaji wa Afya ulioandaliwa umeweka wazi njia ambayo Tanzania inaweza kutoa huduma za Afya za uhakika wa kifedha kwa raia wote kupitia mfumo mmoja wa Bima ya Afya ya Taifa.
Kwa mwaka 2016/2017, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto itatafuta kibali kutoka Mpango Mkakati wa ugharamiaji Afya na itaandaa hatua muhimu za utekelezaji wa Mkakati ikiwa ni pamoja na kuhamasisha kupitishwa kwa Sheria ya Mfuko Mmoja wa Kitaifa wa Bima ya Afya na kuleta pamoja mitazamo mbalimbali ya Mfuko wa Afya ya Jamii.
Vilevile, wizara itafanya uhamasishaji ili kuongeza rasilimali za ndani kwa ajili ya Sekta ya Afya na kuongeza jitihada za Wizara mbalimbali katika kuboresha matumizi yenye ufanisi wa rasilimali fedha zilizopo.
Wizara na Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa zitaunda Mfumo rahisi wa utoaji taarifa kuhusiana na mipango, bajeti na fehda, kwa ajili ya vituo vya utoaji huduma za afya, ili kuwezesha ugatuaji wa kifedha kutoka wilaya kwenda ngazi ya vituo vya afya.
  1. UTAWALA NA UONGOZI
Kuna miundo mbalimbali ya utawala na uwajibikaji ndani ya Serikali na katika jamii inayofanya kazi katika ngazi ya wilaya hususani katika masuala ya Afya kama vile Kamati za Uongozi za Vituo vya Afya na zile zenye mamlaka makubwa zaidi kama vile Kamati za Maendeleo za kata. Zote hizo zinajukumu la kuhakikisha uwajibikaji katika utoaji huduma za Afya kwa wananchi.
Kwa mwaka 2016 Wizara, Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Wadau wengine zitaweka wazi mahusiano kati ya miundo hii katika ngazi ya wilaya kuhusiana na Usimamizi wa Mipango, bajeti na fedha kwa ajili ya Afya. Vilevile ili kuendeleza agenda ya ugatuaji, Wizara itashirikiana na Wizara ya Fedha kusimamia mgawanyo wa fedha katika ngazi ya vituo vya kutolea huduma za Afya.
  1. RASILIMALIWATU KATIKA SEKTA YA AFYA.
Kuvutia na kuwezesha idadi kubwa ya watumishi kuendelea na kazi katika utoaji huduma bora za Afya hususan katika maeneo ya vijiji na maeneo ambayo huduma za Afya hazifiki kwa urahisi, ni changamoto nchini Tanzania, maendeleo ya kuridhisha yamefanyika kupitia Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa na Program nyingine.
Ili kuendeleza zaidi mafanikio yaliyofikiwa, mwaka 2016 Wizara, Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa zitaendeleza Sera ya mabadiliko yanayohitajika ili kutekeleza mpango wa mabadiliko makubwa sasa (BRN) kuhusiana na rasilimali watu katika nyanja za afya na zitashirikiana na Serikali za Mitaa kuwezesha utekelezaji wa Sera ya Malipo na motisha.
Ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya, Wizara itakamilisha mwongozo wa kushirikiana katika majukumu, kuweka wazi majukumu ya kila kada na kukamilisha mwongozo wa kujiendeleza kitaaluma.
  1. DAWA, VIFAA NA VIFAA TIBA
Uboreshaji wa usimamizi na utawala wa Dawa, vifaa na vifaa tiba katika vituo vya kutolea huduma za afya hususan katika ngazi ya wilaya ni kipaumbele chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa na Mpango wa Nne wa HSSP.
Matatizo ya kifedha yana maanisha kwamba rasilimali zilizopo hazina budi kutumiwa kwa ufanisi na namna nyingine za ugharamiaji wa dawa na vifaa vingine muhimu hazinabudi kutafutwa. Ili kuhakikisha haya yanafanyika, mwaka 2016 Wizara itajielekeza katika kuboresha utendaji na ufanisi wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) ikiwa ni pamoja na kuwezesha ulipaji wa deni.
Kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Wizara vilevile itahakikisha rasilimali zilizopo na nyingine mpya kwa ajili ya usambazaji wa vifaa zitaelekezwa katika vipaumbele vya mpango wa Matokeo Makubwa Sasa na itatoa miongozo sahihi ya Kisera inayoainisha Mfumo mmoja wa ununuzi wa dawa na vifaa tiba muhimu itakayofuatwa na mamlaka ya Serikali za Mitaa na vituo vya kutolea huduma za Afya.
  1. UFUATILIAJI, TATHMINI NA USIMAMIZI WA TAKWIMU
Maboresho mengi yamefanywa katika mfumo wa usimamizi wa takwimu kwenye Sekta katika miaka ya hivi karibuni, hata hivyo bado kuna changamoto hususan kwa upande wa uhamiaji kwenda katika Mfumo wa kielektroniki na matumizi ya takwimu katika utoaji wa matumizi.
Uwepo wa takwimu sahihi utasaidia wilaya kupanga vizuri matumizi yao.
Wizara imedhamiria kukamilisha Mpango wa kuimarisha ufuatiliaji na tathmini ya huduma za afya kufikia mwisho wa mwaka 2016, ikiwa ni pamoja na kuhama kutoka mfumo wa kutumia karatasi kwenda mfumo wa kielektroniki na pia katika kuongeza uwezekano wa kuunganisha mifumo ya takwimu.
Ili kuendeleza dhana ya utoaji uamuzi unaotokana na ushahidi, Wizara itashirikiana na Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa katika masuala ya takwimu muhimu zinazotokana na mamlaka za Serikali za Mitaa na watumiaji wengine kwa wakati katika mfuko rafiki unaowezesha utoaji wa taarifa za mipango na utoaji wa maamuzi.
  1. UTOAJI HUDUMA
Mwaka 2015 Wizara ilianzisha Mfumo wa tathmini wa vituo vya msingi vya utoaji huduma za afya.
Mfumo nyota ambao unazingatia vigezo vya ubora wa huduma (quality of service) za madaraja katika kuanzisha viwango vya utoaji huduma. Mwaka 2016 Wizara kwa ushirikiano na TAMISEMI itahakikisha kwamba tathmini ya Matokeo ya nyota inatafsiriwa katika uboreshaji huduma katika vituo na kwamba ugharamiaji unawekwa katika Mpango Kabambe wa Afya wa kituo na Halmashauri. Mfumo nyota unaonyesha vituo katika kazi mkoa, rufaa na Taifa utakamilika 2018.
Vilevile, Wizara itaipitia miongozo iliyopo ya usimamizi ili kuainisha majukumu ya ukaguzi na usimamizi.
UZINDUZI WA MPANGO MKAKATI WA NNE WA SEKTA YA AFYA 2015-2020
Utangulizi
Mpango mkakati wa nne (HSSPIV) ni mpango ulioandaliwa kwa kuwashirikisha wadau wote wa sekta ya Afya ikiwa ni pamoja na Serikali, Wadau wa Maendeleo, Sekta binafsi, taasisi za kijamii na Ustawi wa jamii.
Lengo kuu la mpango huu ni :kufikisha huduma bora muhimu za Afya na Ustawi wa jamii katika ngazi za kaya zote nchini.
Mpango unaainisha Mikakati mitano:
1.Kuboresha kiwango cha Ubora wa huduma katika ngazi zote za afya ya msingi kwa kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafikiwa na kitita bora cha afya na ustawi wa jamii
  1. Kuboresha Uwiano wa upatikanaji wa huduma bora za afya na ustawi wa jamii kwa kuondoa tofauti zilizopo za kijografia, kiuchumi na makundi maalum kama vile wazee, watoto, wajawazito na walemavu.
  2. Kuboresha Ushirikishwaji wa jamii katika kupanga na kusimamia huduma za Afya na Ustawi wa jamii. Hii inajumuisha uhamasishaji wa mifuko ya afya ya jamii, usimamiaji wa vituo vya huduma, uwepo wa dawa vituoni, utambuzi wa wasiojiweza ili wapate huduma, na uwajibikaji wa watoa huduma kwa wanajamii husika.
4.Uwekezaji katika mikakati na njia za kisasa na ubunifu
kama : Ugharamiaji
-Mkakati wa Bima moja ya Afya kwa wote
-Ushirikiano na sekta binafsi
-Ushirikiano wa wadau wote wa sekta ya afya maendeleo na ustawi waj amii.
5.Kutambua Ushiriki wa jamii na Sekta nyingine katika afya. Afya bora siojukumu la wizara moja; Hii inajumuisha uhamasishaji wa wa kila sekta kuwa na mkakati wa Afya. Hii itasaidia kushughulikia mambo muhimu kama; Lishe na afya za watoto, Maji safi, elimu ya afya, Usafi wa mazingira, umuhimu wa barabara na mawasiliano katika dharura ya kiafya na itapunguza magonjwa kama kipindupindu, vitambi, presha

