Mkuu Mkoa Singida, Dk. Parseko Kone alifungua kikao cha 13 cha bodi ya barabara mkoa Singida
Meneja wa TANROADS Mkoa Singida, Yustaki Kangole akifafanua hoja juu ya ujenzi wa moja ya barabara zinazohudumiwa na ofisi yake
Kamati ya ulinzi na usalama, Ramadhani Isango (kushoto) na RPC Singida, Linus Sinzumwa (katikati), wakisikiliza kwa makini
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moshi Chang'a (Mbele kulia), DC wa Wilaya Iramba, Yahaya Nawanda(kushoto) na DC wa Wilaya Ikungi
Meneja wa TANROADS Mkoa Singida, Yustaki Kangole akifafanua hoja juu ya ujenzi wa moja ya barabara zinazohudumiwa na ofisi yake
Kamati ya ulinzi na usalama, Ramadhani Isango (kushoto) na RPC Singida, Linus Sinzumwa (katikati), wakisikiliza kwa makini
Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Moshi Chang'a (Mbele kulia), DC wa Wilaya Iramba, Yahaya Nawanda(kushoto) na DC wa Wilaya Ikungi
Sehemu ya Wajumbe wa bodi ya barabara mkoa Singida
Singida,
SERIKALI
imeagiza viongozi, watendaji na wataalamu kutoa elimu ya kutosha katika
maeneo ambayo barabara ya lami imejengwa, ili kuepuka uharibifu wa
alama za barabarani, unaofanywa na baadhi ya Wananchi wasiokuwa
waaaminifu, kwa kuzing’oa kwa makusudi.
Amesema
barabara ni chachu ya maendeleo ya jamii katika kukuza uchumi wao na
nchi kwa ujumla, hivyo ni lazima zitunzwe ili ziweze kudumu kwa muda
mrefu.
“Wito
wangu kwenu, tushirikiane kuwadhibiti watu hawa, mimi binafsi
nilikwishaanza zoezi la kutoa elimu, Februari 2012 nilifanya mikutano
katika vijiji vya Kititimo na Kinyamwenda…..Wakuu wa Wilaya,
Wakurugenzi na Polisi, hii iwe ni sehemu ya kazi zenu,”alisisitiza Dk.
Kone.
Baadhi
ya wajumbe walilalamikia ung’oaji vyuma vilivyowekwa kwa ajili ya alama
barabarani na kwenda kuuza kama vyuma chakavu, na kuomba jeshi la
polisi kudhibiti hali hiyo.
Hata
hivyo wajumbe wengine wametoa tahadhari ya biashara ya vyum,
iliyoshamiri nchini, hali inayohatarisha usalama wa magari, ambayo
hukatwa katwa vipande na kupakiwa kwenye Fusso kwa ajili ya
kusafirishwa jijini Dar es Salaam, kuuzwa kama vyuma chakavu.
Na Elisante John
No comments:
Post a Comment