Pages

KAPIPI TV

Tuesday, August 26, 2014

HOFU YA EBOLA,KIGOMA WAANZA KUCHUKUA TAHADHARI

 
Na Magreth Magosso,Kigoma

Kufuatia hofu ya ugonjwa wa Ebola,Serikali mkoani Kigoma imeanza kuchukua hatua za makusudi kwa kutoa elimu kwa kuwatangazia  wananchi mkoani humo waweze kujihadhari na ugonjwa huo hatari kutokana na kuwepo kwa muingiliano wa watu mbalimbali kutoka nchi jirani.

Akifafanua hilo kigoma ujiji jana mbele ya wandishi wa habari, Mkuu wa mkoani wa Kigoma kanali mstaafu Issa Machibya alisema kutokana na mwingiliano na mahusiano ya nchi jirani za DRC-Congo na Burundi  kuna uwezekano mkubwa ugonjwa huo kuingia nchini kupitia mkoani humo hali inayolazimu kuanza kuchukua hatua za tahadhari  kwa kutoa elimu umma.
 
Kanali Machibya ametoa  maelekezo kwa katibu tawala mkoani humo,atafute  gari lenye uwezo wa kubeba vipaza sauti ili utekelezaji wa zoezi la kutangaza kuhusu janga la ugonjwa huo hatari liendelee kwa muda wa siku tatu mfululizo katika manispaa ya Kigoma Ujiji na wilaya zote za mkoa huo na hasa kwa vijiji vilivyojirani na mpakani.    
 
Akithibitisha hilo Katibu tawala wa Mkoa wa Kigoma Eng.John Ndunguru alisema mchakato huo unaanza leo(jana) kwa mujibu wa maelekezo kutoka wizara ya afya juu ya kujihami  na ugonjwa huo  sanjari na viashiria kwa wahanga wa maradhi hayo kulingana na mwingiliano wa raia ili hali  tiba maalum haijathibitika.
 
Alibainisha kuwa wamekusudia kuyadhibiti maeneo yote ya mialo,uwanja wa ndege kwa kufanya ukaguzi kwa watu waingiao sambamba na kutoa elimu ya ugonjwa huo na dalili zake wakatihuohuo vifaa na mavazi ya wataalam vipo tayari kwa mganga mkuu Kigoma.

No comments: