Sunday, October 19, 2014
ZOEZI LA KIJESHI USHIRIKIANO IMARA BURUNDI 2014
Brigedia Jenerali Joseph
Chengelela (kushoto)akimkabidhi bendera ya Afrika Mashariki msaidizi wa
zoezi mara baada ya kukabidhiwa kutoka kwa mgeni rasmi hayupo pichani
siku ya ufunguzi wa zoezi USHIRIKIANO IMARA 2014-BURUNDI.
Meja Jenerali James Mwakibolwa wa
nne kulia akiwa na Brigedia Jenerali Joseph Chengelela wa tano kulia na
Mwambata wa JWTZ nchini Burundi kanali Venant Mutashobya wa tatu kulia
mara baada ya ufunguzi wa zoezi USHIRIKIANO IMARA 2014-BURUNDI.
Picha ya Pamoja ya maofisa wa serikali ya Burundi na Maafisa
Wakuu wa Majeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya ufunguzi wa
zoezi USHIRIKIANO IMARA 2014-BURUNDI
Majeshi hayo yakiwa katika mazoezi.
………………………………………………………………………..
Zoezi la Ushirikiano Imara
linalojumuisha nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki limefunguliwa leo
nchini Burundi na Makamu wa Kwanza wa Rais wa chi hiyo. Gwaride maalumu
linalojumuisha majeshi yote ya nchi wanachama lilikuwa limesimama mbele
ya wageni mbalimbali katika uwanja wa kambi ya kijeshi ya Muzinga nje ya
mji wa Bujumbura wakati Makamu huyo wa Kwanza wa Rais alipokabidhi
Bendera ya jumuiya kuashiria kuanza rasmi wa mazoezi hayo.
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa
Tanzania (JWTZ) liliwakilishwa na Meja Jenerali James Mwakibolwa ambaye
ni Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita Makao Makuu ya Jeshi.
Mazoezi haya ya medani hufanyika
kila mwaka katika moja ya nchi wanachama kwa utaratibu wa kupokezana
yakiwa na lengo kuu la kudumisha ushirikiano katika masuala ya ulinzi na
usalama.
Pamoja na mambo mengine, mazoezi
haya yatatoa fursa kwa nchi wanachama kuandaa na kuweka mikakati ya
pamoja katika kukabiliana na matishio mbalimbali yanayoweza kutokea
katika ukanda wetu wa afrika mashariki.
Maudhui makuu ya zoezi la mwaka huu yanajikita katika
kukabiliana na changamoto katika ulinzi wa amani, majanga ya asili na ya
kibinadamu, ugaidi, pamoja na uharamia ambavyo vimekuwa tishio katika
maeneo mengi duniani.
Aidha, kutakuwa na mazoezi ya kuyaweka tayari majeshi yetu
katika kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ili kupunguza na kuzuia kabisa
madhara ya magonjwa hayo.
kwa ujumla, mazoezi haya ni kipimo cha jinsi gani nchi yetu
imejiandaa na kujiweka tayari kupambana na changamoto hizi kwa mujibu wa
taratibu zilizowekwa na jumuiya.
JWTZ limejiadaa vyema katika ushiriki likishirikisha waajeshi wa
fai malimali ili kutimiza malengo ya nchi yetu na jumuiya kwa ujumla
katika kukabiliana na changamoto zilizotajwa.
Aidha, kikosi cha Tanzania kupitia kitengo cha Uhusiano na Raia
(Civil Military Cooperation) kimepanga kutoa misaada mbalimbali kwa
wananchi wa Burundi waishio maeneo ya karibu na kambi ikiwa ni pamoja na
vifaa kwa ajili ya wanafunzi. Ikumbukwe kuwa, jeshi bora ni lile ambalo
askari wake wamefunzwa vizuri na kupata mzoezi ya mara kwa mara katika
kutimiza majukumu yao, mazoezi ndiyo hulifaya jeshi letu kuwa tayari
wakati wote kuwatumikia wananchi.
Friday, October 17, 2014
WANAFUNZI WABAKANA KILA BAADA YA MUDA WA MASOMO,WALIMU WATUPWA LUPANGO.
