Pages

KAPIPI TV

Friday, November 27, 2015

WANAHARAKATI WA TANZANIA WANATOA WITO KWA JAMII KUCHUKUA HATUA ILI KUMLINDA MTOTO APATE ELIMU BORA NA SALAMA

  Eda Malick kutoka Tanzania Women and Children Welfare center akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia
 Afande Christina Onyango, Afisa wa Polisi, mkoa wa kipolisi Ilala akielezea namna ambavyo dawati la jinsia wamejipanga kufikisha ujumbe wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
  Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini Tanzania wakihudhuria mkutano na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.
 Bahati Mandago kutoka shirika la Tanzania Human Rights fountain akielezea mikakati ya shirika lake katika kufikisha ujumbe wa Funguka. Chukua Hatua Mlinde Mtoto apate elimu.

Wadau kutoka katika mashirika mbalimbali wanaoshiriki kikamilifu katika utekelezaji wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari
 Dr. Judith Odunga Mkurugenzi wa Shirika la WiLDAF akisoma taarifa kwa vyombo vya habari kuhusiana na kuanza kwa siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

FUNGUKA! CHUKUA HATUA MLINDE MTOTO APATE ELIMU

Katika kuadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia kuanzia tarehe 25 Novemba mpaka 10 Desemba, WiLDAF, Mashirika ya Haki za Binadamu, Wadau wa Maendeleo na Asasi za Kiraia watatoa elimu na kuhamasisha umma kuchukua hatua kumlinda mtoto ili apate elimu bora na salama. Ulinzi wa mtoto ni pamoja na kuzuia vitendo vyote  vya ukatili wa kijinsia.

Maadhismisho ya SIku 16 za kupinga Ukatili wa kijinsia mwaka huu yanalenga zaidi kuzungumzia suala zima la usalama  mashuleni, lengo kuu ikiwa kuhamasisha umma kuhusu ukubwa wa tatizo la ukatili wa kijinsia kwa vijana na watoto wetu mashuleni, kwani vitendo vingi vya ukatili wa kijinsa vimekuwa vikiripotiwa.

Utafiti uliyofanywa na Chuo cha Tiba Cha Muhimbili (MUHAS) kwa kushirikiana na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika, (WiLDAF) umetambua hatari zinazochangia ukatili wa kijinsia ikiwa ni pamoja na wazazi kutowajali watoto na kutoa adhabu kali kwao na hivyo kuwafanya watoto kuwa na hofu. Wakati mwingine watoto kufanyiwa ukatili bila wao kufahamu. Aidha, adhabu ya viboko inahusishwa kama moja ya aina za ukatili dhidi ya watoto. Hii inaathiri maendeleo ya elimu ya watoto katika taifa letu.

Kukosekana kwa usawa kati ya watoto wa kiume na wa kike hunapelekea kuwajengea hofu watoto wa kike,  na wakati huo kuwajengea watoto wa kiume ujasiri wa kuona kuwa ni sahihi kwao kufanya  vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Aidha, tafiti kuhusu Ukatili Dhidi ya Watoto (VAC) uliofanywa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto (UNICEF) wa mwaka 2011 ulionesha kwamba watoto 3 wa kike kati ya 10 na mtoto 1 kati ya watoto 7 wa kiume wenye umri kati ya miaka 13-24 wamewahi kufanyiwa ukatili wa kingono. Aidha, asilimia 6 ya watoto wa kike wamelazimishwa kufanya tendo la ngono kabla ya miaka 18. Pia utafiti huo unaonesha kuwa watoto wa kike wanafanyiwa vitendo vya kingono  na wanaume waliowazidi umri wakati watoto wa kiume wanafanyiwa ukatili na watoto wenye umri sawa.

Tafiti pia imeonesha kuwa vitendo hivyo vinafanywa na watu wanaowafahamu wakiwemo majirani, wapenzi wao, watu wenye mamlaka (walimu). Ni  asilimia 32.2 tu ya watoto wa kike na asilimia 16.6 ya watoto wa kiume wamefanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia na watu wasiofahamika na watoto. Vitendo hivi hufanyika maeneo ambayo uangalizi wa watu wazima unahitajika kuwepo kwa mfano mashuleni, njiani, majumbani na wakati mwingine katika vyombo vya usafiri.

Ni dhahiri kwamba kwa mazingira, mila na utamaduni ikijumuisha familia za Kitanzania, vimekuwa vikichangia vitendo vya ukatili wa kijinsia. Vitendo vya ukatili na udhalilishaji vina madhara makubwa ya kiafya kwa watoto kwani hukatisha uwezo wao wa kielimu, mahudhurio ya shule na hivyo kupelekea matokeo mabaya ya  katika ufaulu wao wakati wa mitihani.

Aidha, mazingira yasiyo salama kwa watoto wa shule yana madhara makubwa. Watoto wanapokuwa mashuleni na kufanyiwa ukatili wa kingono wapo katika hatari kubwa zaidi ya kupata maambukizi ya UKIMWI kwa mathlani mara tatu zaidi ya wale ambao hawajawahi kufanyiwa ukatili.

Tunaamini kwamba kuondolewa kwa vikwazo vinavyo chochea ukatili wa kijinsia kwa watoto wa shule kutachangia katika kuleta usawa wa kijinsia kwa watoto wa kiume na wa kike. Pia mazingira mazuri ya shule yatasaidia mahudhurio mazuri ya watoto mashuleni na  kuleta matokeo mazuri katika ufaulu.

