Pages

KAPIPI TV

Tuesday, May 12, 2015

RATIBA YA USAJILI WA TMT SEASON 2 KWA MIKOA YA MBEYA, MTWARA NA DAR

CHAWATIATA TABORA YATOA ONYO KALI KWA WAGANGA WA TIBA ZA ASILI

Na  Allan Ntana,Tabora

WAGANGA wanaojishughulisha na utoaji tiba asilia mkoani Tabora wameonywa kutojihusisha na vitendo vyovyote vinavyochochea uvunjifu wa amani kwa kuhamasisha mauaji ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi(albino).

Kauli  hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Waganga na tiba asilia (CHAWATIATA) katika Manispaa ya Tabora  Bw.Ramadhani Rajabu alipokuwa akizungumza na  Mwandishi wa gazeti hili kuhusu tuhuma zinazowakabili baadhi ya wananchama wake kujihusisha na vitendo hivyo viovu.

Alisema anaunga mkono kauli ya Serikali ya kuwakamata waganga wote wanaojihusisha na vitendo hivyo ikiwa ni pamoja na wale wanao tumia ramli chonganishi kwani wanaweza kuondoa amani ya nchi yetu ikiwa ni pamoja na kuwapa hofu ya kuishi wazee na albinism.

Alisema kila halmashauri ya wilaya mkoani humo inatakiwa kuwatambua waganga wa kienyeji waliopo na wenye  vibali vya kufanya kazi hiyo kutoka kwenye chama na endapo mamlaka husika na kubainisha kuwa yule atakayebainika kwenda kinyume na masharti ya katiba ya chama hicho atachukuliwa hatua kali za kisheria na ikiwemo kufikishwa mahakamani ili kujibu tuhuma hiyo.

“Haiwezekani mganga anayetibu ama kutoa tiba ya kweli amshawishi mteja wake kuleta viuongo vya maalbino, huyo siyo mganga na hakuna tiba yoyote ya asili inayo tumia kiungo cha binadamu isipokuwa viungo vya baadhi ya wanyama ila sio binadamu,''alisema Rajabu.

Alisema inasikitisha  sana  kuona waganga wa tiba asili wakituhumiwa kuhusika na mauaji ya albino  pamoja vikongwe jambo linawachafua hata waganga wengine ambao wanafuata maadili ya utoaji tiba hizo, na kuongeza kuwa hao ni matapeli na ni wenye tamaa ya fedha.

Hili haliwezi kuvumilika nilazima hatua kali zichukuliwe dhidi yao, aliongeza.

Aliitaka Jamii kutambua kuwa hakuna Mganga ambaye anaweza kumwagiza mteja wake kumletea kiungo cha albno ili kuweza kutibiwa kwani hata waganga wana watoto ambao ni albinism, ndugu na wengine ni baba zao, mama zao,shangazi au wajomba hivyo suala hilo linatakiwa kupigwa vita kwa nguvu zote ili kuwaokoa hawa wenzetu wanao wamaoangamia bila sababu.

Aidha alisema  Serikali inatakiwa kulitambua hili kama janga la kitaifa na siyo kwamba mauaji haya yanawahusu waganga wa kienyeji wote kama inavyoonekana bali inatakiwa kukaaa chini na kulitafutia ufumbuzi kwani mauaji hayo ni sawa na vita ambayo inaaza kwa kuwabagua walemavu hao na vigongwe.

Hata hivyo aliomba wanachi kuungana kwa pamoja kuhakikisha ulinzi dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi unakuwepo na kutoa taarifa sehemu husika pale inapotokea albino au kikongwe kufanyiwa unyama wa aina yoyote ile ili kumaliza janga hili linalowakabili. 

Aidha ameyataka medhehebu yote ya dini kuungana kwa pamoja kuliombea taifa juu ya janga hili la mauaji ya albino na vikongwe linalo zidi kushika kasi hapa nchini ikiwa ni pamoja taifa kupata sifa mbaya kwenye anga za kimataifa.  

TANZANIA MEDIA IN THE FRONTLINE: JOURNALISTS TARGET POLITICAL HATE IN UPCOMING ELECTION

hate specch banner
Journalists and African media leaders from the region are meeting this week to highlight the role of media and journalism in combating hate-speech and intolerance in the upcoming election campaign.
The meeting, organised by the International Association of Women in Radio and Television (IAWRT) and the Ethical Journalism Network (EJN), opens in Dar Es Salaam today (Tuesday) and comes after fresh regional conflict with recent terrorist attacks in Kenya and fears of genocidal violence in Burundi.
The meeting will involve a workshop at the Peacock Hotel on how journalists and media can help stop the spread of hateful political propaganda and will reinforce the Africa-wide campaign,Turning the Page of Hate, which was launched last year in Kigali to mark the 20th anniversary of the Rwandan genocide.
Among the speakers will be Mohammed Garba, President of the Federation of African Journalists and Imelda Lulu Urio, from the Tanzanian Legal and Human Rights Centre.
“This conference could not come at a more important time for Tanzanian journalists,” said Rose Haji Mwalimu, head of IAWRT for Tanzania. “Media here are in the frontline of a struggle for democracy and pluralism. We have to ensure that we keep a lid on the voices of hate and, at the same time, give people the right to free speech.”
This challenging task will involve helping journalists to identify hate-speech and to lower the temperature of confrontation that often comes at election time, she said. The journalists and media will be encouraged to use a special 5-point test for hate-speech that has been developed in co-operation between media and the United Nations human rights commission.
“The violence in recent months inspired by terrorists in Kenya and the continuing shadows over Burundi suggest that it’s a matter of urgency for journalists to eliminate the voices of intense hatred and incitement,” said Aidan White, Director of the EJN. “This meeting comes only a few months before the hotly-contest general election in Tanzania when the political temperature will rise and media have to guard against being used by hate-mongers.”
In recent years, Tanzania has seen much foul play by candidates from all parties with hate speech and threats on all sides. There have been reports of acid attacks, kidnappings and killings. This meeting will focus on practical actions for journalists to help reduce the level of confrontation.
The meeting will:
1. Call upon government and all political leaders to respect the freedom of the press and ensure that journalists operate in a safe environment;
2. Call on media and journalists to boycott hate speech or any language that can stir violence;
3. Promote ethical standards at all levels of the press, broadcasting and online communications;
4. Call on politicians to ban hate speech in their own ranks;
5. Call upon citizens to boycott meetings or activities where candidates or political activists use hateful, violent and discriminatory language to promote their brand of politics.
6. Reiterate the need for all media to be aware of legal restrictions, including the Newspaper Act of 1976 that could see media banned for hate speech;
7. Call upon the Tanzanian Parliament to review provisions in the Statistics Act as well as the Cyber Crime Act which may violate the freedom of the press as well as the right to information.
“None of this will be easy,” said Rose Haji Mwalimu, “But this is an important opportunity for journalists and media to strengthen their role in ensuring the coming elections are a beacon for democracy and not an excuse for settling political score by acts of hatred and violence.”
More information:
Rose Haji Mwalimu:rohamu2004@yahoo.co.uk or 0754270856/0655434444
Aidan White: aidanpatrickwhite@gmail.com or 00447946291511

WAKAZI WILAYA YA KAKONKO WATAKIWA KUJIUNGA NA MFUKO WA AFYA YA JAMII CHF-KIGOMA

Katibu tawala wilaya ya Kakonko Bi.Zainab Mbunda akifungua Mkutano wa wadau wa Mfuko wa Taifa wa Afya ya Jamii CHF uliofanyika katika Ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma ambapo alisisitiza umuhimu wa wananchi kujiunga na Mfuko huo wa hiari ambao unawawezesha kupata huduma za matibabu kwa muda wa mwaka mzima baada ya kujiunga na kuchangia kiasi cha shilingi elfu kumi.
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kakonko Bi.Jaina Msangi akizungumza namna ambavyo Halmashauri inavyosimamia Mfuko huo wa CHF na kueleza kuwa wamekuwa wakihamasisha Jamii kujiunga na Mfuko huo ili waweze kunufaika na huduma za Afya.
Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF Bw.Rehan Athuman akitoa maelezo mafupi kuhusu Mfuko wa Afya ya Jamii CHF na namna ambavyo ulivyoweza kuwafikia watanzania na kunufaika na huduma za Mfuko huo unaolenga kuboresha afya za wananchi hususani wenye kipato cha chini na cha kati.
Baadhi ya Wadau wa Mfuko wa Bima ya Afya waliohudhuria katika Mkutano huo wakiwemo Madiwani,Watendaji wa vijiji,Kata na Vitongoji,Viongozi wa Dini,Vyama vya Siasa,Mashirika,Asasi mbalimbali na Wazee Maarufu wa wilaya ya Kakonko(Picha zote na  KAPIPIJhabari.COM) 






THE GOVERNMENT OF TANZANIA EXPANDS ITS NEW BIRTH REGISTRATION SYSTEM TO MWANZA

Baby Veronica being registered
Baby Veronica being registered.
The new system is set to drastically increase the number of children under 5 with birth certificates
The Deputy Minister of the Ministry of Constitutional and Legal Affairs of the United Republic of Tanzania, Honorable Ummy Ali Mwalimu, launched today in Mwanza the new simplified birth registration initiative for children under-five in Tanzania. The event took place in Mwanza, the second largest city in mainland Tanzania. Mwanza will be the second region, after Mbeya, to benefit from the new, easily accessible and free birth registration system which is set to register over 400,000 children under-five by December 2015.
This new birth registration system, which is being supported by a generous contribution from the Government of Canada through the Department of Foreign Affairs, Trade, and Development, was first field tested in 2012 in Temeke, the largest district of the city of Dar es salaam and in 2014 was officially launched in Mbeya. According to the Acting Chief Executive Officer of RITA, Ms. Emmy Hudson, this simplified system marks a significant shift in accelerating birth registration in Tanzania after years of stagnation.
“RITA has embarked on several initiatives to improve birth registration in Mainland Tanzania, especially to newborn babies to ensure that each baby is captured and registered shortly after birth and closest to home. Through this initiative we see this dream realized and thank our development partners for unwavering support. Temeke and Mbeya have set good examples and we hope to register even better results in Mwanza.”
The 2010 Tanzania Demographic and Health Survey showed that only 16 per cent of children in Tanzania under the age of five were registered with civil authorities, and only about 8 per cent have a birth certificate.[1] Registration in Zanzibar is much more widespread than on the mainland with 78.7 per cent of under-fives registered (63 per cent with a certificate) versus 14.6 per cent registered (6.2 per cent with a certificate) on the mainland.[2]
Prior to the roll-out of the Birth Registration Initiative in Mbeya it was estimated that only 8.7 per cent of the under-five population had a birth certificate. In less than two years after the roll-out, Mbeya saw approximately a 48 per cent increase and now it is estimated that nearly 56 per cent of under-fives in Mbeya have a certificate.
[1] See Tanzania Demographic and Health Survey (2010), pg. 27.
[2] Ibid. and See p.28, Table 2.11 Birth Registration for Children Under Five
Baby Veronica and her Birth Certificate
Baby Veronica and her Birth Certificate.
The new decentralized birth registration and certification system capitalizes on the existing health infrastructure and personnel to register newborn babies soon after birth or within 12 months when visiting health facilities for vaccinations. Registration information is uploaded using mobile phone technology to a centralized data-base resulting in real-time data availability, and a certificate is issued the same day.
This new birth registration and certification system will be operational in Mwanza soon after today’s launch. With financial support from the Canadian Government, this new system will also be rolled out over the next five years to ten additional regions, namely, Mara, Shinyanga, Simiyu, Geita, Iringa, Njombe, Tabora, Kagera, Kigoma and Dodoma.
Paul Speech
UNICEF Tanzania Deputy Representative, Paul Edwards.
UNICEF Tanzania Deputy Representative, Paul Edwards, commended the Government of Tanzania for its commitment to prioritizing child rights and reaffirmed UNICEF’s commitment and support towards making birth registration and certification a reality for all children.
“With this initiative RITA has taken an important step towards facilitating birth registration. Registration Assistants are now able to upload information instantly over mobile phones, making data available in ‘real time.’ This type of information is crucial in planning for Tanzania’s future. And it goes without saying that the certificate itself provides protection for children - proof of age informs the State as to who is a child, and provides protection against the exploitation of children and child marriage.”
Tigo Lake Zone Director, Ally Maswanya said: “The support provided by Tigo towards this initiative is in line with the company’s corporate social responsibility strategy which aims at empowering community with information and communication technology tools such as mobile phones. The under-five birth registration initiative demonstrates our commitment as telecommunication experts and attests the potential of mobile technology in development programs.”
The VSO Country Director Jean Van Wetter praised the strong partnership between Government, UN, private sector and civil society: “Birth registration is fundamental to guarantee child rights and further improve the social services delivery system in the country.”

TAASISI YA IMETOSHA YATOA MSAADA KWA KITUO CHA BUHANGIJA SHINYANGA


Toka kushoto ni Kathrin Hoff, kijana Paulo, Masoud Kipanya na Balozi Henry Mdimu.
Taasisis ya Imetosha ya jijini Dar es Salaam leo hii imepeleka misaada mbali mbali katika kijiji cha watoto wasioona cha Buhangija, Shinyanga ambacho kwa sasa kinahifadhi pia watoto na vijana wenye ualbino takriban 300. Misaada hiyo ikiwemo mabelo ya mitumba 2 moja la masweta na jingine la suruali za jeans, unga, mchele, maharage, sukari, chumvi, ndoo 3 za mafuta ya kupikia, sabuni za kufulia box 8, vile vile box 3 za vifaa vya hedhi vitakavyodumu miezi miwili pamoja na nguo za ndani dazeni 12 vyote hivo  imegharimu Tsh milioni mbili na elfu sitini(2,060,000) ambazo zimetolewa na wanachama wa taasisi hiyo iliyojikita kupambana na mauaji ya watu wenye ualbino kwa njia ya elimu.

Akiongea na watoto na vijana hao Mwenyekiti Masoud Kipanya alisema taasisi hiyo inaangalia jinsi ya kutengeneza mazingira kwa kituo hicho kujijengea uwezo wa kujipatia chakula badala ya kutegemea wasamaria wema huja pale watakapojisikia wakati watoto katika kituo hicho wanahitaji kula kila siku.

Mkuu wa kituo hicho alisema anashukuru taasisi ya Imetosha kwa kuonesha mapenzi ya dhati na watoto wa kituo hicho na kuguswa na changamoto zinazowakuta, kwani si mara nyingi sana watu au taasisi kurudia kupeleka misaada kituoni hapo kitu ambacho Imetosha wamekifanya. Wiki 3 zilizopita taasisi hiyo ilipeleka msaada wa chakula kituoni hapo.

Awali mtafiti wa masuala yahusuyo watu wenye ualbino mJerumani Bi Kathrin Hoff alielezwa kufurahishwa na jitihada zinazooneshwa na Imetosha kwa uhamasishaji inayoufanya kwa jamii ya Ki Tanzania, pia amepongeza sana hatua ya Imetosha kutaka kukifanya kituo cha Buhangija kujitegemea badala ya kubaki tegemezi kama ilivyo sasa. Kathrin Hoff ni mhitimu toka chuo kikuu cha Mainz nchini Ujerumani.
Baadhi ya missada iliyotolewa na Imetosha pembeni kulia ni mabelo mawili ya mguo.
Mkuu wa kituo hicho Bw Peter Ajali akiongea na watoto wa kituo hicho akieleza dhamira ya ya asasi ya Imetosha kwao.


Hapa wakimsikiliza Masoud Kipanya
Baadhi ya wasichana wa kituoni hapo wakifurahia msaada wa nguo za ndani na vifaa vya hedhi walivyokabidhiwa na mjumbe wa Imetosha aishiye Shinyanga Bibi Herriet

Picha na habari kwa hisani ya TBN kanda ya kati.

TIMU TANZANIA YASHIRIKI MATEMBEZI YA SUSAN G. KOMEN WASHINGTON, DC


Timu Tanzania ikipata picha ya pamoja kabla ya kuanza matembezi ya saratani ya matiti ya Susan G. Komen yaliyofanyika Washington, DC siku ya Jumamosi May 9, 2015.

Wanusurika wa saratani ya matiti wakipata picha ya pamoja.

Matembezi yakianza.

Kushoto ni msaniii toka uingereza Matt Goss aliyeimba wimbo maalum wa Strong kwa ajili ya matembezi haya ya Susan G. Komen ambaye mwaka jana mama yake mzazi alifariki kutokana na maradhi ya saratani ya matiti akipeana mkono na watembeaji wa saratatani ya titi. Kati ni Nancy G. Brinker mdogo wake Susan G. Komen akipeana mkono na watembeaji siku ya maadhimisho ya matembezi ya saratani ya matiti kwa kumuenzi dada yake kwa kuanzisha oganaizesheni ya kupigana na gonjwa hili hatari mwaka 1982 kama ahadi aliyomwekea dada yake.

Mmoja ya watembeaji na mnusurika wa saratani ya titi akipatiwa huduma ya kwanza na watembeaji wenzake baada ya kuanguka na kupata majeraha kwenye paji la uso huku wakisubili gari la wagonjwa.

Timu Tanzania ikichanja mbuga kwenye matembezi hayo.

Mwanahabari wa Kwanza Production na Vijimambo Media Mubelwa Bandio(kulia) akiwa sambamba na mwimbaji Matt Goss na Nancy G. Brinker CEO wa Susan G. Komen

Timu Tanzania ikiwa imemaliza matembezi yao ya maili 3 takribani na kilomita 5

Watoto wa wazazi Watanzania wakipata picha ya pamoja baada ya kumaliza matembezi hayo na wazazi wao.

Picha ya pamoja ya kumaliza matembezi hayo pamoja na mmoja wa kikosi cha zima moto wa TDF aliyejumuika kupiga picha na timu Tanzania.

Picha zote na Kwanza Production na Vijimambo Media & Entertainment.
Kwa picha zaidi bofya HAPA

Friday, May 8, 2015

MIPANGO NA SERA ZITEKELEZWE KUMUOKOA MAMA NA MTOTO MCHANGA

DSC_0334
Mratibu wa Mawasiliano na uhamisishaji wa mradi wa Mama Ye unaoendeshwa na asasi ya Evidence for Action linalofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID), Chiku Lweno akielezea jitihada zinazofanywa na mradi wa Mama Ye katika kukabiliana na vifo vya Mama na mtoto ambapo aliwataka waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuelemisha jamii ili iweze kuepukana na vifo vya mama na mtoto ambalo nalo ni janga la taifa.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).

Na Mwandishi wetu, Musoma
SERIKALI imeshauriwa kuhakikisha sera na mipango mizuri iliyopo kwa afya ya mama na mtoto mchanga inasimamiwa na kutekelezwa ili kuliondoa taifa katika janga la kupoteza mama na watoto wakati wa uzazi.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Mawasiliano na uhamisishaji wa mradi wa Mama ye unaoendeshwa na asasi ya Evidence for Action linalofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID), Chiku Lweno katika mafunzo kwa waandishi wa habari mjini Musoma.

Alisema bila kutekeleza mipango mizuri ambayo Rais Jakaya Kikwete amekuwa championi wa masuala ya wanawake na watoto kitaifa na mataifa, tatizo la vifo kwa wanawake wenye pingamizi za uzazi na watoto wachanga.

Alisema kutokana na haja ya kutoa msukumo katika masuala ya uzazi wameamua kuwapatia elimu waandishi wa habari ili wawe chachu ya kutambua umuhimu wa ukunga na uzazi salama.
"Tunafunza waandishi wa habari ili waweze kusukuma mbele shahuri hili ili kila mtu katika nafasi yake atetee nafasi yake" alisema Lweno.

Alisema suala la mama na mtoto mchanga ni masuala mtambuka ambapo mambo mengi lazima yaunganishwe yafikiriwe na kutambuliwa ili kudhibiti vifo vya wanawake na watoto wachanga.

Alitaja masuala hayo kama upangaji wa bajeti ya kueleweka kwa ajili ya kusaidia kupatikana kwa wakunga wataalamu na vifaa vyao vya kazi na maeneo ya kufanyia kazi. Aidha kuwapo kwa ukubali wa wakunga na elimu ya uzazi.

Alisema ni vyema waandishi wa habari kama watia chachu kuelimishwa mambo mengi yanayohusiana na uzazi salama ambapo ndani yake kuna masuala ya bajeti na ufuaji wa wataalamu na ufuatuiliaji wa sera na sheria zilizopo katika kuhakikisha usalama wa mama na mtoto.

Alisema anaamini waandishi wa habari wakielewa mambo hayo watasaidia kukomaa nalo na kuwezesha kila mtu kuwajibika.
DSC_0278
Kaimu Muuguzi Mkuu wa Serikali kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Ama Kasangala akifafanua jambo kwa washiriki wa mafunzo ya siku moja yaliyofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) kuelekea kwenye kilele cha sherehe za maadhimisho ya siku ya wakunga duniani ambapo kitaifa imefanyika mkoani Mara.

Naye Afisa Muuguzi mwandamizi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii, Saturini Manangwa akiwasilisha mada kwa waandishi wa habari alisisitiza haja za waandishi kutambua dhana ya afya ya mama na mtoto kuwa ni kitu mtambuka kutokana na suala la lenyewe kutegemeana.

Alisema serikali inapohimizwa kuwekeza kwa mkunga kunatokana na ukweli kuwa huduma ya mama na mtoto mchanga itakujwa bora kwa kuwa na mkunga bora mwenye vifaa na anayefahamu wajibu wake kuanzia ujauzito wa mama hadi kujifungua kwake.

Alisema uwekezaji huo unagusia changamoto nyingi zilizopo sasa kama upungufu wa wakunga, vituo vya kutolea huduma, dawa, miundombinu na masuala anuai ambayo yameegemezwa na utambuzi wa bajeti na umuhimu wake kama kipaumbele.

Alisema kwamba katika upangaji bajeti kila kitu kinategemea huwezi kusema unazidisha hiki na unakiacha hiki.

Alisema mathalani katika hali bora ya ukunga na uwezo wa kumsaidia mhusika ,viwango vya dunia vilivyoweka na Shirika la Afya Duniani (WHO) kila mkunga mmoja ahudumie angalau watu sita, lakini sehemu kubwa ya dunia haifikii hivyo.

Aidha alisema kwa Tanzania kiwango ni mkunga mmoja ahudumie watu 20-25 lakini kwa sasa Tanzania mkunga mmoja anahudumia zaidi ya watu 50.

Kimsingi alisema Tanzania ina tatizo la wakunga na pamoja na serikali kuanzisha vyuo vya kufunza wakunga na kukubali mashirika ya dini nayo kufanya hivyo hali bado ni tete.
Hata hivyo alisema ni kupitia wakunga waliowataalamu upo uwezekano wa kuzuia vifo visivyo vya lazima.
DSC_0253
Mratibu wa Chama cha Wakunga nchini (TAMA), Martha Rimoy akizungumzia nia ya chama hicho ni kuhakikisha kwamba kila mwanamke mwenye uwezo wa kuzaa anapata huduma za mkunga mtaalamu.

Muuguzi huyo mwandamizi pia alisema katika juhudi za serikali kunaanzishwa mafunzo ya mwaka mmoja ambapo yatatoa maofisa afya ambao kazi yao kubwa itakuwa kujua idadi ya wanawake wajawazito na wagonjwa katika maeneo yao na kutoa taarifa kwa zahanati iliyo karibu.

Alisema ofisa huyo kazi yake haitakuwa hospitalini au kwenye zahanati bali kwenye jamii akitambua idadi ya wagonjwa wake na kutoa taarifa sahihi ya hali ya afya ya kitongoji chake kwenye zahanati.

Mmoja wa washiriki Belina Nyakeke ambaye ni mwandishi wa habari wa magazeti alisema kwamba amefurahishwa na mafunzo hayo ambayo yamempa nafasi ya kutambua wajibu wake katika kusaidia kuondoa tatizo la vifo vya mama na mtoto mchanga.

Alisema japokuwa mafunzo ni ya muda mfupi lakini yamemfumbua macho kutambua wajibu na haki kwa wananchi na serikali.

Naye Ahmed Makongo akizungumzia mafunzo hayo alisema yamemfanya atambue wajibu wake kusaidia kusukuma mambo yaende sawa kwa upande wa waamuzi na pia wananchi husika kwa kuzingatia mafunzo hayo yaliyoletwa kwao na Mama Ye na UTTPC chini ya Ufadhili wa Shirika la Mpango wa watu Duniani (UNFPA)
DSC_0219
Afisa muuguzi mwandamizi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Saturini Manangwa akizungumzia changamoto za upungufu wa wakunga, vituo vya kutolea huduma, dawa, miundombinu n.k wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari wa mjini Musoma mkoani Mara.
DSC_0299
Afisa wa Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu (UNFPA) anayeshugulikia mifumo ya Afya, Felista Bwana akitoa takwimu za nchi zinazoongoza kwa vifo vya mama na mtoto kwenye mafunzo ya waandishi wa habari mjini Musoma.
DSC_0244
Mwandishi wa habari wa gazeti la The Citizen, mkoani Mara, Belina Nyakeke (katikati) akishiriki kwenye mafunzo ya waandishi wa habari yaliyofanyika mjini Musoma na kufadhiliwa na Shirika la UNFPA.
DSC_0207
Mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima mjini Musoma, Igenga Mtatiro akiuliza swali kwa Afisa muuguzi mwandamizi kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Saturini Manangwa (hayupo pichani).
DSC_0229
Pichani juu na chini ni baadhi ya waandishi wa habari wa mkoani Mara ambao pia wanachama wa vilabu vya Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) walioshiriki mafunzo hayo yaliyoratibiwa na Mradi wa Mama Ye kwa kushirikiana na UTPC na kufadhiliwa na UNFPA.
DSC_0267
DSC_0260
DSC_0197
Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akisisitiza jambo kwa washiriki wa mafunzo hayo.
DSC_0242
Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya (kushoto) akibadilishana mawazo na Mratibu wa Chama cha Wakunga nchini (TAMA), Martha Rimoy mara baada ya kuhitimisha mafunzo hayo.

PROIN PROMOTIONS IN BELGIUM - LAUNCHING OF TANZANIA FILMS ONLINE.

 Mwenyekiti wa Proin Group Tanzania ndugu Johnson Lukaza akizungumza machache na kuwashukuru watu wote waliohudhuria uzinduzi wa manunuzi ya filamu za kitanzania kupitia mtandao (online) hapo jana katika ukumbi wa ACP House jijini Brussel nchini Ubelgiji na kuudhuriwa na watu wa mataifa mbalimbali.Uzinduzi huo ulifanywa na balozi wa Tanzania Mheshimiwa Diodorus Kamala.

UNESCO, SERIKALI WATIA SAINI MRADI WA MAFUNZO YA TEHAMA KWA WALIMU

DSC_0023
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (wa pili kulia), Balozi wa China nchini, Mh. LU Youqing (kushoto), Afisa utawala na fedha wa UNESCO, Spencer Bokosha (kulia), Ofisa anayeshughulikia masuala ya Elimu Kitaifa wa UNESCO, Tumsifu Mmar pamoja na mkalimani wa Balozi wa China wakifurahi jambo wakati Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome (hayupo pichani) akiwasili kwenye chumba cha mikutano Wizara ya Elimu kwa ajili ya hafla fupi ya kutiliana saini mkataba utakaowezesha kutekelezwa kwa mradi wa kuwezesha walimu wa Tehama vyuoni nchini. (Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog)

Na Modewji blog team
SERIKALI na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) jana wametiliana saini mkataba utakaowezesha kutekelezwa kwa mradi wa kuwezesha walimu wa Tehama vyuoni nchini.

Akizungumza baada ya kutiwa saini kwa mkataba huo Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome alisema mradi huo ni mkombozi mkubwa katika maandalizi ya kufundisha kwa kutumia Tehama nchini.

 Alisema mpango huo wenye kuwezesha walimu kujifunza Tehama unafadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China ambao ndio wamepitisha fedha zao UNESCO.

Katika utiaji saini huo ambapo Balozi wa China nchini Dk. Lu Youqing alikuwepo, katika jumla ya uhai wa mradi ambao ni miaka miwili , miundombinu ya ufundishaji masomo ya sayansi na hesabu katika vyuo vya walimu vya Monduli na Tabora itaboreshwa.

Katika mradi huo walimu watafundishwa elimu ya Tehama, namna ya kufundisha na kujifunza.

Katibu mkuu Mchome alisema kwamba vyuo hivyo viwili vitawezeshwa kuwa na mtandao ambao utaunganishwa na vyuo vingine vinane vya masomo ya sayansi na hesabu kwa ajili ya kubadilishana taaluma.

Pia vyuo hivyo vitawezeshwa kuandaa programu zenye kuelezea mfumo wa utoaji huduma za Tehama kwa ajili ya walimu wa masomo ya sayansi na hesabu.
DSC_0037
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (katikati) akisalimina kwa furaha na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome (kulia) na kushoto ni Balozi wa China nchini, Mh. LU Youqing (aliyeipa mgongo kamera).

Profesa Mchome alisema ili taifa liweze kusonga mbele katika mpango wake wa kufundisha kwa kutumia Tehama ni vyema kuandaa walimu na fedha za China kupitia Unesco zitasaidia maandalizi hayo.

“Tunaamini tukiwekeza katika vifaa vya kupromoti Tehama, walimu wakifundishwa na kuandaliwa vyema, wataenda kusaidia kufundisha na kuwezesha matumizi ya Tehama katika shule zao.” Alisema Profesa Mchome.

Alisema japo zipo program ndogo nyingine , program waliyotia saini jana ilikuwa kubwa na yenye tija itakayoimarisha ubora wa elimu kwa kuwapa wanafunzi elimu ya kujitegemea, elimu yenye kuwakwamua kiujuzi na kuutumia ujuzi huo kwa maendeleo yao na taifa.

Tanzania ni miongoni mwa mataifa barani Afrika ambayo mapema wametambua thamani ya kufundisha kwa njia ya Tehama ili kuboresha elimu na mfumo wa elimu.

Taasisi zitakazohusika na mradi huo ni pamoja na Chuo Kikuu Huria (OUT) na Taasisi ya Elimu nchini(TIE) kwa kuratibiwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
DSC_0074
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome (kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (katikati) pamoja na Balozi wa China nchini, Mh. LU Youqing (kushoto) kabla ya kutiliana saini mkataba huo.
DSC_0080
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza jambo kabla ya kusaini mkataba huo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome na Kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dr. Moshi Kimizi. Waliosimama wakishuhudia tukio hilo kutoka kushoto ni Joel Nanauka wa UNESCO, Afisa tawala msaidizi wa UNESCO, Rahma Islem, Afisa mipango wa utamaduni wa UNESCO, Rehema Sudi, Balozi wa China nchini, Mh. LU Youqing, Ofisa anayeshughulikia masuala ya Elimu Kitaifa wa UNESCO, Tumsifu Mmar pamoja na Afisa utawala na fedha wa UNESCO, Spencer Bokosha.
DSC_0084
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome wakitiliana saini mkataba utakaowezesha kutekelezwa kwa mradi wa kuwezesha walimu wa Tehama vyuoni nchini unaofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China. Wanaoshuhudia tukio hilo waliosimama ni Balozi wa China nchini Tanzania, Mh. LU Youqing (wa pili kushoto), Ofisa anayeshughulikia masuala ya elimu kitaifa wa UNESCO, Tumsifu Mmar (wa pili kulia), Afisa mipango wa utamaduni wa UNESCO, Rehema Sudi (kushoto), Afisa utawala na fedha wa UNESCO, Spencer Bokosha na Kulia aliyeketi ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya UNESCO, Dr. Moshi Kimizi.
DSC_0086
Zoezi la kusaini mkataba likiendelea.
DSC_0089
Wakifurahi kwa pamoja mara baada ya zoezi la kutia saini kukamilika.
DSC_0090
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues (kulia) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Sifuni Mchome wakibadilishana hati za mkataba utakaowezesha kutekelezwa kwa mradi wa kuwezesha walimu wa Tehama vyuoni nchini unaofadhiliwa na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa China nchini Tanzania, Mh. LU Youqing(wa pili kushoto) pamoja na Afisa utawala na fedha wa UNESCO, Spencer Bokosha (kulia).
DSC_0091
DSC_0103
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza jambo baada ya kutiliana saini mkataba huo.
DSC_0068
Afisa utawala na fedha wa UNESCO, Spencer Bokosha (kulia) akizungumza jambo na Afisa wa ubalozi wa China (katikati) na Kushoto ni Afisa Utawala msaidizi wa UNESCO, Rahma Islem.