Pages

KAPIPI TV

Saturday, October 10, 2015

MAADHIMISHO YA MIAKA 70 YA UMOJA WA MATAIFA NCHINI TANZANIA KUFANYIKA OKTOBA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR

Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro Rodriguez akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu maandalizi ya sherehe za miaka 70 ya Umoja wa Mataifa pamoja na kutolea ufafanuzi malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs) yenye lengo la kufuta kabisa umaskini.(Picha zote ne Geofrey Adroph wa Pamoja Blog).
DSC_0181
Naibu Katibu Mkuu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahya akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu maadhimisho ya kuundwa kwa Umoja wa Mataifa yatakayofanyika siku ya Jumanne Tarehe 13, Oktoba katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro Rodriguez.
Baadhi ya Maofisa wa Umoja wa Mataifa na maofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiendelea kufuatilia yanayojiri kwenye mkutanoni na waandishi wa habari.
Waandishi wa habari wakifuatilia kinachoendelea mkutanoni.
Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi Mkazi wa UNDP Bw. Alvaro Rodriguez (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kulia) wakiwa wameshikilia lengo namba 1 na 13 kati ya malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.

Mwanafunzi wa shule ya msingi ya Agha Khan, Iman Kawambwa akiwa ameshikilia lengo namba 4 kati ya malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.
Wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakiwa wameshikilia lengo namba 5 na 10 kati ya malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.
Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akiwa ameshikilia lengo namba 17 kati ya malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.
Afisa Habari wa Shirika la kazi duniani (ILO) Tanzania, Magnus Minja na Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Stella Vuzo wakiwakilisha lengo namba 1 na 8.
Baadhi ya wandishi wa habari wakiwa wameshika namba mbalimbali za malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia.
Na Mwandishi wetu Kila Oktoba 24 ya kila mwaka, Umoja wa Mataifa huadhimisha siku ya kuundwa kwake. Kwa mwaka huu Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania yanayofanya kazi kama taasisi moja yameendelea kujishughulisha na kazi mbalimbali za kijamii zenye lengo la kuadhimisha miaka 70 ya kuundwa kwa umoja huo. Akizungumza na waandishi wa habari Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini na Mwakilishi wa UNDP Bw. Alvaro Rodriguez kuhusu umuhimu wa malengo hayo amesema "Kwa hakika maadhimisho ya miaka 70 ya Umoja wa Mataifa ni wito wa kujitazama, kuona yale tuliyofanya kwa miongo kadhaa na kujikita kuona namna ya kuabiliana na umaskini hapa nchini Tanzania na Duniani kwa ujumla "Malengo ya Maendeleo endelevu ni wito wa kuwajibika kwetu sote. Hakuna mtu anayeweza kufanikiwa akiwa peke yake. Inabidi tufanye kazi kwa pamoja,wadau wote,serikali na bunge, vyama vya kiraia, madhehebu ya kidini, wafanya biashara, wajasiliamali, na wanazuoni.Na hakika tukishirikiana kwa nguvu pamoja na amani tunaweza kufikia malengo ya maendeleo endelevu" Pia alisistiza kuwa “Malengo ya dunia yaliyojengwa katika Malengo ya Milenia yamelenga kukabiliana na matatizo ya zamani kwa mbinu mpya. Zimelenga kukabiliana na tatizo la umaskini na ukosefu wa usawa katika masuala ya uchumi. SDGs haiwezi kufanikiwa bila kuyaangalia masuala ya mabadiliko ya tabia nchi, usawa wa jinsia, haki za biandamu na kukabiliana na mfumo inayobagua.” Akizungumzana waandishi wa habari Naibu Katibu Mkuu katika Wizara hiyo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahya amesema kuwa nia ya serikali ni kuendelea kushirikiana na mashirika ya umoja wa mataifa na kuwatakawatengeneze sera nzuri ambazio zitahakikisha hakuna mtu anayeachwa nyuma katika mipango ya maendeleo ya kitaifa. Aliendelea kufafanua kwa kusema Tanzania inafurahishwa na ukweli unaoonekana kwenye malengo mapya ya maendeleo endelevu kwani yamechota pia yale malengo ya milenia ambayo yalikuwa bado hayajamaliziwa kwani katika hayo kunaweza kuleta mabadiliko ya kuwezesha kuondokanana umaskini katika sura zake zote ifikapo mwaka 2030. Maadhimisho ya Umoja wa mataifa yatafavyika katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam siku ya Jumanne Oktoba 13 badala ya siku iliyozoelekaya Oktoba 24 ili kupisha uchaguzi mkuu wa Tanzania unaofanyika Oktoba 25. Na kauli mbiu ya maadhimisho ya Umoja wa mataifa mwaka huu ni "Umoja wa Mataifa uliothabiti, Dunia bora".

Friday, October 9, 2015

MPIGIE KURA MO DEWJI KUSHINDA TUZO YA HESHIMA BARANI AFRIKA #FAPOY2015

mohammed-dewji_416x416
“NINAFURAHA KUKUARIFU KUWA NIMETEULIWA KUWANIA TUZO YA “ FORBES PERSON OF THE YEAR 2015” #FAPOY2015
KWA HESHIMA NA TAADHIMA NINAOMBA KURA YAKO; Bonyeza Link hii: [ ttp://t.co/8mPEDbghsB] KUNIPIGIA KURA ILI TUIPEPERUSHE BENDERA YA TANZANIA JUU ZAIDI NA KUIWAKILISHA VYEMA AFRIKA MASHARIKI.”
MO DEWJI
"I am humbled to be one of the nominees for Forbes Person of the Year and i hope to make Tanzania/East Africa & Africa Proud. Please share with your friends and cast your votes here: http://t.co/8mPEDbghsB

Thursday, October 8, 2015

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU YASEMA MFUMUKO WA BEI UMESHUKA KUFIKIA ASILIMIA 6.1

  Mkurugezi wa Takwimu za Jamii na Sensa ya Watu wa NBS, Ephraim Kwesigabo.
  Mkurugezi wa Takwimu za Jamii na Sensa ya Watu wa NBS, Ephraim Kwesigabo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo kuhusu, Fahirisi za bei za Taifa kwa mwezi Septembva, 2015.
 Taarifa ikichuliwa na wanahabari.
 Mwanahabari Hilda kutoka gazeti la Daily News akichukua taarifa hiyo kwa umakini zaidi.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Na Dotto Mwaibale

OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS) imesema mfumuko wa bei  umeshuka hadi asilimia 6.1  kwa Septemba kutoka asilimia 6.4 kwa kipindi cha Agost 2015.

Akizungumza Dar es Salaam leo  Mkurugezi wa Takwimu za Jamii na Sensa ya Watu wa NBS, Ephraim Kwesigabo alisema kushuka kwa mfumuko wa bei kunachangiwa na kushuka kwa  bidhaa za vyakula zinazotumiwa majumbani na kwenye migahawa pamoja na vinywaji baridi.

Alisema mfumuko wa bei za bidhaa za vyakula na vinywaji baridi kwa Septemba 2015 umepungua hadi kufikia asilimia 9.6 kutoka aslimia 10.2 kwa Agost 2015

''Bidhaa za huduma kwa mwaka huu Septemba umepungua ikilinganishwa na kiasi cha bei kilichokuwepo Agost mwaka uliopita ambapo farihisi za bidhaa zimeongezeka hadi 159.4 na kutoka 149.93 Septemba 2014,' alisema.

Kwesigabo alisema mfumuko wa bei kwa kipimo cha mwaka unapima unapima kiwango cha badiliko la kiasi cha bei za bidhaa pamoja na huduma zote zinazotumiwa na kaya binafsi.

''Mfumuko wa bei ambao haujumlishi bei za vyakula na   na nishati  umebakia kuwa asilimia 22 kwa Septemba 2015 kama ilivyokuwa  Agost 2015,''alisema

Alisema thamani ya shilingi inatafsiriwa katika matumizi ya mlaji wa bidhaa mbalimbali ambapo shilingi ya Tanzania imeonekana kununua bidhaa na huduma zilezile katika vipimo tofauti tofauti.

''Uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma imefikia shilingi 62 na senti 88 kwa Septemba 2015 kutoka Septemba 2010,''alisema.

Mkurugezi huyo alisema farisihi za nishati na mafta zimekuwa na mwendendo wa hali ya juu kwa kipindi chote zikilinganishwa na farihisi nyingine.

Alisema mfuko wa bei kwa kipindi cha mwezi mmoja umeongezeka kwa aslimia 0.1 ukiwa umechangiwa na baadhi ya bidhaa zisizo za vyakula  kama vile mkaa,pamoja na huduma za saluni. 

KATIBU MKUU KIONGOZI BALOZI OMBENI SEFUE AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA TAKWIMU DAR ES SALAAM LEO

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (kushoto), akihutubia wakati akifungua mkutano wa wadau wa takwimu Dar es Salaam leo asubuhi. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Profesa Adolph Mkenda na Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk.Albina Chuwa. Mkutano huo uliandaliwa na NBS.
Mkurugenzi Mkuu Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dk.Albina Chuwa akihutubia kwenye mkutano huo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Profesa Adolph Mkenda  akizungumza katika mkutano huo.
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Dk.Rogers Dhliwayo akizungumza kwenye mkutano huo.
Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini, Bella Bird akizungumza kwenye mkutano huo.
Mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masula ya Uchumi na Kijamii (ESRF), Oswald Mashindano (Ph.D), akizungumza katika mkutano huo.
Muongozaji wa mkutano huo, Maria Sarungi akitoa maelekezo.
Wadau mbalimbali wa masula ya takwimu wakiwa katika mkutano huo.
Mkutano ukiendelea.
Viongozi wakiwa Meza kuu.
Washiriki kutoka mashirika ya maendeleo ya kimataifa wakiwa kwenye mkutano huo.

Na Dotto Mwaibale

KATIBU Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amewataka watendaji wa Serikali kutoa takwimu mbalimbali za maendeleo na kuziweka katika mitandao ili wananchi waweze kuziona na kuhoji mipango ya maendeleo iliyofanyika hama kukwama.

Hayo aliyabainisha wakati akifungua mkutano wa wadau wa takwimu ulioandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dar es Salaam leo asubuhi kwa ajili ya kukubaliana jinsi ya kushirikiana katika kuhakikisha takwimu za viashiria vya Mpango wa Maendeleo Endelevu zinapatikana kwa wakati. 

Alisema takwimu mbalimbali ni lazima zioneshe mipango ya maendeleo iliyofanyika au kumalizika badala ya kuwa siri na kuwafanya wananchi kushindwa kuhoji.

"Takwimu mbalimbali za maendeleo zikiwa wazi itasaidia wananchi kufahamu miradi ya maendeleo iliyopo na iliyokwama jambo ambalo litasaidia kusukuma maendeleo ya nchi" alisema Sefue.

Alisema lengo la  lengo la kuelimishana juu ya kukamilika kwa utekelezaji wa Malengo ya Milenia (MDGs) na kuanza kwa Malengo mapya ya Maendeleo Endelevu - Sustainable Development Goals (SDGs).


Aliongeza kuwa utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia - MDGs ulikuwa ni wa miaka 15 kuanzia mwaka 2000 hadi 2015. Mpango huu wa MDGs unakamilika mwaka huu na kuanza kwa mpango mpya wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) ambao pia ni miaka 15 ijayo.

Alisema Tanzania ni nchi ya kwanza kuanza kufanya vikao vya kutekeleza mpango huo wa maendeleo jambo ambalo linaonesha kuwa na kasi ya kuyafikia maendeleo hayo ya dunia.

Mkutano huo ulioandaliwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ulihudhuriwa na wadau wa takwimu takribani 100 kutoka Wizara, Idara, Wakala na Taasisi za Serikali, Wadau wa Maendeleo, Wadau wa Sekta Binafsi pamoja na Wadau wa Taasisi za Elimu ya Juu.


Septemba mwaka huu, viongozi wa nchi mbalimbali duniani akiwemo Rais Jakaya Kikwete walikutana nchini Marekani kwa ajili ya kutathmini utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo ya Milenia – MDGs ambapo ilionekana kwamba kuna baadhi ya malengo yalikuwa yamefanikiwa na mengine hayakufanikiwa.

MAADHIMISHO YA SIKU YA MTINDIO WA UBONGO DUNIANI KITAIFA YAFANYIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Chama cha Wazazi wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo Tanzania (Chawaumiviata), Hilal Said wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya Siku ya Mtindio wa Ubongo Duniani yaliyoadhimishwa viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.
 Mzazi mwenye mtoto mwenye changamoto ya maradhi hayo, Titus Chengula akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho hayo.
Mzazi  Ester Peter kutoka Makuburi eneo la Ubungo akizungumza na waandishi wa habari kuhusu changamoto walizonazo kuwalea watoto wenye matatizo hayo.
 Wanachama wa Chama cha Wazazi wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo Tanzania (Chawaumiviata), wakiwa na viongozi wao kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mtindio wa Ubongo Duniani yaliyofanyika hapa nchini kitaifa viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.
 Mama akimsaidia mtoto wake kutembea katika maadhimisho hayo.
 Hapa wakiwa katika picha ya pamoja.
 Burudani zikiendelea.
Picha zikipigwa na mmoja wa wafadhili wao

Na Dotto Mwaibale

WAKUU wa Shule mbalimbali wametakiwa kuwapokea watoto wenye mtindio wa ubongo kujiunga na darasa la kwanza badala ya kuwakataa kwa maelezo shule zao hazina walimu maalumu wa kuwafundisha.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Chama cha Wazazi wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo Tanzania (Chawaumiviata), Hilal Said wakati akizungumza na waandishi wa habari katika maadhimisho ya Siku ya Mtindio wa Ubongo Duniani yaliyoadhimishwa viwanja vya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.

"Changamoto kubwa waliyonayo watoto wenye utindio wa ubongo hapa nchini ni kukataliwa na wakuu wa shule mbalimbali pale wanapokwenda kuandikishwa darasa la kwanza kwa madai ya shule hizo kutokuwa na walimu wa kuwafundisha" alisema Said.

Said alisema walimu hao wanapaswa kuwapokea watoto hao badala ya kuwakataa jambo litakalo wafanya wajione hawanyanyapaliwi.

Alisema baadhi ya walimu wamekuwa wakiwaeleza wazazi wao kuwa wawapeleke watoto hao katika shule maalumu zenye walimu ambazo pia haziwasaidii watoto hao kwa kuwa wakiwa katika shule hizo wanakuwa ni watoto wenye matatizo yanyofanana.

Said alisema kuwachanganyanga watoto hao na watoto wengine katika shule za kawaida inawasaidia kuwachangamsha na kujiona kama walivyo wenzao.

Mmoja wa wazazi wa mtoto mwenye matatizo hayo Ester Peter kutoka Makuburi eneo la Ubungo alisema maadhimisho kama hayo yamekuwa yakiwakutanisha wazazi na watoto wao wenye matatizo hayo ambapo ubadilishana mawazo ya namna ya kuwalea watoto hao na kupata ushauri kutoka kwa wataalamu.

Mzazi mwingine Titus Chengula kutoka Ubungo External alisema wazazi wenye watoto wenye matatizo ya afya wasiwafungie ndani badala yake wawasaidi na kuwapekeka shule na vituo vinavyo wasaidia katika mazoezi ya viungo.

KAMPUNI YA SIMU YA TIGO, UHURU ONE YAANZISHA MFUMO MPYA WA MTANDAO WA 4G LTE

Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (kushoto), akizungumza katika mkutano na  waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam jana kwenye mkutano juu ya kampuni ya Tigo kuanza kutumia mfumo wa kwanza Afrika wa mawasiliano ya 4G DVNO ikishirikiana na Uhuru One.
Mkurugenzi Mkuu wa mradi huo Uhuru One, Rajab Katunda (kushoto), akizungumza katika mkutano huo kuhusu mradi huo. (katikati) ni Meneja Mradi huo wa Tigo, Kobbina Awuch.
Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa mradi huo kutoka  Uhuru One, Rajab Katundu wakifuatilia mkutano huo.
Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa mradi huo kutoka  Uhuru One, Rajab Katunda wakiwa katika picha ya pamoja.
Meza kuu. Kutoka kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Uhuru One, Baraka Mtunga, Mkurugenzi Mkuu wa Mradi huo kutoka Uhuru One, Rajab Katunda, Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez na Meneja Mradi huo wa Tigo, Kobbina Awuch
Wadau mbalimbali wakiwa kwenye mkutano huo.

Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya Tigo imeanzisha mfumo wa kuunganisha mtandao wa 4G LTE kwa wateja wa mtandao huo na wakazi wa Dar es Salaam kwa lengo la kuboresha mawasiliano.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja Mkuu wa kampuni hiyo, Diego Gutierrez alisema upanuzi wa 4G umetokana na mafanikio yaliyopatikana katika awamu ya majaribio yaliyofanywa na kampuni hiyo maeneo ya Mliman Cioty na Masaki Peninsula April mwaka huu.

Alisema upatikanaji wa 4G jijini kote unaridhisha na kwamba dhamira ya tigo ni kuendeleza mageuzi ya kidijitali nchini na kuongoza katika utoaji wa huduma zaidi na za uhakika kwa kutumia teknolojia ya kisasa kwa wateja.

Gutierrez alisema mtandao wa 4G LTE unamaanisha ongezeko la kasi ya kuperuzi na kupakua habari kutoka kwenye intaneti, kupiga simu kwa njia ya skype. pia inamwezesha mteja kupata mtiririko wa video au kufanya mkutano kwa njia ya mtandao kwa ubora wa hali ya juu.

"Upanuzi huu unamaanisha wateja wa tigo waliopo katika wilaya za Kinondoni, Ilala na Temeke waishio maeneo ya Upanga, Posta, Tegeta, Mbagala, Tabata, Kimara, Mbezi, Ukonga, Salasala, Mikocheni, Msasani, Sinza sasa watapata huduma bora na upatikanaji wa intaneti ya kasi zaidi kupitia mtandao wetu,"alisema Gutierrez.

Aliongeza kuwa kampuni hiyo ipo mbioni kuzindua huduma ya 4G katika miji ya Arusha , Dodoma, Morogoro, Moshi, Mwanza na Tanga mwezi ujao na hivyo kuifanya kampuni hiyo kuwa na mtandao mkubwa na wa kasi zaidi wa 4G nchini.

Wakati huohuo kampuni hiyo imeanzisha ushirikiano na kuunda mfuno wa utoaji huduma za kimtandao usiotumia muindombinu asilia ya mawasiliano ambao utaiwezesha UhuruOne kupanua upatikanaji wa teknolojia ya 4G na kwamba mfumo huo ni wa kwanza barani Afrika.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Mradi huo kutoka Uhuru One, Rajab Katunda alisema ''tunaiona Afrika ikichipua kiteknolojia lakini kujumuisha uwanda mpana wa mawasiliano na dijitali kwenye uchumi wetu kutautendea uchumi wetu jambo ambalo litatuneemesha sisi wenyewe na kutuinua kimaisha".