Jamii inahaswa kuweka mazingira mazuri ya shule ikiwa ni pamoja na kuwepo miundombinu kama mabweni, vyoo, madawati, uzio kuzunguka mashule na vyombo rafiki vya usafiri. Haya yote yatawezekana tu ikiwa kutakuwa na dhamira ya dhati kwa watunga sera, wazazi, walimu, wanafunzi na jamii kwa ujumla katika kuzuia ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto. Kuna haja ya makusudi kabisakutofumbia macho  masuala ya ukatili kwa ujumla wake ili kujenga jamii imara.

Siku 16 za Kupinga ukatili wa kijinsia  ni tukio la kimataifa la kila mwaka ili kuwa na nguvu ya pamoja  katika kuzuia kuenea kwa janga hili . Ndani ya siku hizi, kuna siku zingine muhimu za kimataifa , mathlani, Novemba 25 ni Siku ya Kimataifa ya Kupinga Ukatili Dhidi ya Wanawake, Novemba 29 ni Siku ya Kimataifa ya Watetezi wa Haki za Binadamu, Desemba 1 ni Siku ya UKIMWI Duniani, Desemba 3 ni Siku ya Kimataifa ya watu wenye Ulemavu, Desemba 6 ni Siku ya Kimataifa ya Kumbukumbu ya Mauaji ya kikatili ya Montreal 1989, ambapo wanawake 14 waliuawa na mtu aliyekuwa anawachukia wanawake. Tarehe hizi zilichaguliwa mahususi ili kuhusianisha kwamba ukatili wa kijinsia unaongeza maambukizi ya UKIMWI na ni Ukiukwaji wa Haki za Binadamu.

Katika kipindi hiki cha Kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia , mamia ya asasi za kiraia na wadau mbalimbali Tanzania wataifikia jamii kwa kauli mbiu inayosema;
FUNGUKA! CHUKUA HATUA MLINDE MTOTO APATE ELIMU.

Kauli hii inalenga kumshawishi mtu binafsi, kuwashawishi walimu, wanafunzi, wazazi na jamii kwa ujumla, kuwalinda watoto dhidi ya  ukatili wa kijinsia na kuhakikisha kwamba shule ni mahala salama. Ni vema kutafakari kwa kina jinsi vitendo vya ukatili wa kijinsia mashuleni vinavyoathiri maendeleo ya watoto wetu kielimu. Hivyo na haja ya kuwa na taifa linalopiga vita vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia. Taifa linalofumbia macho ukatili wa kijinsia  haliwezi kupiga hatua kimaendeleo.

Kampeni ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa kijinsia ina lengo la kushawishi watunga sera, wadau na jamii kwa ujumla, kuchukua hatua dhidi ya ukatili wa kijinsia . Pia ina taka jamii kufichua vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia ili kuwa  na jamii isiyovumilia ukatili wa aina yoyote.

Hivyo basi WiLDAF na wadau mbalimbali wanaopinga vitendo vya ukatili wa kijinsia wanaitaka serikali kufanya yafuatayo;
1)    Kufutwa kwa adhabu ya viboko mashuleni na walimu kutafuta mbinu za kutoa adhabu mbadala.
2)    Kutengeneza muongozo wa utekelezaji wa sera  ya elimu ya mwaka 2014 utakaolekeza upatikanaji wa elimu ya msingi iliyo bora na salama.
3)    Kuboresha miundo mbinu rafiki kwa watoto wa shule ikiwa ni pamoja na  kuwepo kwa vyoo bora, mabweni, madawati, usafiri, uzio kuzunguka shule na mengineyo kwa ustawi wa watoto wa shule.
4)    Kuunda mabaraza yatakayokuwa yanasimamia malalamiko ya wanafunzi mashuleni.
5)    Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Wizara ya sheria na Katiba zitunge sheria ya kudhibiti Ukatili Majumbani na kubadilisha Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971inayoruhusu mtoto wa kike chini ya miaka 18 kuolewa, ama kwa ridhaa ya wazazi, mlezi au Mahakama.

Katika kipindi hiki cha siku 16, za kupinga ukatili wa kijinsia kutakuwa na shughuli mbalimbali na midahalo ili kuleta mabadiliko katika nchi yetu. Tunatoa wito kwa jamii kwa ujumla kupaza sauti na kukemea vitendo vyote vya ukatili wa kijinsia. Jamii ihamasishe usawa wa kijinsia, mahusiano yasiyo na ukatili na  isibague au kunyanyapaa waathirika wa ukatili wa kijinsia. Tusikae kimya bali tufichue ukatili wa kijinsia na kuchukua hatua kuwalinda watoto wetu iliwapate elimu bora na iliyo salama. Kwa pamoja kupitia kauli mbiu ya mwaka tunasisitiza;
FUNGUKA!  CHUKUA HATUA MLINDE MTOTO APATE ELIMU.

Imefadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Watu wa Marekani (USAID Tanzania)
Imetolewa na;
Dkt. Judith N. Odunga (MKURUGENZI)
Kwa niaba ya:
Shirika la Wanawake Katika Sheria na Maendeleo Barani Afrika (WiLDAF)
S.L.P 76215
DAR ES SALAAM    
 

KIPINDI CHA JUKWAA LANGU NOVEMBA 23,2015

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk John Magufuli akizindua Bunge la 11
Kipindi hiki hukujia kila jumatatu kuanzia saa 11 jioni kwa saa za Marekani ya Mashariki kuijadili Tanzania ya sasa na ile tuitakayo
Katika kipindi hiki tumejadili (mbali na mambo mengine) muelekeo wa serikali ya Tanzania baada ya kuzinduliwa kwa Bunge la 11.
Mjadala huu ambao ulifuata HABARI kutoka magazeti mbalimbali, umehusisha wadau toka Marekani, Canda na India
Karibu
Waweza kutusikiliza kupitia tovuti zetu www.kwanzaproduction.com na www.vijimamboradio.com

UNDP YAKABIDHI MRADI WA DOLA ZA MAREKANI 150,000 WA KUKABILIANA NA MABADILIKO LA TABIANCHI KIJIJI CHA CHAMWINO

IMG_9773
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo akikata utepe kuzindua Kisima cha maji safi na salama katika kijiji cha Machali A wilayani Chamwino mkoa wa Dodoma mwishoni mwa juma lililopita.
Na Modewjiblog team, Chamwino
KIJIJI cha Manchali kilichopo wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, kimekabidhiwa mradi wa dola za Marekani 150,000 wenye lengo la kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Mradi huo ulikabidhiwa kijiji hicho na Mratibu wa mashirika ya Umoja wa mataifa nchini na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bw. Alvaro Rodriguez.
Mradi huo umelenga kusaidia jamii inayoishi katika kijiji hicho kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Mradi huo wa nishati ya jua umelenga kutatrua tatizo la nishati na kufanya matumizi bora ya ardhi na teknolojia ya maji.Mradi huo unasaidia familia 600.
Kwa uzoefu wa Tanzania na maeneo mengine duniani, familia maskini ndizo zinazopigika vibaya na mabadiliko hayo na ndio haizna uwezo wa kukabiliana nayo.
Kwa mradi huo wananchi wa Manchali wanatarajia kukabiliana vilivyo na mabadiliko ya Tabia nchi.
Akizungumza katika kijiji hicho cha Manchali, Mkurugenzi Mkazi wa UNDP, Bi. Awa Dabo alisema kwamba ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi uwezeshaji wananchi kiuchumi ni muhimu sana ili kufanya familia kustawi.
IMG_9772
Kisima kilichozinduliwa na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo.
“Athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa watu maskini ni kubwa na ndio wanaoathirika zaidi” alisema Mkurugenzi Mkazi UNDP Bi. Dabo.
Aidha alisema kwamba anaishukuru serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuhangaikia suluhu ya watu kukubali kuwapo kwa mabadiliko ya tabia nchi na kufanya juhudi ya kukabili hali hiyo.
“Hii imo katika malengo ya maendeleo endelevu kwani malengo manne kati ya 17 yanahusiana na mabadiliko ya tabia nchi na kuhifadhi mazingira.kwa kutumia fedha kutoka kwa wadau wa maendeleo, UNDP imefanikiwa kusaidia wananchi wa kijiji cha Manchali kufanyia kazi maeneo kadha muhimu ili kufanya uragibishi kuhusu mabadiliko ya tabia nchi, kuongeza kasi ya upoandaji wa miti na matumizi ya nishati jadidifu.” alisema.
Bi Dabo amesema kwamba mradi huo wa Manchali umekamilika ni mmoja wa mradi yenye mafanikio inayosimamiwa na UNDP.
Aliwapongeza wananchi wa Manchali kwa ushiriki wao na kuufanya mradi huo kuwa wakwao hali iliyosababisha kuwepo na matunda yenye tija katika kijiji hicho.
“Sisi UNDP kutokana na mafanikio haya tunaangalia maeneo mengine ya kufanya mradi kama huu” alisema Bi Dabo.
UZINDUZI-MRADI
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja waMataifa la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akizindua mradi wa kupunguza na kukabiliana na mabadiliko ya Tabianchi kwa kutumia nishati jadidifu ya jua (Mitigating Climate change in vulnerable communities of Dodoma region, Machali village, Chamwino District), kijijini humo.
Naye Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Bw. Alvaro Rodriguez alisisitiza ushiriki wa wananchi katika kufaniukisha miradi na kusema kwamba mradi huo umefanikiwa kutoka na ushiriki wa wananchi na hasa kitendo chao cha kuufanya mradi huo kuwa mali yao.
Aliongeza kwamba kitendo cha kufanya mradi wao na kuwa viongozi wa maendeleo yao wao wenyewe kumefanya mradi uwe na tija kubwa kwao.
“Mradi huu umeleta maendeleo makubwa kwa wananchi wa hapa kutokana na wao kuanza kutumia nishati jadidifu, watoto wanakwenda shule na maeneo yameanza kurejewa na misitu.”
Mratibu huyo aliongeza kwamba mabadiliko ya tabia nchi ni ya kweli na wala si ya kuyafanyia mzaha, mashirika ya umoja wa mataifa na Umoja wenyewe wanatazama sana athari zake mbaya.
Alisema kijiji cha Manchali kimefanikiwa katika kuanza kukabili mabadiliko ya tabianchi kwa kubadili mambo yanayowazunguka na kurejesha uoto wa asili na kuacha kuharibu mazingira huku shughuli za maendeleo zikichukua sura mpya yenye kujali mabadiliko ya tabia nchi.
IMG_9802
Bango la mradi uliozinduliwa na Bw. Alvaro Rodriguez.
IMG_9786
Kutoka kushoto ni Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja waMataifa la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na viongozi wa kijiji wakiwakilisha wananchi ambao watanufaika na mradi huo.
IMG_9842
Kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo, Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Umoja waMataifa la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum katika picha ya pamoja.

