Pages

KAPIPI TV

Monday, August 13, 2012

MAJAMBAZI YAMJERUHI BABU KWA RISASI,MSTAAFU JWTZ AJERUHIWA VIBAYA NA KUMPORA BAISKELI

 Mzee Rashidi Ndyuki mkazi wa Nyakato-Masagala akiwa amelazwa  hospitali ya mkoa wa Tabora Kitete kufuatia kujeruhiwa kwa kupigwa risasi kwenye goti la kushoto na kupigwa nondo kichwani na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi baada ya kumvamia katika nyumba aliokuwa akiishi huko Nyakato,majambazi hayo yalimpora kuku wapatao kumi na sanduki la nguo zake.  
 Sehemu ya mguu wa Mzee Ndyuki uliojeruhiwa kwa risasi
 Mzee Nduki akiwa amekaa kitandani Wadi namba moja akisubiri matibabu
Mstaafu wa Jeshi la wananchi Jwtz Tabora,Bw.John Manumbu ambaye ni mkazi wa Nyakato akiwa amelazwa hospitali ya Kitete kufuatia kuvamiwa na watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi wakati akiwa njiani akitokea mjini Tabora majira ya saa moja na nusu usiku ambapo majambazi hayo yalimjeruhi kwa kumpiga maeneo mbalimbali ya mwili wake kiasi cha kufanya apoteze fahamu na kisha kumpora Baiskeli,mafuta ya kupikia na shilingi elfu tano. 

No comments: