Pages

KAPIPI TV

Friday, March 27, 2015

ASILIMIA 40 YA WANAWAKE Z’BAR WANAISHI MAISHA DUNI

DSC_0081
Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi (aliyefunikwa mwamvuli) akiwasili kwenye sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicious Women Group na kufanyika ndani ya ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel mwishoni mwa wiki.

Na Mwandishi wetu, Zanzibar
UTAFITI uliofanywa na taasisi ya wanawake nchini Zanzibar ya Zanzibalicious Women umeonyesha kuwa asilimia 40 ya wanawake Zanzibar, wanaishi katika mazingira duni ya umasikini kwa kutojitambua na kukosa elimu ya uelewa jinsi ya kukabiliana na mazingira waliyomo.

Akisoma risala siku ya wanawake mbele ya mgeni rasmi mke wa rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi , Mama Mwanamwema Shein , katika siku ya wanawake hafla iliyofanyika hoteli ya Bwawani, Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Shekha Hilal alisema hali hiyo ni changamoto kubwa na sasa kunatafutwa namna ya kumfikia mwanamke huyu ambaye ameshagota katika jamii yetu.

“Mama Shein asilimia hii ni kubwa saana, na sisi kama wanawake ambao tayari tumejaaliwa elimu na tunajitambua, ikiwa ni pamoja na tayari tumepiga hatua kimaendeleo katika nyanja mbalimbali, tumeguswa sana sana na suala hili.” Alisema Shekha.

Zanzibalicious ni umoja wa wanawake wanaoishi Zanzibar,ulioanzishwa mwaka 2011,na kusajiliwa rasmi mwaka 2013, ikiambatana na uzinduzi uliofanyika tarehe 28 Machi 2014.
DSC_0227
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein akiwasili kwenye sherehe ya siku ya Wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicous Women Group mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Salama, Bwawani Hotel.
Mweka hazina huyo alisema kwamba wanajiuliza maswali mengi kama mwanamke huyo elimu ya kujikwamua imemfikia au kama kuna jitihada zozote za kumfikishia elimu hiyo.
“Je hili ni jukumu la serikali peke yake? Au sisi tunatakiwa tujumuike na serikali? mheshimiwa mgeni rasmi tumeona ya kwamba tuungane pamoja na serikali katika kutekeleza suala hili.” Alisema Shekha akielezea nia ya taasisi hiyo ya kuondoa umaskini miongoni mwa wanawake nchini Zanzibar.
Alisema taasisi yao inajipanga kutoa elimu za aina mbili ili awali kumuwezesha kujikimu kupitia ujasiriamali, kwa kumpatia elimu kwa vitendo,kwa mfano:-ushonaji,ufugaji na utengenezaji wa bidhaa mbali mbali na pili kumtoa katika hali ya upweke ili elimu atakayopata imfikishe kwenye mifuko mbali mbali pamoja na mfuko wa Rais Dk. Ali Mohammed Shein .
Alisema katika program hiyo wanatarajia baada ya miaka 2 wanawake 100 watakuwa wanajitegemea wenyewe na kuwa mabalozi katika kuelimisha wanawake wengine zaidi.
DSC_0471
Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein akisoma hotuba wakati wa sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyoandaliwa na Zanzibalicous Women Group na kufanyika ndani ukumbi wa Salama, Bwawani hoteli mwishoni mwa wiki. Kushoto ni Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi akifuatiwa na Mwenyekiti mstaafu wa Zanzibalicious Women Group, Bi. Ummukulthum Ansel.
“Na kama kila mwanamke akiweza kuelimisha wanawake katika kaya yake ,baada ya miaka kadhaa, Zanzibar itakuwa na wanawake walioweza kujikomboa katika dimbwi hili la kuishi maisha duni.” Alisema.
Akizungumzia mafanikio ya asasi hiyo alisema kwamba imefanikiwa kutoa elimu na kuwawezesha kina mama kuunda vikundi vidogo vidogo vya maendeleo kwa kuanzisha miradi mbalimbali, kwa mfano kina mama wa Chaani na Matemwe.
Aidha imetoa misaada ya hali na mali kwa waathirika wa madawa ya kulevya ikiwa ni moja ya kumkwamua mwanamke na kutoa misaada mbali mbali kwa wanawake wasiojiweza ikiwemo hospital kuu ya Mnazi mmoja na kina mama wajane.
Alisema pamoja na mafanikio hayo bado wanawake wanakabiliwa na changamoto za ndoa za utotoni, uzazi salama, ukatili wa kijinsia,mfumo dume, ubaguzi na mimba za utotoni.
Mhe.Mgeni rasmi, Umoja huu umekuwa ukiendesha shughuli zote tokea mwaka 2011 kwa kutegemea michango yetu sisi binafsi.
DSC_0314
Baadhi ya wakinama waliohudhuria sherehe hiyo wakionekana kufurahishwa na hotuba ya Mke wa Rais wa Zanzibar (hayupo pichani).
Changamoto hii imesababisha kutokutimiza kwa malengo yetu kwa muda tulioupanga kutokana na kukosa fedha za kutosheleza utekelezaji wa malengo hayo.
Akijibu risala hiyo Mke wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mama Mwanamwema Shein, ameikumbusha jamii kuunganisha nguvu zao kuwakomboa wanawake kujiendeleza kimaisha na kujiongezea kipato.
Alisema hatua hiyo itaongeza kasi ya kuimarisha ustawi wa familia na jamii hususan wanawake wanaoishi vijijini ambao wanakabiliwa na changamoto zaidi.
Alisema sherehe ya siku ya wanawake duniani inakuwa na maana zaidi kama juhudi zitafanyika kuangalia changamoto na kujipanga kuzifanyia kazi.
“Rai yangu ni kuwa tuwazingatie zaidi akina mama wanaoishi vijijini na wenye mahitaji maalum kutokana na kukosa fursa kama hizo za kuwaendeleza kimaisha”, alisisitiza.
DSC_0344
Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Bi. Shekha Hilal akisoma risala kwa mgeni rasmi Mke wa Rais wa Zanzibar (hayupo pichani) Kulia ni Mwenyekiti wa Zanzibalicous Women Group, Bi. Evelyne Wilson.
Aidha, aliongeza kuwa wanawake ni jeshi kubwa ambalo likiandaliwa vyema linaweza kushinda katika mapambano yanayokusudiwa huku akisisitza mshikamano ili kufikia malengo yanayowekwa.
Akizungumzia ujumbe wa sherehe hizo ambao ni kuhamasisha hatua mathubuti kumwendeleza na kumtambua mwanamke, alitoa rai kwa wanawake kushirikiana na serikali katika kampeni za kupambana na madhila wanayokabiliana nayo ikiwa ni pamoja na ukatili wa watoto na wanawake.
Kuhusu uzoefu wake katika maisha na malezi ya watoto, alisema amebahatika kupata watoto 11 ambao amewalea katika mazingira mbalimbali ikiwa ni kwenda na kurudi kazini na kuwa pekee huku mumewe akiwa safarini kikazi.
Aidha, aliwataka wanawake kuwa wastahamilivu katika malezi ya watoto hasa watoto Njiti ambao huzaliwa kabla ya kufikisha muda.
Hata hivyo aliwaonya wanawake wanaojali kujiremba na kuwa sahau watoto na kukumbusha kwa ‘watoto ni wageni’ kwamba wanahitaji matunzo na ukarimu mkubwa kutoka kwa wazazi wao.
IMG_6571
Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akizindua Mfuko wa Zanzibalicious Women Group kwa kuchangia shilingi milioni tano, wakati wa maadhimisho ya sherehe ya wanawake duniani visiwani Zanzibar yaliyoandaliwa na Zanzibalicious Women Group na kufanyika katika ukumbi wa Salama uliopo Bwawani Hotel Zanzibar. Kulia ni Mwenyekiti wa Zanzibalicious Women Group, Bi Evelyne Wilson Baruti.
DSC_0082
Mweka hazina wa Zanzibalicious Women Group, Shekha Hilal akinakili majina ya watu waliokuwa wakichangia kwenye harambe ya mfuko wa Zanzibalicous Women Group uliozinduliwa rasmi na Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein (hayupo pichani).
DSC_0074
Mbunifu nguli wa mavazi Mama wa mitindo, Asia Idarous akinadi moja ya nguo alizotengeneza kwa ajili ya kuchangia mfuko wa Zanzibalicious Women Group.
DSC_0075
Mke wa Naibu Waziri wa Afya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bi. Zakhia Kombo akitangaza dau la kununua nguo hiyo iliyokuwa ikinadiwa kwenye harambe ya mfuko wa ZWG iliyozinduliwa na Mama Mwanamwema Shein.
DSC_0091
Meza kuu kwenye picha ya pamoja na Zanzibalicous Women Group.
Unaweza kutembelea mtandao wao na kuona shughuli mbalimbali walizozifanya hapa http://www.zanzibalicious.org/
DSC_0388
Mmoja wa wadhamini ZANLINK wanaotoa udhamini kwa Zanzibalicious Women Group wakisikiliza kwa makini yaliyokuwa yakijiri ukumbini hapo. Kwa picha zaidi bofya link hii

JEMBE FM YA MWANZA YAPEWA LESENI

DSC_0644
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma akizungumza kwenye hafla fupi ya kukabidhi leseni kwa redio ya Jembe FM ya jijini Mwanza kwenye ofisi za makao makuu ya TCRA jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).
Na Mwandishi wetu
MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Profesa John Nkoma ametaka matumizi sahihi ya masafa ya radio yanayatumiwa kurusha vipindi vya radio kwa ajili ya maendeleo ya umma.
Kauli hiyo ameitoa jana wakati akikabidhi leseni kwa radio Jembe FM.
Alisema matumizi yasiyo sahihi yatasababisha mamlaka hiyo kunyang’anya leseni walioitoa kwa ajili ya maslahi ya taifa.
Alisema pamoja na haja ya kushiriki katika ushindani, kituo hicho kipya kinatakiwa kufuata masharti ya utangazaji ambayo yamo katika leseni waliyoiomba.
Alisema radio hiyo ya Mwanza inaongeza ushindani katika eneo hilo katika jumla ya radio FM 12 zinazosikika mjini humo, radio za kitaifa saba, za kikanda 11 na radio ya jamii 1.
Aliwataka kuwa waangalifu na kufuata kanuni za kitaalamua kufanyakazi wanasotahili za kuelimisha na kuburudisha.
DSC_0650
Alisema si radio tu ambayo ina nguvu ndiyo inayoweza kuhimili ushindani lakini pia ufuataji wa kanuni na maadili katika utekelezaji wa majukumu yao.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Jembe FM, Dk. Sebastian Ndege amesema kwamba wameanzisha radio hiyo kwa lengo la zaidi ya kuburudisha na kuelimisha bali kusaidia vijana kushika hatamu na kujitengenezea uwezo wa ajira.
Alisema kwamba ili kuhakikisha kwamba wanafanyakazi kitaaluma wameajiri watu ambao wamesomea kazi husika ili kuhakikisha kwamba hawaendi kinyume na leseni yao.
Alisema kwamba wanaamini kwamba wana nafasi kubwa ya kujaza mapengo ambayo yapo katika urushaji wa matangazo kwa sasa ili kuhudumia mji wa Mwanza ambao unakua kwa kasi kwa sasa.
DSC_0676
Mkurugenzi wa sheria wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA), Fortunata Mdachi (kushoto) akisisitiza jambo kwa uongozi wa JEMBE FM wakati wa hafla ya kukabidhi leseni kwa uongozi huo iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam makao makuu ya ofisi za TCRA.
Alisema vipindi vyao vimezingatia haja ya jamii katika uchumi, elimu na afya.
Aidha amesema kwamba wanategemea kuwa na vipindi vizuri zaidi hasa kutokana na na uzoefu waliokuwa nao hasa wa uandaaji wa njia ya panda.
Jembe FM inamilikiwa na Jembe Media Limited.
DSC_0669
Mkurugenzi Mkuu wa Jembe FM Dk Sebastian Ndege (wa kwanza kushoto) na uongozi wa juu kabisa wa Jembe Media Limited wakimsikiliza kwa makini kabisa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA (hayupo pichani) wakati wa hafla fupi ya kukabidhiwa leseni rasmi ya kurusha matangazo ya redio ya JEMBE FM ya jijini Mwanza.
DSC_0655
Baadhi ya wawakilishi wa kampuni ya Ndege Insurance inayomilikiwa na Dk. Sebastian Ndege waliojumuika kwenye hafla hiyo fupi.
DSC_0665
Maofisa mbalimbali kutoka Mamlaka ya mawasiliano Tanzania (TCRA) wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo.
DSC_0683
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma (kulia) akimkabidhi rasmi leseni ya kurusha matangazo ya redio ya JEMBE FM ya jijini Mwanza, Mkurugenzi Mkuu wa Jembe FM, Dk Sebastian Ndege (katikati) katika hafla fupi iliyofanyika makao makuu ya ofisi za TCRA jijini Dar. Kushoto ni Mkurugenzi wa sheria wa Mamlaka ya Mawasiliano Nchini (TCRA), Fortunata Mdachi.
DSC_0712
Mkurugenzi Mkuu wa Jembe FM, Dk Sebastian Ndege akitoa neno la shukrani ambapo pia maeahidi kuwa atafuata masharti na kanuni zote zilizowekwa na mamlaka hiyo.
DSC_0725
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma (wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa juu kabisa wa Jembe Media Limited. Kutoka kushoto ni Mwanasheria wa Jembe Media Ltd. Justine Ndege, Mkurugenzi Mkuu wa Jembe FM, Dk Sebastian Ndege pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Jembe Media Ltd, Renata Ndege.
DSC_0733
Mkurugenzi Mkuu wa Jembe FM, Dk Sebastian Ndege na Mwanasheria wa Jembe Media Ltd. Justine Ndege wakionyesha leseni hiyo iliyoambatanishwa na miongozi ya Mamlaka ya Mawasiliano ya TCRA kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) waliohudhuria hafla hiyo.
DSC_0743

TAHARIRI: TABIA HII YA WAUZA MITUMBA SOKO LA MCHIKICHINI NI UDHALILISHAJI WA KIJINSIA

Baadhi ya wateja wa nguo wakichagua nguo kwenye soko la Mchikichini
Baadhi ya wateja wa nguo wakichagua nguo kwenye soko la Mchikichini jijini Dar es Salaam.

Na Andrew Chale wa Modewji blog
Miongoni mwa mambo ya aibu katika jamii ni pamoja na masuala ya udhalilishaji wa kijinsia ukiwemo ule wa maungoni hasa kwa wanawake.

Kwa muda mrefu mtandao huu umekuwa ukifuatilia vitendo hivyo vibaya kwa jamii vinavyofanywa na watu waliokosa ustaarabu hasa jamii ya vijana katika maeneo ya mikusanyiko ya watu wengi karibu maeneo mengi ikiwemo jiji la Dar es Salaam.
Miongoni mwa eneo linaloongoza kwa kuwadhalilisha wanawake ni eneo la soko la Mchikichini lililopo Ilala Mkoa wa Dar es Salaam.

Mtandao huu umekuwa ukishuhudia vitendo hivyo vibaya kwa jamii ambapo wengi wa vijana wamekuwa wakifanya kwa makusudi kuwadhalilisha wanawake hasa wasichana wadogo kwa kuwashika maungoni (makalio, kifua/maziwa) huku wakiwalazimisha kununua bidhaa zao.

Vitendo hivi vimekuwa ni kama mchezo wa kawaida kwani vijana hao wamekuwa wakiendeleza hali hiyo kwa muda mrefu sasa huku wasichana/wakike hao wanaofanyiwa vitendo hivyo wakiwa hawana wa la kufanya, Mtandao huu tunasema huo ni udhalilishaji na unatakiwa kuchukuliwa hatua za haraka kukomeshwa kwani unakiuka maadili na utu wa mwanamke.
ka - kobe 528
Tunatambua ipo mamlaka husika zinazoweza kulichukulia hatua suala hili basi kama zipo zianze sasa kwani udhalilishaji huu huko mbele unaweza kuleta madhara makubwa kwa mtendewa na hata anayetenda kwani akiachwa sasa baadae anaweza kufanya tukio kubwa na likafumbiwa macho ikiwemo kubaka.

Nachelea kuamini kama vijana hawa wanafanya hivi kwa kujiamini ama kuna nguvu ya msukumo nyuma yake? Kipindi cha nyuma sote tumekuwa tukishuhudia vijana hao wakiwachania nguo wanawake waliokuwa wakivaa vimini waliokuwa wakipita katikati ya mitaa ya Kariakoo wakati huo huo wamesahau kuwa nguo hizo wamewauzia wao, tukiacha hilo pia wapo hawa Makondakta wa daladala nao ni miongoni mwa watu wanaoongoza kufanya vitendo vya kidhalilishaji wanawake.

Mtandao huu umeweza kuliona hilo kwa upande wa Makondakta wa Daladala nyingi hasa nyakati za abiria wa kike anapopanda hatua ya kwanza wao wanapeleka mkono kwenye ‘Makalio’ ya Mwanamke na kumvutia ndani ya daladala, yaani kama sapoti ya kumuingiza ndani.

Kondakta anafanya hivyo wakati huo amekaa mlangoni mwa daladala yake, lakini anapopanda mwanaume usogea ndani ama hushuka chini bila hata ya kumshika, lakini akipanda Mwanamke tu utakuta Konda anamshika makalio kuona kwamba ni jambo la kawaida, Hivyo ni wakati sasa wa kubadilika jamani vitu vingine hivi ni kushusha utu wa mwanamke hivyo tubadilike na tuchukue hatua, Asante.

Wednesday, March 25, 2015

MO DEWJI FOUNDATION YAMPATIA BAISKELI KIJANA ALIYEPOOZA MGUU

DSC_0370
Mtendaji Mkuu wa MO DEWJI FOUNDATION, Gerald Mgesi David akimkabidhi rasmi kijana Paulo Ezekiel (23) msaada wa baiskeli ya magurudumu matatu (tricycle) itakayomsaidia katika kutembelea kwenye shughuli zake za kila siku.

Na Andrew Chale wa Modewji blog
Taasisi ya MO DEWJI FOUNDATION inayojishughulisha na miradi ya kusaidia jamii Tanzania katika masuala mbalimbali ikiwemo Afya, elimu na maji mwishoni mwa wiki imeweza kumpatia kijana Paulo Ezekiel (23) msaada wa baiskeli ya magurudumu matatu (tricycle) itakayomsaidia katika kutembelea kwenye shughuli zake za kila siku.

Tukio hilo la makabidhiano limefanyika katika ofisi za Mo Dewji Foundation jijini Dar es Salaam ambapo Mtendaji Mkuu wa MO DEWJI FOUNDATION, Gerald Mgesi David alikabidhi msaada huo kwa kijana Paulo Ezekieli

Akizungumza na Modewjiblog, Mtendaji mkuu wa Mo Dewji Foundation amesema, waliguswa na usumbufu aliokuwa anaupata kijana na hivyo kuona ni vyema kumsaidia ili aweze kumudu kuendesha shughuli zake za kila siku.

Mo Dewji Foundation imejikita katika kutekeleza miradi ya kijamii ambayo inalenga kusaidia jamii ya kitanzania katika kujikwamua katika hali ya umaskini na kuinua kipato.
DSC_0399
Kijana Paulo Ezekiel (kulia) akiwa kwenye mahojiano na mwandishi wa habari wa modewjiblog, Andrew Chale.
Kijana Paulo Ezekiel:

Kwa upande wake, kijana Paulo Ezekiel ambaye muda mfupi baada ya kukabidhiwa baiskeli hiyo, alifanya mahojiano maalum na mtandao huu ambapo alieza kuwa, tatizohilo la kulemaa mguu, lilimtokea ghafla wakati yupo mitaa ya Kariakoo kwenye shughuli zake binafsi.

“Nakumbuka nilikuwa kwenye matembezi maeneo ya Kariakoo, ghafla nilipata kuhisi hali ya kupooza mguu mmoja wa kulia na kupoteza nguvu wasamaria wema waliniokota na kunipeleka Muhimbili” anaeleza Paulo Ezekiel.

Alieleza kuwa, alikaa Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa muda wa miezi sita huku akipatiwa matibabu na baadae aliruhusiwa.

“Niliporuhusiwa hali ilikuwa ngumu sana. Kwani nilianza kuomba omba kwa watu msaada ikiwemo kifaa cha kuniwezesha kunisaidia kutembelea. Kule Muhimbili nilikuwa natumia baiskeli kutembelea hivyo nilivyoruhusiwa iliniwia vigumu sana kutumia vifaa vya ulemavu ikiwemo haya magongo.

Kuna siku katika kuomba omba. Nilikutana na mtu mmoja ambaye alinielekeza kwa Mh. Dewji. Nilipofika kwake msaidizi wake alinitaka nifuatilia kuona kama watafanikisha kwani tayari bajeti ilikuwa imeshafungwa hadi kipindi kingine” alieleza Paulo Ezekiel.
DSC_0373
Hata hivyo Paulo Ezekiel alibainisha kuwa, wakati yupo nyumbani kwao, alipigiwa simu juu ya kuitwa kukabidhiwa baiskeli hiyo.

“Sikuamini kama ningeweza kupata msaada huu. Hadi nilipofika hapa kukabidhiwa namshukuru Mungu pia namuombea kwa Mungu Mh. Mohammed Dewji kwa msaada wake, kwani simjui na wala hanijui..Ilikuwa ni kama bahati kufika katika ofisi yake na kuomba msaada huu asante sana na namuombea maisha marefu Dewji na familia yake, wafanyakazi wake wote popote pale kwani kuniwezesha mimi ni ubinadamu mkubwa sana” alimalizia kijana Paulo Ezekiel.

Paulo Ezekiel anabainisha kuwa, ilikua vigumu sana kwa yeye kutembelea magongo siku za mwanzoni ambapo anasema hakuwahi kutegemea kama siku moja atakuja kuwa mlemavu.

“Hujafa, hujaumbika naamini hilo, kwani awali nilikuwa najitafutia riziki zangu za kujikimu kimaisha lakini nilipopata tatizo hili la kupooza mguu na kulemaa ndoto zangu zote zimeyeyuka ila sijakata tama” Hivi ndivyo anavyomalizia Paulo Ezekiel ambaye anaishi Mbagala, Temeke Jijini Dar es Salaam, Tanzania.
DSC_0397
Mwandishi wa habari wa modewjiblog, Andrew Chale (kushoto) akifanya mahojiano na Paulo Ezekiel mara baada ya kukabidhi msaada wa baiskeli ya magudumu matatu.

Kijana huyu awali alikua akifanya shughuli za kutafsiri Lugha kwa wageni wanaokuja kununua bidhaa kwenye maduka ya Kariakoo na Bandari ya Dar es Salaam hasa wafanyabiashara wanaotoka Congo, Rwanda, Zambia, Malawi, Burundi na maeneo mbalimbali.

Paulo Ezekiel ni mtoto wa pili kati ya watoto nne, anatokea Mkoa wa Kilimanjaro na kabila lake ni Mchaga.
DSC_0317-1024x682
MO DEWJI FOUNDATION: Ni taasisi iliyoanzishwa na Mbunge wa Singida Mjini (CCM) na mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji maarufu ‘MO’ (pichani) ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya kiongozi bora aliyejitolea kwa kiasi kikubwa katika jamii na kuleta mabadiliko Afrika kwa mwaka 2014.

Tuzo hiyo aliyotunukiwa MO iitwayo African Philanthropist of the year Award 2014, Ilitolewa na jarida la uongozi la Uingereza, jijini Dubai wakati wa Jukwaa la Viongozi wa Afrika.

Kabla ya kukabidhiwa tuzo hiyo, sifa kuu aliyokuwa nayo MO kama alivyofafanua wakati wa kukabidhiwa tuzo hiyo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa jarida hilo, Dk Ken Giami alisema wataalamu waelekezi walimchagua Dewji kuwa mshindi kutokana na: Uongozi bora katika Kampuni yake ya Mohammed Enterprises (MeTL GROUP) Pia kigezo kingine kilichompa ushindi ni namna anavyojihusisha na kazi mbalimbali za kijamii.

Pia Mchango wa MO katika elimu ni sehemu kubwa ya mafanikio yake hususan kwa kuendeleza ujenzi wa shule mbili hadi 12, pamoja na kujitolea kiasi cha zaidi ya Sh520 milioni katika kuendeleza sekta hiyo ya elimu ndani ya jimbo lake hilo la Ubunge la Singida Mjini.

MO pia amekuwa akisaidia sekta ya afya kwa ushirikiano na Taasisi ya Bilal Muslim Mission ya Tanzania kwa kuwaleta madaktari waliowafanyia upasuaji wagonjwa wa macho na 179 kupata miwani, kusambaza maji safi na salama kwa kuchimba visima vingi vya maji ndani ya jimbo na n.k.

Kwa sasa MO ndie Bilionea kijana Afrika kwa mujibu wa jarida la Forbes. Unaweza kusoma zaidi kupitia http://www.forbes.com/profile/mohammed-dewji/

Kwa hali hiyo pia Dewji ameingia katika orodha ya Philanthropist duniani pia waweza kuona watu wengine waliotunukiwa tuzo kama hiyo kupitia hapa: http://en.wikipedia.org/wiki/List_of_philanthropists
Msomaji wetu unaendelea kuperuzi mtandao wako wa Modewji blog, tutakuletea makala maalum juu ya tatizo hili la kupooza ghafla kwa viungo hadi kusababishia kilema. Endelea kuwa nasi. Asante pia waweza kutuma maoni yako kupitia hapo chini ndani ya mtandao huu ama kupitia simu 0719076376 au 0689858799 au email info@modewjiblog.com

2 DAY FINANCE FOR NON FINANCE MANAGERS TRAINING BY PEOPLE POWER

11079613_931612566871198_4439145404160629075_n
Join our 2-day workshop to acquire greater confidence and working knowledge of important finance concepts.
When: 29th & 30th April, 2015, Where: The Colosseum, DSM For further details and registration, visit www.peoplepower.co.tz (click on 'Finance for Non Finance Managers') or call us on +255-752-124-124

Tuesday, March 24, 2015

WALIONG’ARA RED CARPET KWENYE SHEREHE YA SIKU YA WANAWAKE ZANZIBAR

Zifuatazo ni picha za matukio mbalimbali kwenye red carpet wakati wa sherehe ya siku ya wanawake duniani iliyowakutanisha wanawake kutoka kila kona ya visiwani Zanzibar ambayo iliandaliwa na Kikundi cha Wanawake cha Zanzibalicious na kufanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya hoteli ya Bwawani.
DSC_0148
DSC_0099
DSC_0095
Mbunifu wa mavazi kutoka bara Mama wa mitindo Asia Idarous (kushoto) akipozi na mbunifu wa mavazi kutoka visiwani Zanzibar Matilda Ishungisa wa Malty design.
DSC_0092
DSC_0106
Makamu mwenyekiti wa kikundi cha Wanawake wa Zanzibalicious, Zaning'ha Otembo.
DSC_0109
DSC_0111
DSC_0055
Mwenyekiti wa kikundi cha Wanawake wa Zanzibalicious Bi. Evelyne Wilson.
DSC_0057
DSC_0034
DSC_0035
DSC_0041
DSC_0043
DSC_0045
DSC_0052
Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe Thuwaiba Kisasi.
DSC_0066
Wanaume nao hawakubaki nyuma kutoa sapoti kwa wanawake.
DSC_0113
Mama wa mitindo Asia Idarous aking'ara kwenye red carpet.
DSC_0119
DSC_0125
DSC_0128
Kutoka kushoto ni Make up artist Sada, Mama wa mitindo Asia Idarous na MC wa sherehe ya siku ya wanawake duniani visiwani Zanzibar, Mishi Bomba ambaye pia ni mtangazaji wa Magic FM.
DSC_0131
DSC_0134
DSC_0139
DSC_0141
DSC_0143
DSC_0155
DSC_0162
Mke wa Naibu Waziri wa Afya serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bi. Zakhia Kombo (kulia) akiwa na Mama wa mitindo Asia Idarous. Kwa picha zaidi bofya link hii