Mmoja
wa wasanii mahiri katika miondoko ya hip hop hapa nchini,Mwana FA
akiwaimbisha wakazi wa mji wa Tabora wimbo wake wa Yalaiti,usiku wa
kuamkia leo katika viwanja vya Ally Hassan Mwinyi,ambapo wakazi wa mji
huo walijitokeza kwa wingi.
Msanii
wa muziki wa kizazi kipya Mabeste akikamua kwenye tamasha la Serengeti
Fiesta 2012 usiku wa kuamkia leo kwenye uwanja wa Ally Hassan
Mwinyi,ambapo katika tamasha hilo wakazi wa mji wa Tabora walijitokeza
kwa wingi na kujishuhudia vipaji mbalimbali vya muziki.
Wakazi
wa Tabora walioamua kujiachia kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012
wakishangwaka vilivyo usiku wa kuamkia leo,tamasha hilo limefanyika jana
katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi,aidha tamasha hilo siku ya jumapili
litakuwa linarindima ndani ya Singida Motel,mkoani humo.
Nikki Mbishi akishusha mistari yake mbele ya wakazi wa mji wa Tabora.
Namna wakazi wa mji wa Tabora wakiwa ndani ya uwanja wa Ally Hassan Mwinyi wakati tamasha la Serengeti Fiesa lilipokuwa linaondoka.
Dj Zero kutoka Clouds FM akikamua katika moja ya mashine za kisasa akikonga nyoyo za wakazi waliofulika ndani ya uwanja wa Ally Hassan Mwinyi,na kulia kwake ni Hamza Balla,
Moja wa zao la Serengeti Fiesta 2012,Supa Nyota Ney Lee akitumbuiza jukwaani.
Msanii Recho akionesha umahiri wake wa kunengua jukwaani akisindikizwa madensa wake.
Palikuwa hapatoshi ndani ya Tabora usiku wa kuamkia leo.
Rich Mavoko akiliongoza skwadi lake kusakata kiduku
Mbunge
wa Tabora Mjini,Mh Ismail Adeni Rage akisoma moja ya namba ya aliyebahatika
kuibuka na bajaji,kulia kwake ni Mkuu wa utafiti wa Clouds .TV,Ruge
Mutahaba.
NI full mzuka mwanzo mwisho kwa mashabiki wa Fiesta Tabora.
Sir Juma Nature akikamua usiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2012
Hamza Balla na marafiki zake wakiwa wamepozi ndani ya tamasha la Fiesta usiku wa kuamkia leo.
No comments:
Post a Comment