WANAFUNZI wa shule ya Msingi ya Kikunku iliyopo Manispaa ya
Kigoma Ujiji,wameamua Kuandamana kwenda kituo cha Polisi kati katika ofisi ya
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Jafari Mohamed ,kwa lengo la kutaka walimu Watatu
wa shule hiyo wasitupwe Mahabusu kwa hofu ya kukosa masomo.
Chanzo cha mandamano hayo ni haki na
ukweli wa kesi dhidi ya walimu hao ambao
ni Baraka Kilatunga (28),Jeje Msiba(34) naMichael Mugumwe(34) ambao wanakabiliwa na tuhuma za kumwadhibu fimbo nne za makalio mwanafunzi wa darasa la tatu aliyetajwa kwa jina la
Abrahaman Ramadhan (9) kwa kitendo cha kushawishi na hatimaye kubaka mwanafunzi wa darasa la pili .
Kwa nyakati tofauti wakifafanua hilo Hajira Ndola na
Jafari Ramadhani walisema baada ya kuona
mwalimu amebebwa kwenye gari la afisa elimu na askari polisi walijua ni ile
kesi ya kutoa adhabu kwa mwenzao, kiuhalisia ana haki ya kupewa adhabu kwa
kuwa wanafanya mapenzi shuleni na
mwanafunzi mwenzake wakati kila baada ya masomo.
Akifafanua hilo mwalimu wa nidhamu Nicolausi Ulimwengu alisema Alhamis
ya wiki iliyopita mzazi wa Tatu Masoud
(8) alienda shuleni hapo kuhoji uchafu
unaofanywa na watoto hao ilihali walimu wanashindwa kukemea huku kijana huchelewa
kufika nyumbani mapema pia ni utovu wa nidhamu.
“ameona ni busara kulileta shule ili uongozi ujue uchafu huo,angekwenda
kwa mzazi wa kiume wangeishia kutoleana lugha chafu,walipoulizwa hilo mbele ya
walimu wanne ,walikiri kufanya hivyo si chini ya mara tano ,tuliwapa adhabu ya
fimbo nne kila mmoja” alisema Ulimwengu.
Cha kushangaza ijumaa ya wiki iliyopita tukapewa taarifa kuwa
Abrahaman ameumizwa vibaya hadi kutundukiwa dripu la maji hospitali ya Rufaa Maweni wakati si kweli yupo darasani, wazazi ni chanzo cha maovu na wakiwajibika
kikamilifu wanasimangwa na jamii husika.
Kwa upande wa diwani wa kata ya Katubuka Moses Bilantanye
alisema kuna upotoshaji wa taarifa zilizopo kituo cha polisi ,ambapo mzazi
anadai kijana amezidiwa na ukiuliza wanafunzi wenzao na baadhi ya walimu wanasema
wana tabia ya kufanya mapenzi kila wakati na kuwataka wazazi wafuatilie tabia
za vijana wao na si kukomoa walimu.
Akithibitisha hilo Kamanda wa Polisi wa hapa Jafari Mohamed alisema
Octoba ,10,2014 saa 6.00 mchana ,katika shule hiyo Abrahaman Ramadhan(9) darasa
la tatu alipigwa na walimu watatu kwa
tuhuma za kumbaka mwanafunzi Tatu Masoud(8) darasa la tatu na watafikishwa
mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.
Awali gazeti hili litonywa kuwa,vijana hao ni kawaida yao
kufanya mapenzi kila watokapo shule,ambapo Abrahaman humpa visenti Tatu vya
kununua barafu na mihogo kwa makubaliano ya kufanya tendo la ndoa kinyume cha
sheria ilihali Tamwa wanataka jamii na wasimamia sheria wawajibike ili
kupunguza matukio ya ubakwaji.
SHIRIKA LA NYUMBA NCHINI NHC LAELEZEA LINAVYOSAIDIA VIJANA KWA MRADI WA MASHINE ZA MATOFALI NA UJENZI WA NYUMBA KWA GHARAMA NAFUU
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo, akimpa maelezo ya ujenzi wa
nyumba za gharama nafuu Mkuu wa Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Bi Susan
Omari alipotembelea mradi huo ulioko eneo la Isikizya Wilayani Uyui
jana. (Picha kwa hisani ya Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa
Jamii cha Shirika la Nyumba la Taifa)
Mwonekanao wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Isikizya Mkoani Tabora.
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo akiendelea kutoa maelezo ya mradi
kwa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii, Bi Susan Omari
Nyumba
38 zilizojengwa karibu kabisa na Makao Makuu ya Wilaya ya Uyui eneo la
Isikizya. Nyumba zingine 12 zimejengwa upande wa pili wa barabara eneo
la Isikizya.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi Susan Omari akitoa maelekezo kwa Meneja wa Mkoa wa Tabora Bw. Chilambo
Msimamizi
wa mradi wa NHC isikizya Bw. Tokimu Mondo akitoa maelezo ya utekelezaji
wa mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu eneo la Isikizya jana.
Sehemu ya nyumba zilizojengwa katika mradi wa nyumba za gharama nafuu eneo la Isikizya Wilayani Uyui zinavyoonekana.
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Chilambo akitoa maelezo kwa Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano na Huduma kwa Jamii Bi. Susan Omari yanayohusu viwanja vya
Shirika vilivyoko eneo la Itetemia Manispaa ya Tabora.
Meneja
wa Mkoa wa Tabora Bw. Erasto Chilambo akielezea hatua mbalimbali
zilifikiwa na Mkoa huo za kutengeneza nyumba za Shirika. Hili ni
mojawapo ya jengo la Hoteli ya Golden Eagle baada ya kufanyiwa
matengenezo.
Sehemu ya mtaa wa Jamhuri/Shule wenye nyumba zilizofanyiwa matengenezo makubwa na NHC Mkoa wa Tabora
Mojawapo wa jengo lililofanyiwa matengenezo na NHC Mkoa wa Tabora linavyoonekana kwa sasa
Sehemu
ya Maafisa Vijana wakisikiliza mada iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi Susan Omari (hayuko pichani)
alipoelezea mpango wa NHC wa kugawa mashine kwa ajili ya kusaidia vijana
kwenye Halmashauri zote za Wilaya hapa nchini. Jumla ya mashine 656
zimeshambazwa kwa ajili hiyo.
Washiriki wa semina iliyotolewa na NHC wakisikiliza mada kwa makini
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii wa NHC, Bi Susan Omari
akitoa mada juu ya mpango wa NHC wa kusaidia vijana mashine za
kufyatulia matofali katika Halmashauri zote za Wilayanchini.
Thursday, October 16, 2014
SERIKALI YAFUTA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA CHETI
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr.Shukuru Kawambwa akizungumza wakati alipotembelea Shule ya Sekondari ya Tabora Wavulana |
Na Allan Ntana, Tabora
SERIKALI imefuta kozi zote za mafunzo ya ualimu
ngazi ya cheti kuanzia mwaka huu kwa lengo la kuboresha kiwango cha elimu hapa
nchini.
Tamko hilo limetolewa jana na Waziri wa Elimu na Mafunzo
ya Ufundi Dr Shukuru Kawambwa alipokuwa akizungumza na wanachuo wa Chuo Cha
Ualimu Tabora kilichoko katika Manispaa ya Tabora.
Alisema kuanzia mwaka huu serikali imeamua kuondoa
mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti ikiwa ni mkakati maalumu wa kuanza kuboresha
kiwango cha elimu hapa nchini ambapo waalimu watakaoajiriwa kufundisha shule za
msingi na sekondari watatakiwa kuwa na elimu ya kiwango cha diploma na
kuendelea.
Alieleza kuwa kuanzia sasa wizara yake inataka ubora
wa elimu upatikane kutokana na ubora wa waalimu huku akibainisha kuwa waalimu
wote watakaoajiriwa katika shule za msingi na sekondari kuanzia mwaka huu
lazima wawe na elimu ya kiwango cha kuanzia diploma na kuendelea huku
akifafanua kuwa wale wasiokuwa na diploma watapewa fursa ya kujiendeleza bila
tatizo lolote.
Aidha alisema waalimu wa shule za msingi na
sekondari na wahitimu wa kidato cha sita waliopata daraja la 1-3 waliochaguliwa
kujiunga na kozi maalumu ya mafunzo ya ualimu tarajali ngazi ya cheti wote
watapelekwa vyuoni kupata masomo ya ngazi ya diploma katika vyuo maalumu
vilivyoandaliwa.
Aidha katika kuhakikisha mpango huu mpya
unatekelezwa, Dr Kawambwa alisema wizara inaandaa waraka maalumu wa maelekezo
utakaotumwa kwa wakurugenzi wote wa halmashauri zote hapa nchini.
|
Akijibu swali la wanafunzi wa chuo hicho waliotaka
kujua ni kwa nini mda wa kwenda kufanya
mazoezi (BTP) umepunguzwa na kuwa wiki 3 badala ya siku 60, waziri alisema
utaratibu huo ni wa dharura tu kutokana na uhaba wa fedha ila akaahidi kuwa
watajitahidi kurekebisha hali hiyo kadri hali ya kifedha itakavyoruhusu.
Aidha kuhusiana na ombi la kuongezwa posho ya
mazoezi kutoka sh 4500 wanazolipwa sasa wanafunzi hao wa mafunzo ya ualimu hadi
sh 7500 wanazolipwa wanafunzi wa ngazi ya shahada, waziri aliahidi kulifanyia kazi
kutokana na bajeti ya wizara yake itakavyokuwa.
Aidha waziri aliwataka wanafunzi wote wa vyuo vya
ualimu kuhakikisha wanafaulu masomo yao yote wanayofundishwa chuoni ili waweze
kuajiriwa na serikali vinginevyo watalazimika kukaa benchi.
‘Wakati naingia wizarani nilisema sitaajiri waalimu waliofeli na
nitaendelea na msimamo huo huo kwa nia njema kabisa, jitahidini kufaulu masomo
yenu yote ya kufundishia na yale ya ziada vinginevyo hatuwapi kazi, alisema Dr
Kawambwa.
RAIS KIKWETE ALIPOTEMBELEA BANDA LA BIMA YA AFYA WAKATI WA WIKI YA VIJANA TABORA
Rais Kikwete akisalimiana na baadhi ya maafisa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya |
Baadhi ya maafisa wa Mfuko wa Bima ya Afya wakiwa na Meneja mwandamizi wa Mfuko wa Bima ya Afya kanda ya Magharibi Bw.Emmanuel Adina |
UJUMBE WA TANZANIA WAKUTANA NA MWAKILISHI WA BENKI YA DUNIA TANZANIA, UGANDA, RWANDA NA BURUNDI
Baadhi
ya viongozi wa Wizara ya fedha wakifuatilia kwa makini mkutano uliokuwa
ukiongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa
serikali Dr. Servacius Likwelile, ambapo ujumbe kutoka Tanzania
ulikutana na Mwakili Mkazi wa Benki ya Dunia kwa Tanzania, Rwanda,
Uganda na Burundi Bw. Phippe Dongier hawapo kwenye picha kwa madhumuni
ya kujadili masuala mbalimbali yanayohusu uchumi wa Tanzania. Kutoka
kushoto ni Bw. John Cheyo ambaye ni Kamishna wa Bajeti, anayefuata ni
Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango Zanzibar Bi Amina na wa kushoto kwake
ni Bw. Said Magonya ambaye ni Kamishna wa Fedha za nje Wizara ya
Fedha.(Picha zote na Ingiahedi Mduma – Washington DC).
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa serikali Dr. Servacius
Likwelile alipokuwa akitoa msimamo wake kuhusu sera zinazopendekewa na
Benki ya Dunia kwa mwakilishi mkazi wa Benki ya Dunia kwa Tanzania,
Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Phippe Dongier.
Dr.
Servacius Likwelile Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa
serikali akiwa pamoja na ujumbe kutoka Tanzania. Kutoka kulia ni Gavana
wa Benki kuu ya Tanzania na kutoka kushoto ni Bi. Natu Mwamba Naibu
Gavana wa Benki kuu ya Tanzania wakimsikiliza kwa makini Bw. Phippe
Dongier ambaye ni mwakilishi mkazi wa Benki ya Dunia kwa Tanzania,
Rwanda, Uganda na Burundi hayupo kwenye picha, alipokuwa akijibu hoja
zilizowekwa mezani.
JK AONGOZA KIKAO CHA KAMATI KUU CCM MJINI DODOMA
Mwenyekiti
wa CCM Taifa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati Kuu
ya Halmashauri Kuu ya Taifa CCM kwenye ukumbi wa NEC,CCM Makao Makuu
Dodoma.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma taarifa fupi ya ufunguzi wa kikao kwenye ukumbi wa NEC mjini Dodoma.
Katibu
wa NEC Uchumi na Fedha Bi.Zakia Meghji akizungumza na Katibu wa NEC
Oganaizesheni Ndugu Mohamed Seif Khatib wakibadilishana mawazo muda
mfupi kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya
Taifa mjini Dodoma.
Naibu
Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Ndugu Mwigulu Nchemba akizungumza na Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye katika ukumbi wa NEC kabla ya
kuanza kwa kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM mjini Dodoma.
Tuesday, October 14, 2014
RAIS KIKWETE AONGOZA MAADHIMISHO YA KILELE CHA MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA MKOANI TABORA
Kiongozi
wa mbio za mwenge 2014 Rachel Kassandra akikabidhi mwenge wa Uhuru kwa
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa maadhimisho ya kilele cha mbio
za mwenge ulius na kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere
zilizofanyika katika uwanja wa michezo wa Ali Hassan Mwinyi mkoani
Tabora leo.Kulia ni Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na michezo
Dkt.Fenela Mkangara.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na mwenge wa Uhuru wakati wa
maadhimisho ya kilele cha mbio za mwenge ziizofanyika mkoani Tabora leo.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa
mbio za mwenge mwaka huu wakati wa maadhimisho ya kilele cha mbio hizo
zilizofanyika katika uwanja wa michezo wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora
lei(picha na Freddy Maro)
Monday, October 13, 2014
WANAFUNZI WA SHULE ZA SEKONDARI TABORA WAUSHAURI MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA KUHAMASISHA MASHULENI
PROF.TIBAIJUKA AFANYA ZIARA YA KUSHITUKIZA USIKU CHUO CHA ARDHI TABORA
Waziri wa ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof.Anna Tibaijuka akikagua moja ya mabweni ya wanafunzi wa Chuo cha Ardhi Tabora ambapo ziara hiyo ameifanya kwa kushitukiza majira ya saa moja usiku. |
Prof.Tibaijuka alitembelea pia maktaba ya chuo hicho ambacho haina kompyuta kama nyenzo muhimu za kujifunzia wanachuo. |
Prof.Tibaijuka alipata fursa ya kuzungumza na wanafunzi na walimu na watumishi wa chuo hicho. |
MAMA KANUMBA NA LULU NDANI YA FILAMU MPYA IITWAYO "MAPENZI YA MUNGU"
Hivi karibu Msanii Mahiri na Nguli katika tasnia ya filamu nchini Elizabeth Michael almaarufu kama LULU ataibuka na filamu yake Mpya na yenye kusisimua iitwayo "MAPENZI YA MUNGU" ambapo moja kati ya washiriki katika filamu hiyo ni Bi Flora Mtegoha ambae ni Mama Mzazi wa aliyekuwa Msanii Nguli wa Kiume Hapa Bongo Marehemu Steven Kanumba.
Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" ni moja ya filamu ambayo Lulu ameonyesha uwezo wa hali ya na kuthibitisha kuwa ni mmoja kati ya wasanii wa kike hapa Tanzania ambae ana kipaji cha hali ya juu katika kuuvaa uhusika ambapo ana uwezo wa kubadilika badilika kutokana na muongozo anaopewa.
Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" itakuwa Sokoni hivi Karibu Kwa Wauzaji wa Filamu kote Nchini.
Filamu hii itasambazwa na Kampuni mahiri ya Proin Promotions Ltd.