BENKI YA STANDARD CHARTERED YATEUA MKURUGENZI WA KWANZA MTANZANIA

Sanjay - 3
Sanjay Rughani (pichani) anakuwa Mtanzania wa kwanza kuiongoza benki ya Standard Chartered Tanzania akipokea uongozi wa benki hiyo kutoka kwa aliyekuwa mkurugenzi wake, Liz Lloyd, ambaye amerudi katika makao makuu ya benki hiyo, London, kuchukua nafasi ya Mshauri wa Kisheria wa benki hiyo.
Sanjay alijiunga na benki ya Standard Chartered Tanzania mwaka wa 1999 akiwa kama Meneja msaidizi wa kitengo cha Fedha. Baada ya miaka miwili Sanjay alipata cheo cha Meneja wa kitengo cha Fedha kwa Bara la Afrika, kazi ambayo aliifanya akiwa katika makao makuu ya benki hiyo, London. Alirudi nyumbani Tanzania mwaka wa 2002 na kupata cheo cha Mkuu wa Kitengo cha Fedha nchini Tanzania, kazi ambayo aliifanya hadi mwaka wa 2006.
Mwaka wa 2007, Sanjay alipata tena cheo kingine, wakati huu akihamishiwa Ghana, ambapo aliongoza Kitengo cha Fedha nchini humo huku pia akisimamia Afrika Magharibi, yaani Gambia, Cote d' Ivoire na Sierra Leone, kazi ambayo aliifanya hadi Mei, 2013.
Juni, 2013 Sanjay alipandishwa tena cheo na kuwa Mkuu wa Operesheni za Kifedha na Mratibu wa Huduma za Kifedha kwa Bara la Afrika akiongoza kitengo hicho ambacho ni sehemu ya Kitengo Kikuu cha Fedha katika nchi kumi na tano za Afrika, akilenga kuboresha huduma za kifedha za benki hiyo zilingane na huduma zake za kimataifa katika nchi zilizoendelea. Sanjay alifanya kazi hii hadi alipoteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Benki hiyo hapa Tanzania hapo mwanzoni wa mwezi huu wa kumi na moja.
Lamin Manjang, Mkurugenzi wa benki ya Standard Chartered Kenya na Afrika Mashariki, amesema, “Nafurahi kumkaribisha tena Sanjay nyumbani Tanzania na kwenye timu yangu ya Afrika Mashariki kufutatia umahiri wake katika kazi mbalimbali ambazo amezifanya katika benki yetu. Pia nafurahi kuwa sasa benki yetu nchini Tanzania ina Mkurugenzi wake wa kwanza wa Kitanzania. Hii inaonyesha ubora wa wafanyakazi wetu nchini Tanzania. Tunaendelea kuweka kipaumbele kwa kuwapa wafanyakazi wetu bora nyadhifa mbalimbali za uongozi barani Afrika ili kuweza kuboresha maendeleo katika nchi mbalimbali ambapo tunafanya shughuli zetu za kibenki.”
Tanzania inaendelea kupewa kipaumbele katika mipango ya benki hiyo katika bara la Afrika na Afrika Mashariki haswa kutokana na ukuaji wake wa kiuchumi na kuweko katika ‘Klabu ya 7%’, ambayo ni listi ya nchi ambazo uchumi wake unakadiriwa kuendelea kukua kwa kasi zaidi katika miaka kumi ijayo.
Kufuatia kuteuliwa kwake Mkurugenzi huyo mpya wa benki ya Standard Chartered Tanzania, Sanjay Rughani alisema, “Tanzania ina fursa nyingi sana za kibiashara na ninafurahi kurudi nyumbani kuiongoza benki ya Standard Chartered kwenda kwenye hatua nyingine ya kimaendeleo. Nchi yetu inaendelea kuchangia mafanikio ya Umoja wa Afrika Mashariki kwa njia mbalimbali ikiwemo ukuaji mzuri wa uchumi. Pia ugunduzi wa hifadhi za gesi nchini Tanzania unatarajiwa kuleta maendeleo zaidi ya kiuchuni hapa nchini kwetu.”
Sanjay ana shahada ya udhamili ya Kifedha na Rasilimali watu, na shahada ya Uchumi. Pia ni mwanachama wa Chama cha Wahasibu, ACCA. Sanjay pia ni Mjumbe wa Bodi wa benki ya Standard Chartered Uganda. Ameoa na ana watoto wawili.

MGOGORO WA ZANZIBAR WATUA IKULU YA MAREKANI

Na Mwandishi wetu Washington 
Wakati vikao vya siri vya kutafuta suluhu ya mzozo wa kisiasa visiwani Zanzibar vikiwa vimeripotiwa, juhudi za kuupatia ufumbuzi mzozo huo zimehamia kutoka Ikulu ya Zanzibar na kufika Ikulu ya Marekani (White House).
Wanachama wa ZADIA kutoka majimbo tafauti Nchini Marekani wakionyesha mabango yao 
Mnamo tarehe 21 mwezi huu, Wazanzibari waishio nchini Marekani waliandamana hadi kwenye Ikulu ya nchi hiyo katika juhudi za kutafuta uingiliaji kati wa kimataifa ili kuupatia suluhisho mzozo huo.

Akizungumza na waandishi wa habari mbele ya Ikulu hiyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazanzibari Waishio nchni Marekani (ZADIA) iliyoandaa maandamano hayo Bwana Omar Haji Ali, alisema kuwa maandamano hayo yanakuja katika juhudi za Jumuiya hiyo za kutafuta uingiliaji kati wa kimataifa katika kuukwamua mgando wa kisisas visiwani Zanzibar.

Aliendelea kusema kwamba maandamno hayo pia yana lengo la kumkumbusha rais Barack Obama wa Marekani kutekeleza ahadi yake ya kuilinda demokrasia Barani Afrika.

"Katika hotuba yake aliyoitoa kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Afrika mapema mwaka huu, rais Obama alisema '.. pale ambapo raia hawawezi kutekeleza haki zao, basi ulimwengu una jukumu la kukemea. Na Marekani itafanya hivyo, hata kama wakati mwengine itakuwa inauma'..", alikumbusha Bwana Ali.

Aliongeza kuwa "Wananchi wa Zanzibar wameshindwa kutekeleza haki yao kwa zaidi ya nusu karne sasa. Wakati umefika sasa kwa ulimwengu kuchukua jukumu lake. Wakati umefika sasa kwa Marekani siyo tu kukemea, lakini pia kuchukua hatua za kivitendo ili kuhakikisha kuwa sauti za Wazanzibari zinasikilizwa na kuheshimiwa"

Alipoulizwa ni hatua gani watakazochukuwa iwapo Serikali ya Marekani haikuchukua hatua yoyote kusaidia kumaliza mgando wa kisiasa Zanzibar, Bwana Ali alisema "Tuna imani na rais Obama, na tumemfikishia barua ya malalamiko yetu, na tunasubiri jibu lake, na imani yetu ni kuwa atachukua hatua madhubuti khususan ikizingatiwa kuwa Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ulikuwa wa mwanzo kutoa taarifa kuelezea kuwa uchaguzi wa Zanzibar ulikuwa wa haki na huru" 

Alidokeza kuwa, iwapo hali itaendelea kubakia kama ilivyo, basi ZADIA itaelekea kwnye Umoja wa Mataifa.

UNIDO YAPIGA JEKI VIWANDA VIDOGO VYA MAFUTA YA ALIZETI DODOMA

IMG_2196
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga akitoa maelezo jinsi kiwanda hicho kinavyofanya kazi zake kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kushoto) aliyeambatana na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (kushoto), Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum (kulia) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto kukagua miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa mjini Dodoma. (Picha na Modewjiblog).
Na Mwandishi wetu
Kutoratibiwa kwa mbegu za alizeti na ukosefu wa mitaji umeelezwa kuwa changamoto kubwa kwa wasindikaji wadogo wa mafuta ya mbegu ya alizeti katika kuendesha viwanda vyao kwa gharama nafuu.
Hayo yameelezwa na Wakala wa uendelezaji Kongano la Mafuta ya Alizeti wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo la Viwanda (UNIDO) Vedastus Timothy wakati akizungumza na waandishi wa habari walioambatana na Mratibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez.
Mratibu huyo alikuwa Dodoma kwa shughuli mbalimbali za ukaguzi wa miradi pamoja na kuhudhuria shughuli za bunge la Tanzania lililomalizika jana.
Timothy alisema kwamba pamoja kuwepo kwa taarifa za kuwepo kwa mbegu za kutosha nchini Tanzania,hali halisi inayoelezwa na wasindikaji inaashiria kwamba sekta hairatibiwi vyema kwani wasindikaji hukaa muda mrefu bila kuwa na mbegu za kusindika.
Aidha alisema kwamba mbegu za alizeti zinazovunwa kuanzia Aprili hadi Julai na huwa na bei nafuu kipindi hicho lakini kama wasindikaji wakikosa mitaji na kununua mbegu chache, msimu unapoisha hawawezi tena kuendelea kufungua viwanda vyao.
Alisema kwamba wasindikaji hao wanakumbana na kiwango kikubwa cha riba kuanzia asilimia 20 kwenda juu , riba ambayo inakwamisha maendeleo ya viwanda hivyo.
IMG_2202
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga (kulia), Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto), Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (wa pili kushoto), Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum (katikati) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto (wa pili kulia) wakipata picha ya ukumbusho katika matanki ya kuhifadhia mafuta ya alizeti kiwandani hapo.
Hata hivyo alipoulizwa wanafanya nini katika kusaidia wasindikaji hao kukabiliana na hali hiyo alisema kwamba kupitia kongano hilo na Shirikisho la wasindikaji wadogo wa alizeti kanda ya mashariki na kati (CEZOSOPA). wana mipango ya kuwezesha wasindikaji hao kuwa na nguvu katika soko na kuwa na uwezo wa kupata mitaji bila gharama kubwa.
Aidha kupitia kongano hilo chama hicho kitawezeshwa uboreshwaji wa viwanda vya wanachama wake ili viweze kushindana na kukidhi viwango vya Shirika la Viwango nchini Tanzania (TBS).
Wakala huyo alisema hayo katika mahojiano yaliyofanyika kufuatia ziara ya mradi wa Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa, Alvaro Rodriguez kwenye kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products kilichopo katika kijiji cha Nzuguni, manispaa ya Dodoma, kinachonufaika na mradi wa ubia wa uboreshaji viwanda kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) na Wizara ya Viwanda na Biashara (TIUMP).
Kwa mujibu wa taarifa ya UNIDO, taasisi hiyo ya Umoja wa Mataifa inachangia kuimarika kwa sekta ya viwanda vidogo na vya kati vya usindikaji mafuta na kuviweka katika ushindani.
Aidha kupitia UNIDO ni viwanda hivyo vinawekwa katika hali ya kukua kuwa viwanda vikubwa.
IMG_2212
Mfanyakazi wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya Alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Alpha Manyanga akiwa kwenye mashine ya kuchujia mafuta kiwanda hapo.
Katika ushirika wa aina hiyo ni matarajio ya mradi huo kufanikisha juhudi za kupunguza umaskini kama moja ya malengo ya maendeleo endelevu yanayotarajiwa na dunia.
Aidha katika upunguzaji huo wa umaskini mradi utachangia ongezeko la fursa za ajira na ukuaji wa uchumi.
Mkoa wa Dodoma wenye viwanda vya kusindika mbegu za alizeti vinavyofanyakazi katika mkaazi wakitumia zana dhaifu na vifungashia visivyokuwa na ishara yoyote ile na kuuza bidhaa zao kando mwa barabara wanahitaji mfumo thabiti wa ukuzaji wa shughuli zao na kueleweka.
Kutokana na mazingira hayo wajasirimali hawa hujikuta wakiingia hasara kubwa kwa kupoteza tija na pia soko lenye uhakika.
Kutokana na madhara hayo na pia kukosa hati ya ubora kwa kukosa mazingira yanayoruhusu hati hiyo kutolewa, TIUMP imelenga kusaidia wasindikaji hawa na teknolojia sahihi inayohitajika ili watoke pale walipo na kuwa na viwanda vidogo au vya kati.
Ingawa kwa sasa UNIDO inasaidia viwanda vinane vya mbegu za alizeti ili kuweza kuboresha bidhaa zao na utendaji kuna muonekano wa maendeleo makubwa siku za usoni hasa kwa wanachama wa CEZOSOPA ambao wameuinganishwa pamoja kwa ajili ya misaada mbalimbali ya kuwawezesha kuwa washindani katika soko.
IMG_2216
Mtaalamu wa Chakula kutoka CEZOSOPA, Sophia Majid (aliyeipa mgongo kamera) akitoa maelezo kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (kushoto) na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto (kulia) walipokua wakikagua mtambo wa kusafisha mafuta (Semi re-finery) uliofadhiliwa na UNIDO kiwandani hapo.
UNIDO wanatumia maarifa waliyojifunza Ethiopia kuimarisha wanachama wa CEZOSOPA ambao tayari wamekubali kuunda kampuni ya pamoja na kuwekeza katika kitu wanachokifanya kwa pamoja kwa lengo la kuongeza uwezo na ushindani katika soko.
Halmashauri ya Chamwino tayari imekubali kuipa ardhi CEZOSOPA kwa ajili ya uwekezaji huo mkubwa.
Aidha UNIDO imewezesha kupatikana kwa teknolojia rahisi kwa ajili ya usafishaji wa mafuta ya alizeti na teknolojia hiyo inafanyiwa kazi na VETA.
UNIDO wamesema teknolojia hiyo hiyo inasaidia kuweka mafuta katika viwango vinavyotakiwa kitaifa na kimataifa na kwamba teknolojia hiyo tayari inafanyakazi nchini katika viwanda viwili na vingine saba vimeonesha nia ya kupata teknolojia hiyo.
Imeelezwa kuwa fedha za mradi huo zinapatikana kutoka UNIDO na wadau wengine kama SIDA na UNDAP.
IMG_2233
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto akipozi kwa picha.
IMG_2237
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akifurahi jambo alipokuwa akipewa maelezo na Mtaalamu wa Chakula kutoka CEZOSOPA, Sophia Majid (kulia) ya mtambo mahususi wa kusafisha mafuta (Semi re-finery) uliofahdhiliwa na UNIDO.
IMG_2252
 
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga (wa pili kushoto) akimuongoza Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na ujumbe wake kukagua mradi huo unaofadhiliwa na UNIDO.
IMG_2324
Wakala wa uendelezaji Kongano la Mafuta ya Alizeti wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo la Viwanda (UNIDO), Vedastus Timothy akizungumza na waandishi wa habari nje ya kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products kilichopo katika kijiji cha Nzuguni, manispaa ya Dodoma.
IMG_2257
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga (kulia) akiendelea kutoa maelezo ya namna wanavyojaza mafuta yao kwenye vigungashio wakati walipotembelea na ugeni kutoka Umoja wa Mataifa ulioongozwa na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez.
IMG_2275
Pichani ni madumu yaliyojazwa mafuta ya alizeti kiwandani hapo yakisubiri kuwekwa nembo maalum na tayari kuingia sokoni kwa mlaji.
IMG_2282
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akijaza mafuta wakati wa ziara kwenye kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha cha Glory Farm & Agricultural Products kilichopo katika kijiji cha Nzuguni, manispaa ya Dodoma, kinachonufaika na mradi wa ubia wa uboreshaji viwanda kati ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) na Wizara ya Viwanda na Biashara. Kulia ni mfanyakazi wa kiwanda hicho, Mike Brighton.
IMG_2313
Kutoka Dodoma, Tunapeleka malengo ya maendeleo endelevu (SDGs) nchini kote .....ni maneno ya Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa nne kulia), Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga (kulia),Wakala wa uendelezaji Kongano la Mafuta ya Alizeti wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo la Viwanda (UNIDO), Vedastus Timothy (wa pili kulia), Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Awa Dabo (wa tatu kulia), Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum (wa pili kuhsoto) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la FAO nchini, Patric Otto (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa kiwanda hicho.
IMG_2319
Meneja Mkuu wa kiwanda cha kuzalisha mafuta ya alizeti cha Glory Farm & Agricultural Products, Justin Nyamoga (wa tatu kushoto) na wafanyakazi wake wakipozi na bango la kuhamasisha utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu (SDGs).
IMG_2381
Afisa Kilimo wa wilaya ya Chamwino, mkoani Dodoma, Aizack Chaula (mwenye suti nyeusi) akitoa maelezo kwenye shamba la zabibu la heka 300 lililopo kwenye maandalizi kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez aliyeambatana na ujumbe wake kwenye ziara ya kukagua miradi inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa mkoani humo.
IMG_2397
Muonekano wa Shamba hilo la heka 300 ikiwa kwenye maandalizi kwa ajili ya kilimo cha Zabibu.
IMG_2428
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (katikati) akizungumza na Mwenyekiti wa kikundi cha wakulima wa Zabibu, Sekian Mavunde ili kujua changamoto zinazowakabili katika kikundi chao. Kushoto ni Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu
IMG_2462
Sehemu ya eneo la shamba la heka 296 zilizopandwa Zabibu.
IMG_2515
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akitembelea na kupewa maelezo na Afisa Kilomo wa wilaya ya Chamwino, Aizack Chaula (kulia) kwenye shamba la Zabibu la Chabuma Amlo’s Ltd. lenye ukubwa wa Heka 296 lililopo katika kijiji cha Chinangali II, wilayani Chamwino mkoani Dodoma ambapo wakulima wa eneo hilo wanaopatiwa msaada chakula kwa vibarua pamoja na kuchimbiwa mitaro bure shambani hapo na Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP). Wengine katika picha ni Mwakilishi Msaidizi wa Shirika la UNFPA, Dk. Hashina Begum ( wa pili kushoto) pamoja na Mwakilishi Mkazi wa FAO nchini, Patric Otto (kushoto) waliombatana na Bw. Rodriguez katika ziara hiyo.
IMG_2521
IMG_2522
IMG_2566

Pichani juu na chini ni miche na vitalu vya Zabibu kabla ya kupelekwa shambani.
IMG_2550
IMG_2582

Bwawa la umwagiliaji wa kilimo cha Zabibu katika shamba hilo.
IMG_2632
Pichani juu na chini ni wakulima za kilimo cha Zabibu wakizungumzia changamoto zinazowakabili katika kilimo hicho kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (hayupo pichani) alipofanya ziara ya kukagua miradi inayofadhiliwa na Mashirika ya Umoja wa Mataifa mjini Dodoma.
IMG_2658
IMG_2664
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na wakulima.

DC MAKONDA AZUNGUMZIA KIFO CHA KATIBU WA CHAMA CHA WAFANYAKAZI MADEREVA TANZANIA (TADWU)


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye ni mlezi wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi nje ya chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa ya kuhusu kifo cha utata cha aliyekuwa Katibu wa chama hicho Tanzania, Rashid Saleh kilichotokea hivi karibuni pamoja na ratiba ya mazishi yake yatakayofanyika jijini Mwanza.
 Marehemu, Rashid Saleh
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda ambaye ni mlezi wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADU), akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Pubrishers LTD, Eric Shigongo (katikati), na wadau wengine kuhusu taratibu za mazishi za katibu huyo.
 Mjumbe wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Stanley Kilave (kulia), akizungumza na Mwenyekiti mstaafu wa chama hicho, Clement Masanja (kushoto), pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Pubrishers LTD, Eric Shigongo (katikati), wakati wa taratibu za mazishi zikifanyika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dar es Salaam leo.

 Msemaji wa familia ya marehemu, Jonas Marinyizu (katikati), akitoa shukurani kwa DC Makonda na wadau wengine kwa kuwezesha msiba huo pamoja na utaratibu wa mazishi utakavyo kuwa.



Mwenyekiti wa Chama hicho, Shaban Mdem akizungumza katika mkutano na wanahabari

 Ndugu na jamaa wa marehu wakiwa katika chumba za kuhifadhi maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakisubiri kufanyika taratibu cha uchunguzi wa mwili huo kabla ya kusafirishwa kwenda jijini Mwanza kwa mazishi.
Ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu wakiwa katika chumba za kuhifadhi maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakisubiri kufanyika taratibu cha uchunguzi wa mwili huo kabla ya kusafirishwa kwenda jijini Mwanza kwa mazishi.


Na Dotto Mwaibale

MWILI wa Katibu Mkuu na Msemaji wa Chama Cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Rashid Saleh umesafirishwa jana kwenda kijijini kwao Kayenze wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza kwa maziko.

Saleh alifariki jana Novemba 20 Majira ya saa 8 mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), wakati akipata matibabu ya maradhi ya figo ili kuokoa maisha yake baada ya kile kinachodaiwa kushindwa kufanya kazi ipasavyo.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambaye pia ni mlezi wa chama hicho, Paul Makonda alisema kuwa wamepata pigo kutokana na umuhimu na umahiri ambao alikuwa nao marehemu hasa katika kutetea haki za madereva wenzake sanjari na kuibua mambo mbalimbali ambayo yatabaki kuwa historia na kumbukumbu kwao.

"Saleh alifariki jana (Novemba 20) baada ya kusikia anaumwa ambapo hali yake haikuwa nzuri na madaktari walishauri nimlete Muhimbili kwa matibabu zaidi ambapo nilimfikisha lakini baada ya muda mfupi wakati madaktari wanahangaika kumtibu na kuokoa maisha yake alifariki,"alisema.

Alisema marehemu amekiacha chama sehemu ya mafanikio makubwa zaidi ya mabadiliko na mikataba ya haki za madereva nchi nzima huku akibainisha mazingira ya kifo na kutaka uchunguzi zaidi ili kujiridhisha na kifo chake uliofanywa chini ya uangalizi wa polisi.


"Hatukuona kama kuna haja ya kumuhifadhi mwili wa ndugu yetu hadi hapo tutakapojua nini chanzo cha kifo chake kwani majibu ndiyo yatatupa picha ya ugonjwa kwani tumehangaika tangu alipokuwa hospitali ya Kairuki ambapo tulipofika hapa ikabainika kuwa figo zake zote mbili hazifanyi kazi,"alisema.

Aliongeza kuwa marehemu alipelekwa hospitalini hapo kwa kitengo maalum huku akibainisha endapo figo zinashindwa kufanya kazi mzunguko mzima wa damu mwilini nao husimama ambapo madaktari walishirikiana lakini hawakuweza kuokoa maisha yake.


Mwenyekiti wa Chama hicho, Shaban Mdem alisema kuwa msiba huo umewasikitisha sana kutokana na mazingira ya kifo chake huku akiitaka mamlaka husika kulisimamia suala hilo la kupatika kwa majibu sahihi juu ya kifo chake.

"Tunataka uchunguzi ufanyike na majibu yatoke yakiwa sahihi na yanayoridhisha juu ya kifo chake kwani amekufa na madai ambayo yapo ndani yao, hivyo serikali itambue kifo cha Saleh ni katika harakati za kudai haki ambayo tuliyawasilisha mbele ya aliyekuwa waziri mkuu Mizengo Pinda,"alisema. 

Alisema Saleh ni kiongozi wa taifa zima hivyo alimtaka rais Magufuli kuingilia kati suala hilo kwani kutokana na hali hiyo watamaliza wafanyakazi wote kwa kuwauwa katika mazingira kama hayo sambamba na kutenga siku rasmi kwa ajili ya maombezo ya msemaji huyo.

Mazingira ya Kifo

Akizungumzia mazingira ya kifo Msemaji wa Familia ya Marehemu Jonas Ernest alisema kuwa Novemba 9 mwaka huu marehemu alipokea simu kutoka kwa rafiki yake ma kumtaka waende kwenye kikao, ambapo baada ya hapo mwenzake alidai kuwa na njaa.

Alidai baada ya hapo walikwenda kuagiza chakula ambapo mwenzake hakula na kumuacha marehemu akiwa anakula huku mwenzake akiwa amemuaga kwenda msalani."Baada ya kurudi msalani alimkuta marehemu akilalamika tumbo linamuuma na hivyo kuondoka eneo hilo pasi na huyo rafiki kula chochote,"alisema.

Alidai kuwa baada ya kuhisi maumivu makali ya tumbo alianza kuharisha na kutapika na alikimbizwa hospitali lakini uchunguzi ulibaini hakuwa na tatizo na kurudishwa nyumbani ambapo siku inayofuata alirudi hospitali na kuambiwa kuwa ana malaria 4.

"Alianza kutumia dawa za malaria na baadaye kujiskia vibaya na kumrudisha tena hospitali ya Kairuki laikini madaktari walidai kuwa anatatizo ndani ya mwili ambalo ni figo kushindwa kufanya kazi vizuri,"alidai na kuongeza kuwa hadi marehemu anafariki alikaririwa akidai kuwa"Nyama inanitenganisha na mwanangu lakini"na kumtaja mmoja wa wafanyakazi wenzake huku akidai kumuona mtoto wake.  

Harakati za kudai haki ya madereva

Saleh alizaliwa mwaka 1966 Mwanza, ambapo hadi anafariki alikuwa katika harakati za kudai na kutetea haki za madereva ambapo Oktoba 2, mwaka huu alikaririwa akisema wamechoshwa na uozo unaoendelea kufanywa na Mamlaka ya Usafirishaji Majini na Nchi Kavu (Sumatra) na Wizara ya Kazi na Ajira kuhusu kufumbia macho kero zinazoitatiza sekta ya usafirishaji hasa kwa madereva wa mabasi ya abiria na magari ya mizigo.