YOUNG DEE ATEMBELEA MADUKA YA TIGO NA KUGAWA ZAWADI MBALIMBALI KWA WATEJA NA MASHABIKI ZAKE

Msanii wa kizazi kipya Young Dee akikabidhi zawadi ya tisheti kwa mmoja wa wateja wa Tigo wa tawi la  Makumbusho mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii .
Msanii wa kizazi kipya Young Dee akifurahi jambo na mmoja wa wateja wa tawi zawadi ya tisheti kwa mmoja wa wateja wa Tigo wa tawi la  Makumbusho mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii. 
Msanii wa kizazi kipya Young Dee akifurahi jambo na mmoja wa wateja wa Tigo tawi la Makumbusho baada ya kumkabidhi  zawadi ya tisheti mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii .



Wafanyakazi wa  Tigo wa tawi la  Makumbusho wakiwa katika picha ya pamoja na msanii wa kizazi kipya Young Dee akiwa  mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii .

Msanii wa kizazi kipya Young Dee akihojiwa na mwandishi Emmanuel Onyango   katika  Tigo wa tawi la  Makumbusho mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii 

Msanii wa kizazi kipya Young Dee akitazama simu zinazouzwa katika duka la  Tigo tawi la Tegeta mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii 

Wafanyakazi wa Tigo tawi la Tegeta wakiwa katika picha ya pamoja na msanii wa kizazi kipya Young Dee mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii .

Msanii wa kizazi kipya Young Dee akitoa zawadi ya tisheti kwa mmoja wa wateja wa tawi la Manzese   simu zinazouzwa katika duka la  Tigo tawi la Tegeta mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii 

Msanii wa kizazi kipya Young Dee akikabidhi zawadi ya tisheti kwa  mmoja wa wateja wa tawi la Manzese zawadi ya tisheti mapema leo alipofanya ziara ya kutembelea maduka matatu ya Tigo ya Makumbusho ,Tegeta na Manzese  na kugawa zawadi na kupiga picha na mashabiki wake kuelekea sikukuu ya wapendanao mwishoni mwa wiki hii 

KPMG YAWA KINARA MICHUANO YA AWESOME BONANZA 2016 KATIKA KUNDI LAO

Kikosi cha timu ya KPMG  Waliosimama kutoka kushoto ni Isyaka,Bakari,Isaya, Nsanyiwa,Hamza(kocha),Getrude(kiongozi wa timu) na Jovin.  Walioinama kutoka kushoto ni  Evans, Denis, Jamal, Thobias, Frank, Ahmed na Amiri.    Aliyelala ni Jim aka Messi wa KPMG katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine



 Kikosi cha wachezaji wa Kampuni ya KPMG katika picha ya pamoja katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

 Wachezaji wa timu ya KPMG wakiwa mapumziko kutoka kushoto walioangalia mbele Bakari , Dennis, hamza (kocha mchezaji) na isyaka katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

Wachezaji wa timu ya KPMG wakishangilia Goli dhidi ya Timu ya Deloitte katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

Wachezaji wa KPMG wakishangilia Goli lilifungwa na mshambuliaji wao machachari Daudi Mbaga dhidi ya  timu ya PWC katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine

 Kiungo wa Timu ya KPMG Bakari Mkupe akiwania mpira na wachezaji wa Timu ya PWC.katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita ambapo michuano hiyo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine
Wafanyakazi  wa kampuni ya KPMG waliokuja kushangilia wenzao  kutoka kushoto ni Asha, Mumtaz,Lilian, Witness, Getrude, patricia, desire na Grace.katika michuano ya Awesome Bonanza mwishoni wa wiki iliyopita imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine



Na Krantz Mwantepele,Dar es salaam                                                                                              


Timu ya mpira wa miguu ya kampuni ya uhasibu ya KPMG ilishiriki michuano ya Awesome Bonanza siku ya Jumamosi tarehe 6-Feb 2016 na kuibuka kinara katika kundi lao lililohusisha timu nyingine za makampuni yanayohusika na uhasibu pia.
 Michuano hiyo ambayo imeandaliwa na Jarida la kila mwezi la Awesome magazine ilianza siku ya jumamosi tarehe 6 feb 2016 ikifanyika katika viwanja vya Jakaya Kikwete Park vilivyopo maeneo ya Mnazi Mmoja zamani kidongo chekundu kwa hatua za Makundi kwa kundi la timu kutoka kampuni  za uhasibu.

Katika kundi hilo zilikuwepo timu kutoka kampuni za uhasibu za Deloitte, PWC na Innovex.
Timu ya kampuni ya  KPMG iliibuka kinara wa kundi hilo kwa kupata ushindi katika mechi zao zote. KPMG ilipata matokeo yafuatayo: KPMG 3-1 PWC, KPMG 4-1 Deloitte , KPMG 2-1 Innovex. Hivyo kuwafanya wasonge mbele katika micuano hiyo itakayoendelea mwezi huu.
Wafungaji wa magoli ya KPMG walikuwa
Jim Mwasigala (3)
Bakari Mkupe (2)
Frank Mboya (2)
Ahmed Mohammed
Daudi Mbaga
Akiongea baada ya mechi hizo kocha mchezaji wa timu ya KPMG, Hamza Mzee amesema ya kwamba timu kampuni ya KPMG imejiandaa vyema na wana uhakika wa kushinda michuano hiyo kwa kuwa wanajali utamaduni wa kufanya mazoezi kupitia michezo kwa kuwa huboresha Afya kwa ujumla.