Wakili Bernadetha Mkandya ambaye pia ni mwanachama wa Chama cha
Wanasheria wanawake TAWLA akizungumza katika semina ya waandishi wa
habari kutoka vyombo mbalimbali iliyoandaliwa na TAWLA inayozungumzia
Mabadiliko ya Katiba na haki ya Afya ya Uzazi inayofanyika kwenye
Hoteli ya Blue Pear Ubungo Plaza jijini Dar es salaam.
Moja ya mada zilizochukuwa muda mrefu kujadiliwa ni kuwa katiba mpya
izungumze wazi kwamba haki ya mtoto wa kike atambulike kuwa ni mtu
mzima akiwa na miaka 18 na pia izungumze wazi juu ya elimu ya mtoto wa
kike, kuwa angalau apate elimu kufikia kidato cha nne.
Pia washiriki wanapendelea kuwa katika katiba iundwe tume ya kushughulikia masuala ya jinsia ya Mwanamke na mwanaume.
Wakili Bernadetha Mkandya ambaye pia ni mwanachama wa Chama cha Wanasheria wanawake TAWLA aakifafanua jambo katika semina hiyo.
Baadhi ya
waandishi wa habari wakiwa katika semina hiyo kutoka kulia ni Martha
kutoka TBC, Oscar Mbuza Habari Leo na Jane Mihanji Uhuru.
No comments:
Post a Comment