Pages

KAPIPI TV

Friday, September 11, 2015

SIMON KAPUFI APANIA KULETA MAENDELEO MPANDA ENDAPO ATACHAGULIWA KUWA MBUNGE

Mgombea ubunge wa jimbo la mpanda Mjini Kwa Tiketi ya CCM Sebastia Kapufi akinadi SERA za chama chake na kuwaonyesha Ilani   ya chama hizo wananchi kwenye mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za Ubunge hawapo pichani katika  mkoa wa Katavi  uzinduzi uliofanyika viwanja vya  Mpanda HOTELI.
Mke wa Mgombea ubunge wa jimbo la Mpanda Mjini Bi Josephine Rupia akiwasalimia wananchi na kumwombea kura mmewe katika mkutano huo wa Kampeni
Umati wa wananchi waliofulika kwenye mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za ubunge kwenye viwanja vya Mpanda Hoteli Mkoani Katavi,wakati wa uzinduzi wa kampeni kuwanadi  wagombea ubunge na udiwani.
 (Picha zote na Kurugenzi ya Habari Wilaya ya Mpanda)

Mgombea ubunge wa jimbo la mpanda Mjini Kwa Tiketi ya chama cha Mapinduzi Sebastia Kapufi akinadiwa kwa wananchi na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi Abdalah Mselem kwenye mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za Ubunge kwa mkoa wa Katavi  uzinduzi uliofanyika viwanja vya  Mpanda HOTELI

 Na KIBADA
Mgombea Ubunge kwa tikekti ya CCM Jimbo la Mpanda Mjini Sebastian Simon Kapufi amesema iwapo atapatiwa ridhaa na wananchi  kuwa mwakilishi wao kwa nafasi ya mbunge  atashirikiana,na wananchi, madiwani na watalaam kwenye Halmashauri pamoja na Wadau wa kuhakikisha wanaleta maendeleo.
 

Kapufi amesisitiza kuwa elimu itakuwa  ni kipaumbele chake cha kwanza na iwapo  atapatiwa nafasi ya uwakilishi tajitahidi kushughulikia suala la uhaba wa madawati,mashuleni na tatizo la chakula kwa wanafunzi mashuleni, pia  atakuwa mbunifu kwa kubuni miradi itakayosaidia kuwaunganisha makundi ya vijana akina mama na wajasilia mali kuanzisha miradi ya ujasiliamali ili kuondokana na umasikini.
 

Awali Katibu wa CCM Mkoa wa KATAVI Avelin Mushi akaaeleza  kuwa kiongozi bora ni Yule asiyewagawa wananchi katika kuleta maendeleo,akakemea suala la udini,ukabila na ukanda kuwa suala hilo halina nafasi katika siasa za nchi hii,viongozi wa namna hiyo hawafai kupewa uongozi wananchi wajiepushe nao.
 

Awaomba wananchi wachague chamacha Mapinduzi ili kuleta maendeleo ya haraka nay a kweli.
Naye  Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi Abdalah Mselem kizungumza katika Mkutano huo amewataka wananchi kuchagua wagombea kutoka CCM kwa kuwa ndiyo chama pekee kitakachoendelea kuwaletea maendeleo na kudumisha amani ya nchi hii.
 

Mselem akatatumia mkutano huo kuwaomba  wale waliokihama chama hicho kutokana na kukosa nafasi baada ya kura za maoni kutotosha  wasihame badala yaka kama walikuwa wamekihama wareje waje wajengee chama na wale wa upande wapili akawaomba kura zao zote wakipigie chama cha mapinduzi na kisha warejea kwenye chama hicho waendelee kukijenga kwa kuwa waliokosa kura za maoni isiwe sababu ya kuhama cha hata wakiwa nje ya CCM hawawezi kupta mafanikio ni vyema wakarudi CCM.
 

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mpanda Beda Katani  amewaasa wananchi kukichagua chama cha mapinduzi kuhakikisha kinaendelea kuongoza kwa kuwa jimbo la mpanda mjini limepotea mikono mwa wapinzani kwa kipindi cha miaka kumi hivyo wanahitaji wananchi maendeleo ya dhati.

No comments: