Mwenyekiti wa kampuni ya Wananchi Group kampuni inayosambaza
vin'gamuzi vya televisheni ya Zuku Afrika hapa nchini Bw. Ali Mufuruki
akizungumza katika hafla ya kutangaza kampuni hiyo ya Zuku Kudhamini
tamasha la kimataifa la Zanzibar International Film Festivala (ZIFF)
katika hafla iliyofanyika jana kwenye ufukwe wa Slipway jijini Dar es
salaam na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa tamasha la ZIFF wakiwemo
wanamuziki, waigizaji wadhamini na wengeni wengi.
Mmoja wa wasanii wa kundi la Shilole akitumbuiza mbele ya wageni mbalimbali waliohudhuria katika hafla hiyo jana jioni.
Waigizaji wa filamu mbalimbali wakiwa wamesimama mbele wakati
walipokuwa wakitambulishwa katika hafla hiyo na mwenyekiti wa ZIFF Bw.
Mahmoud Thabit Kombo.
Kutoka kulia ni Jacob Steven. Raymond Kigosi na Cloud waigizaji wa filamu za Bongomovie wakiwa katika hafla hiyo..
Mchekeshaji Steve Nyerere kulia akiwa na wadau kutoka kampuni ya kusambaza filamu ya Steps Entertainment.
Mwigizaji Jaquiline Walper kushoto akiwa na waigizaji wengine katika
hafla hiyo wa tatu kutoka kulia ni mchezaji wa timu ya Simba Uhuru
Selemani.
Mwigizaji Aunt Ezekiel kushoto akiwa na waigizaji wenzake.
Mwanamuziki Shilole akitumbuiza na kundi lake katika hafla hiyo.
Mwenyekiti wa ZIFF Bw. Mahmoud Thabit Kombo akiwatambulisha waigizaji pamoja na wasanii mbalimbali katika hafla hiyo jana.
No comments:
Post a Comment