Pages

KAPIPI TV

Monday, August 6, 2012

MSTAHIKI MEYA JERRY SILAA AJITOSA KUGOMBEA UVCCM TAIFA

Mstahiki Meya wa manispaa ya Ilala Bw.Jerry Silaa akimkabidhi fomu  za kugombea nafasi ya ujumbe wa UVCCM-NEC kwa katibu wa UVCCM mkoani Mwanza Bw Elias Mpanda, jana katika ofisi za CCM Jijini Mwanza. 
 
Mstahiki meya wa Manispaa ya Ilala Bw Jerry Silaa anagombea nafasi ya ujumbe wa UVCCM-NEC ngazi ya taifa.
 
Katika kauli yake Mstahiki meya  Bw.Silaa aliweka wazi nia yake ya kutaka kuwawakilisha vema vijana wa kitanzania kwenye UVCCM-NEC na huku akiwaasa vijana wengine nchini  kushiriki kwenye mchakato huo na  kwamba yuko tayari kufanya kazi kokote nchini kwa maslahi ya wananchi, 
Katika hatua nyingine Mstahiki  meya huyo alitumia fursa hiyo kuwaasa  viongozi wa kada mbalimbali nchini kuwajibika na kutimiza ahadi zao walizozitoa kwa wananchi huku wakiweka mbele   maslahi ya taifa na sio yao binafsi.


No comments: