Monday, March 23, 2015
WAZIRI LUKUVI AFUNGUA NYUMBA ZA NHC MRARA BABATI
Sunday, March 22, 2015
TANZANIA CHILDREN'S PROJECT YAFANYA HARAMBEE KUSAIDIA WATOTO TANZANIA COLUMBIA,MARYLAND
Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula akihudhuria harambee ya Tanzania Children's Project inayoshughulisha na miradi ya afya na elimu Tanzania iliyofanyika siku ya Jumamosi March 21, 2015 Columbia, Maryland. Kulia ni Timothy Lynch ambaye ni Rais wa NGO hiyo, Mhe. Balozi Liberata Mulamula aliongozana na Afisa wa Ubalozi Switebert Mkama(pichani kushoto)
Rais wa Tanzania Children's Project Bwn. Timothy Lynch katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Liberata Mulamula.
Wadau mbalimbali waliohudhuria harambee ya Tanzania Children's Project iliyofanyika siku ya Jumamosi March 21, 2015 Columbia, Maryland nchini Marekani.
picha ya pamoja
Picha ya pamoja
Kikundi cha muziki kikitoa burudani.
Saturday, March 21, 2015
ZIARA YA WAZIRI WA ARDHI MH. WILLIAM LUKUVI BABATI MKOANI MANYARA
Mkuu wa mkoa wa Manyara ,Mhe.Joel Nkaya Bendera akizungumza katika kikao cha viongozi wa wilaya zote za mkoa huo kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Babati,kushoto ni Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mhe.William Lukuvi na kulia ni Mkuu wa wilaya ya Babati,Crispin Meela.Mhe.Bendera amesisitiza nidhamu ya kazi katika kuhudumia wananchi na ameapa kuwaondoa watendaji wabovu mkoani humo.
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mhe.William Lukuvi akizungumza katika kikao cha viongozi wa wilaya zote za mkoa wa Manyara kilichofanyika ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Babati.Ameuagiza uongozi wa mkoa huo kumaliza migogoro ya ardhi ifikapo mwezi Mei mwaka huu.
Mratibu wa Tume ya Waziri Mkuu ya kuhakiki na kuweka mipaka kwenye maeneo yenye migogoro ya ardhi mkoani Manyara,ambaye pia ni Mrasimu Ramani Mwandamizi,Bw.Benedict Mugambi akitoa maelezo ya hatua waliyofikia katika kuweka mipaka mkoani Manyara na kusema kuwa migogoro mingi ya mipaka inasababishwa na wanasiasa. Baadhi ya watendaji wa sekta ya Ardhi Kanda ya Kaskazini na baadhi ya waheshimiwa wabunge akiwemo Mbunge wa Kiteto,Benedct Ole Nangoro na Mbunge wa Viti Maalum,Pauline Gekul wakifatilia maelekezo ya Mhe Lukuvi alipozungumza na watendaji wa mkoa wa Manyara jana.
Wananchi wa mkoa wa Manyara wakimsikiliza Waziri wa Ardhi(hayupo pichani)alipokutana nao kusikiliza kero za migogoro ya ardhi inayosababishwa na watendaji wa sekta hiyo kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Babati.
Wananchi wa mkoa wa Manyara wakipeana maelekezo yaliyotolewa na Waziri wa Ardhi ya namna ya kuwasilisha malalamiko yao kwa maandishi alipokutana nao kusikiliza kero za migogoro ya ardhi inayosababishwa na watendaji wa sekta hiyo kwenye ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Babati.
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mhe.William Lukuvi akizungumza na wananchi wa mji wa Babati waliojitokeza kuwasilisha kero zao zinahusu migogoro ya ardhi.Kikao hicho kilihudhuriwa pia na wabunge wa mkoa wa Manyara.
Baadhi ya watendaji wa wizara ya ardhi wakiratibu malalamiko ya wananchi katika kikao kilichofanyika ofisi za halmashauri ya wilaya ya Babati,mkoa wa Manyara. Katibu Tawala wa mkoa wa Manyara,Mhandisi Omar Chambo akisoma taarifa ya migogoro ya ardhi mkoani humo kwa Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Mhe.William Vangimembe Lukuvi kwenye ziara yake ya kusikiliza kero za ardhi.
Friday, March 20, 2015
KINANA AENDELEA NA ZIARA YAKE MKOANI ARUSHA
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kugonga kokoto pamoja na akina mama wajasiriamali katika kata ya Elerai mjini Arusha wakati alipowatembelea na kukagua shughuli zao, ambapo aliwaambia "Asiwasumbue mtu wala kuwaambieni muondoke kwani ninawafahamu kwa muda mrefu toka nikiwa Mbunge wa jimbo hili la Arusha mjini miaka ya nyuma", aliwaagiza viongozi wa CCM wa kata hiyo kutojiingiza hata kidogo na kuleta mgogoro na wananchi hao ambao wanajitafutia rizki katika kazi yao hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana yuko katika ziara ya kikazi ya mkoa wa Arusha akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali ya CCM na kuhimiza uhai wa Chama Cha Mapinduzi CCM akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-ARUSHA)Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kuchimba mfereji wa kupitisha mabomba ya maji katika mradi wa maji kata ya Olmot Olkaryan jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kufungua maji ya bomba katika mradi wa maji kata ya Olmot Olkaryan jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kuchimba mfereji wakati alipokagua ujenzi wa barabara ya Sombetini kwa Mromboo jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi wa Sombetini kwa Mrombo mara baada ya kukagua barabara hiyo jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi mbalimbali jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifungua shina la wakereketwa la Sakina kwa Shamsi Arusha Raha jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wa pili kutoka kushoto akiongozana na Nape Nnauye na viongozi wa mkoa na wilaya ya Arusha wakati akielekea kutembelea soko la Kirombero jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana wakati alipowasili katika soko la Kilombero jijini Arusha. Kada wa CCM Viola naye akimwaga maneno ya sumu wakati wa mkutano wa katibu Mkuu wa Ndugu Abdulrahman Kinana na wafanya biashara wa soko la Kilombero jijini Arusha. Nape Nnauye akizungumza na umati wa wafanyabiashara na baadhi ya wananchi mbele ya jengo la Soko la Kilombero jijini Arusha. Baadhi ya wafanyabiashara na wananchi wakiwa katika mkutano huo. Kiongozi wa wafanyabiashara wa soko la Kilombero jijini Arusha akisoma risala kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana huku Nape Nnauye akiwa amemshikia kipaza sauti. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi alipowasili katika soko la Kilombero jijini Arusha. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi katika kata ya Remala Arusha kulia ni Diwani wa kata hiyo Bw.Karim Mushi. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikabidhi pikipiki Mwenyekiti wa kikundi cha Vijana Maendeleo Group Peter Samwel iliyotolewa na diwani wa kata ya Remala Bw. karim Mushi kulia. Mwenyekiti wa kikundi cha Vijana Maendeleo Group Peter Samwel akijaribu kuendesha pikipiki mara baada ya kukabidhiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pikipiki hiyo imetolewa kwa kikundi hicho na diwani wa kata ya Remala Bw. Karimu Mushi