Pages

KAPIPI TV

Thursday, June 7, 2012

MTAALA WA KUTETEA WAANDISHI WA HABARI WAWAPO KAZINI


MWENYEKITI Mstaafu wa clabu ya waandishi wa habari mkoa wa Morogoro Boniventure Mtalimbo, ameviasa vyuo vya uandishi wa habari nchini, kuwa na mtaala wa masomo unaojali ulinzi na usalama kwa wandishi wanapokuwa kazi.

Rai hiyo ameitoa rai, wakati akichangia maoni kwenye warsha ya waandishi wa habari iliyoandaliwa na mtandao wa jinsia Tanzania (TNGP), yenye lengo la kuimarisha zaidi wajibu wa klabu za waandishi na redio jamii, katika kuandika na kuripoti habari za kijinsia kama sehemu ya kutangaza kampeni ya haki za uchumi ili rasilimali ziyanufaishe makundi yote wakati wa mchakato wa katiba mpya.

Mwandishi Tumain Msowoya anaripoti kuwa ,Mtalimbo alisema, ikiwa mtaala huo utaanzishwa kwenye vyuo hivyo utasaidia wanahabari kujua namna ya kujikinga na mambo mbalimbali hatarishi wawapo kazini.

Alitolea mfano katika chaguzi zilizopita, ambapo alisema kulikuwa na ulinzi mdogo kwa wanahabari hali ambayo inahatarisha maisha yao.

Aidha aliyaomba mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, Taasisi pamoja na wanaharakati wakishirikiana kwa pamoja kuangalia namna ya kuwapa waandisi wa habari mafunzo ya kujilinda.

Naye Mwandishi Mwandamizi wa gazeti la Mwananchi Venance George, alishauri wanahabari kuwa na bima ya maisha ili wanapopata matatizo ikiwemo kufariki wawapo kazini familia zao ziweze kutambuliwa na bima ili kupata haki stahiki.

“ Tunatakiwa tuwe na bima ya afya ili hata ukiuwawa uki kiwa kazini familia inabaki na kitu cha kuwasaidia, bila hivyo unakufa ukiwa kazini watoto na mke wanaendelea kuteseka”
Kwa upande wake Mwandishi wa habari wa Itv na Redio one John Chacha aliwashauri wanahabari kuwa na kazi mbadala ikiwemo ujasiliamali badala ya kutegemea habari pekee.
Hata hivyo, muwezeshaji wa ,mafunzo wa wanahabari Alisema kwa kufanya hivyo kutasaidia kukwepa kutumika na baadhi ya watu wanaotaka kunufaika kwa kutumia kalamu zao, na baadae kuwadharau.
Na Francis Godwin

No comments: