Pages

KAPIPI TV

Saturday, January 30, 2016

WAZANZIBAR WAANDAMANA NCHINI CANADA KUPINGA KURUDIWA KWA UCHAGUZI ZANZIBAR

Na Mwaandishi wetu Washington 
Wakati hali ya kisiasa Visiwani Zanzibar ikiwa inazidi kutokota, bila kujali theluji na baridi kali, Wazanzibari waishio nchini Canada mnamo tarehe 27 mwezi huu walifanya maandamano katika Mji Mkuu wa nchi hiyo, Ottawa katika juhudi za kutafuta uingiliaji kati wa kimataifa katika kusaka suluhisho la amani kwa mgogoro wa kisiasa Visiwani humo.
Mandamano ya Wazanzibari waishio nchini Canada wakiwa mwenye ofisi ya European Union  Mjini Ottawa
Wazanzibari hao waliandamana hadi kwenye Ofisi ya Waziri Mkuu wa Canada kwa lengo la kufikisha ujumbe wao kukhusiana na hali mbaya ya kisiasa huko Zanzibar.
Akizungumza na Swahilivilla, mmoja wa waandaaji wa maandamano hayo Bwana Zamil Rashid alisema kuwa lengo la maandamano hayo ni kuwaunga mkono ndugu zao Wazanzibari katika harakati za kudai demokrasia ya kweli na kupinga hatua za kufutwa kwa uchaguzi Mkuu Zanzibar.
"Madhumuni ya maandamano yetu yalikuwa ni kuwaunga mkono ndugu zetu wa Zanzibar kwa mambo yaliyofanyika, na kwamba hatukubaliani nayo" alisema Bwana Zamil na kuendelea "Wazanzibari walioko nchini Canada wanapinga jambo hilo lilofanywa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na matamshi aliyoyatoa Bwana Jecha Salim Jecha ya kufuta uchaguzi"
Aidha maandamano hayo yalikuwa na lengo la kuiomba Serikali ya Canada kuingilia kati katika kuupatia ufumbuzi mgogoro wa kisiasa Visiwani Zanzibar kabla hali haijawa mbaya zaidi.
Mbali na Ofisi ya Waziri Mkuu wa Canada, Wazanzibari hao pia waliandamana hadi kwenye Ofisi za Umoja wa Ulaya nchini humo kwa dhumuni hilo hilo.
"Vilevile tumefikisha ujumbe wetu kwa Umoja wa Ulaya (EU) ili walishighulikie swala hili haraka iwezekanavyo kabla hayajatokea maafa kwa Wazanzibari", alisema Bwana Zamil.
Katika Risala yao kwa pande zote mbili, waandamanaji hao wametoa wito wa kutangazwa mshindi badala ya kurejewa kwa uchaguzi kama ilivyotangazwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Bwana Jecha Salim Jecha. "Tumetoa wito wa yule aliyeshinda uchaguzi atangazwe, na siyo kurejea uchaguzi" alisisitiza Bwana Zamil.
Kwa kufikisha ujumbe wao kwa Umoja wa Ulaya, wazanzibari hao pia walikuwa na lengo la kutoa wito kwa nchi nyengine duniani kusaidia katika kuupatia suluhu mzozo wa kisiaza Zanzibar, ikiwemo pia kusitisha missada ya kiuchumi kwa Tanzania.

THE TONY ELUMELU FOUNDATION, UNITED BANK FOR AFRICA PLC AND THE UNITED STATES DEPARTMENT OF CPMMERCE PARTNER TO ENABLE ENTREPRENEURSHIP IN AFRICA

Group Shot
U.S Secretary of Commerce, Penny Pritzker; Select Tony Elumelu Foundation Entrepreneurs; Kehinde Yinusa, Evans George, Nosakhare Oyegun, Belema Alagun and Founder Tony Elumelu Foundation, Mr. Tony Elumelu during the panel and roundtable discussion between members of the U.S. Presidential Advisory Council on Doing Business in Africa (PACDBIA) and a diverse community of entrepreneurs hosted by Tony Elumelu Foundation and UBA Plc in Lagos yesterday.
PO SEC TOE
Group Managing Director United Bank for Africa (UBA) Plc, Mr. Phillips Oduoza; US Secretary of Commerce, Penny Pritzker; UBA Chairman, Mr. Tony Elumelu during the panel and roundtable discussion between members of the U.S. Presidential Advisory Council on Doing Business in Africa (PACDBIA) and a diverse community of entrepreneurs hosted by Tony Elumelu Foundation and UBA Plc in Lagos yesterday.

The Tony Elumelu Foundation and United Bank for Africa Plc (UBA) partnered with the United States Department of Commerce to host a panel and roundtable discussion between members of the U.S. Presidential Council on Doing Business in Africa (PCDBIA)and a diverse community of African entrepreneurs.

The 11 person U.S. delegation, along with representatives of several U.S. government trade and investment-focused agencies, was led by the Honourable Penny Pritzker – U.S. Secretary of Commerce. The Council visited Lagos as part of a fact-finding mission to help inform their upcoming report to President Obama on how to strengthen commercial engagement between the U.S. and Africa, which will result in mutually-beneficial growth.

The event – titled “Unleashing Africa’s Entrepreneurs: Strengthening the Entrepreneurial Ecosystem to Empower the Next Generation of Africa’s Business Leaders” – brought together American business leaders and Nigerian entrepreneurs to discuss challenges, solutions and innovations in the current African business environment. The event was designed to allow representatives of the U.S. Government to participate in direct and substantive discussions with Africa’s emerging business leaders – an opportunity to engage in a dialogue that has the potential to influence U.S. foreign policy for Africa.

"President Obama believes, as I do, that the American private sector, working in partnership with the African business community, and African entrepreneurs can help address many of the continent’s most pressing challenges, including creating jobs and opportunity for young people across the continent," said U.S. Secretary of Commerce Penny Pritzker. "I am proud to lead our Administration’s effort to support and empower aspiring entrepreneurs, both in the United States and across the globe."

UBA Chairman Tony O. Elumelu, through his eponymous Foundation, hosted the delegation, and expressed gratitude for the collaborative approach the Council and U.S. Commerce Department are taking in engaging local entrepreneurs as part of their deliberations.

“Too often, well-meaning foreign policy-makers develop strategies to help Africans without actually engaging us,” he said. “In order to effectively help or support people, we should ask them what kind of help they want. So, I thank you for doing that with African businesses.”

For the U.S. Government, this trip begins the Road to GES 2016 – the Global Entrepreneurship Summit; an annual gathering of entrepreneurs at all stages of business development, designed to demonstrate the U.S. Government’s commitment to fostering entrepreneurship around the world.

Expressly designed to address the needs of and provide opportunities for the next generation of African entrepreneurs, the entrepreneurs in attendance included SMEs supported by UBA Plc, UNCTAD’s EMPRETEC Nigeria Foundation and those selected for the Tony Elumelu Entrepreneurship Programme (TEEP) – a 10-year, $100 million commitment by the Tony Elumelu Foundation to empower the next generation of Africa’s entrepreneurs with businesses that have the potential to generate income and jobs for their nations.

The Tony Elumelu Entrepreneurs in attendance were selected from the Agriculture, Media & Entertainment, ICT, Transport, Healthcare and Financial Services sectors. Their startups reflect the potential that entrepreneurship holds for spurring Africa's transformation; already, they have begun creating jobs in their local communities and generating tax revenues for governments earning them recognition in both local and international media.

WANAMAUZO 4,760 WAPEWA ELIMU YA UJASILIAMALI NA TIGO

Baadhi ya wanamauzo wa kanda ya pwani ya Tigo wakiwa katika picha ya pamoja siku ya mahafali yao ya kuhitimu mafunzo maalum ya ujasiriamali yaliyotolewa na Tigo





Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

jitihada za kuwawezesha wafanyakazi wake wa kujitegemea kumudu changamoto mbalimbali za kikazi na kimaisha, Tigo imewapa wafanyakazi hao wapatao 4,767 mafunzo maalum ya ujasiriamali kupitia mpango wake wa mafunzo kazini.

Mpango wa Tigo wa mafunzo kazini kwa wanamauzo wakujitegemea uitwayo Tigo Sales School (TSS) ulianzishwa mwaka 2012 ambapo kwa mujibu wa Meneja wa TSS Justine Kwizera, kampuni inatarajia kutoa mafunzo hayo kwa wanamauzo wake wote wapatao 10,000 katika kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Alisema kila mwaka Tigo huwekeza kiasi cha 600m/- katika mpango huu ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kampuni hiyo wa kuimarisha utoaji huduma kwa wateja wake. Tigo ina zaidi wateja milioni kumi.

“Mpango wa TSS unalenga katika kuwajengea uwezo wa kiutendaji kazini wanamauzo wa kujitegemea wa Tigo pamoja kuwapa mbinu za kujikimu katika kukabiliana na changamoto mbalimbali maishani,”amesema Kwizera katika mahojiano maalum.

Mafunzo yanayotolewa na TSS ni pamoja na stadi za mauzo, ujasiriamali, usimamizi wa fedha na huduma kwa wateja, alisema Kwizera na kuongeza kwamba mafunzo hudumu kwa muda wa siku nane darasani  na kufuatiwa na mafunzo kwa vitendo kwa miezi mitatu.

“Mafanikio ambayo tumeyashuhudia kutokana na mafunzo haya ni ongezeko kubwa la mauzo na kuimarika kwa huduma kwa wateja sambamba na mabadiliko chanya katika hali ya maisha ya wanamauzo wetu,” alisema meneja huyo wa TSS.

Aidha alisema Tigo inaendeleza kutoa mafunzo kwa wanamauzo katika kila duka na ofisi zake 24 za mauzo  nchi nzima ili kuendeleza watendaji wakezaidi.

SUMAYE AIANGUKIA SERIKALI WANANCHI KUVAMIA SHAMBA LAKE LA EKARI 33 MABWEPANDE JIJINI DAR ES SALAAM

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akisalimiana na Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye  Dar es Salaam leo asubuhi mara baada ya kuwasili eneo la Mabwepande nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam kuangalia eneo la ekari 33 la Sumaye lililovamiwa na wananchi.
 WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye (wa pili kulia), na mke wake mama Esther (kushoto), wakimuonesha Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia) eneo la shamba lake la ekari 33 lililopo Mabwepande Manispaa ya Kinondoni lililovamiwa na wananchi walipotembea eneo hilo Dar es Salaam leo asubuhi.
 Hapa Sumaye na viongozi wengine wakitafakari jambo.
 DC Makonda akihutubia katika mkutano huo. Kulia ni Diwani wa Kata ya Mabwepande, Suzan Masawe.
 Mheshimiwa Sumaye (kushoto), akiongoza kuonesha mpaka wa shamba lake.
 Mhe. Sumaye akielezea uhalali wake wa kumiliki eneo hilo.
 Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mji Mpya,  Justine Chiganga (kulia), akizungumza katika mkutano huo 
 Moja ya kibanda kilichojengwa na wananchi waliovamia eneo la Mhe Sumaye.
 Baadhi ya vibanda vilivyojengwa na wananchi katika eneo la Sumaye.
 Askari Polisi wakiimarisha ulinzi wakati wa mchakato wa kutembelea eneo hilo lililovamiwa.
 Wananchi wa eneo la Mabwepande wakiwa kwenye mkutano huo.
 Mkazi wa eneo hilo Athuman Mnubi akielezea jinsi walivyovamia eneo la Sumaye.
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Mabwepande Abdalla Omari Kunja akizungumza katika mkutano huo.
 Diwani wa Kata ya Mabwepande, Suzan Masawe akizungumza katika mkutano huo.
Ofisa Ardhi Manispaa ya Kinondoni, Matinga Ernest akitoa ufafanuzi kuhusu masuala ya Ardhi katika Manispaa hiyo.

Dotto Mwaibale

WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, ameiangukia serikali na kuomba msaada baada ya wananchi kuchukua sheria mkononi na kuvamia eneo lake la ekari 33 lililopo Mabwepande katika Manispaa ya Kinondoni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.

Serikali imemuahikikishia Sumaye kuwa haina mpango wa kumkandamiza mtu mnyonge wala tajiri hivyo itahakikiha inatoa haki kwa kila mmoja baada ya wiki mbili kwa kua imesikiliza pande zote mbili katika mgogoro huo. 

Akizungumza katika kikao cha pamoja kati ya wananchi wa kitongoji  cha Kimondo mtaa wa mji mpya Kata ya Mabwepande na Sumaye  Dar es Salaam leo asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda alisema ili kumaliza mgogoro huo ambao Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye ameiomba serikali kuingilia kati ni lazima busara kutumika.

Alizitaka pande hizo mbili kuiachia serikali kwa wiki mbili ili kutafuta njia bora ya kumaliza tatizo hilo huku wananchi wakitakiwa kuache kuendelea na ujenzi na kugaiana maeneo katika shamba hilo.

“Serikali ya Rais Magufuli ni sikivu na ndio maana ilikuwa tayari kumsikiliza Waziri Mkuu wetu Mstaafu Sumaye na kusikiliza wananchi ili kutenda haki tunatambua migogoro ya ardhi ilivyokuwa na athari kwa jamii hatuna mpango wa kumkandamiza tajiri wala mnyonge,”alisema.

Alisema katika eneo hilo anajua jinsi wananchi walivyotumia nguvu katika kuwekeza ujenzi na rasilimali zao lakini kwa sasa wasitishe shughuli hizo na kuendelea kugawana maeneo na Sumaye pia kuacha uwekezaji ili kutafuta suluhu.

Zipo njia nyingi tutazitumia kumaliza mgogoro huu ikiwemo kufuata sheria kwa kuangalia iwapo mzee wetu alikiuka taratibu kweli za kumiliki ardhi kama ilivyodaiwa na wananchi hatua gani serikali tuchukue,”alisema.

Alisema pia wanaweza kukaa na Sumaye na kuzungumza naye ili kukubali hasara kwa kutoa eneo kidogo na kuwapatia wananchi  hao ambao hawana makazi au Manispaa kutafuta eneo mbadala na kuwauzia kwa bei nafuu.

Alizitaka pande hizo mbili kutambua umuhimu wa kulinda amani katika mgogoro huo kwa changamoto zilizopo kutatuliwa bila kutumia nguvu.

Makonda pia aliagiza serikali ya kijiji kufanya utambuzi wa wananchi hao wenye makazi katika shamba la Sumaye.

Awali katika mkutano huo Sumaye alimueleza Makonda jinsi serikali ilivyo na kazi ngumu ya kushughulikia migogoro ya ardhi na kuomba kutumia busara zake kumpatia eneo hilo analomiliki kihalali.

“Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya kama nilivyokueleza awali serikali yetu inakazi ngumu sana hasa kutokana na viongozi wa chini kutokuwa wasikivu na wakweli eneo hili namiliki kihalali nina nyaraka zote na ninalipia kila mwaka na nilikuwa katika mpango wa kutafuta wafadhili ili kuliendeleza kwa kujenga Chuo Kikuu,”alisema.

Alisema  yeye na familia yake waliuziwa eneo hilo toka mwaka 1997 na anaamini serikali itatenda haki.

 Diwani wa kata hiyo Suzan Masawe alisema anauthibitisho kuwa eneo hilo lilikuwa pori na Sumaye alilitelekeza kwa muda mrefu na kusababisha uhalifu ikiwemo wanawake kubakwa,mali za wizi kufichwa na uhalifu mbalimbali.

Alisema kutokana na hatua hiyo   walimtafuta Sumaye lakini hakuwa na ushirikiano kwakuwa hata alipofanya uwekezaji kwa kuchimba kisima cha maji alikataa kuwapa wananchi .

Suzan alisema kutokana na hasira za wananchi hao kwa kukosa huduma za kijamii kwa muda mrefu ikiwemo eneo hilo kutokuwa na shule,Zahanati wala kituo cha polisi waliamua kuvamia na kujigaia maeneo. 

Mmoja wa wananchi hao Athuman Mnubi alikiri kweli hawana umiliki halali wa eneo hilo na katika hatua ya kutafuta makazi walivamia msitu huo uliotelekezwa na Sumaye.
Alisema wanaamini kutokana na ahadi ya serikali ya Rais Magufuli katika kupora maeneo yaliyotelekezwa  na wawekezaji watasaidiwa.

WAKATI huo huo Makonda alisimamisha na kukamata baadhi ya malori ya kokoto na mchanga, wafanyakazi na Mwekezaji wa kigeni kutoka India  Sules Waljan wanaochimba mchanga,kokoto na kifusi katika eneo la Mabwepande.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuona uharibifu mkubwa wa mazingira na alipowahoji wafanyakazi na Mwekezaji huyo kama wanavibali walisema hawana.

Makonda amewafikisha watuhumiwa hao kituo cha polisi cha Wazo Hill ili kutoa maelezo ya kina na kusema kuwa serikali inatumia gharama kubwa kwa uhalibifu huo wa mazingira ambao pia unafanywa katika vyanzo vya maji na matengenezo ya madaraja yanayoharibiwa ni makubwa.

Sunday, January 24, 2016

TIGO WAZINDUA UDHAMINI WA MBIO ZA NUSU MARATHON MJINI MOSHI

Meneja Mawasiliano wa Tigo, John Wanyancha akiongea na waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu udhamini wa Tigo katika mbio za Kili NusuMarathon ambapo mbio hizo zitafanyika Februari 28, Wilayani Moshi na zitahusisha wanariadha wa ndani na nje ya nchi kutoka pande mbalimbali za dunia.Uzinduzi huo ulifanyika Kibo Palace Homes.

 Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo, akifafanua jambo   kwa waandishi wa habari kuhusu udhamini wa Tigo kwa mbio za Nusu Marathon mbio hizo zitafanyika Februari 28, Wilayani Moshi na zitahusisha wanariadha wa ndani na nje ya nchi kutoka pande mbalimbali za dunia.Uzinduzi huo ulifanyika Kibo Palace Homes.

Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Novatus Makunga(watatu kushoto, ).akizindua mbio za Kilimanjaro Marathon kwa upande wa Moshi. Wengine ni wadhamini wakuu wa mbio hizo kutoka kushoto, Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini, Henry Kinabo, Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania-Kilimanjaro na Tanga, Richard Temba, Mwenyekiti wa Chama Cha Riadha Mkoa wa Kilimanjaro, Listone Metacha na Meneja Masoko wa Kampuni ya mafuta ya GAPCO, Caroline Kakwezi.Uzinduzi huo ulifanyika Kibo Palace Homes.

Wageni waalikwa ambao  ni wadhamini wa Kili Marathon wakifurahia jambo baada ya Mkuu wa wilaya Mh Novatus Makunga kuzindua mbio za Kili Marathon kwa upande wa Moshi ambapo zitafanyika hizo zitafanyika Februari 28, Wilayani Moshi na zitahusisha wanariadha wa ndani na nje ya nchi kutoka pande mbalimbali za dunia.Uzinduzi huo ulifanyika Kibo Palace Homes.

Mbio za Nusu Marathon 2016 zimezinduliwa jana mjini Moshi, huku ikiwa imebaki mwezi moja kabla za mbio hizo kufanyika.

Meneja Mawasiliano wa Tigo, John Wanyancha akiongea na waandishi wa habari alisema mbio hizo zitafanyika Februari 28, Wilayani Moshi na zitahusisha wanariadha wa ndani na nje ya nchi kutoka pande mbalimbali za dunia.
“Tumeonelea ni vizuri kuzindua mbio hizi rasmi hapa Moshi  ambako zitafanyika ili kuashiria kuwa mambo yamekamilika,” alisema.
“Tigo imeingia mwaka wake wa 2 kama mdhamini wa mbio za kilomita 21.2 hizi. Kwa mujibu wa Meneja huyo, wadhamini wengine wa mashindano hayo ni Kilimanjaro beer 45, Gapco kwa km 10 viti vya magurudumu na baiskeli ya kunyonga kwa mkono na Grand Malt kwa km 5.
Wengine ni KK Security, TPC Limited, FNB, Kibo Palace, Kilimanjaro Water, CMC Automobile, Rwandair na Keys Hotel.
Alisema Tigo imewekeza zaidi ya Sh Millioni 200 katika mashindano hayo na kuwa hapo badaye watatangazo mchanganuo mzima wa zawadi zitakazotolewa.
Alitoa shukrani za pekee kwa mkoa wa Kilimanjaro na chuo kikuu cha Ushirika MOshi (MoCu), zamani kikiitwa MUCCoBS kwa kuwa wenyeji wa mashindano hayo.
Akizindua mbio hizo mjini hapa, Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Novatus Makung, aliwapongeza Kilimanjaro Premium Larger,Tigo wadhamini wengine na wandaaji kwa kujielekeza vyema  kila mwaka, akiongeza kuwa mashindanoyametokea kuwa moja ya matukio makubwa zaidi ya kimichezo ndani na nje ya nchi.
“Mashindano haya pia yamekwenda mbali zaidi katika kukuza utalii, kwani wanariadha wa kimataifa na wageni wao hufanya utalii baada ya mashindano na hiyo kufaidisha uchumi wan chi,” alisema Makunga.
Makunga aliawataka wanariadha wa Tanzania kuhakikisha wanajiandaa vyema ili watwae zawadi nyingi zaidi kwa kadiri zilivyopangwa kwa kila mbio. Aliongeza kwamba wizara yake inaunga mkono kabisa ubunifu kama huo na kuzitaka kampuni nyingine kufuata nyayo hizo kwa kudhamini mashindano hayo kila mwaka.

Aliwapongeza wandaaji, Wild Frontiers, waratibu wa kitaifa Executive Solutions, Chama cha Riadha Tanzania (RT) na wizara yenye dhamana ya michezo kwa kuhakikisha siku zote kwamba tukio hili linafikiwa .
“Mbio hizi zimeleta mwamko mpya katika riadha hapa nchini kwa kuwapa fursa vijana wetu wanaochipukia kuweza kujipima na wanariadha mashuhuri kimataifa. Changamoto hii imekuwa na faida kubwa,ambapo vijana wetu wameweza kutambua uwezo wao na kuweza kujiamini  zaidi wanapokwenda kushiriki mashindano mbalimabli kwenye nchi za kigeni,” alisema.

Meneja wa Tigo Kanda ya Kaskazini Henry Kinabo, alisema kwamba kampuni yake imefurahishwa kupata fursa ya kudhamini mbio za nusu marathoni kwa kilimota 21 kwa mwaka wa pili mfululizo.
“Natoa rai kwa washiriki wajiandae vizuri ili safari hiituweze kunyakua mataji mengi,” alisema Kinabo.

Meneja Masoko wa Gapco Tanzania, Caroline Kakwezi, ambaye kampuni yake inadhamini mbio za kilomita 10 kwa wanaotumia viti vya magurudumu na wale wanaonyonga baiskeli kwa mikono ambazo wanazidhamini, alisema zimekua na mvuto mkubwa na ushindani mkubwa pia na kwamba katika mwaka wao wa tano katika udhamini wameshuhudia mbio hizo zikikua.

“Tunawashukuru wateja wetu wote kwa kuendelea kutuunga mkono, safari hii tutatoa usafiri, malazi na chakura kwa washiriki wote kutoka Dar es Salaam katika mbio hizi za walemavu na yote haya hayawezekani bila ushirikiano tunaoupata kutoka kwa wateja wetu”alisema.


RIPOTI YA TATHMINI YA MAZINGIRA YA KISHERIA KATIKA MWITIKIO WA UKIMWI KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA ZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

 Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar (ZAC), Dk.Ali Ali (katikati), Kaimu Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Jumanne Issango (kushoto) na Naibu Mkurugenzi Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo (UNDP), Titus Osundina wakikata utepe kwa pamoja kuashiria uzinduzi wa ripoti ya tahmini ya mazingira ya kisheria katika mwitikio wa ukimwi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uliofanyika Makao Makuu ya Tacaids Dar es Salaam leo asubuhi.
 Viongozi hao wakiwaonesha wageni waalikwa na wadau mbalimbali ripoti hiyo. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Sheria wa Tacaids, Elizabeth Kaganda na kilia ni Dk.Bwijo Bwijo kutoka UNDP.
 Naibu Mkurugenzi Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo (UNDP), Titus Osundina, akihutubia wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo.
  Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Ukimwi Zanzibar (ZAC), Dk.Ali Ali (kushoto), Kaimu Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Jumanne Issango (katikati) wakimpongeza Naibu Mkurugenzi Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo (UNDP), Titus Osundina baada ya kuhutubia.
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Wanahabari wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Uzinduzi ukiendelea.
Wadau wakiwa katika uzinduzi huo.
Picha ya pamoja na viongozi.
Wasanii wa Hisia Threatel Group kutoka Sandali Temeke jijini Dar es Salaam wakionesha igizo linalohusu ukimwi katika uzinduzi huo.

(Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062) 

WAZIRI UMMY MWALIMU ATEMBELEA MNADA WA NYAMA CHOMA DODOMA

IMG-20160123-WA0051
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na wafanyabiashara wa eneo la Msalato lililopo mkoani Dodoma sehemu ambayo inatumika kufanyia mnada wa nyama choma ikiwa ni moja ya ziara zake kufatilia hali ya ugonjwa wa kipindupindu katika maeneo mbalimbali ya nchi, akiwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Jasmine Tiisekwa (mwenye skafu shingoni) pamoja na Afisa Afya Mkuu wa Manispaa ya Dodoma Bw. Alek Barakena (mwenye suti nyeusi).
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu ametembelea eneo la Msalato lililopo mkoani Dodoma sehemu ambayo inatumika kufanyia mnada wa nyama choma ikiwa ni moja ya ziara zake kufatilia hali ya ugonjwa wa kipindupindu katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Baada ya kutembelea mnada huo, Mhe. Ummy aliwataka wananchi wa eneo hilo kutambua kuwa bado ugonjwa wa kipindupindu upo na unaendelea kusambaa maeneo mbalimbali ya nchi hivyo ni wajibu wao kama wananchi kuweka mazingira yao katika hali ya usafi ili kutokomeza uonjwa huo.
Aidha ili kuzidi kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa kipindupindu, Waziri Ummy ameagiza kuendelea kutekelezwa kwa agizo la Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Jasmine Tiisekwa ambaye aliagiza kusimamishwa kwa shughuli za kuuza nyama nyoma katika eneo hilo la Msalato mpaka uongozi wa wilaya hiyo utakapojiridhisha kuwa ugonjwa wa kipindupindu umetoweka mkoani Dodoma.
“Kipindupindu kimesambaa sehemu nyingi nchini ikiwepo hapa Dodoma na hivyo naagiza katazo la Mkuu wa Wilaya, Dkt Jasmine Tiisekwa liendelee kuwepo hadi ugonjwa wa kipindupindu uishe Dodoma na niwajibu wa kila mwananchi kuhakikisha kipindupindu kinakwisha,” alisema Waziri Mhe. Ummy.
Pamoja na hayo pia Waziri huyo wa Afya ameutaka uongozi wa Manispaa ya Dodoma kufanya kikao cha pamoja na wafanyabiashara hao wa nyama choma ili kuona ni jinsi gani wanaweza kuendelea na biashara zao huku wakizingatia kanuni za usafi wa afya na mazingira bila kusababisha kuzidi kusambaa kwa kipindupindu.
IMG-20160123-WA0050
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akifafanua jambo kwa wafanyabiashara wa eneo hilo.
IMG-20160123-WA0045
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akitoa maagizo ya wafanyabiashara hao kusitisha shughuli zao mara moja katika eneo hilo la Msalato mpaka uongozi wa wilaya hiyo utakapojiridhisha kuwa ugonjwa wa kipindupindu umetoweka mkoani Dodoma.
IMG-20160123-WA0043
IMG-20160123-WA0044

Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (wa pili kushoto), Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Jasmine Tiisekwa (wa tatu kulia) na Afisa Afya Mkuu wa Manispaa ya Dodoma Bw. Alek Barakena (kushoto) wakisikiliza hoja kutoka kwa mmoja wa wafanyabiashara wa eneo hilo (hayupo pichani).
IMG-20160123-WA0046
Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akisikiliza hoja kutoka kwa mmoja wa wafanyabiashara wa eneo la Msalato lililopo mkoani Dodoma sehemu ambayo inatumika kufanyia mnada wa nyama choma ambaye jina lake halikupatikana alipofanya ziara ya katika eneo hilo.

Thursday, January 14, 2016

MWANDISHI WA HABARI WA ITV SPENSOR LAMECK ALAMBA NONDO CHUO CHA DIPLOMASIA

1
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Augustine Mahiga akihutubia jana wakati wa mahafali ya Chuo cha Diplomasia yaliyofanyika jana chuoni hapo Kurasini jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na wahitimu wa shahada mbalimbali, Wahadhiri na wageni waalikwa ambapo mmoja wa Mwanahabari kutoka kituo cha Televisheni cha ITV Bw. Spensor Lameck alikuwa ni mmoja wa wahitimu.
2
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Augustine Mahiga akiwa katika jukwaa kuu na viongozi mbalimbaliwa chuo hicho pamoja na wahadhiri wakati wa mahafali hayo.
6
Mwanahabari kutoka kituo cha Televisheni cha ITV Bw. Spensor Lameck akipata picha ya pamoja na wahitimu wenzake wakati wa mahafali hayo.
7
8
Mwigizaji wa filamu Christina Manongi maarufu kama Sinta kulia akiwa na mhitimu mwenzake wakati wa mahafali hayo.
9
10
Mwanahabari kutoka kituo cha Televisheni cha ITV Bw. Spensor Lameck akipata picha ya pamoja na Christina Manongi maarufu kama Sinta kulia na mhitimu mwenzao.

WATEJA WA TIGO PESA WAANZA KUVUNA GAWIO LA ROBO MWAKA

Mkuu wa Fedha na Tahadhari wa Huduma ya Fedha kwa njia ya mtandao wa Kampuni ya simu ya Tigo, Obedi Laiser (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu gawio la mwaka huu  kwa watumiaji wa Tigo Pesa ambalo watumiaji hao wameanza kulipata kuanzia jana. Kulia ni Meneja wa Mawasiliano wa Tigo, John Wanyancha.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Meneja wa Mawasiliano wa Tigo, John Wanyancha (kulia), akizungumza katika mkutano huo.


Na Dotto Mwaibale

Kampuni inayongoza katika kuleta maisha ya kidijitali kwa jamii, Tigo, imetangaza tena malipo ya robo mwaka ya shilingi bilioni 4.4 (dola milioni 2.1) kwa watumiaji wake wa huduma ya Tigo Pesa wapatao milioni 4.6. 

“Gawio hili la faida linalipwa kwa watumiaji wote wa Tigo Pesa wakiwemo wateja binafsi, mawakala wa rejareja na washirika wetu wa kibiashara, kila mmoja kutokana na thamani  ya fedha aliyojiwekea katika akaunti yake ya Tigo Pesa,” alisema Mkuu wa Fedha na Tahadhari wa Huduma ya Fedha kwa njia ya mtandao, Obedi Laiser.

 Akizungumza katika mkutano wa waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Laiser alisema  kuwa hii itakuwa ni mara ya kwanza Tigo kuwalipa gawio la faida watumiaji wa Tigo Pesa kwa mwaka wa 2016  akibainisha kuwa malipo hayo ni faida inayopatikana kutokana na amana ya mfuko wa Tigo Pesa uliyowekezwa katika benki za kibiashara hapa nchini. 

“Tunayo furaha kubwa kutangaza gawio hili la faida kwa mara ya saba mfululizo tangu tulivyoanza kufanya hivi mwaka 2014. Bila shaka hii inaonyesha ni jinsi gani Tigo inajizatiti kuwaletea watanzania maisha bora ya malipo kwa njia ya mtandao,” amesema Laiser.

Tigo ilikuwa kampuni ya kwanza duniani kutoa gawio kwa wateja wake mwaka 2014 

“Tunaamini gawio hili la kwanza la faida ya Tigo Pesa kwa mwaka 2016 litakuwa ni kivutio kikubwa kwa mamilioni ya watumiaji wa Tigo Pesa katika kufanikisha mahitaji  yao mbalimbali ya kifedha ya mwanzo wa mwaka,” amesema Laiser.

Malipo haya kwa watumiaji wa Tigo Pesa hutolewa kwa mujibu wa mwongozo wa Benki Kuu uliotolewa mnamo Februari mwaka 2014. Mpaka sasa Tigo imelipa jumla ya bilioni 35.5 kwa wateja wake tangu kuanzishwa kwa utaratibu huu mwaka juzi na kampuni hiyo. 


Wednesday, January 13, 2016

TIGO YASHEHEREKEA SIKU YA MAPINDUZI NA WATEJA ZANZIBAR



Mkazi wa Malindi Salim Salim akipokea zawadi ya Tisheti kutoka kwa mfanyakazi wa duka la Tigo Zanzibar Moses Kalyata wakati wa siku ya maadhimisho ya mapinduzi ya visiwani humoHE
Mkazi wa Bumbwini Ally Said akikabidhiwa zawadi ya Kofia na  Magnus Saulo  mmoja wa wafanyakazi wa duka la Tigo Zanzibar ikiwa ni moja ya shughuli zilizofanyika katika sherehe za mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika jana nchini humo 
Mkazi wa Bububu Rashid Salehe  Akipokea zawadi ya kofia kutoka kwa  mfanyakazi wa duka la Tigo Zanzibar  Magnus Saulo kama moja ya shughuli zilizofanyika jana wakati wa maadhimisho ya mapinduzi ya Zanzibar 
Mkazi wa Malindi akipokea zawadi ya Tisheti kwa mmoja wa wafanyakazi wa duka la Tigo Zanzibar  Moses Kalyata katika moja zilizofanyika katika maadhimisho ya siku ya mapinduzi jana visiwani humo
Vinywaji na chakula vikiwa vimeandaliwa tayari kwa ajili ya wateja wote waliotembelea duka la tigo linalopatikana Mtaa wa Malindi Zanzibar katika maadhimisho ya siku ya Mapinduzi visiwani humo