Pages

KAPIPI TV

Friday, July 18, 2014

NAIBU WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA ANGELLAH KAIRUKI AKIFANYA MAJUMUISHO YA WIZARA YAKE ALIYOIFANYA WIKI HII

PIX 1 (1)
PIX5Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angellah Kairuki akiongea na wanahabari(hawapo pichani) kutoa maelezo ya majumisho ya ziara yake ya siku tano ya kuzitembelea Taasisi zinazotoa Huduma ya Msaada wa Kishria Mkoani Dar es Salaam.
Picha na Rose Masaka-MAELEZO.

SEMINA ELEKEZI AIRTEL RISING STARS KUFANYIKA DAR

JOS ARS 2012
Semina elekezi ya michuano ya Airtel Rising Stars kwa mikoa sita inafanyika kesho (Julai 19 mwaka huu) saa 4 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 Washiriki wa semina hiyo ni kutoka mikoa ya Mbeya (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Mwanza (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Morogoro (Katibu), Ilala (Katibu na mwakilishi wa wanawake).
 Temeke (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Kinondoni (Katibu na mwakilishi wa wanawake), Dar es Salaam (Mwenyekiti na Katibu), na Chama cha Mpira wa Miguu Zanzibar (ZFA) kitakachowakilishwa na mwakilishi wa wanawake.
 Washiriki wengine katika semina hiyo ambayo mgeni rasmi atakuwa Katibu Mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine ni wajumbe wa Kamati ya Mpira wa Miguu wa Vijana ya TFF.
 BONIFACE WAMBURA
OFISA HABARI NA MAWASILIANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

MBUNGE RIDHIWANI KIKWETE AENDELEA KUFANYA MAMBO JIMBO LA CHALINZE, SAFARI HII NI ZAMU YA JESHI LA POLISI

1A
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akizungumza na uongozi wa polisi Mkoa wa Pwani na Wilaya ya Kipolisi ya Chalinze pamoja na wananchi waliojitokeza katika hafla ya makabidhiano ya vifaa mbalimbali kwa jeshi hilo zikiwemo kompyuta, mifuko ya Saruji pamoja na fedha vilivyotolewa na mbunge huyo, Kwa ajili ya kutatua matatizo mbalimbali yanayolikabili jeshi la polisi katika utekelezaji wa majukumu yake ya ulizni na usalama wa raia na mali zao. Pamoja na kukabidhi kompyuta hizo zitakazosaidia katika utunzaji wa kumbukumbu pia mbunge huyo ametoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya polisi vya Mbwewe na Kiwangwa ambavyo thamani inafikia zaidi ya shilingi milioni 11, Kushoto kwake ni Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei, hafla ya makabidhiano hayo imefanyika jana kwenye kituo kikuu cha polisi Chalinze.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-CHALINZE)
1
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete kompyuta Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Kamanda ACP Ulrich Onesphory Matei zilizokabidhiwa na mbunge huyo kwa ajili ya kuboresha shughuli za jeshi hilo jimbo la Chalinze katikati ni Mkuu wa kituo cha polisi Chalinze Afande J. S. Magomi.
2
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akikata utepe kufungua ili kuonyesha kompyuta hizo huku viongozi wa jeshi hilo mkoani Pwani na jimbo la Chalinze wakishiriki shghuli hiyo.
3
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimuonyesha moja ya kompyuta Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei.
4
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani ACP Ulrich Onesphory Matei wakati alipokuwa akitoa shukurani zake kwa niaba ya jeshi la polisi mkoani Pwani mara baada ya kukabidhiwa kompyuta hizo , katikati ni mkuu wa ituo cha polisi cha Chalinze Afande J.S Magomi.
5
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akimsikiliza Mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya Chalinze Mzee Bw. Kamis Kameza wakati alipokuwa akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa shule hiyo ambayo inajengwa na jeshi la kujenga taifa JKT kambi ya Ruvu.
6
Baadhi ya wanajeshi wa kambi ya JKT Ruvu wanaoshiriki katika ujenzi wa shule hiyo.
7
Moja ya madarasa ya shule hiyo ambayo yako katika hatua za mwisho za kukamilisha ujenzi wake.
8
Baadhi ya madarasa na maktaba ya shule hiyo yakiwa katika hatua mbalimbali za ujenzi wake.
9
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akisalimiana na wanafunzi wa darasa la saba wa shule ya msingi ya Chalinze Mzee wakati alipokagua ujenzi wa shule hiyo.
10
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete akiendelea kufanya ukaguzi wa ujenzi shuleni hapo kushoto ni Diwania wa kata ya Bwilingu Chalinze Bw. Ahmed Nasser.
11
Mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikweteakikagua ujenzi wa Maktaba ya shule hiyo akiwa ameongozana na Diwani wa kata ya Bwilingu Ahmed Nasser mbele na Mwalimu mkuu wa shule hiyo Khamis Kameza.
12
Baadhi ya wananchi waliohudhuria wakati wa hafla kukabidhi kompyuta kituo cha polisi Chalinze.
13
Diwani wa kata ya Bwilingu Chalinze Bw. Ahmed Nasser akizungumza wakati mbunge wa jimbo la Chalinze Mh. Ridhiwani Kikwete alipolokabidhi jeshi la polisi kompyuta kwa ajili ya kuboresha shughuli za jeshi hilo.

WANANCHI WATAKA STAMICO IPEWE NGUVU KUSIMAMIA SEKTA YA MADINI NCHINI.

index 
• Waunga mkono kauli ya Waziri wa Nishati na Madini 

• Wataka wenye uwezo kuacha ubinafsi na ubepari 

• Wataka raslimali za madini ziwanufaishe Watanzania wote

Na. Issa Mtuwa – STAMICO  
Wananchi wameiomba serikali kuhakikisha rasilimali za Madini zinawanufahisha Watanzania wote na sio wachache wenye uwezo. Kauli ambayo imewahi kutolewa siku za hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo.  

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati walipotembelea katika banda la Shirika la Madini la Taifa STAMICO katika maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa (SABASABA) 2014, wananchi hao wamesema ili azma hiyo iweze kutimia ni vyema Serikali ikaijenga uwezo STAMICO kifedha na vitendea kazi ili iweze kutekeleza miradi ya uchorongaji na uchimbaji madini itakayowanufaisha wananchi. Akizungumza kwa niaba ya wenzake alioambatana nao katika banda la STAMICO, Mkazi wa mkoa wa Mara, Bw. Joel M. 

Changarawe amesema katika kujenga uwezo wa kifedha wa Shirika hilo, Serikali haina budi kuendeleza azma yake ya kuikabidhi STAMICO migodi yote mikubwa ya Madini iweze kumiliki kwa niaba ya Watanzania na kuzalisha ili kuongeza tija kwa Taifa.

Jacqueline Aisaa akitoa maoni yake kuhusu sekta ya Madini wakati wa maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba 2014. Anae msikiliza ni Bw. Issa Mtuwa Afisa Uhusiano wa STAMICO. 

 “Nashauri Watanzania tuache ubinafsi na ubepari. Naishauri serikali Migodi yote ya Madini yenye RESERVE (akiba) kubwa imilikiwe na STAMICO kwa niaba ya Watanzania badala ya kukabidhi kwa Watanzania wachache wenye tamaa ya utajiri ambao wanamiliki vitalu vya madini kupitia migongo ya kampuni za kigeni” alisema Bwana Joel kwa kuandika kwenye kitabu maalum cha Maoni, ushauri na kero za Wananchi. 

 Naye Jacqueline Aisaa mkazi wa Masama-Moshi, ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa tatu wa Shahada ya kwanza katika Chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) alisema serikali iipe meno STAMICO ya usimamizi wa hisa zote za serikali kwenye migodi yote na usimamizi wa jumla katika sekta ya Madini ili Wananchi waweze kunufaika na raslimali hizo.

CHADEMA KIGOMA YAENDELEA KUPASUKA,VIGOGO WAHAMIA ACT


Na Magreth Magosso wa KAPIPIJhabari.COM-Kigoma


Aliyekuwa Mwenyekiti  na Katibu wa  Chama  cha  Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) mkoani hapa,wamen`gatuka rasmi jana na kuhamia chama cha Alliance Conservative For Transiparecy(ACT),kwa lengo la kukuza demokrasia ya chama hicho.


Hayo yamebainika kigoma ujiji  katika ofisi ya chama cha wandishi wa habari mkoani humu(KGPC) ,ambapo viongozi hao  walifika katika ofisi hiyo kwa dhima ya kutangazia umma kuwa wao si wafuasi wa chama cha chadema.


Miongoni mwa waliokuwa viongozi wa mkoa  ni pamoja na Mwenyekiti  Jaffar Kasisiko,Katibu Msafiri  Wamalwa sanjari na katibu wa baraza la wanawake chadema  Malunga Simba sambamba na wanachama wawili waliokuwa chama hicho.


Jaffar Kasisiko alisema  kukihama chama hicho hakina uhusiano na Mbunge wa jimbo la kigoma kaskazini Zitto Kabwe bali ni kutokana na urasimu,ubinafsi na utashi wa viongozi wa chama hicho hasa mwenyekiti wa chama husika.


“sijutii kuachia ngazi ,najua watahisi namfuata Zitto,ukweli aliyenivuta kisiasa ni Mwenyekiti wa ccm mkoa Dr.Kabourou enzi hiyo chadema ni taifa kubwa haswa   ,sitaki cheo napenda niwe mshauri wa chama hicho lengo kubadilisha fikra mpya” alibainisha Kasisiko .


Ashauri vyama vya siasa  viepuke  migogoro isiyo na maslai ya umma na chama ,hali inayochangia kushindwa kushika hatamu katika chaguzi za kitaifa na kutaka  viwajibishe wanachama kwa katiba husika na si utashi.


Kwa upande wa Msafiri Wamalwa na Malunga Simba kwa nyakati tofauti walisema chama hicho sawa na timu ya Brazili , hakina tija na umma bali kipo kwa masali ya wachache.


Aidha Aprili,4,2014 Mlezi wa   chadema mkoa  Aidan Ndowa amekiri chama kipo katika  wakati mgumu ambapo kati ya viongozi 209 walipo kigoma , viongozi  99 kutimkia  chama cha ACT.

Ndowa alisema hao waliojiengua leo(jana) ni miongoni mwa hao 99 waliowabaini kwenye tathimini yao ya uhalisia wa uhai wa chama,wakati huohuo chama cha ACT kimechukua kata 8 kati ya 11 zilizokuwa za chadema kati ya kata 19 zilizopo manispaa ya kigoma ujiji.

Juma Ramadhan mratibu wa chama cha ACT anakiri chama hicho kina mvuto kwa umma husika ambapo kwa sasa wana wananchama 7,000 na kudai  hitaji la kadi ni 10,000 kwa wakazi wa manispaa ya hiyo.

Katibu Taifa chama cha NRA na katibu mwenezi  ccm mkoa Kalembe masoud kwa nyakati tofauti wakiri baadhi ya viongozi wa chama hicho wajiunga na ACT baada ya kuvuliwa nyadhifa kwa mbunge wa jimbo la kigoma kaskazini na mfumo wa ubinafsi wa chadema.

Thursday, July 17, 2014

ZIARA YA RAIS KUFUNGUA NYUMBA ZA GHARAMA NAFUU MKUZO, SONGEA


Rais Jakaya Kikwete na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Mh. Saidi Mwambungu kulia , Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa shirika la Nyumba NHC Bw. David Shambwe wakikata utepe kwa pamoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi huo.
 Rais Dr. Jakaya Kikwete akipata taarifa ya mradi huo wa nyumba za gharama nafuu kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa shirika la Nyumba NHC Bw  David Shambwe
  Rais Dr. Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo 
 Rais Dr. Jakaya Kikwete akiwasili  katika eneo la mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na Shirika la Nyumba  (NHC) na kupokelewa na Ndg. David Shambwe Kaimu Mkurungenzi Mkuu NHC na Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara wakati alipokagua mradi huo uliopo katika wilaya ya Songea mkoani Ruvuma  akiwa katika ziara yake ya kikazi leo, Rais Dr. Jakaya Kikwete anaendelea na ziara mkoani  humo leo. (PICHA ZOTE KWA HISANI YA KITENGO CHA MAWASILIANO NA HUDUMA KWA JAMII CHA NHC)
 Rais jakaya Kikwete akipata maelezo ya kuhusu Mashine za kufyatulia matofali  ambazo zimegawiwa kwa kila wilaya za mkoa wa  Ruvuma
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka akizungumza katika hafla hiyo mchana huu
 Akiwasalimia wananchi waliofika kushuhudia
Vikundi vya nguma na burudani ikiburudisha katika tukio hilo mchana wa leo

"MBUNGE ADAIWA KUMPIGA BABA YAKE MZAZI"-KASULU

Na Magreth Magosso,Kigoma


MBUNGE wa Jimbo la Kasulu mjini Moses Machali anatuhumiwa kumtwanga baba yake mzazi  Mzee Machali  sambamba na kumfukuza nyumbani kwake,kutokana na kitendo chake cha kulewa kupindukia ambayo imekuwa adha kwa mbunge huyo na kupelekea mgogoro mkubwa baina yake na mzazi  huyo .


Mbunge huyo amefikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na ulevi huo na kupelekea kumpa kichapo kilichosababisha kuteguka kwa mkono  sanjari na kumtupia nguo zake nje na hatimaye mzee huyo kukimbilia kwa Balozi wa nyumba kumi  Dickson Joaqim kwa msaada wa kisheria.

Awali Julai ,15, 2014 usiku mzee alichelewa kurudi nyumbani na alipomgongea mwanae afungue mlango ndipo akapata kichapo kutoka kwa mbunge huyo baada ya kuona adha hiyo ni sugu kwa mzee wake.


Mwandishi wa KAPIPIJhabari.COM mkoani Kigoma  amemuhoji mbunge huyo  ambapo alisema mzazi wake  anapenda kunywa pombe kupindukia hali inayomfanya kila wakati wagombane juu ya tabia hiyo ambapo kwa upande wa pili kisiasa inamuathiri katika uwajibikaji wake kwa wananchi.


Alisema baba yake anatumiwa na chama  cha ccm  kwa lengo la kumdhoofisha kisiasa hasa katika kipindi hiki cha majeruhi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwakani na kumtaja balozi wa mtaa wa mwilavya  Dickson Joaqim ni miongoni mwa watu wanaomshawishi mzee wake  kituo cha polisi kumshtaki.


“sijafikia hatua ya kumpiga mzee wangu,najitambua ndio maana namsihi baba achane na pombe ambapo mimi najiskia vibaya kuona  analewa sasa tukiwekana sawa baadhi ya watu wanadai nampangia sheria na ndo hivyo wanazusha ya kuzusha” alibainisha Machali.


Alisema kwa  kuthibitisha  hilo umma kuwa hajampiga mzee wake  na kwenye  mkutano wa hadhara wilayani hapo, atakuwa sambamba na mzee huyo na kukiri mzee wake amefuta kesi dhidi yake na kusisitiza ccm  watumie mbinu za ziada na kudai hawana jipya.

Shuhuda mmoja jina kapuni akiri kumuona  mzee huyo akiwa na `PF3' akitembea kwa shida huku mkono wake ukiwa umevimba akipatiwa matibabu katika moja ya zahanati ya wilayani hapo


Akithibitisha  tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Frasser Kashai alisema ni kweli mzee wake alifungua jalada la kumshataki mbunge huyo,pamoja na kupatiwa maelezo ya watu walioshuhudia tukio hilo ingawa Mbunge huyo nae alipatikana na kutoa maelezo.
Hata hivyo Kamanda Kashai alisema wakati Jeshi la Polisi likiandaa taratibu za kuwapeleka mahakamani,mlalamikaji  Mzee Machali aliomba waende nyumbani wakafanye suluhu kifamilia hatua ambayo haikupingwa na Polisi.
"Baada ya Mzee wake kuamua hivyo sisi kama Jeshi la Polisi tuliona hatuna namna ya kufanya kwakuwa hatuwezi kumlazimisha mlalamikaji kwenda mahakamani wakati mwenyewe hataki na pia tuliangalia ukubwa wa tatizo,tukaona kuwa wamefanya uamuzi mzuri kuyamaliza kifamilia"alisema Kamanda Kashai. 

TAARIFA RASMI KWA WAANDISHI WA HABARI KUTOKA CCM

2
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Jana tarehe 16/07/2014 Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ilifanya kikao cha kawaida cha siku moja mjini Dar es salaam. Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete.

Pamoja na mambo mengine kikao hicho kilipokea taarifa ya mazungumzo yanayoendelea kati ya CCM kwa upande mmoja na CHADEMA, CUF na NCCR-Mageuzi kwa upande wa pili.

Mazungumzo hayo yanayosimamiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Jaji Francis Mutungi yana lengo la kuangalia kwa kina ni kwa nini baadhi ya wajumbe wachache wa Bunge Maalum la Katiba walisusia na kutoka nje katika awamu ya kwanza ya Bunge hilo, na kuangalia namna watakavyorudi ili kukamilisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba nchini.

Kwa ujumla Kamati Kuu ya CCM imeridhishwa na mwenendo wa mazungumzo hayo na kupongeza juhudi hizo zilizofanywa na Msajili wa Vyama vya Siasa na Vyama husika. Kamati Kuu inapenda kueleza imani yake kuwa mazungumzo hayo yatazaa matunda kwa wajumbe wachache waliosusia Bunge Maalum la Katiba, kurejea Bungeni na kumalizia sehemu ya mchakato uliobakia. 

Kamati Kuu inayatakia kila la kheri mazungumzo hayo.
Kamati Kuu pia ilipokea taarifa za harakati za baadhi ya wanachama wa CCM walioonesha nia ya kuomba ridhaa ya CCM kugombea Urais. Baada ya kutafakari kwa kina, Kamati Kuu inapenda kuwakumbusha wote kuwa ili wasipoteze sifa za kugombea, ni muhimu wakazingatia Katiba, Kanuni na taratibu za Chama zinazosimamia masuala hayo.

Kuhusu wale waliopewa adhabu na Kamati Kuu kutokana na kukiuka baadhi ya taratibu za Chama kwa suala hili, Kamati ya Usalama na Maadili ya Chama itafanya mapitio ya mwenendo wao wa utekelezaji wa adhabu hiyo mwezi wa nane (Agosti 2014), na kama itabainika kuwa hawatekelezi ipasavyo masharti ya adhabu zao, itapendekeza kwa Kamati Kuu kuongezwa kwa adhabu kulingana na ukubwa wa uvunjaji wa masharti ya adhabu husika.

Ni muhimu wanachama wote wakakumbuka kuwa Chama ni pamoja na Katiba, Kanuni na taratibu zake, hivyo kutoziheshimu na kuzifuata ni kukivuruga, jambo ambalo halivumiliki.

Nia ya CCM kusimamia haya ni kuhakikisha Chama kinakuwa na umoja na mshikamano ambao ni muhimu sana, hasa tunapoelekea kukamilisha kazi ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2010/2015 na Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
 
 Aidha, Kamati Kuu imewatakia kheri na fanaka Watanzania wote wakati huu wanapomalizia mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Imetolewa na:-
 Nape M. Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
17/07/2014

MTOTO WA MIAKA MINANE ADAIWA KULAWITIWA NA MWENDESHA BODABODA,MZAZI ALALAMIKIA POLISI KUMPA DHAMANA MTUHUMIWA

Mtoto mwenye umri wa miaka minane jina limehifadhiwa anadaiwa kufanyiwa kitendo cha kulawitiwa na mtu mmoja ambaye amemtaja kuwa ni mwendesha Bodaboda ya baiskeli.Katika maelezo yake mtoto huyo anadai akiwa  anatoka shule na mwenzake njiani walisimama wakawa wanaokota matunda(Ntalali)ghafla mtuhumiwa alitokea na kumtaka mtoto huyo ampeleke nyumbani kwao kwakuwa alikuwa wakifahamiana kabla ya hapo.Mtoto alisema alikubali kuondoka na bwana huyo na kupakizwa kwenye baiskeli hadi eneo la maficho karibu na mlima na ndipo alianza kufanyiwa kitendo hicho.Baada ya kurejea nyumbani mtoto huyo alimweleza mama yake mzazi  na kuanza harakati za kufika  kituo cha Kikubwa cha Polisi.Hatua za kumkamata mtuhumiwa zilifanyika ingawa aliachiwa kwa dhamana jambo ambalo mama mzazi wa mtoto huyo amelilalamikia huku akidai kuwa huenda kuna hujuma dhidi ya kitendo kibaya alichofanyiwa mtoto wake.

WANANCHI WAKOMAA NA MANISPAA-KIGOMA UJIJI

Na Magreth Magosso,Kigoma

TATIZO la mgogoro wa  ardhi baina ya wananchi na mwekezaji katika eneo la kituo cha Afya cha Kakunku kata ya Gungu Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani hapo,limebaki kuwa sintofahamu kutokana na serikali kushindwa kuthibiti mgogoro huo.

Mgogoro huu wa kugombea ardhi baina yao na mwekezaji wa taasisi ya kuhudumia makanisa mkoani Kigoma (JOY IN THE HARVEST) lipo kwa miongo saba,ambapo imepelekea wananchi  kuwa na mashaka ya kuporwa  eneo hilo  ambalo kwa sasa kuna ujenzi wa uzio ili kudhibiti vibaka wanaopora mali za watumishi na wagonjwa katika kituo hicho.

Pamoja na wananchi kutetea eneo hilo ,ambalo ni chachu ya kupunguza  vifo vya uzazi na umbali kwa kina mama kufuata huduma hiyo katika hospitali ya mkoa maweni, ambapo kituo hicho kinatoa huduma ya matibabu kwa zaidi ya kata tano.

Tukio la mwekezaji kutumia vyombo vya dola na kubomoa uzio wa kituo hicho cha afya kimewapa wakati mgumu wananchi na kuomba manispaa kutatua tatizo hilo ili wapate haki ya kutibiwa katika kituo hicho kilichokaribu na wakazi wa kata hizo,  ambapo Julai ,11,2014 mwenyekiti wa mtaa wa Kikunku na wajumbe wawili watupwa mahabusu kutokana na mgogoro huo.

Bakari Genda,Ladslausi Mugabo,Hamis Paya,Crispian Daniel na Chaila Richard ni  kamati ya wafuatiliaji  wa sakata hilo watakiwa kumlipa fidia  ya usumbufu kwa mwekezaji  huyo kiasi cha sh.milioni 600 na kutoa maelezo zaidi ya  mara tano kituo cha polisi kati mkoani hapo.

“Manispaa yenyewe inajichanganya awali walijenga kituo cha wagonjwa wa kipindupindu katika eneo hilo pia wameweka eneo la mapumziko ya wagonjwa katika eneo hilo na wanatarajia kufanya ujenzi wa wodi ya upasuaji kwa kina mama,pia wameleta mkandarasi kwa ajili ya uzio na wakamuonyesha mipaka cha ajabu baada ya ujenzi asubuhi tunakuta pamebomolewa yani hatuelewi kunanini kati ya manispaa na mwekezaji huyo” walieleza wahanga hao.

Wakizungumzia hilo Hadija Issa,Christina Bugabo,Mnyonge Juma na Sophia Issa washangaa serikali kuuza eneo ndani ya kituo cha afya na kukiri uwepo wa kituo ni tija kwao kiafya na kiuchumi,awali walitozwa sh.20,000 za usafiri kutoka eneo la gungu hadi katika hospitali ya rufaa ya Maweni kwa ajili ya kujifungua .

Akifafanua hilo Mwenyekiti wa mtaa Manga Said ambaye pia ni mwenyekiti wa bodi ya afya wa zahanati hiyo, akiri kuwepo kwa mgogoro huo ambapo imeonekana kuwepo kwa utata baina ya wananchi na manispaa kutokuwa wawazi katika mgogoro huo.

 “wandishi semeni uhalisia wa tukio ,kwa nini wakumbatie hili kwa miongo kadhaa,mwekezaji aliuziwa pasipo jamii kujua, ije izungumze na raia wake  aseme kweli  na si kupatiwa vitisho bali tukae chini na kutatua tatizo lililopo “ alisema Saidi. 

 Mujibu wa wakazi hao na viongozi wanadai agizo la waziri wa tamisemi Hawa Ghasia limepuuzwa la kuhakikisha mgogoro huo unatatuliwa ikiwa ni pamoja na kuweka uzio katika kituo hicho cha afya.
Kwa upande wa mkuu wa Wilaya ya Kigoma Ramadhani Maneno na katibu wa chama cha NRA taifa Hamisi Kiswaga  alitoa wito kwa manispaa kutatua mgogoro huo kwa kuzungumza na mwekezaji huyo ikiwa ni pamoja na kumlipa fidia au kupatia eneo mbadala ili eneo hilo libaki kuwa kituo cha afya kwa faida ya wananchi wa eneo hilo.
Aidha mwekezaji wa eneo hilo, ameeleza kuwa eneo hilo analimiliki kihalali kwa kwa mujibu wa sheria za manispaa kwa muda mrefu ambapo hatua za ulipiaji wa eneo hilo risiti zipo na inatambuliwa kuwa eneo hilo lipo chini ya taasisi hiyo ya kidini.

Hata hivyo afisa mipango miji manispaa ya Kigoma ujiji alisema eneo hilo halina mgogoro, eneo la mwekezaji lipo na linajieleza pamoja na eneo la zahanati tatizo lililopo ni manispaa kuweka ujenzi wa eneo la kupumzikia katika eneo la mwekezaji huyo jambo ambalo litafanyiwa marekebisho.

WAZIRI MAKALLA ATOLEWA CHINI YA ULINZI WA POLISI BAADA YA MKUTANO WAKE KUFANYIWA VURUGU NA CHADEMA

 Gari lililombeba Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla, likilindwa na polisi lililopokuwa linaondoka baada mkutano wa hadhara kuvunjika kulikosababishwa na vurugu ambazo waziri alidai kuwa zilipangwa kwa makusudi na wafuasi pamoja na viongozi wa Chadema waliokuwa wakirumbana na viongozi wa CCM, katika Kata ya Goba, Kinondoni, Dar es Salaam. Makalla alikuwa katika ziara ya kukagua miradi ya maji katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
 Makalla akijadiliana na maofisa wa CCM na Polisi kabla ya kwenda kupanda gari na kuondoka.
 Poilisi wakiwadhibiti baadhi ya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakisababisha vurugu katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Makongo. Kinondoni.
 Polisi wakimdhibiti mmoja wa viongozi wa Chadema wakati wa mzozo uliotokea jukwaa kuu katika mkutano wa Naibu Waziri wa Maji, Makalla na wananchi wa Kata ya Goba.
 Kiongozi wa cHADEMA AKIZOZANA NA WA ccm jukwaani katika mkutano wa Makongo Juu.
 Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee akizoza jukwaani katika mkutano uliofanyika katika Kata ya Goba na hatimaye kuvunjika
 Polisi wakimdhibiti mfuasi wa Chadema asiendelee kufanya fujo katika mkutano wa Waziri na Wananchi wa Kata ya Goba
 Askari wa FFU, akilinda doria wakati waziri Makalla akikagua nyumba ambazo watu wamejiunganishia isivyo halali eneo la Bonde la Msimbazi, Dar es Salaam.
 Makalla na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (kushoto) wakiangalia pampu zinazotumika kujazia maji kwenye malori yanayonyonywa kutoka kwenye mabomba ya Dawasa. Pampu hizo zilinaswa uani mwa nyumba katika eneo la Bonde la Mto Msimbazi Dar es Salam
 Waziri Makalla na viongozi wengini wakishanga kuona tanki kubwa la maji lililojengwa chini ya moja kati ya nyumba tano katika eneo hilo ambazo wamiliki wake wamejiunganishia maji ya Dawasa  isivyo halali
 Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (kulia), akimhoji mchezaji wa zamani wa Simba, Dua Said ambaye alikuwa miongoni mwa watu watano waliokamatwa kwa tuhuma za kujiunganishia maji isivyo halali  kutoka kwenye mabomba ya Mamlaka ya Maji Safi na Taka (Dawasa), kwenye nyumba zao zilizopo Bonde la Mto Msimbazi, Kigogo, Dar es Salaam. Makalla alikuwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya maji Dar es Salaam
 Askari wakilinda doria katika eneo hilo
 Moja ya malori yanayojazwa maji katika eneo hilo. Nalo liko chini ya ulinzi
 Waziri Makalla akielezea athari zinazotokana na wizi huo wa maji ambapo alisema kuwa katika nyumba hizo tano kila siku wanaiba maji lita laki tatu, hivyo kila siku kuikoseasha serikali mapato ambapo kwa mwezi yanafikia sh. bil 1.4.
 Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika akielezea jinsi atakavyoshirikiana na Serikali katika mapambano dhidi ya ufisadi wa maji jijini na kwamba atakuwa bega kwa bega kuhakikisha mswada wa adhabu kubwa kwa wezi wa maji unapelekwa Bunge la Novemba mwaka huu.
 Mchaezaji wa zamani wa Simba, Dua Said akielezea kwa wanahabari na mbele ya Waziri Makalla, jinsi anavyoshirikiana na Shirika la Maji Safi na Taka Dar es Salaam (DAWASCO), katika biashara ya kuuza maji. Dua Said alikuwa ni miongoni mwa watu watano waliokamatwa kwa tuhuma za kujiunganishia maji ya Dawasco isivyo halali katika eneo la Bonde la Msimbazi
 Bomba jipya la maji likitandazwa eneo la Makongo tayari kwa maandalizi ya kusafirisha maji kutoka Mtambo wa Ruvu Chini ambao upanuzi wake umekamilika hivi karibuni.
 Makalla akiuliza swali kwa wakandarasi kuhusu utandazaji wa bomba hilo, wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maji Dar na Pwani.
 Waziri Makalla akiwa na Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee, Mwenyekiti wa CCM, Salum Madenge, (KUSHOTO)  Deusdedit Mtiro (kulia) walipokuwa wakimlaki alipowasili kwenye mkutano katika Kata ya Makongo.
 WAFUASI WA CHADEMA WAKISHANGILIA NA KUMTAKA WAZIRI AWAHAKIKISHIE UPATIKANAJI WA MAJI MAKONGO JUU
 Chadema na CCM wakishangilia katika mkutano huo
 Waziri Makalla akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Makongo
 Moja wa wananchi akilalamika mbele ya waziri kuhusu adha kubwa wanaipata ya maji eneo la Makongo juu
 Msafara wa viongozi wa Chadema na CCM ukielekea kwenye mkutano wa wananchi katika Kata ya Goba ambao hata hivyo ulivunjika baada ya kutokea vurugu
 WanaCCM wakimshangilia Waziri Makalla alipokuwa akihutubia wananchi katika Kata ya Makongo
 Chadema wakishangilia wakati Halima Mdee akihutubia Makongo Juu
 Mfuasi wa Chadema akilalama
 Mdee akizungumza na wanahabari baada ya mkutano wa Kata ya Goba kuvunjika
 Wana CCM WAKISEREBUKA
 MNYIKA AKIZUNGUMZA NA WAFUASI WA cHADEMA BAADA YA MKUTANO KUVUNJIKA