Pages

KAPIPI TV

Sunday, April 26, 2015

RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI AFUNGA KIKAO CHA MABALOZI WA HESHIMA


Rais mstaafu awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi akiingia chumba cha mkutano cha Nyerere ndani ya mjengo wa Ubalozi Washington, DC siku ya Ijumaa April 24, 2015 kulikokua na kikao cha Mabalozi wa heshima kilichoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani chini ya Balozi Liberata Mulamula kwa ajili kuongelea maswala mbalimbali zikiwemo changamoto za utalii na uwekezaji nchini Tanzania na jinsi gani ya kukabiliana nazo, mbali na Mabalozi hao wa heshima na marafiki zao wengine waliohudhuruia kikao hicho ambacho kilikua sehemu ya maadhimisho ya miaka 51 ya Muungano ni wawakilishi wa Taasisi za Diaspora za Kitanzania zinazopigana kusaidia maswala ya uwekezaji na Utalii kwa nchi yao Tanzania. Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi pia aliongozana na mkewe Mama Sitti Mwinyi.
Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na mwenyeji wake Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula wakiwemo Mabalozi wa heshima wakisimama kwa ajili ya nyimbo za Taifa za Tanzania na Marekani.

Mhe. Liberata Mulamula Balozi wa Tanzania nchini Marekani akimtambulisha Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kwa Mabalozi wa heshima wakiwemo viongozi wa  taasisi mbalimbali za Kimarekani zinazotangaza utalii wa Tanzania nchini Marekani na baadae kumkaribisha kuongea nao.

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na mkewe mama Sitti Mwinyi akimsikiliza Balozi wa Tanzania nchini Marekani anyoamtambulisha mbele ya mabalozi wa heshima na kwamba yeye Rais mstaafu ndiye aliyefanya mageuzi ya mfumo wa uchumi Tanzania tunaoendelea nao hivi sasa.

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiongea na Mabalozi wa Heshima kuwashukuru kwa kuipenda na kuitangazaTanzania nchini Marekani na kuwaasa wasichoke kwa wao wamekua chachu ya maendeleo ya nchi aipendayo Tanzania.

Mbalozi wa heshima wakiwemo viongozi wa taasisi zinazotangaza Utalii na uwekezaji Tanzania wakimsuikiliza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi.
 Picha ya pamoja.
Mayor De  Andre Windom wa mji wa Highland Park jimbo la Michigan akipata picha na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi
Balozi wa Tanzania nchini Marekani akimuaga Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na mkewe mama Sitti Mwinyi wakati walipokua waiondoka baada ya Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kumaliza kufunga kikao cha Mabalozi wa Heshima Ubalozini hapo.
Picha zote na Vijimambo, Kwanza Production

BALOZI LIBERATA MULAMULA AONGOZA MKUTANO WA MABALOZI WA HESHIMA

Balozi Liberata Mulamula, Balozi wa Tanzania nchini Marekani akifungua mkutano wa Mabalozi wa Heshima uliofanyika siku ya Ijumaa April 24, 2015 Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani. Mkutano huo ulizungumzia  uwekezaji na Utalii zikiwemo Changamoto zake na jinsi ya kukabiliana nazo. Pia katika mkutano huo uliokua sehemu ya maadhimisho ya miaka 51 ya Muungano uliudhuria pia na Viongozi wa Taasisi za Diaspora wa Tanzania ambao wanaguswa na kuiona nchi yao ikipiga hatua ya maendeleo katia sekta ya uwekezaji na Utalii.

Abdul Majid mwanaDiaspora Mtanzania anayeishi California nchini Marekani akielezea huduma kwa wateja bado ipo kiwango cha chini nchini Tanzania na jinsi gani ikiboreshwa inavyoweza kunua uchumi wa Tanzania.

Balozi wa Heshima Mhe. Kjell Berch akichangia na kuelezea majukumu ya Balozi wa heshima.

Rais wa East Africa Diaspora Business Counsil Benedict Kazora ambaye pia ni mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Dallas, Texas akichanganua na kutoa maelezo yanayoweza na kurahisiha maswala ya uwekezaji na kukosoa baadhi ya makampuni yanavyowekeza Afrika kwa kujinufaisha yenyewe.

Karen Hoffman Rais wa The Bradford Group kutoka New York akielezea sekta ya Utalii na utangazaji wa Utalii wa Tanzania nchini Marekani.

Balozi wa Heshima Mhe.Cemil Teber kutoka New Mexico akichangia jambo.

Balozi wa Heshima kutoka Ohio Mhe. Patrick Griswold akielezea sekta ya uwekezaji na changamoto inazokutana nazo huku akitoa mfano wake mwenyewe alipokua meneja mkuu wa General Tire miaka ya nyuma na tangia alipoondoka kiwanda kikafa na sasa anatarajiwa kwenda tena Tanzania kujaribu kukifufua upya kiwanda hicho.

Mkutano wa Balozi Liberata Mulamula na Mabalozi wa Heshima ukiendelea

Wakati wa chakula. Picha zote na Vijimambo, Kwanza Production

MWANDISHI WA VITABU YASIN KAPUYA AKUTANA NA RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI WASHINGTON DC.

Mwandishi wa vitabu Yasin Kapuya akimwelezea Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ya jinsi gani vitabu vyake vinavyoweza kumkwamua mwananchi wa hali ya chini na kumfikisha juu katika kumboreshea maisha mapya. Akijitolea mfano wake mwenyewe alipoanzia shimoni Kariakoo mpaka kufika nchni Marekani na sasa kualikwa katika mikutano mikubwa ya kutoa semina ya jinsi gani unavyoweza au kampuni inavyoweza kuwa namba moja katika sekta ya biashara.
Mwandishi wa vitabu Yasin Kapuya akichangia jambo na Katibu Mkuu wa Rais mstaafu Bwn. Abdallah Makame (kulia) aliokua akiongea na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi siku ya Ijumaa April 24, 2015 jijini Washington, DC nchini Marekani.
Mwandishi wa Vitabu Yasin Kapuya wakiwa katika picha ya pamoja na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi wakishikilia bango la kitabu chake kipya kitakachotoka hivi karibuni.

Mwandishi wa Vitabu Yasin Kapuya akimkabidhi Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi moja ya vitabu vyake.

Mwandishi wa Vitabu Yasin Kapuya akiagana na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi. Picha na Vijimambo, Kwanza Production


Saturday, April 25, 2015

TEMBO KUTOWEKA TANZANIA MIAKA 10 IJAYO - NYALANDU

DSC_0089
Pichani juu na chini ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akizungumza na katika mkutano uliohusisha wadau wa mashirika ya Kimataifa na asasi za kijamii ukiwa na lengo la ushirikishaji wa jamii katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori uliofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Mpingo House uliopo Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewji blog).

Na Modewji blog team
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amesema kama watanzania wasiposhirikiana katika kudhibiti ujangili wa Tembo waliopo watatoweka kabisa katika kipindi cha miaka 10 ijayo.

Kauli hiyo ameitoa jana kwenye mkutano wa ushirikishwaji wa jamii katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori uliofanyika wizarani kwake.

“Uhifadhi kama tunavyoujua, hautaweza kufanikiwa kama kila mtu kwenye nchi hii atafikiria ni kazi ya serikali kuu peke yake.

Na vilevile kama kila mtu atafikiria ni kazi ya wahifadhi peke yao”. alisema Nyalandu kwenye mkutano huo.

Nyalandu alibainisha kuwa, majadiliano hayo, yatakuwa chachu kubwa ya maendeleo katika wizara hiyo huku akiwashukuru wadau hao mbalimbali wakiwemo wanahabari kwa kufika kwao, ili kuangalia suala la uhifadhi kwa mapana yake.

Alisema wakati ujangili wa Tembo nchini umeshamiri sana, wakati umefika kwa watanzania kuhakikisha kwamba wanakomesha hali hiyo ili taifa kuendelea kuwa na wanyama wake.

Alisema mathalani Tembo katika hifadhi ya Selous wamepungua kutoka Tembo 38,975 katika sensa ya mwaka 2009 hadi Tembo 1,384 kwa sensa ya mwaka 2014 na akasema kwa kasi hiyo katika miaka 10 ijayo Tembo Tanzania wataisha kabisa.

“Hili ni muhimu watu wakafahamu, upana wa hivi vita ni mkubwa kiasi gani na watu wanaohusika ni wengi kiasi gani ndani na nje ya nchi," alisema Nyalandu akiongeza kuwa mitandao ya kihalifu imetanda ulimwenguni kote.

Alisema suala la hifadhi halipo kwa wanyama pekee bali lipo katika upana wote na hata katika misitu.

Alisema ili kukabiliana na ukatwaji hovyo wa miti kutoka katika misitu ya miombo wanajipanga kuhakikisha kwamba miombo inayodaiwa kuingizwa nchini kutoka Zambia inakamatwa ili kulinda miombo iliyopo magharibi ya nchi.

Akizungumzia suala la mifugo na mbuga zinazopakana nazo amesema kwamba wanaanda rasimu ya kuhakikisha kwamba kuna mahusiano mazuri kati ya wenye mifugo na hifadhi wakiwa tayari kuyaachia baadhi ya maeneo kwa lengo la kuhakikisha kwamba wafugaji hawaingizi mifugo yao katika hifadhi.

Aidha amesema kwamba wanajipanga namna ya kuhakikisha kwamba hakuna mgongano wa maeneo kati ya wanyama na binadamu na kwamba wanavijiji wanafundishwa namna ya kuishi na wanyama katika maeneo yenye mwingiliano mkubwa.

Aidha alisema kwamba meno ya Tembo kilo 1,763 yalikamatwa mwaka jana na jitihada zinaendelea za kukabiliana na majangili kwa kutanua mtandao wa kiintelejensia ndani na nje.

Alisema kwa sasa wanamsaka raia wa China anayeshutumiwa kutorosha nyara za serikali kwa kushirikiana na jeshi la Polisi la Kimataifa (Interpol).

Kwa nje ya nchi, meno ya Tembo yaliyokamatwa, Kilo 40 katika miji ya Hong Kong, China.
Aidha alisema watuhumiwa 1,711, walikamatwa kuanzia Januari hadi Desemba mwaka jana na kesi zao zinaendelea katika mahakama mbalimbali hapa nchini. Pia silaha 85 zimekamatwa ikiwemo silaha za kivita ambazo walikuwa wakizitumia mbugani.

Alisema ukichanganya na silaha zilizokamatwa kwenye operesheni tokomeza, jumla silaha 1,199 zimekamatwa.

Kwa upande wake, Ali Said Mosee aliyehudhuria mkutano huo kutoka Tanzania Association on Climate Change, alishauri ushirikishaji wa wadau mbalimbali kutatua migogoro kwenye mipaka ya mbuga na pia mgongano wa kimaslahi kati ya hifadhi na wanadamu.

Aidha wadau walishauri Wizara kuhakikisha inapunguza misafara ya wanyama ya kuhamahama kutoka sehemu moja hadi nyingine ikiwemo kwa kuzalisha miti na mazao yanayopendwa na wanyama hao.

“Wanyama wetu wanatakiwa wafanyiwe utafiti na kujua nini Nyati anapendelea kula porini, basi wapande hiyo miti na vyakula vyake kwa ujumla hata kwa Tembo hivyo hivyo.Wapande hiyo miti hapa hapa kwani hata siye binadamu tunavyovyakula tunavyovipenda, naamini hata kwa wanyama ni hivyo hivyo, rai yangu ni kuwa tufanye utafiti na kujua ili kuzuia misafara hii” alisema Ali Said Mosee.

Tanzania inahifadhi za taifa 16 na asilimia 40 ya ardhi ya nchi ni maeneo yaliyohifadhiwa. Kati ya maeneo hayo yaliyohifadhiwa hadi mwezi uliopita mwaka huu 2015, maeneo 19 yanamilikiwa na wananchi na yameshasajiliwa. Pia alisema kwamba kuna mapori ya akiba, 28 nchi nzima.

“Watu wengi wanadhani kwamba misitu yote inamilikiwa na serikali kuu. Ukweli ni kwamba serikali kuu inamiliki asilimia 35 tu ya misitu ya nchi yetu, misitu mingine yote inamilikiwa na vijiji, wilaya na watu binafsi asilimia 7. " alibainisha waziri huyo.

Aliwataka watendaji wa Serikali za mitaa kukabiliana na changamoto ya kutoweka kwa kasi kwa misitu ili taifa lisitumbukie katika jangwa.
 
DSC_0082
DSC_0096
Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu akifafanua mazungumzo na wadau wa mashirika ya kimataifa na asasi za kijamii ukiwa na lengo la ushirikishaji wa jamii katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori uliofanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Mpingo House uliopo Wizara ya Maliasili na Utalii jijini Dar es Salaam.
DSC_0135
Naibu Waziri wa Maliaisli na Utalii, Mahmoud Mgimwa akitoa salamu kwa wadau wa taasisi za kirai. Kushoto Waziri wa Maliasili na Utalii, Mh. Lazaro Nyalandu.
DSC_0124
Mratibu wa Uhakiki wa Ubora kutoka Haki Elimu, Robert Mihayo akitoa maoni kwa Waziri Mh. Nyalandu ambapo amemuomba kushirikisha wadau wa elimu katika kutoa elimu ya uhifadhi wa wanyamapori kuanzia ngazi ya elimu ya msingi ili kuwaanda vijana ambao ni taifa la kesho.
DSC_0110
Mkurugenzi Mtendaji wa Foundation for Civil Society, Francis Kiwanga akishiriki kutoa maoni katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori pamoja na kutokemeza ujangili wa Tembo.
DSC_0105
Mwandishi wa gazeti la Daily News, Diriham Kimathi akiuliza swali kwa Waziri Nyalandu (hayupo pichani).
DSC_0129
Pichani juu na chini ni baadhi ya wadau kutoka asasi za kijamii na mashirika ya kimataifa waliohudhuria mkutano ulioitishwa na Waziri Nyalandu ambao umefanyika jana katika ukumbi wa mikutano wa Mpingo House uliopo ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii.
DSC_0131
DSC_0059
DSC_0005
DSC_0143   DSC_0149  
Waziri Nyalandu akisalimiana na baadhi ya wadau kutoka mashirika ya kimataifa na asasi za kijamii waliohudhuria mkutano huo.
DSC_0158
 
Mdau kutoka Tanzania Association on Climate Change, Ali Said Mosee akitoa maoni yake juu ya kuhusiana na nini kifanyike katika masuala ya uhifadhi wa wanyamapori katika mkutano uliotishwa na Waziri Nyalandu (hayupo pichani).

RAIS MSTAAFU ALI HASSAN MWINYI APENDEZESHA SHEREHE YA CHAUKIDU SILVER SPRING,MARYLAND NCHINI MAREKANI

Meza kuu toka kushoto ni Rais wa CHAUKIDU Prof.Lioba Moshi, Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na Mama Sitti Mwinyi wakuhudhuria sherehe ya Chama cha Ukuzaji wa Kiswahili Duniani. Mhe. Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiwa mgeni rasmi sherehe iliyofanyika Silver Spring, Maryland nchini Marekani siku ya Alhamisi April 23, 2015 na kuhudhuriwa na wadau wa Kiswahili kutoka mataifa mbalimbali wakiwemo Wamarekani wanaozungumuza lugha ya Kiswahili.
Dr. Hamza Mwamoyo mkuu wa idhaa ya Kiswahili Voice of Amerika (VOA) akimsabahi Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi huku wakipata picha ya kumbukumbu wenginine kwenye picha ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na Mama Sitti Mwinyi.
Farida(kulia) wa Farida Catering akiwaelekeza Rais msataafu Ali Hassan Mwinyi, Mama Sitti Mwinyi na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula aina ya vyakula alivyopika katika kuhitimisha sherehe ya CHAUKIDU siku ya Alhamisi April 23, 2015 Silver Spring, Maryland nchini Marekani. Hii ni mara ya pili kwa Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuonja mapishi ya Farida Catering mara ya kwanza ilikua katika shere ya miaka 3 ya Vijimambo iliyofanyika mwaka 2013 Capitol Heights.
Farida akiwaonyesha ustadi wa ukutaji matunda Rais mstaafu Mhe. Ali Hassan Mwinyi, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na Mama Sitti Mwinyi.
Prof. Lioba Moshi akiongea machache ya kumshukuru Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuhudhuria sherehe ya CHAUKIDU tangia mchana na usiku bila kuchoka pia alimshukuru Balozi wa Tanzania nchini Marekani kwa kuwezesha kuja nchini kwa Rais Msataafu aliyependezesha na kunogesha sherehe ya chama chao na baadae alimkaribisha Balozi Liberata Mulamula kuongea machache.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akitoa shukurani zake kwa CHAUKIDU kwa kufanikisha sherehe yao na baadae aliwatambulisha maafisa na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani akiwemo Balozi wa heshima Ahmed Issa na wadau mbalimbali wakiwembo waandishi wa vitabu Kapuya kutoka California na Mzee Safari kutoka Maryland na baadae kumkaribisha Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi kuongea na wadau wa Kiswahili nchini Marekani.
Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiongea na wadau wa Kiswahili katika kuhitimisha sherehe ya CHAUKIDU iliyofanyika siku ya Alhamisi April 23, 2015 Silver Spring, Maryland. Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi mbali na kuwashukuru CHAUKIDU pia alitumia fulsa hiyo kuweka sawa baadhi ya maneno la lugha ya Kiswahili ambayo hukosewa kutamkwa ipasavyo kwa kutoa mfano alisema katika kiswahili kahuta tarehe 1 au tarehe 2 usahihi ni tarehe mosi na tarehe pili huku akitolea mfano kwa lugha ya kiingereza kwamba hata nao hutamka 1st na 2nd mfano mwingine alisema unaposema nawaahidini ni ahadi unayotoa kwa watu wasiokuwepo mbele yako lakini unaposema ninakuahidini ndio sahihi kwa ahadi unayotoa kwa watu waliopo mbele yako na mengine mengi.
Kamati nzima ya CHAUKIDU ikipata picha ya kumbukumbu 

SHEREHE YA CHAUKIDU YA MCHANA CHUO CHA HOWARD YAFANA

Rais wa CHAUKIDU Prof Lioba Moshi watatu toka kushoto akimkaribisha Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi mara tu alipowasili kama mgeni rasmi chuo kikuu cha Howard Washington, DC katika sherehe ya chama cha ukuzaji wa Kiswahili Duniani siku ya Alhamisi April 23, 2015 kulia ni Prof Venessa White Jackson 
 Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akimtambulisha mkewe mama Sitti Mwinyi kwa mwenyeji wao Prof Lioba Moshi pia na yeye akimtambulisha mama Sitti Mwinyi kwa Prof Venessa White Jackson kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula .  
Prof Lioba Moshi Rais CHAUKIDU akielezea historia fupi ya CHAUKIDU na baadae kumkaribisha Rais mstaafu kuongea na wadau wa Kiswahili waliohudhuria sherehe ya chama hicho iliyofanyika siku ya Alhamisi April 23, 2015 katika chuo kikuu cha Howard kilichopo Washington, DC.

Ms Mamburi Lyambaya (kushoto) akimtambulisha Prof Venessa White Jackon na yeye kuwasalimia wadau wa Kiswahili waliohudhuria sherehe ya CHAUKIDU iliyofanyika katika chuo kikuu cha Howard Washington, DC.


Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akiwa meza kuu kulia ni prof Venessa White Jackson '

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi akitoa hotuba kwa kuwashukuru CHAUKIDU kwa kummpa mwaliko na kwa kuwa yeye ni mdau mkubwa wa lugha ya Kiswahili hakusita kukubali kuja kujumuika nao pia Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi aliwapongeza kwa kuitangaza lugha ya Kiswahili nchini Marekani.

Kutoka kushoto ni Balozi wa Umoja wa Afrika Mhe. Amina Salum Ali, Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula na mama Sitti Mwinyi wakifuatilia hotuba ya Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi.

Wanafunzi wa chuo kikuu cha Howard wakiimba nyimbo za Kiswahili kwa ustadi mkubwa kuliko wastajabisha Watanzania na wadau wengine wa Kiswahili.

Wadau wa Kiswahili wakifuatilia sherehe ya CHAUKIDU