Pages

KAPIPI TV

Sunday, September 7, 2014

WANAWAKE SIKONGE KUNUFAIKA NA MSAADA WA KISHERIA

Na Allan Ntana, Sikonge

SHIRIKA lisilokuwa la kiserikali la Association for Community Change limeanzisha mradi maalumu utakaojihusisha na utoaji wa msaada wa kisheria ili kuimarisha upatikanaji haki za wanawake katika wilaya ya Sikonge mkoani Tabora.

Akitambulisha mradi huo utakaotekelezwa kwa kipindi cha miezi 30 kwa viongozi wa serikali, wazee maarufu na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini wilayani humo, mwezeshaji wa mradi huo Edward Simon alisema lengo lao ni kusaidia wanawake kutambua haki zao.

Alisema mradi huo unatarajia kushughulikia ulinzi wa haki za wanawake kwa njia ya  utoaji msaada wa kisheria na uwasilishaji ambao utakuwa ukifanywa na wasaidizi watakaopatikana miongoni mwa jamii hiyo na kupewa mafunzo maalumu ya kisheria katika wilaya hiyo.

Aidha alisema timu ya wasaidizi watakaopatikana kwa kufanyiwa usaili miongoni mwa wanajamii hao watawezeshwa na kusajiliwa kama taasisi huru itakayofanya kazi kwa uhuru bila kuingiliwa.

Mwenzeshaji huyo alisema mradi huo unatarajia kushughulikia pia ulinzi wa haki za wanawake kwa  njia ya uhamasishaji wa jamii ambao utakuwa  unafanywa na wasaidizi wa  kisheria 25 watakaopata mafunzo katika  ngazi ya  Wilaya.

Aliongeza kuwa hadi sasa wanajamii walio wengi hawana  uelewa wa kutosha wa haki  za  wanawake jambo ambalo  limesababisha ukatili wa  kijinsia dhidi ya wanawake kuongezeka.

Aliongeza kuwa kufuatana na tafiti  zilizo kwishafanyika imegungulika kuwa kuna ukiukwaji mkubwa wa haki za wanawake uliojengwa juu ya mila na desturi zilizopitwa  na wakati.

Alitoa mfano wa ukatili unaofanyika majumbani kila siku kuwa ni vipigo vya mara kwa mara, ngono za kulazimishwa, kunyimwa mahitaji ya msingi katika ndoa au ukoo, kuthibitiwa juu ya rasilimali binafsi na kiwango duni cha elimu.

Aliongeza kero nyingine kwa wanawake kuwa ni ukosefu wa taarifa sahihi juu ya haki za  wanawake, uelewa mdogo wa wanawake juu ya  haki zao, unyonge wa wanawake unaochangiwa na  mfumo dume uliojengeka katika jamii unaofanya wanawake kuwa tegemezi kwa wanaume.

Friday, September 5, 2014

ZIARA YA MAKAMU WA PILI WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR KATIKA MRADI WA UNYAKUMI


Picha zote kwa hisani ya kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa Jamii cha Shirika la Nyumba la Taifa *****************
 
MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa ( NHC) kuhakikisha kuwa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa kwa ajili ya makazi zinakidhi mahitaji ya familia.
 
Balozi Seif Idd alitoa mwito huo mjini Singida mara baada ya kutembelea shughuli za ujenzi wa nyumba 20 katika eneo la Unyakumi, Manispaa ya Singida, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa nyumba 15,000 zinazojengwa na shirika hilo kote nchini kwa ajili ya makazi.
Alisema ingawa baadhi ya mashirika yamekuwa na nia njema ya kusaidia wananchi kumiliki nyumba kwa bei nafuu badala ya kuendelea kupanga, baadhi ya nyumba zinazojengwa ni ndogo kiasi cha kutokidhi mahitaji ya wanafamilia wanaonunua, wengi wao wakiwa wastaafu.
 
Kutokana na hali hiyo, Balozi Idd alisema kuwa ipo haja kwa Shirika hilo la Nyumba nchini kuhakikisha kuwa nyumba 15,000 zinazoendelea kujengwa kote nchini zinakuwa na ubora na viwango vinavyokidhi mahitaji ya familia.
 
Kaimu Meneja wa NHC Mkoa wa Singida, Peter Luheja alisema kuwa zaidi ya Sh milioni 900 zitatumika kugharimia ujenzi wa nyumba hizo 20 katika eneo la Unyakumi, Manispaa ya Singida.
Luheja alisema kuwa mradi wa ujenzi wa nyumba za gharama nafuu katika Manispaa ya Singida unatarajiwa kukamilika na nyumba kuanza kuuzwa kwa wananchi ifikapo Oktoba mwaka huu.
SOURCE:HABARI LEO

DIAMOND AELEZA ALIVYODHALILISHWA!!!


Stori: Shakoor Jongo
SIKU chache baada ya kufanyiwa fujo katika shoo yake nchini Ujerumani, staa wa Mdogo Mdogo, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameibuka na kueleza namna ambavyo alidhalilishwa nchini humo.
Diamond aliponea chupuchupu kupewa kipigo baada ya kuchelewa kwenye shoo iliyokuwa ifanyike katika Ukumbi wa Sindelfingen katika mji wa Stuttgart, Ujerumani.

Staa wa Mdogo Mdogo, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Akizungumza na paparazi wetu baada ya kutua Bongo Jumanne iliyopita, Diamond alisema anasikitika kwani alidhalilishwa wakati alipokuwa akidai haki ya kumaliziwa malipo yake ya shoo euro 250 (zaidi ya sh 500,000).GPL(P.T)



“Inaniuma sana kwani mimi pale nilikuwa nasimamia haki yangu, kwani nilikuwa nawadai euro 250 sasa nikaona wananizungusha na nilipokomaa zaidi huku wakiona muda wa shoo unapita, ndipo walipoanza kunitukana bila sababu.

“Wamenitukana mimi, wamewatukana hadi ndugu zangu ambao hawakuhusika na chochote na wala hawakuwepo kule. Wamenidhalilisha bila kosa. Kimsingi sikutaka kupanda jukwaani pasipo kumaliziwa fedha zangu licha ya kuwa si nyingi kiivyo,” alisema mtoto huyo wa Tandale.

Hali halisi ya ukumbi nchini Ujerumani ulivyoharibiwa na mashabiki waliovurugwa kwa kucheleweshewa shoo ya Diamond.

Kwenye maelezo menginena paparazi wetu, Diamond alisema baada ya kutokea vurugu hizo alilazimika kurejea nchini pasipo kumaliziwa fedha zake lakini promota wa shoo hiyo, Kamabritts aliahidi kuandaa shoo nyingine ya bure ili kujisahihisha kwani kosa lilikuwa la kwake.

Kwenye mvutano huo kati ya msanii na promota huyo, Diamond alitegemewa kupanda jukwaani saa nne usiku lakini ilishindikana hadi ilipofika saa 10 alfajiri kitendo ambacho kilisababisha mashabiki wafanye vurugu kwa kuvunja viti na thamani nyingine za ukumbi zinazokadiriwa kufikia Euro 128,222 (Sh. milioni 280).
KWAHISANI YA MJENGWA BLOG

MKUU WA WILAYA YA TEMEKE AKABIDHI MASHINE ZA KUFYATULIA MATOFALI ZILIZOTOLEWA NA (NHC)KWA VIKUNDI VYA VIJANA

 5Mkuu wa wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema akikabidhi mashine ya kufyatulia matofali mwenyekiti wa kikundi cha Mbagala  Youth Group Said Mponda  baada ya kuzipokea kutoka kwa Shirika la Nyumba la Taifa NHC ambalo limetoa mashine kwa vikundi hivyo ili kusaidia serikali katika kupambana na tatizo la ajira nchini kwa vijana mashine hizo zilikabidhiwa kwa mkuu wa wilaya na Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC tawi la Temeke Bw. Wencenslaus Tillya. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
3Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema akipokea mashine za kufyatulia matofali kutoka kwa Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC Wilaya ya Temeke  Bw. Wencenslaus Tillya ambazo zilikabidhiwa kwa vikundi vya vijana wilayani humo.

4Mkuu wa Wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema akikabidhi mashine kwa mwenyekiti wa kikundi cha Sokoine Youth Development William Gabriel.
6Mkuu wa wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema akikabidhi mashine ya kufyatulia matofali mwenyekiti wa kikundi cha Chang’ombe Youth Development Eunice Mlwale baada ya kuzipokea kutoka kwa Shirika la Nyumba la Taifa NHC 8Mkuu wa wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema akikabidhi mashine ya kufyatulia matofali mwenyekiti wa kikundi cha Chapakazi Youth Youth Nathanaeli Daniel Kidaila baada ya kuzipokea kutoka kwa Shirika la Nyumba la Taifa NHC 9Mkuu wa wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema  akiwa katika picha ya pamoja na vikundi hivyo mara baada ya kukabidhi mashine za kufyatulia matofali kwa vikundi vya vijana vya Temeke ambazo zimetolewa na   Shirika la Nyumba la Taifa NHC Kulia kwa Mkuu wa Wilaya ni Wencenslaus Tillya Meneja wa NHC Temeke na kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw. John Bwana. 10Mkuu wa wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema  akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba NHC na baadhi ya maofisa wa Manispaa ya Temeke. 11Baadhi ya waandishi wa habari na vijana waliojitokeza katika makabidhiano hayo wakiwa katika hafla hiyo12Baadhi ya mashine za kufyatulia matofali zilizokabidhiwa kwa vikundi hivyo.13Mkuu wa wilaya ya Temeke Bi. Sophia Mjema akimzikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw. John Bwana wakati alipokuwa akitoa shukurani zake kwa shirika la Nyumba NHC kwa kutoa mashine hizo, wa pili kutoka kulia ni Wencenslaus Tillya Meneja wa NHC wilaya ya Temeke.

Thursday, September 4, 2014

NHIF YAENDELEA KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA



kurugenzi wa Fedha, Mipango na Uwekezaji kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bw. Deusdedit Rutazaa akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mpango wa kuanza kutoa mikopo ya dawa kwa vituo ambavyo vimesajiliwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya. Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko na Utafiti kutoka Mfuko huo Bw. Raphael Mwamoto.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwasikiliza wawasilishaji kutoka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.
(Awadh Ibrahim wa Mjengwa Blog/ kwanza jamii radio)

MKONGO WA TAIFA WASAIDIA KUSHUKA KWA GHARAMA ZA MAWASILIANO NCHINI


Msemaji wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Bi. Prisca Ulomi akiongea na waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu mafanikio ya mkongo wa Taifa ikiwamo kusaidia kushuka kwa gharama za Mawasiliano nchini. Kushoto ni Mkurugenzi huduma za mtandao wa TTCL Mhandisi Joram Lujara.

Mratibu wa Ufundi kutoka Ofisi ya Mkongo wa Taifa Mhandishi Anifa Chingumbe akiwaonesha waandishi wa Habari (hawapo pichani) maeneo ambayo mkongo wa Taifa umepita, Wakati wa Mkutano uliofanyika Jijini Dar es Salaam.

Serikali imesema Mkongo wa Taifa umesaidia kushuka kwa gharama za  mawasiliano kwa watumiaji wa mwisho nchini kutoka sh.147 kwa dakika mwaka 2009 hadi shilingi 62 kwa dakika mwaka 2013.

Hayo yamesemwa na Msemaji wa Wizara ya Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mawsiliano Sayansi na Teknolojia Bi Prisca Ulomi wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
 
Akifafanua Bi Prisca amesema kuwa mkongo wa taifa umesaidia pia kushuka kwa gharama za intaneti kutoka shilingi 36,000 hadi shilingi 9000/Gb kufikia mwaka 2013.

“Mkongo wa Taifa umesesaidia kuharakisha usambazaji wa huduma za mawasiliano katika maeneo yasiyokuwa na mvuto wa kibiashara”alisisitiza bi Ulomi.Katika hatua nyingine, Bi Ulomi alisema faida nyingine ya Mkongo ni kuongezeka kwa upatikanaji wa huduma za mawasiliano na uwezo wa kusafirisha masafa.

Akieleza kuhusu gharama Bi Prisca amesema gharama za maunganisho ya mawasiliano ya simu za mkononi kutoka  kampuni moja kwenda nyingine  (interconnection fees) ambapo sasa gharama imepungua kutoka sh. 115 hadi shilingi 34.92 kwa dakika.

Mkongo wa Taifa umesaidia kuongeza ushirikiano wa kikanda  kati ya nchi za Afrika Mashariki na kati ambapo nchi za Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi, Uganda, na Kenya ambapo hali hiyo imeongeza fursa za kibiashara na kukuza uchumi wa nchi.

Kufikia mwaka 2013 makampuni yafuatayo yalikuwa yameunganishwa na mkongo wa Taifa ni TTCL, TIGO, Zantel,  Airtel, Vodacom, Simbanet na infinity.

MKURUGENZI NHC ATEMBELEA ENEO LA MRADI WA NYUMBA ZA WATUMISHI HALMASHAURI YA BUSOKELO MBEYA

Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Kyando Mchechu wa kwanza kulia mbele akitembelea eneo la ujenzi wa nyumba za gharama nafuu zitakazojengwa  katika Halmashauri ya Busekelo Mkoani Mbeya alipotembelea Halmashauri hiyo  Septemba 3 mwaka huu .Picha na Saguya wa NHC.
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Mchechu akielezea mpango wa shirika wa kujenga nyumba za watumishi wa Halmashauri ya Busekelo alipotembelea Halmashauri hiyo jana .Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Busokelo Bw. Meshack Mwakipunga  na kulia  kwa Mkurugenzi Mkuu wa  NHC ni Mkurugenzi wa  Halmashauri ya Busekelo Bw Saidi Mderu .
 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Busokelo Bw,Meshack Mwakipunga akiutembeza ujembe wa shirika la Nyumba la Taifa  kwenye eneo la viwanja vitakavyojengwa  nyumba  na NHC hivi karibuni.
Ujumbe wa NHC na Halmashauri ya Busokelo ukiendelea kutambua  viwanja vitakavyojengwa Nyumba na NHC hivi karibuni
 
Mkurugenzi Mkuu wa NHC Bw.Nehemia Mchechu akitoa maelezo ya kuridhia eneo walilopewa na Halmashauri ya Busekelo ili kujenga nyumba hivi karibuni.
Ujumbe ukikagua kazi ya kutengeneza matofali kwa ajili ya kujengea nyumba katika Halmashauri ya Busokelo.
Mhandisi wa  miradi ya nyumba wa NHC Kanda ya Mbeya Bw.Mtili akitoa maelezo ya hatua iliyofikiwa ya ufyatuaji wa matofali ya  kujengea nyumba katika Halmashauri hiyo.
 
Ujumbe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC  ulipata fursa ya kutembelea shamba la mwekezaji wa Kilimo cha Maparachichi baada ya kumaliza ziara yake katika Halmashauri ya Busokelo,ambapo kupitia uwekezaji huo wananchi wa busokelo na maeneo mengine wamepata fursa ya ajira.
Ujembe wa Mkurugenzi Mkuu wa NHC ukipewa maelezo na Meya wa Jiji la Mbeya Bw.Athanas Kapunga yanayohusu fursa za uwekezaji ambazo NHC inaweza kuzitumia kukuza uchumi wa jiji hilo.

MGODI WA NORTH MARA WACHANGIA BILIONI 7.5 KATIKA SHUGHULI ZA JAMII


Picha Na 2Mwenyekiti wa Jopo la Majaji kwa ajili ya kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji Prof. Samwel Wangwe (kushoto) akisalimiana na Afisa Mahusiano wa Mgodi wa North Mara Bw. Zakayo Kalebo (kulia) mara baada ya jopo hilo kuwasili kwenye mgodi huo.
Picha Na 3Meneja Mahusiano wa Mgodi wa North Mara Bi Fatuma Mssumi (mbele) akielezea shughuli za mgodi wa North Mara mbele ya jopo la majaji waliotembelea mgodi huo ili kuendelea na zoezi lake la kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji.
Picha Na 5Afisa Uhusiano wa Kijiji cha Matongo Bw. Magesa Wanjara akionesha jinsi ya kutumia bomba la kisima cha maji kilichofadhiliwa na mgodi wa North Mara mbele ya timu ya majaji, sekretarieti na wajumbe wengine.
Picha Na 7Mwenyekiti wa Umoja wa Kikundi cha Vijana cha Nyakegema Bw. Zacharia Mwita ( wa pili kutoka kulia) akitoa maelezo mbele ya timu ya majaji na wajumbe wengine kuhusu mchango wa mgodi wa North Mara kwa kikundi hicho kupitia mradi wake wa mboga za majani. Kikundi hicho kina jumla ya vijana 578 kutoka katika vijiji saba vinavyouzunguka mgodi huo.
Picha Na 9Mwenyekiti wa Jopo la Majaji kwa ajili ya kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji Prof. Samwel Wangwe (kushoto) akisalimiana na Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Ingwe Bw. Alfred Joseph mara timu hiyo ilipofanya ziara kwenye shule hiyo iliyofadhiliwa na mgodi wa North Mara.
……………………………………………

Na Greyson Mwase, Tarime
Imeelezwa kuwa mgodi wa North Mara uliopo wilayani Tarime mkoani Mara umechangia jumla ya shilingi bilioni 7.5 katika kipindi cha mwaka 2013 kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo   katika vijiji saba vinavyouzunguka mgodi huo.

Akizungumza mbele ya timu ya majaji kwa ajili ya kumtafuta mshindi wa Tuzo ya Rais ya Huduma za Jamii na Uwezeshaji chini ya mwenyekiti wake Prof. Samwel Wangwe Meneja Mahusiano wa Mgodi huyo Bi Fatuma Mssumi alitaja vijiji hivyo kuwa ni pamoja na Nyangoto, Nyamwaga, Nyakunguru, Kerende, Kewanja, Genkuru na Matongo.

Bi Mssumi alisema kuwa kupitia sekta ya elimu, mgodi ulichangia madawati 2700 yenye thamani ya shilingi milioni 251.9 kwa ajili ya shule mbalimbali za msingi na sekondari na kuongeza kuwa mgodi ulijenga shule ya sekondari ya Ingwe kwa shilingi bilioni 1.1 miradi ambayo imekamilika.

Alisema kuwa mgodi ulifanya ukarabati pamoja na ujenzi wa shule ya sekondari ya Kemambo kwa gharama ya shilingi milioni 905.5, na shule ya msingi ya Bong’eng’e kwa gharama ya shiligi milioni 827.

Aliongeza kuwa mgodi huo katika awamu yake ya kwanza ulichangia shilingi milioni 605. 8 kwa ajili ya ujenzi wa shule ya sekondari ya Nyamwaga mradi ambao bado unaendelea.

“ Pia   mgodi uligharamia shilingi milioni 12.7 kwa ajili ya wanafunzi waliofanya vizuri kusoma katika shule na vyuo mbalimbali”, alisema Bi Mssumi

Aliongeza kuwa nia ya kuwekeza katika elimu katika wilaya ya Tarime ni kuhakikisha wanajenga msingi utakaopelekea kupatikana wataalamu kwa ajili ya kufanya kazi katika mgodi huo.

Akielezea mchango wa mgodi huo katika sekta ya afya Bi Mssumi alitaja miradi mingine kuwa ni pamoja na ukarabati na ujenzi wa zahanati ya Genkuru uliogharimu shilingi milioni 61.2, upimaji wa macho kwa wanakijiji 3,000 kwa shilingi milioni 19 pamoja na upimaji wa virusi vya Ukimwi kwa wanakijiji 1067 uliogharimu shilingi milioni tano.

Aliendelea kusema kuwa mgodi huo ulitoa msaada kwaajili ya upasuaji kwa wanakijiji 11 ambapo jumla ya shilingi milioni 12.2 zilitumika

Akielezea sekta ya maji Bi. Mssumi alisema kuwa mgodi ulichimba visima katika vijiji sita kwa thamani ya shilingi milioni 888.3 pamoja na usambazaji wa maji katika vijiji vya Nyangoto, Kewanja, Matongo na Kerende uliogharimu shilingi bilioni 1.2

Alisema kuwa mgodi pia ulifanya ukarabati katika kituo cha afya cha Nyangoto kwa gharama ya shilingi milioni 481.7 pamoja na usafi katika vijiji vya Nyangoto, Kerende, Kewanja na Nyamwaga uliogharimu shilingi milioni 544.4

Alisisitiza kuwa ili kuhakikisha kuwa wachimbaji wadogo wananufaika na sekta ya madini kupitia kujiajiri mgodi huo ulichangia shilingi milioni 91.4 kwa kikundi cha wachimbaji wadogo Tarime kwa ajili ya ununuzi wa mashine kwa ajili ya kusaga kokoto.

Bi Mssumi aliongeza kuwa hatua iliyofikiwa sasa ni mkandarasi kufanya kazi ya kutoa umeme kutoka mgodi wa North Mara hadi mashine ilipo ili ianze kazi mara moja.

Alisema kuwa mgodi pia ulifadhili   miradi mbalimbali kwa gharama ya shilingi milioni 252.5 pamoja na vikundi vya kijamii/kidini kwa gharama ya shilingi bilioni 1.8

Akizungumzia mchango wa mgodi huo katika sekta ya miundombinu Bi Mssumi alisema kuwa mgodi huo ulikarabati barabara yenye urefu wa kilomita 47.9 kwa gharama ya shilingi milioni 469 pamoja na uunganishaji wa umeme kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) katika vijiji vya Kerende na Matongo kwa gharama ya shilingi milioni 472

Alitaja miradi mingine kuwa ni pamoja na ujenzi wa kituo cha polisi uliogharimu shilingi milioni 555.5 na ujenzi wa mahakama ya mwanzo Nyamongo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa nyumba za wafanyakazi wa mahakama hiyo kwa shilingi milioni 182.9 mradi ambao haujakamilika bado.

Akizungumzia changamoto katika   utekelezaji wa miradi hiyo, Bi. Mssumi alisema kuwa kumekuwepo na tatizo la wanavijiji kuhujumu miundombinu ya maji iliyowekwa hali inayopelekea mgodi huo kuingia gharama kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu hiyo.

“Wapo wanakijiji wasio waaminifu ambao huharibu miundombinu ya maji kwa makusudi ili kufanya biashara ya maji jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo ya vijiji hivyo” Alisisitiza Bi. Mssumi.

MAJAMBAZI WATANORAIA WA BURUNDI WAUWAWA KIGOMA WAKUTWA NA MABOMU 3 SILAHA 2 RISASI 64

Kamanda wa Polisi Mkoani Kigoma Kamishina Msaidizi Japhari Muhamed akionyesha siraha walizokuwa nazo majambazi waliouwawa leo alfajiri.
Mabomu, bunduki na vyakula vyenye nembo ya kutoka nchi ya Burundi walivyokutwa navyo majambazi
Silaha walizokuwa nazo majambazi katika eneo la tukio Kigoma


Na Magreth Magosso,Kigoma

Jeshi la Polisi Mkoa wa Kigoma limefanikiwa kuyauwa Majambazi watano raia kutoka nchi ya Burundi leo(jana) alfajiri katika   Barabara Kuu ya Kasulu Kibondo eneo la pori la malagarasi wakiwa tayari kuteka mabasi ya abiria mbalimbali yaendayo mikoani.
 
Pia walikuta mfuko wa salfeti uliokuwa na mabonu matatu ya kutupa kwa mkono,silaha za moto  mbili moja aina ya AK 47 yenye namba UA40501997,SMG namba 691220 ,magazine tatu  pamoja na risasi 64.
 
Akifafanua hilo jana ofisini kwake kigoma Ujiji Kamishna Msaidizi wa polisi Jaffari Mohamed  alisema  Septemba ,3,mwaka huu  saa 11.45 alfajiri  askari polisi wakiwa wamejipanga katika eneo la tukio hilo waliwakuta wakiandaa silaha zao tayari kufanya mashambulizi kwa walengwa.
 
“tulibaini njama  hizo kutoka kwa wadau wetu,askari walipofika eneo hilo walishuhudia harakati zao badae nao walibaini  askari wetu na walianza kufyatua risasi bila mpangilio mungu ni mwema tumeyauwa  na maiti zipo hospitali ya wilaya ya kasulu”alianisha Mohamed.

Alisema  wananchi kwa kushirkiana na wajumbe wa vikao vya kamati ndogo na kubwa za ulinzi hasa polisi jamii zimechangia kufanikisha hayo ambapo hivi karibuni wilaya ya buhigwe majambazi watano  raia wa nchi hiyo waliua watu wanne na kujeruhi saba kwa kutupa bomu katika basi la abiria.
 
Kwa upande wa Naibu kamishna idara ya uhamiaji wa hapa Ebrosy Mwanguku alibainisha kuwa,changamoto ya matukio ya uhalifu katika mkoa huo ni kutokana na uhalisia wa mipaka ambayo ina vipenyo vingi visivyo na vituo vya uhamiaji na askari polisi hali inayochangia wahalifu kutoka huko kushambulia raia wa hapa.
 
Naye Mkuu wa wilaya ya kasulu Danny Makanga alisema kupitia vikao vya ujirani mwema unaoshirikisha  nchi  tatu ambazo zinapakana na kigoma(Drc Kongo,Burundi ) wahakikishe wanakusanya silaha zilizozagaa nchini kwao ili kuheshimu madhimio 12 yaliyoadhimiwa katika kikao cha Agost,15,mwaka huu.  
 
Ubalozi mdogo wa Burundi Johnbosco Ngayikengurukiye alipoulizwa kwa nini raia wa Burundi hukutwa katika matukio yasiyorasmi hasa uhamiaji haramu na uhalifu akiri changamoto hiyo inamumiza kichwa na kubainisha ukosefu wa ardhi na ajira chachu ya hayo.

Jamboleo limebaini bidhaa zilizokutwa katika kiroba cha majambazi hayo ni mikate iliyookwa kiasili na juisi iliyosindikwa  `Zaam Zam Orange'ambayo ni moja yakinywaji kiwanda  cha  Mona`s,ambavyo huvila pale wanapohisi njaa katika safari ya kuja hapa.

Hivyo changamoto ya mipaka mikubwa  isiyokuwa na idara nyeti za ulinzi  kuingia kinyemela usiku kwa usiku na kufanya uhalifuambapo hitaji  la vituo  ni 14 ni chachu ya  kuimarisha ulinzi lakini  kwa sasa kigoma ina vituo  viwili tu venye  huduma hiyo hali inayochangia majanga ya uhalifu kushamiri kila kukicha.

Wednesday, September 3, 2014

UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU HAPA NCHINI UNAANZIA PALE MTU ANAPOKAMATWA NA VYOMBO VYA DOLA


DSC_0478SULEIMAN MSUYA
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (CHGG) imesema asilimia kubwa ya ukiukwaji wa haki za binadamu hapa nchini unaanzia pale mtu anapokamatwa na vyombo vya dola kwenye mahojiano pamoja na mahabusu.
 
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Huduma za Kisheria (CHGG) Nabor Assey wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo jijini Dar es Salaam.
 
Assey alisema utafiti unaonyesha kuwa wengi wao wanakamatwa pasipo utaratibu, kudhalilishwa, kuteswa, kubambikiwa kesi, kuwekwa muda mrefu bila kufikishwa mahakamani na kuwepo mazingira magumu ya dhamana jambo linalokiuka haki za binadamu zilizoainishwa katika ibara ya12 mpaka 24 ya Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na sheria zingine za nchi na mikataba ya kimataifa iliyoridhiwa.
 
Mkurugenzi huyo utafiti huo unaonyesha kuwa asilimia 50 ya watu wanaoshikiliwa maeneo mbalimbali nchini ni mahabusu ambao ama wanasubiri kufikishwa mahakani au kesi zao zinaendelea katika mahakama mbalimbali bado hawajahukumiwa.
 
“Napenda kuweka wazi kuwa hii ni Idara huru ya Serikali tunachokisema hapa ni katika juhudi za kusaidia serikali kutatua changamoto ambazo zinaikabili jamii yake hasa katika masuala ya haki za binadamu” alisema.
 
Assey alisema ni wazi kuwa vyombo vya dola hasa jeshi la polisi limekuwa likishutumiwa kwa ukiukwaji wa haki za binadamu hali ambayo inahitaji elimu zaidi ambayo inaweza kusaidia kutatua tatizo hilo.
 
Alisema ni vema dhana halisi ya jina la polisi (Police Force) kubadishwa na kuwa (Police Service) ili kuwapatia uelewa kuwa wanapaswa kutoa huduma na sio kutumia nguvu zaidi kama njia ya kukabiliana na tatizo.
 
Mkurugenzi huyo alisema pia kuna mapungufu katika mfumo wa sheria za jina za Tanzania akitolea mfano ibara ya 13(6) (e) ya Katiba ya Tanzania ya 1977  inakataza utesaji kwa watuhumiwa na kuelekeza mamlaka za nchi kutunga sheria kwa minajili hiyo.
 
Alisema bado kuna  upungufu katika sheria kwani kifungu cha 29 cha sheria ya ushahidi  sura ya 6 ya sheria za Tanzania kinakata ushahidi uliopatikana kwa shinikizo la aina yoyote kutumika kama ushahidi halali mbele ya mahakama.
 
Assey alisema pamoja na sheria hizo kuonyesha ukatazo bado hazijaonyesha ni hatua gani atachukuliwa mtumishi yeyote ambaye atabainika kufanya vitengo vinavyokiuka haki za binadamu.
 
Alisema Tume yao ipo katika mchakato wa kuhakikisha kuwa vyombo vya usalama vinapatiwa elimu yakutosha juu ya nini majukumu yao pale ambapo wanamshikilia mtu ambaye amefanya kosa.
 
Mkurugenzi huyo alisema jitihada hizo zinatakuwa zikishirikisha wananchi hasa kwa kudai haki zao ambazo hazipo kisheria ambao wanaonekana kuwa waathirika wakubwa kutokana na vyombo vya dola hasa Jeshi la Polisi

Tuesday, September 2, 2014

NISHATI NA MADINI WAIMARISHA MKAKATI WA UTUNZAJI MAZINGIRA

day 2 - pic 1Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Emmanuel Shija akiwasilisha mada kuhusu ‘Uchimbaji mdogo wa Madini na Mazingira’ wakati wa semina ya mafunzo kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa. Semina hiyo ya siku nne inafanyika jijini Mwanza (Septemba 1-4, 2014) na imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara husika.
day 2 - pic 2Katibu Mtendaji wa TAREA (Tanzania Renewable Energy Association) Tawi la Kanda ya Ziwa, Bw. Jacob Ruhonyora akizungumzia uzoefu wake kuhusu faida za matumizi ya nishati jadidifu,kwa Wajumbe wa semina ya mafunzo ya mambo ya mazingira inayoendelea jijini Mwanza kuanzia Septemba 1, 2014. Semina hiyo ya siku nne imeandaliwa na Kitengo cha Mazingira cha Wizara ya Nshati na Madini.
day 2 - pic 3Afisa Misitu Mkuu kutoka Kitengo cha Mazingira – Wizara ya Nishati na Madini (Kulia), Theodory Silinge akitoa ufafanuzi kuhusu umuhimu wa kuhimiza jamii kutumia nishati mbadala wakati wa semina ya mafunzo kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza, Septemba 1 – 4, 2014 day 2 - pic 4Afisa Sheria kutoka Wizara ya Nishati na Madini Renatus Damian, akiwasilisha mada kuhusu masuala ya sheria katika utunzaji mazingira wakati wa semina kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza Septemba 1 – 4, 2014.
day 2 - pic 5Afisa Mazingira kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Nassor Abdullatif (Kushoto), akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa kufanya Tathmini ya Mazingira (Environmental Impact Assessment – EIA) kabla ya kuanza utekelezaji wa mradi wowote katika siku ya pili ya semina kwa Maafisa Mazingira wa Wilaya kutoka Kanda ya Ziwa, inayofanyika jijini Mwanza Septemba 1 – 4, 2014.