Kichanga kilichotupwa katika moja ya Bar mjini Shinyanga na mwanamke mmoja ambaye hadi sasa bado hajafahamika, Picha na Shaban Alley - Shinyanga
Jeshi la Polisi mkoani Kigoma linamsaka mwanafunzi
mmoja wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Mwike mjini Kigoma
Bi. Rehema Issa(22) ambaye ni mkazi wa eneo la Kamara kwa tuhuma za
kujifungua na kukitumbukiza kichanga chake chooni.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo SSP Francis Mwakabana,
amesema kuwa kichanga hicho ambacho kiliokolewa na wanafunzi wa shule moja ya msingi kikiwa hai lakini kilifariki muda mfupi wakati
kilipokuwa kikipelekwa Hospitalini kwa matibabu.
Kufuatia tukio hilo, Kaimu Kamanada wa Polisi mkoani kigoma ametoa wito kwa
wananchi kuendelea kutoa taarifa za kuwafichua wahalifu ili wakamatwe na
kukabili mkono wa sheria.
0784 886488, 0715 886488, 0767 886488
No comments:
Post a Comment