Pages

KAPIPI TV

Tuesday, May 29, 2012

MKUTANO WA JUWASAWINGO NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU BARABARA YA MTOWAMBU-LOLIONDO/MUGUMU

 Makamu Mwenyekiti wa JUWASAWINGO Bw.Onesmo Ole Ngurumwa akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari

MKUTANO NA VYOMBO VYA HABARI- UBUNGO PLAZA 27 MEI, 2012
UMUHIMU WA BARABARA YA  MTOWAMBU-LOLIONDO/MUGUMU-MAKUTANO KWA WANANCHI WA  WILAYA YA  NGORONGORO NA  TANZANIA

JUWASAWINGO ni umoja  wa watu wa Wilaya ya  Ngorongoro, waliojitoa kutetea maslahi ya jamii ya wanangorongo ambao wamekuwa pembezoni kimaendeleo kwa miaka mingi. Jukwaa hili huwaunganisha  wanangorongoro wenye taaluma mbalimbali kama wanachama ambao kwa sasa wanafikia 2000. Na wanachama wa Jukwaa hili wanatoka vijiji vyote vya Wilaya Ngorongoro.

Kutokana na kuguswa sana na suala zima la ujenzi wa barabara ya lami inayounganisha mikoa ya Arusha na Mara,  Wana-JUWASAWINGO wanapenda kuweka wazi maoni na msimamo wa  Wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro juu ya suala hilo.

JUWASAWINGO imetambua kuwa kwa miaka mingi sasa, serikali yetu imekuwa na nia nzuri ya kujenga barabara ya Mtowambu-Loliondo/Mugumu Makutano ambayo itawanufaisha wakazi wa Wilaya za Ngorongoro, Monduli, Longido  , Serengeti  na Tanzania  kwa ujumla.

Tunaamini kwa dhati kuwa upinzani wowote juu ya  ujenzi wa barabara hiyo,  uwe unatoka kwa nje ya nchi au ndani, kwa watu binafsi au vikundi vya watu,  unapingana na matakwa ya wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro.Wapinzani hawana, hawajui au wameamua kuupuuza ukweli wa mambo juu ya mradi huo wa barabara.

Serikali imekuwa ikifikiria kuijenga barabara hiyo  tangia miaka ya mwanzo ya 1980. Katika miaka ya karibuni, serikali iliibua upya kusudio lake hilo na ikaamua kuendelea na utekelezaji wa mpango wa ujenzi huo uliowekwa pembeni kwa siku nyingi.

Wapinzani wa mpango huu wamekuwa wakijifanya kuifahamu jiografia ya eneo hili la nchi yetu kuliko wenyeji na wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali ili kuungwa mkono na jamii ya kimataifa ikiwemo mbinu ya kuibatiza kimakosa barabara hiyo na kuiita”Barabara Kuu ya Serengeti” au kwa Kiingereza “Serengeti Super Highway”!
 






No comments: