Pages

KAPIPI TV

Monday, July 6, 2015

SHAMRASHAMRA ZA MANUNUZI YA BIDHAA KATIKA BANDA LA MeTL GROUP MAONYESHO YA SABASABA

IMG_6798
Ofisa Mtendaji wa Masoko wa Kampuni ya bima ya MO (MO ASSURANCE), Tawheeda Isaack, akisikiliza maoni kutoka kwa mmoja wa wananchi aliyetembelea banda la Kampuni ya MO Assurance lililopo ndani ya banda la MeTL Group katika maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea kutimua vumbi kwenye viwanja vya Mwl. J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
IMG_7151
Meneja mwendeshaji wa Kampuni ya bima ya MO, (MO ASSURANCE), Ravinshankar Venkatrama (kulia) akifurahi jambo na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group, Hussein Dewji alipotembelea banda la MO Assurance kwenye maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea kutimu vumbi jijini Dar.
IMG_7148
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group, Hussein Dewji, akipata maelezo kutoka kwa kijana anayetoa huduma kwenye bidhaa za Sundries zinazotengenezwa na kampuni ya MeTL Group. Kulia ni msimamizi wa duka la bidhaa za Sundries, Sandeep Gaur alipotembelea maonyesho ya Sabasaba.
IMG_7157
Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo wa Makampuni ya MeTL Group, Hussein Dewji, akisalimiana Meneja wa LG tawi la Nkurumah, Bw. Yasin Lodhi (wa pili kulia) alipowasili kwenye banda la bidhaa za LG ambapo kampuni ya Mohammed Enterprises Limited Tanzania (MeTL) ndio msambazaji rasmi wa bidhaa hizo nchini.
IMG_7078
Mfanyakazi wa kampuni ya 21st Century Textiles Ltd, Hidaya Kapera akitoa ufafanuzi kwa wateja waliotembelea banda hilo linalouza vitenge vya aina mbali mbali kutoka kampuni za Afritex Ltd, Musoma Textiles Ltd na Novatexmoque ambazo zote ziko chini ya MeTL GROUP.
IMG_7074 IMG_7081
Mfanyakazi wa kampuni ya 21st Century Textiles Ltd, Regina Waitara, akielezea ubora wa vitenge na mashuka yanayozalishwa na kampuni hiyo kwa mmoja wa wateja aliyetembelea banda hilo.
IMG_6821
Balozi wa bidhaa za LG, Albert Laurent akitoa maelezo ya bidhaa za LG ambazo zipo katika punguzo la bei la 15% katika msimu huu wa maonyesho ya Sabasaba na mwezi mzima wa Ramadhan kwa wateja waliotembelea banda hilo ndani ya viwanja vya Mwl. J.K. Nyerere.
IMG_6841
Wananchi wakijipatia huduma ya vinywaji baridi vya MO vikiwemo MO Cola, MO Portello, MO Embe, MO Chungwa sambamba na kinywaji cha MO BOMBA kinachokuburudisha na kukupa nguvu wakati wote.
IMG_7071
Wateja wakiwa wamefurika kujipatia bidhaa za sabuni katika banda la bidhaa za kampuni ya Royal Soap & Detergent Industries Limited lililopo ndani ya banda la MeTL Group.
IMG_7082
Mfanyakazi wa kampuni ya Royal Soap & Detergent Industries Limited, Saumu Hamza, akionyesha bidhaa tofauti za sabuni za unga zinazopatikana katika banda hilo.
IMG_7084
Wateja wakifurahia sabuni za wa kampuni ya Royal Soap & Detergent Industries Limited.
IMG_7086
Wafanyakazi wa kampuni ya Sundries chini ya MeTL Group, Shomu Bhergava (kushoto) na Sandeep Gaur (kulia) wakitoa maelezo kwa mteja alitembelea banda lao katika maonyesho ya Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwl. J.K. Nyerere, barabara Kilwa, jijini Dar es Salaam.
IMG_6897
Balozi wa bidhaa za LG, Balbina Gabriel akimwonyesha mteja bidhaa ya Microwave ya kampuni ya LG aliyetembelea katika banda la MeTL Group kwenye maonyesho ya sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
IMG_7066  
Mdhibiti ubora idara ya sabuni za kampuni ya MeTL GROUP, Cuthbert Sangiwa Msuya akitoa maelezo kwa mmoja wa wananchi juu ya ubora wa mafuta ya kulainisha ngozi (Lotion) inayoyazilishwa na kampuni hiyo.
IMG_7063
IMG_7271
Wafanyakazi wa duka la vifaa vya LG lililopo ndani ya banda la MeTL Group katika picha ya pamoja na Msimamizi wa banda hilo Sakina Alloo (aliyepiga magoti).

Sunday, July 5, 2015

SUKY CLASSIC BOUTIQUE YAINGIA MKATABA NA MEDO KUSAIDIA UTOAJI WA ELIMU MKOANI MOROGORO

 Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Maendeleo Mkoa wa Morogoro, James Mbaligwe.
 Mkurugenzi Msaidizi wa Suky Classic Boutique, Kiki Mussa.
  Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Maendeleo Mkoa wa Morogoro, James Mbaligwe, akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu mkataba huo walioingia na Suky Classic Boutique wa kusaidia elimu nchini
  Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Taasisi ya Maendeleo Mkoa wa Morogoro, James Mbaligwe na  Mkurugenzi Msaidizi wa Suky Classic Boutique, Kiki Mussa wakipeana mkono huku wakifurahi baada ya kuzungumza na wanahabari kuhusu jambo hilo la kusaidia changamoto za elimu kwa watoto wa kike.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale

TAASISI ya Maendeleo ya Elimu Mkoa wa Morogoro (Medo), imepata udhamini wa asiliamia tano kutoka duka la nguo za kisasa la Suky Classic la Kinondoni Manyanya jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa duka hilo Dar es Salaam juzi, Mkurugenzi Msaidizi wa  duka hilo, Kiki Juma alisema waliguswa na mradi huo wenye lengo la kusaidia mahitaji ya watoto hao ili wapate elimu.

"Tunapenda kuwasapoti watoto hawa waliochini ya mradi 
unaoendeshwa na Medo kwa kuwasaidia mahitaji muhimu kama peni. daftari, sare za shule na mahitaji mengine" alisema Juma.

Meneja Uhusiano na Mawasiliano  wa Taasisi ya Maendeleo ya Elimu Mkoa wa Morogoro, James Mbuligwe alisema msaada huo umetolewa wakati muafaka ukizingatia ni msimu wa kufungua shule ambapo watoto hao waliochini ya mradi wanamahitaji mengi.

"Kwasasa taasisi yetu imezindua kampeni maalumu ya 'Nisaidie 500 Yatosha kunipa elimu ambapo balozi wa mradi huo ni Msanii Wastara Sajuki" alisema Mbuligwe.

Alisema wasanii na watu maarufu mbalimbali wameguswa kusaidia mradi huo ambapo Linah Sanga amejitolea kuandaa chakula cha hisani baada ya mfungo wa ramadhani kwa lengo la kuchangisha fedha za kusaidia watoto walio ndani na nje ya mradi kujengewa kituo cha elimu mkoani Morogoro.

Alisema msanii Kajala Masanja, Mshereheshaji Pilipili na mshindi wa Big Brother Afrika kwa umoja wao wamejitolea kusaidia watoto hao kwa kuchangisha fedha kupitia mitandao yao ya kijamii kwa ajili ya kusaidia mradi huo.

Mbuligwe alitumia fursa hiyo kuwaomba watanzania popote walipo kuusaidia mradi huo ili uweze kuwafikia watoto wengi zaidi kote nchini.(Imeandaliwa na mtandao wa habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)

Saturday, July 4, 2015

MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM MH. MECK SADICK AONGOZA ZOEZI LA KUOSHA MAGARI MEDIA CAR WASH FOR CANCER LEADERS CLUB LEO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadick akizindua zoezi la kuosha Magari katika viwanja vya Leaders Club kwa ajili ya kuchangia Fedha kwa waandishi wa Habari ambao wanamatatizo ya Kiafya ikiwemo Saratani 
 Mkuu wa Wilaya ya Kinomdoni Paul Makonda Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam kuongea na Waandishi wa Habari pamoja na wadau 
 Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mh. Meck Sadick akiongea na waandishi wa Habari pamoja na Wadau mbalimbali waliofika kuosha Magari yao kwa ajili ya kuwachangia waandishi wa Habari wenye Matatizo ya Saratani
 Wakielekea kuosha Magari
Mkurugenzi Mkuu wa Habari Maelezo(wa kwanza kushoto)  Athur Mwambene Akiosha Gari
 Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe akiosha Gari wakati wa  Shughuli hiyo maalum kwa ajili ya Kuchangia waandishi wenye udhoofu wa afya zao.
Mzee wa Father Kidevu Blog  Ambaye pia ni mwana TBN  akiendelea na yake....
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akiosha Pikipiki wakati wa shughuli hiyo
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Paul Makonda akiendelea Kuosha moja ya Magari yaliyofika kuoshwa katika Media Car Wash for Cancer. Ikiwa ni kuchangia waandishi wa habari wenye magonjwa mbalimbali ikiwemo Saratani.
Ankali Issa Michuzi wa Libeneke la Michuzi Blog na Michuzi Media Group na Mwana TBN  akiwa Bizeee... Anaosha Moja ya Magari kwa ajili ya kuchangie waandishi wa habari ambao wanamaradhi ya Saratani
 Watu wanazidi kuchangia .....
Hapa ni zaidi ya Tsh 1,600,000 zimechangishwa na kukabidhiwa 
Chezea Changizo wewe
 Waandishi wakichukua kwa Makini Tukio zima
Picha ya pamoja ya waandishi wa Habari pamoja na Baadhi ya Viongozi 

Unaweza Changia pia kupitia M-Pesa 0766 970240
au
Tigo Pesa 0653 155 808

(Picha zote na Fredy Tony Njeje wa Blogs za Mikoa.)

BRIGHTERMONDAY TANZANIA YATOA FURSA KWA WANAOTAFUTA AJIRA KUWATEMBELEA KWENYE MAONESHO YA SABASABA

DSC_9352
Meneja Masoko wa kampuni ya Brightermonday Tanzania, Lugendo Khalfan ndani ya hema la banda la Jakaya Kikwete akiwa tayari kukuhudumia wewe mtanzania utakayetembelea banda lao katika viwanja vya maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara ‘Sabasaba’, yanayoendelea kurindima kwenye viwanja vya Mwl. J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.( Picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)


Watafuta ajira kote nchini Tanzania wamehamasishwa kujisajili na tovuti ya Brighter monday ili wapate fursa ya kuunganishwa na watoa ajira.

Akifanya mahojiano na mtandao wa habari wa modewjiblog.com, Meneja Masoko wa Brighter monday Tanzania Khalfan Lugendo, amesema usajili huo mbao ni bure, utamwezesha mhusika kupata taarifa mbalimbali na kuweza kuomba nafasi tofauti za kazi ambazo zimewekwa katika tovuti hiyo.

Amesema Brightermonday inajivunia kuwa ndio tovuti namba moja ya ajira nchini Tanzania kwa kuwa idadi ya kazi wanazoziweka katika mtandao huo ni nyingi kuliko chanzo chochote kile cha ajira nchini Tanzania.

Bw. Lugendo ameongeza kuwa kwa mwaka jana 2014 waliweza kuweka nafa za ajira 30,000 na hivyo kuwarahisishia waajiri mchakato mzima wa kuajiri na kupata watu wenye viwango bora zaidi.

Aidha ametoa wito kwa watu wote wanaotembelea maonyesho ya mwaka huu ya kimataifa ya biashara Sabasaba, kutembelea banda lao lililopo katika hema la Jakaya Kikwete ambapo watapata maelekezo kuhusu namna ya kuweza kupata ajira kwa urahisi.

Ametaja namna ya kuwapata ni kupitia anuani ya tovuti ambayo ni www.brightermonday.co.tz au e-mail : info@brightermonday.co.tz,
Simu: +255688 333 334,

Katika mitandao ya kijamii wanapatikana kwa anuani zifuatazo
facebook: brightermondaytz,

Instagram: brightermondaytz pia katika Googleplus na Twitter.
DSC_0109
Key Account Manager wa Brightermonday Tanzania, Gloria Nyiti kwenye sehemu maalum ya kupokea wageni katika banda lao lililopo ndani ya hema la Jakaya Kikwete.
DSC_0310  
Wafanyakazi wa Brightermonday Tanzania wakitoa huduma kwa mmoja wa wateja aliyetembelea banda lao lilipo ndani ya hema la Jakaya Kikwete kwenye maonyesho sabasaba.
DSC_9343
Gloria Nyiti akiwahudumia watafuta ajira katika banda la Brightermonday lililopo ndani ya hema la Jakaya Kikwete.
IMG_6607
Gloria Nyiti akitoa maelekezo ya namna ya kujisajili kwenye mtandao wa Brightermonday kwa mmoja wa wateja aliyetembelea banda lao kwenye maonyesho ya sabasaba yanayoendelea kupamba moto jijini Dar.
DSC_0318  
Timu ya wafanyakazi wa Brightermonday Tanzania wakiwa nadhifu katika banda lao tayari kuwahudumia wateja kwenye maonyesho ya Sabasaba.

UMOJA WA MATAIFA WAIBUKA KIDEDEA KATIKA UHABARISHAJI NA UTOAJI ELIMU KWENYE TUZO YA MAONESHO YA 39 YA SABASABA

DSC_0178
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkadhi Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez (kushoto) cheti na tuzo katika kipengele cha Uelimishaji bora kupitia Uandishi wa machapisho na mpangilio bora wa maonyesho, baada ya Umoja wa Mataifa kuibuka mshindi wa kwanza katika maonyesho ya 39 ya kimataifa ya biashara ya Sabasaba yalipozinduliwa rasmi. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tan Trade), Jacqueline Mneney Maleko (kushoto) pamoja na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe.Dkt. Abdallah Kigoda (kulia).
DSC_0179 FullSizeRender_2
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa wanaohudumia banda hilo kwenye maonyesho ya Sabasaba wakisheherekea mara baada ya kutwaa tuzo hiyo.
UN Tanzania inawakaribisha Watanzania wote wanaotembela maonyesho sabasaba kufika katika banda lao lililopo Karume Hall na kuweza kushiriki kutoka maoni ya juu ya utendaji wa kazi za Umoja wa Mataifa Tanzania kwa njia ya mtandao wa simu yako bila kutozwa malipo yoyote ukitumia huduma hiyo, kwa wateja wote mitandao ya Airtel, Tigo na Vodacom.
Jinsi ya kutuma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS), kwa kuandika neno UN au UMOJA WA MATAIFA ambapo kwa watumiaji wa mtandao wa Airtel watatuma ujumbe wao kwenda namba 15453, kwa watumiaji wa mtandao wa Tigo wanatuma kwenda 15055 au 15453 na kwa Vodacom ni namba 15055.
Njia nyingine ya kuwasilisha maoni yako moja kwa moja kupitia mtandao (Online) bofya link hii http://gpl.cc/UN2
FullSizeRender  

Friday, July 3, 2015

CHADEMA YAANDAA KONGAMANO LA WAZEE, KUFANYIKA KESHO HOTELI YA BLUE PEARL UBUNGO JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Hashim Juma Issa (kulia), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana, kuhusu kongamano litakalo wakutanisha wazee wote bila kujali itikadi za vyama vyao litakalo jadili mustakabali wa taifa kuelekea uchaguzi mkuu litakalofanyika  kesho ukumbi wa Hoteli ya Blue Pearl Ubungo jijini Dar es Salaam.
 Makamu  Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Suzan Lymo, akizungumza katika mkutano huo.
 Baadhi ya wazee wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye mkutano huo.
 Baadhi ya wazee wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Mkoa wa Dar es Salaam wakiwa kwenye mkutano huo.



Na Dotto Mwaibale

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeandaa 
kongamano la wazee ambalo litafanyika Hoteli ya Blue Pearl jijini Dar es Salaam kesho.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari leo mchana 
Mwenyekiti wa Baraza la Wazee la chama hicho, Hashim Juma Issa alisema kongamano hilo litawahusisha wazee wote nchini bila ya kujali itikadi za vyama vyao.

Alisema dhima kubwa ya kuanzisha kongamano hilo ni kuwapa elimu wazee bila kujali itikadi zao za kisiasa  hasa katika kipindi hiki cha  kuelekea uchaguzi mkuu. 

"Wazee wengi wamekuwa hawafahamu nini majukumu yao kama wazee lakini kongamano hili litakuwa ndiyo chanzo kikubwa cha 
kuwafahamisha wazee majukumu yao hasa katika wakati huu wa 
kuelekea uchaguzi," alisema Issa.

Alisema kila mtu anafahamu  binadamu huwa anapitia hatua muhimu za maisha nazo ni utoto,ujana na utu uzima hivyo hamna budi wazee hawa kuelewa lengo kuu katika katika uchaguzi mkuu huo kuwa katika mstari ulinyooka. 

"Kumekuwa na tabia ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwatumia wazee kwa ujanja tena hasa wakiwa na matatizo na kuwabagua wa vyama vingine lakini sisi katika kongamano hili hatutobagua mzee wa chama chochote katika kongamano hili kwani wazee wote ni hazina,"alisema

"Hakuna asiyefahamu kuwa kwa sasa nchi inaelekea katika uchaguzi mkuu ambao uchaguzi huu utakuwa ni mkubwa na wa aina yake hivyo kwa kuwaita wazee hawa itakuwa ni muendelezo wa kupata hekima zao kama wazee"alisema.

Issa alisema katika uchaguzi mku wazee wana jukumu kubwa la 
kuhakikisha kushiriki kikamilfu katika zoezi zima la kujiandikisha na kupiga kura ipasavyo.

Alisema hatua hiyo haina budi kuwasahawisi watoto na watu wakubwa na wajukuu kushiriki kwa ukamailifu katika tukio hili kwani kila mtu anahitaji mabadiliko katika nchi.

Hata hivyo Issa alisema wazee pia wana jukumu kubwa la kutatua 
migogoro ,kushawisi na kusimamia maadili lengo likiwa ni uthubutu wa kukemea viongozi wanaopata madaraka kwa njia ya rushwa na ufisadi.

Alisema wanahitaji wazee watakaosimama kidete na kupaza sauti zao katika kukemea maovu na watenda maovu bila kuona haya.

Alisema katika kongamano hilo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho Wilbroad Slaa huku mada mbalimbali zitatolewa na Mabere Marando pamoja na viongozi wa dini ili kuwapa elimu wazee kutokana na maadili ya nchi kumomonyoka kwa kiasi kikubwa. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com-simu namba 0712-727062)