Pages

KAPIPI TV

Tuesday, July 24, 2012

AZAM YAFUZU KUCHEZA NUSU FAINALI KOMBE LA KAGAME

 
Timu ya Azam FC imeibuka kidedea kwa kuifunga  mabao  matatu kwa moja timu ya Simba ya Tanzania katika michuano ya Kombe la Kagame iliyokuwa ikichezwa jioni hii katika uwanja wa Taifa jijini Dar-es-salaam hatua ambayo imeipa nafasi ya kuingia nusu fainali ya mashindano hayo ya klabu bingwa ya soka kwa nchi za Afrika Mashariki na kati. 

Mchezaji  wa Azam aliyeng'ara katika mtanange huo wa leo  alikuwa John Raphael Bocco maarufu ‘Adebayor’ aliyefunga mabao yote matatu, ambapo bao moja la kwanza alilifunga katika kipindi cha kwanza na mengine kipindi cha pili.

Aidha kwa upande wa mahasimu wao timu ya Simba ilijipatia bao la kufutia machozi kupitia mchezaji wake  Shomari Kapombe ambaye alilifunga bao hilo  kwa juhudi zake bina mnamo  dakika ya 53.

Sasa Nusu Fainali zote  katika mashindano hayo ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati zitafanyika keshokutwa Uwanja wa Taifa jijini  Dar es Salaam, ambapo Azam wataanza na Vita na baadaye Yanga na APR saa 10:00 jioni.
 
Katika mchezo wa leo, kikosi cha Azam kilikuwa na wachezaji ; Deo Munishi, Ibrahim Shikanda, Erasto Nyoni, Said Mourad, Aggrey Morris, Kipre Michael Balou/Ramadhan Chombo, Kipre Herman Tcheche/George Odhiambo ‘Blackberry’, Salum Abubakar, John Bocco, Ibrahim Mwaipopo na Khamis Mcha ‘Vialli’/Jabir Aziz.
 
Wakati kikosi cha wekundu wa msimbazi  Simba SC kilikuwa na ; Juma Kaseja, Haruna Shamte, Shomary Kapombe, Lino Masombo, Juma Nyosso, Mussa Mudde, Uhuru Suleiman/Kiggi Makassy, Mwinyi Kazimoto, Felix Sunzu, Haruna Moshi na Jonas Mkude/Amri Kiemba.

No comments: