Pages

KAPIPI TV

Tuesday, May 26, 2015

UNESCO YASISITIZA UPENDO KWA WATOTO WENYE ALBINISM

DSC_0945
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues (katikati) akiambatana na Mbunge wa viti maalum CCM, anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir (kushoto) walipotembelea shule msingi Mitindo ya watoto wenye ulemavu wa ngozi, macho na masikio iliyopo katika wilaya ya Misungwi nje kidogo ya jiji la Mwanza. Kulia ni Mtaalamu wa Jinsia na Haki za Binadamu kutoka UNESCO Tanzania, Bi. Annica Moore.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)

Na Modewjiblog team
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)Tanzania, Zulmira Rodrigues amesisitiza umuhimu wa kuwapenda watoto wenye ulemavu wa ngozi katika jamii baadala ya kuwatenga .

Zulmira alisema hayo alipotembelea watoto wenye ulemavu wa ngozi katika shule ya msingi ya Mitindo iliyopo katika wilaya ya Misungwi nje kidogo ya jiji la Mwanza mwishoni mwa juma
Shule hiyo ya serikali ina wanafunzi zaidi ya 1000 wakimo wenye ulemavu 202 .

Kati yao 81 ni wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi ambao wanahifadhiwa na serikali katika shule hiyo maasa 24 kufuatia wimbi la mauaji la watu wenye ulemavu wa ngozi katika mikoa ya kanda ya ziwa .

Hata hivyo Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa UNESCO Tanzania alionekana kupatwa huzuni kubwa kutokana hali ya maisha ya watoto hao .

“ Nimehuzunika sana (I am so sad). Sio tabia ya watu wa Afrika kuwatenga watu wanyonge (weak people)”alisema huku akitokwa na machozi mara baada ya kuwatembelea watoto hao na kuongea nao pamoja na uongozi wa shule hiyo.

Alisema ni muhimu watoto hao wenye ulemavu wa ngozi kuwa wanavaa nguo za mikono mirefu ili kuwakinga na jua kwa ajili ya kulinda afya zao.

Hata hivyo Zulmira alipongeza jitihada zinazofanywa na serikali ya Tanzania kulinda watu wenye ulemavu wa ngozi na kutoa wito kwa wadau wote kuunga mkono juhudi hizo.
DSC_0955
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mwalimu msingi Mitindo iliyopo katika wilaya ya Misungwi nje kidogo ya jiji la Mwanza.

Katika ziara hiyo, Zulmira alikuwa amefuatana na mbunge wa viti maalum anayewakilisha watu wenye ulemavu wa ngozi (albinism) Mh. Al shaymaa Kwegyir.

Mbunge huyo pia alisema kitendo cha watoto wenye ulemavu wa ngozi kukosa malezi na mapenzi ya wazazi ni changomoto kubwa iliyopo kwa sasa.

Alisema ni jukumu la watu wote kulinda na kusadia kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu wa ngozi.

“Ufumbuzi wa matatizo ya wetu wenye ulemavu wa ngozi sio kazi ya serikali tu, ni jukumu la kila mtu”,mbunge huyo alisisitiza.

Aliahidi kuwasilisha bungeni baadhi ya changamoto zinazowakabili wanafunzi walemavu waliopo katika shule hiyo ya Mitindo.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Kurwa Ng’hwelo alisema serikali inatumia zaidi ya shilingi milioni 10 kuwa ajili ya mahitaji ya chakula kwa wanafunzi wote wenye ulemavu wapatao 202 kila mwezi.

Shule hiyo inakabiliwa na upungufu mkubwa wa watumishi wanaosadia wanafunzi hao walemavu.
DSC_0968
Mwalimu wa shule ya msingi Mitindo, Kulwa Ng'hwelo akitoa maelezo ya idadi ya wanafunzi wenye ulemavu wanaosoma shuleni hapo ambao ni 202 huku 81 wakiwa na albinism kwa Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues (kushoto) aliyetembelea shule hiyo kuangali changamoto zinazowakabili watoto wenye ulemavu wa ngozi.
DSC_0979
Mwalimu wa shule ya msingi Mitindo, Kulwa Ng'hwelo akimwonyesha mazingira ya eneo la shule hiyo Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues aliyeambatana na Mbunge wa viti maalum CCM, anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir.
DSC_0989
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues akisalimiana na baadhi ya wanafunzi wa kutwa wanaosoma katika shule ya msingi Mitindo mara baada ya kuwasili shuleni hapo akiwa ameambatana na Mbunge wa viti maalum CCM, anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir.
DSC_0993
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza na wanafunzi hao waliofurahia ujio wake.
DSC_0997
Pichani ni moja ya jengo lililojengwa na Ubalozi wa Japan nchini Tanzania.
DSC_1009
Mmoja wa watoto wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) akitoka bwenini kuelekea chumba maalum kwa ajili ya kujipatia chakula cha mchana katika shule ya msingi Mitindo huku akionekana kutembea kwenye jua kali pasipo na kuwa na nguo ndefu ya kufunika hadi mikononi kujikinga na mionzi ya jua inayopelekea kupata saratani ya ngozi.
DSC_1017
Mtoto mwenye ulemavu wa ngozi (Albinism) ambaye jina lake halikuweza kupatikana kiurahisi akila chakula cha machana huku akijikuna kutokana na maumivu makali anayosikia ya majeraha ya mionzi ya jua iliyoharibu mikono yake na kubadilika rangi ambayo athari yake baadae ni saratani ya ngozi.
DSC_1025
Na hii ndio hali halisi ya binti huyu katika mikono yake kutokana na kutembea kwenye jua bila kusitiri mikono yake na nguo ndefu.
DSC_1026
Baadhi ya watoto wa bweni wenye Albinism wakijipatia chakula cha mchana jikoni.
DSC_1043
Mtoto mwingine aliyeathiriwa na mionzi ya jua miguuni na kupelekea kubadilika rangi kuwa mwekundu kutokana na kukosa nguo ndefu za kujisitiri na mionzi ya jua... wakiendelea kujinoma na chakula cha mchana.
DSC_1033
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues akionyesha uso wenye huzuni kubwa kutokana na mazingira magumu waliyonayo watoto hao shuleni hapo. Kushoto ni Mbunge wa viti maalum CCM, anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir aliyeambatana na Bi. Zulmira Rodrigues kutembelea shule hiyo. Katikati ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya msingi Mitindo, Kulwa Ng'hwelo.
DSC_1068
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akisisitiza jambo kwa Mwenyekiti wa kamati ya shule ya msingi Mitindo, Kalunde Cosmas alipofanya ziara fupi ya kutembelea shule hiyo na kujionea changamoto zinazowakibili watoto wenye ulemavu wa ngozi (Albinism).
DSC_1036
Mbunge wa viti maalum CCM, anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir akimwonyesha mwandishi wa modewji blog (hayupo pichani) majeraha ya kuungua na jua kwa mmoja wa watoto mwenye albinism shuleni hapo.
DSC_1053
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza jambo na mtoto mwenye ulemavu wa ngozi aliyekuwa akijipatia chakula cha mchana.
DSC_1073
Mdau Semeni Kingaru akimsimamia kula chakula cha mchana mtoto mdogo kuliko wote mwenye albinism aliyeonekana kukosa upendo wa wazazi wake kwa kipindi kirefu na kufarijiwa na ugeni huo uliofika shuleni hapo.
DSC_1101
Mbunge wa viti maalum CCM,anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir akibadilishana mawazo na mabinti wa shule ya msingi Mitindo alipowatembelea na Bi. Zulmira Rodrigues.
DSC_1106
Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) akisaidiana na Mdau Semeni Kingaru kugawa zawadi ya juisi kwa watoto wa shule ya msingi Mitindo.
DSC_1113
Mtaalamu wa Jinsia na Haki za Binadamu kutoka UNESCO, Bi. Annica Moore aliyeambatana na Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues (hayupo pichani) akifurahi jambo wakati akigawa zawadi ya juisi mmoja watoto wenye albinism shuleni hapo.
DSC_1119
Mkuu wa ofisi na Mwakililishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiendelea na zoezi la ugwaji zawadi ya juisi kwa watoto wenye ulemavu wa ngozi, macho na masikio wa shule ya msingi Mitindo iliyopo katika wilaya ya Misungwi nje kidogo ya jiji la Mwanza alipowatembelea mwishoni mwa juma akiwa ameambata na Mbunge wa viti maalum CCM,anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir (hayupo pichani).
DSC_1085
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wa macho wakijumuika na wenzao wenye ulemavu wa ngozi na masikio kujipatia chakula cha mchana.
DSC_1087
Mtoto mdogo kuliko wote mwenye albinism anayeonekana kukosa lishe bora inayostahili kutokana na umri wake ambapo modewjiblog imebaini kuwa mtoto huyu ana "Utapiamlo" kutokana na kukosa lishe hiyo bora. Dalili moja wapo ni tumbo lake kuwa kubwa na gumu.
DSC_1137
Mkuu wa ofisi na Mwakililishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimnywesha juisi mtoto mdogo kuliko wote anayelelewa kwenye shule ya msingi Mitindo ya watoto wenye uhitaji maalum ambao ni walemavu wa ngozi, macho na masikio alipofanyia ziara fupi mwishoni mwa juma mkoani Mwanza.
DSC_1144
Mkuu wa ofisi na Mwakililishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akimnyeshwa juisi mtoto menye ulemavu wa macho alipotembelea shule ya msingi Mitindo iliyopo wilaya ya Misungwi nje kidogo ya jiji la Mwanza.
DSC_1160
Mkuu wa ofisi na Mwakililishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiwa na uso wa huzuni kutokana na mazingira ya watoto hao na kupelekea kumwaga machozi kwa uchungu yeye kama mama mwenye kuthamini upendo. Kushoto ni Mh. Al Shaymaa Kwegyir.
DSC_1163
Bw. Abdulaziz Mbegele wa kitengo cha Logistic kutoka UNESCO, akimnywesha juisi mtoto mwenye ulemavu wa macho wakati wa ziara hiyo na Mkuu wa ofisi na mwakilishi wa UNESCO nchini Tanzania.
DSC_1091
Mtoto alyefahamika kwa jina moja tu Kevin mwenye umri wa miaka 11 ambaye alifikishwa kwenye shule hiyo akiwa mdogo sana na wazazi wake kumtelekeza hadi leo huku akiwa hamjui mama, baba, mjomba, dada, kaka wala shangazi..... kisa amezaliwa na albinism....!
DSC_1097
Mtoto Kevin akipata "self" na mjomba wake mpya Zainul Mzige wa modewjiblog aliyeambatana na ugeni huo.
DSC_1202
Mkuu wa ofisi na Mwakililishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza na waandishi wa habari na kutoa hisia zake kuhusiana na changamoto zinazowakabili watoto wenye ulemavu wa nguvu na kusisitiza upendo kwa watu wenye albinism.
DSC_1195
DSC_1216
Mbunge wa viti maalum CCM, anayewakilisha watu wenye ulemavu, Mh. Al shaymaa Kwegyir akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani).

TAMASHA LA GOSPEL CONCERT & CONFERENCE MEMORIAL WEEKEND, COLUMBUS, OH.


Mwimbaji mahili wa nyimbo za injili kutoka Tanzania Upendo Nkone akiimba moja ya nyimbo zilizowainua watu vitin kwenye tamasha la Gospel linaloendelea mjini Columbus tangia siku ya Ijumaa May 22 na kuhitimishwa leo siku ya Jumapili May 24. Tamasha lilihudhuriwa na watu kutoka mataifa mbalimbali wengine wakiwa wamesafiri kutoka majimbo ya mbali na Ohio.

Mwimbaji kutoka Jamhuri ya Congo akienda sambamba na mwimbaji mahili wa nyimbo za injili Upendo Nkone kwenye tamasha la Gospel lililofanyika siku ya Jumamosi May 23, 2015 6230 Busch Blvd suit 260, Columbus, OH 43229.

 Nnunu Nkone akitoa neno la Mungu na kuimba kwenye Tamasha la Gospel lililofanyika
Mchungaji Donis Nkone ambaye ni kaka ya mwimbaji Upendo Nkone akitoa ukifanya utambulisho kwa bendi iliyokuwa ikitumbuiza nyimbo za injili kwenye tamasha la Gospel lililofanyika siku ya Jumamosi May 23, 2015 mjini Columbus.

Mchungaji Donis Nkone na mkewe Nnunu Nkone wakifuatilia tamasha la Gospel

Bendi ikienelea kupiga moja ya nyiimbo za mwimbaji wa nyimbo za injili kutoka Tanzania Upendo Nkone.

Bendi ikitumbuiza.

Kwa picha zaidi bofya soma zaidi.





MITAZAMO HASI KITAMADUNI CHANZO CHA MAUAJI YA WATU WENYE ALBINISM

DSC_0569
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Bi. Zulmira Rodgrigues, akiwasilisha mada katika warsha ya siku tatu iliyofanyika katika kijiji cha Nyakahungwa wilayani Sengerema mkoani Mwanza kuhusu ushirikishaji jamii katika kuandaa na kutekeleza mikakati itakayochangia kuzuia na kutokomeza unyanyasaji na dhulma zinazofanywa dhidi ya watu wenye albinism iliyoshirikisha waganga wa asili, wauguzi na wakunga, viongozi wa dini, walimu pamoja na watu maarufu iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)

Na Modewjiblog team, Mwanza
Mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albinism) yanayoendelea nchini yanatokana na mitazamo hasi kitamaduni miongoni mwa wanajamii.

Hayo yameelezwa na washiriki wa warsha ya siku tatu inayoendelea katika kijiji cha Nyakahungwa kata ya Nyakahungwa wilayani Sengerema yenye lengo la kubadili mitazamo iliyojengeka katika jamii na kusababisha madhara makubwa kwa watu wenye albinism iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO).

Warsha hiyo ni miongoni mwa mlolongo wa warsha nne zitakazofanyika katika wilaya za Sengerema, Mwanza, Kahama na Bariadi kwa kuzishirikisha jamii kuibua masuala mbalimbali yanayobagua, kunyanyapaa na kuwatenga watu wenye albinism katika maeneo husika.

Warsha hizo zinafanyika katika kipindi ambacho kumetokea mauaji ya mtoto wa kike, msichana na kijana wenye albinism wilayani Sengerema wakati tarehe 14 Mei 2015 mwanamke mmoja alikatwa mkono wilayani Bariadi.
DSC_0522
DSC_0532
Afisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Sengerema, Bw. Bushaija Vicent (kulia), akitoa takwimu za idadi ya za wanafunzi wenye albinism katika wilaya yake kwa Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO Bi. Zulmira Rodgrigues.

Kwa mujibu wa Afisa Maendeleo Jamii wilayani Sengerema Bwana Bushaija Vicent kati ya shule za msingi 191 wilayani humo ni Shule zenye watoto wenye albinism ni 14, Idadi yao ni 16 katika shule ya awali watoto 4 wana albinisim, vyuo mbalimbali Sengerema vijana 4 wana albinism na katika Shule za sekondari 48, watoto wenye albinism 4.

Akitoa mada kuhusu uhamasishaji jamii katika masuala ya albinism, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO Bi Zulmira Rodgrigues amesema miongoni mwa masuala ambayo warsha italenga ni kutafakari kwa kina kwa nini watu wenye albinism wanauawa, kubaguliwa, kutengwa na mambo yanayosababisha Tanzania kuongoza katika mauaji hayo ikilinganishwa na nchi nyingine ambazo pia zina watu wenye albinism.

“Watu wenye albinism hawauwawi katika sehemu nyingine duniani, kwa nini Tanzania? Ikiwa mauaji hayo yako kwa wingi nchini Tanzania basi kuna tatizo kubwa ambalo linatakiwa kufanyiwa kazi, na si serikali, UNESCO wala taasisi yoyote ambayo inaweza kuleta mabadiliko hayo isipokuwa jamii yenyewe,” alisema Rodrigues.

Tatizo kubwa lililotajwa kuhusiana na mauaji ya watu wenye albinism ni utamaduni uliojengeka katika fikra za watu na kuwa na imani kwamba watu wenye albinism si watu wa kawaida, hawana hadhi na hawastahili kuishi.

Watu wenye albinism ni watu wa kawaida wanaostahili heshima na kulindwa kama binadamu wengine kulingana na kanuni na sheria za nchi na za kimataifa zinazopinga ubaguzi wa rangi, jinsia, tabaka na kukatisha maisha ya mtu. Tofauti ni kwamba rangi yao inatokana na ukosefu wa vinasaba asili vijulikanavyo kama melanin, vyenye uwezo wa kuzalisha rangi ya nywele, macho na ngozi.

Utamaduni uliojengeka katika jamii wa kuwabagua, kuwatenga na kuwapuuza watu wenye ulemavu wa ngozi kumehalalisha mauaji ambayo kwa hivi sasa imekuwa biashara ya kuuza viungo vya watu wenye albinism kwa waganga wa asili kwa lengo la kupata utajiri, cheo na madaraka.

“Mara nyingi waganga wa asili wamekuwa wakitajwa kuwa ndio chanzo cha mauaji hayo kwa ajili ya imani potofu ya kujipatia utajiri, vyeo na madaraka. Biashara hiyo inaonekana kushamiri kwa kuwa hakuna mifumo mahsusi kudhibiti maafa hayo,” alisema mmoja wa washiriki anayeshughulikia masuala ya usalama.
DSC_0545
Mratibu na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO Bi. Rose Haji Mwalimu, akichangia mada kuhusu ushirikishaji jamii katika kuandaa na kutekeleza mikakati itakayochangia kuzuia na kutokomeza unyanyasaji na dhulma zinazofanywa dhidi ya watu wenye albinism iliyoshirikisha waganga wa asili, wauguzi na wakunga, viongozi wa dini, walimu pamoja na watu maarufu iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO). 

Katikati ni Mratibu ambaye pia ni Afisa Mradi wa Elimu ya Afya na VVU/UKIMWI kutoka UNESCO, Bw. Herman Mathias na Kulia ni Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Bi. Zulmira Rodgrigues.

Akichangia mada wakati wa majadiliano yanayokusudiwa kuzalisha mikakati ya kukomesha maovu hayo, Mratibu na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO Bi Rose Haji Mwalimu alisema kwamba wakati umefika wa kutambua kitu gani kizuri katika tamaduni zilizopo zitakazoweza kusaidia kuleta mafanikio na kuachana na zile ambazo hazina tija na zinasababisha maafa katika maendeleo na ustawi wa jamii.

“Ni kweli kuna changamoto nyingi katika jamii zinazosababishwa na kuhalalisha tamaduni zinazolenga kupotosha badala ya kujenga. Tukiendelea kuzikumbatia tutajikuta tunajenga taifa lisiloona mbali kimaendeleo kuhadaiwa na watu wenye ubinafsi kutoka nje na ndio maana Tanzania imekuwa soko kubwa au shamba lenye rutuba ya kupandikiza mbegu ambazo mavuno yake hupatikana kwa urahisi”, alisema Bi Mwalimu.

Katika warsha hiyo washiriki walibaini maeneo makuu matatu ya kuyawekea mpango kazi. Maeneo hayo ni Kuzuia mauaji, ubaguzi, unyanyapaa na kuwatenga, eneo la pili ni kuwalinda watu wenye albinism katika maeneo ya makazi, mashuleni, katika jamii na familia zao na la tatu ni hatua za kisheria wale wote watakaoonekana kuhusika moja kwa moja au kwa namna nyingine katika kuwatendea maovu watu wenye ulemavu wa ngozi kuanzia ngazi za kimataifa, kitaifa, kifamilia na shuleni.
DSC_0553
Mganga wa jadi kutoka kijiji Nyanzenda, wilayani Sengerema, Maimuna Musa akizungumzia jinsi anavyotoa huduma za kutibu watoto magonjwa mbalimbali ya watoto ikiwemo na huduma ya kuzuia mwanamke asizae mtoto mwenye ulemavu wa ngozi.
DSC_0549
Mganga wa jadi kutoka kijiji cha Nyakasungwa, Omary Mongongwa akitoa msimamo kuhusu uwezo wa tiba kwa waganga wa jadi unavyotofautiana na kuwasihi waganga wenzake wa jadi wanapojadili wazungumzie kazi za mtu binafsi na utendaji wake na si kuusemea moyo wa mganga mwingine.
DSC_0596
Mzee maarufu kutoka kijiji cha Bukokwa, Felician Buhumbi, akifafanua hatua zilizokuwa zikichukuliwa wakati wa Ukoloni dhidi ya waganga asili wenye kupiga ramli chonganishi wakati wa warsha ya siku tatu iliyofanyika katika kijiji cha Nyakahungwa wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
DSC_0511
Sehemu ya washiriki wa warsha hiyo ya siku tatu iliyowashirikisha, Waganga wa Jadi, Viongozi wa dini, walimu shule za msingi na sekondari, wazee maarufu, Wakunga, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Shirika la Under the Same Sun, Baraza la taifa la dawa asilia, Afisa wa polisi wa dawati la jinsia pamoja na Maafisa wa mkoa wa Mwanza na wa wilaya ya Sengerema.
DSC_0652
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Bi. Zulmira Rodgrigues aliyeambatana na mbunge wa viti maalum CCM anayetetea maslahi ya watu wenye albinism, Mh. Al-Shaymaa Kwegyir wakiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki.