Pages

KAPIPI TV

Wednesday, May 16, 2012

RAIS WA ZANZIBAR DK.SHEIN AMEFANYA UTEUZI WA VIONGOZI TAASISI ZA SERIKALI



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohd Shein amefanya uteuzi wa viongozi katika taasisi mbali mbali za Serikali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee Dkt Shein kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 50 (4) cha katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, Rais amemteuwa Mdungi Makame Mdungi kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Zanzibar.

Aidha Dkt. Shein kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya kifungu cha 61 (2) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 amemteuwa Khamis Jabir Makame kuwa Mkuu wa Wilaya Kaskazini B Unguja.

Uteuzi huo unaanza leo tarehe 16 Mei 2012,

IMETOLEWA NA IDARA YA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

No comments: