Pages

KAPIPI TV

Tuesday, November 8, 2016

DKT. POSSI AIPONGEZA UNESCO KUPUNGUA KWA UKATILI DHIDI YA ALBINO


Naibu Waziri (Ofisi ya Waziri Mkuu), Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, Dkt. Abdallah Possi amelipongeza Shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) kwa kusaidia kutoa elimu kwa wananchi kuhusu watu wenye ualbino pamoja na kufanya tathmini jinsi wananchi walivyo na uelewa kuhusu watu hao.

Dk. Possi ameyasema hayo katika mkutano wa kuelezea tathmini ambayo imefanywa na UNESCO kwa wananchi wa wilaya nne ambazo tathmini ilifanyika na kusema kuwa ni jambo zuri ambalo limesaidia kuonyesha hali jinsi ilivyo na ni njia gani ambayo serikali inaweza kutumia ili kumaliza vitendo vya ukatili kwa watu wenye ualbino.

"Watu wenye ualbino wamekuwa wakiteseka kwa kipindi kirefu, wanakosa nafasi ya kusoma, kufanya biashara na mambo mengi yanawakabili, watu wa mashirika sio suluhisho ni jamii yenyewe, watu wengi bado hawana elimu ya kutosha kuhusu ualbino,

"Inabidi ifike hatua watu wenye ualbino waishi sawa na watu wengine na serikali imekuwa ikifanya jitihada kumaliza vitendo hivyo lakini inabidi jamii itambue hili sio jukumu la serikali peke yake ni muhimu kila mmoja akashiriki kuvitokomeza vitendo vya ukatili, UNESCO imetuonyesha njia ya kuiwezesha serikali kufanikisha nia yake," alisema Dkt. Possi.

Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues akizungumza machache kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt Abdallah Possi kutoa hotuba kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. (Habari picha na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Kwa upande wa UNESCO kupitia Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues alisema UNESCO imnatambua kila mwanadamu ana haki ya kuishi kama binadamu wengine na kupitia utafiti wao ambao uliambatana na kutoa elimu wanaamini kuwa ni muda wa jamii kushirikiana ili kutokomeza vitendo vya kikatili kwa maalbino.

"UNESCO imeamua kujihusisha sana na hili jambo na kujitahidi kutoa elimu kwa jamii, tumeanza kulifanyia kazi jambo hili la kikatili kwa maalbino na mashambulizi ambayo wamekuwa wanakutana nayo sababu ya imani za kishirikina ambazo ni kinyume na haki za kibinadamu,

"Utafiti huu utaweza kusidia kumaliza vitendo vya kikatili kwa watu wenye ualbino, kila mtu ana haki za kimsingi na hilo ndilo ambalo UNESCO inalisimamia, na katika kufanikisha hili kila mtu katika jamii kwa nafasi yake ana wajibu wa kushiriki kumaliza vitendo hivi, ni lazima kushirikiana kumaliza jambo hili," alisema Rodrigues.

Tathmini hiyo imefanyika katika wilaya nne ambazo ni Misungwi na Sengerema kwa Mwanza, Msalala iliyopo Shinyanga na Bariadi mkoani Simiyu.

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt Abdallah Possi akizungumza katika mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya watu wenye Alibinism Tanzania (TAS) Nemes Temba akitoa neno kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mhadhiri Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kiongozi mkuu wa tathmini hiyo, Dkt. Nandera Mhando akiainisha mambo muhimu yaliyobainika kwenye tathmini wakati mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Sweden nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnitt akitoa maoni kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. Kulia ni Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp.
Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp akizungumza jambo kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini, Dr. Qasim Sufi akifafanua jambo wakati wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi akifafanua jambo kwenye mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Picha juu na chini ni Sehemu ya washiriki wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) wakiwemo wadau kutoka mashirika na taasisi mbalimbali uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.



Mshehereshaji wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism), Mathias Herman akiendesha mjadala kwa washiriki katika mkutano huo uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi akibadilishana mawazo na Balozi wa Sweden nchini Tanzania Bi. Katarina Rangnitt (wa pili kushoto), Balozi wa Uturuki nchini, Yasemin Eralp (wa pili kulia) pamoja na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) nchini, Dr. Qasim Sufi wakati wakijiandaa na zoezi la picha ya pamoja.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu Mhe. Dkt. Abdallah Possi katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa UNESCO unaoangalia tathmini ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albinism) uliofanyika leo katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
-- Zainul A. Mzige, Operation Manager, MO BLOG, www.modewjiblog.com +255714940992.

KUTOKA VOA Swahili: ZULIA JEKUNDU

Zulia Jekundu ni kipindi cha televisheni cha kila wiki ambacho hukuletea habari mbalimbali za burudani zinazotamba. Humu utapata kujua juu ya habari za mastaa zinazogonga vichwa vya habari, kujua baadhi ya wanaosherehekea siku zao za kuzaliwa wiki husika na hata filamu 5 zilizoongoza kwa mauzo katika wiki hiyo.
KARIBU

WANAFUNZI WA NELSON MANDELA WATAKIWA KUWA MSTARI WA MBELE KUSAIDIA KUTATUA MATATIZO YA MAZINGIRA,MAJI

Pichani juu na chini ni Balozi wa Umoja wa nchi za Ulaya EU kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akihutubia wanafunzi wa vyuo mbalimbali katika ukumbi Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela ambapo alifanya ziara ya kutembelea Chuo jijini Arusha.(Picha na Ferdinand Shayo).

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau akifafanua jambo katika ziara ya Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer alipotembelea chuo hicho.
Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki Roeland Van De Geer akisalimiana na Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau, wakati wa ziara ya balozi huyo chuoni hapo.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela wakiwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) kwa nchi za Afrika Mashariki, Roeland Van De Geer.
Picha ya pamoja ya washiriki wa semina ya malengo ya dunia ya Umoja wa Mataifa katika Chuo cha Nelson Mandela jijini Arusha.

Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela Profesa Karoli Njau (wa pili kulia) katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa, Hoyce Temu (wa pili kushoto) na Amon Manyama (kushoto).
-- Zainul A. Mzige, Operation Manager, MO BLOG, www.modewjiblog.com +255714940992.

TEKNOLOJIA INAVYOBADILI MIENDENDO YA WASAFIRI

Na Jumia Travel Tanzania

Miaka kadhaa iliyopita kabla ya matumizi ya tekinolojia kuingia na kushika kasi mtu ulikuwa ukitaka kusafiri itakubidi kuulizia kwa watu ambao tayari wameshawahi kuwepo kwenye eneo unalolitarajia kwenda.

Baadae kidogo simu zilivyoanza kuingia zilirahisisha mambo watu wakawa wanapigiana simu na kuulizana hali na mazingira kwa ujumla ya eneo wanalotaka kwenda ili kujiandaa vema.

Lakini sasa hivi kwa msaada wa tekinolojia ni wewe tu aidha na simu au kompyuta yako iliyounganishwa vizuri na mtandao wa intaneti ambapo unaweza kupata taarifa lukuki bila ya kumuhusisha mtu yeyote yule. 

Kadiri ya maendeleo ya tekinolojia yanavyokua sehemu mbalimbali duniani na ndivyo huduma mbalimbali zinavyosogezwa na kurahisishwa zaidi kumzunguka binadamu.

Leo hii mtu huna haja ya kupata shida ya kuanza kusumbuka kutembea umbali mrefu au kumuuliza jirani, ndugu au jamaa kuhusu huduma kama vile za usafiri, malazi, bidhaa, na bei zake kwani kila kitu kimo na kinaweza kupatikana kwa njia ya mtandao wa intaneti.

Vivyo hivyo kwa upande wa huduma za usafiri na utalii zilivyorahisishwa na mitandao ya huduma za hoteli kama vile Jumia Travel, Expedia, Airbnb, TripAdvisor, Booking.com na kadhalika.

Wasafiri na watalii wengi wa siku hizi kutoka sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi wanapenda kupata huduma wazitakazo kwa urahisi zaidi na uhakika wakiwa mahali popote.

Wanataka kwamba wakiingia kwenye mtandao aweze kupata taarifa zote juu ya sehemu anayotaka kwenda kama vile atafika kwa njia gani pamoja na sehemu atakayofikia.

Kwa upande wa malazi mitandao iliyotajwa hapo juu imekuwa na nafasi kubwa sana katika kuhakikisha msafiri anapata sehemu ya uhakika anayoihitaji, gharama na hadhi yake.

Mitandao hii inatoa uwanja mpana wa kuweza kupata huduma zote sehemu moja, za uhakika tena ndani ya muda anaoutaka msafiri.

Tofauti na kipindi cha nyuma kidogo ambapo ilimbidi mtu afanye taratibu za malazi kwa sehemu anayokwenda mpaka atakapofika.

Kwa namna moja ama nyingine mitandao hii ya huduma za hoteli kwa mtandao na tekinolojia kwa ujumla imeleta msaada mkubwa na mapinduzi ya hali ya juu kwa watoa huduma nchini na sehemu zingine duniani.

Licha ya maendeleo hayo na madhumuni mazuri ya tekinolojia katika kuboresha maisha ya binadamu lakini bado kuna changamoto kubwa kwa watumiaji hususani wasafiri kuiamini na kuitumia mara kwa mara lakini pia hata kwa wenye hoteli na sehemu zingine zinazotoa huduma za malazi kwa ujumla.

Bado wasafiri wengi wanaamini kuwa huduma za kweli na uhakika utazipata mara utakapofika eneo husika licha ya kuwa kwenye mitandao hii kuna picha, huduma, gharama na mawasiliano ya wahusika.

Na kwa upande wa wamiliki wa sehemu za malazi kama vile hoteli bado nao hawana imani kubwa na wamiliki wa hii mitandao. Wao wanadhani kwamba wanaweza kutumia hoteli zao kuwatapeli wateja na kunufaika wao binafsi, dhana ambayo si kweli.

Ukweli wa mambo ni kwamba kwa watumiaji wa huduma hizi, wateja na wamiliki wa hoteli ambao huitumia mara kwa mara wamethibitisha imekuwa na msaada mkubwa sana.

Kwa mfano, hoteli nyingi hutegemea umaarufu wa sehemu husika ndio mteja aende na kutumia huduma zao kitu ambacho kwa dunia tuliyopo na tunayokwenda nayo kinapitwa na wakati.

Kupitia mitandao hii wamiliki wa hoteli na sehemu zingine za malazi wana wigo mpana wa kuwapata wateja kutoka maeneo mbalimbali kwani huduma zao zinakuwa tayari kwenye mitandao hiyo.

Jumia Travel ni miongoni mwa mitandao hiyo ambayo inayo orodha ndefu ya hoteli takribani 1,500 za nchini Tanzania bara na visiwani ambazo zinaweza kufikiwa na watu wa ndani na nje ya nchi.

Hii ni fursa kwa wamiliki wa hoteli kuweza kutambua wateja wao ni watu wa aina gani na wanatarajia vitu gani kutoka kwao. Wateja wa sasa wanategemea kwa kiasi kikubwa kukuta taarifa zote kuhusu huduma za hoteli husika kuwepo kwenye mtandao na kupatikana mara moja pale wanapozihitaji.

Kwa bahati mbaya si hoteli na sehemu za malazi zote ambazo taarifa zake unaweza kuzikuta mtandaoni na hapo ndipo mitandao hii inapokuja kuziba hilo pengo.

Mitandao ya huduma za hoteli imekuja kuziba pengo lililokuwepo kwa muda mrefu baina ya watoa huduma hizo na wateja ambapo athari zilikuwa kwa pande zote mbili.

Wamiliki kwa kiasi kikubwa wamekuwa wakikosa wateja wengi ambao wangeweza kuwafikia kwa njia ya mtandao kwa kutegemea ambao wanakwenda moja kwa moja na hivyo kupoteza mapato mengi. Na pia kwa wateja ambao walikuwa na shauku ya kujua sehemu husika kabla ya kwenda walikuwa wanakosa fursa hiyo kwa sababu hakukuwa na mbadala wa huduma hiyo. 

Kuhusu Jumia Travel
Jumia Travel (travel.jumia.com) ni mtandao nambari moja unaongoza wa huduma za hoteli kwa njia ya mtandao wenye orodha ya hoteli zaidi ya 25,000 kwa nchi za Afrika na zaidi ya hoteli 200,000 duniani kote.

Dhumuni letu ni kuleta kila aina ya huduma za malazi kwenye mfumo wa mtandao na kutengeneza njia rahisi na nafuu zaidi kwa wateja kuzilipia.

Hapa Jumia Travel, tunao mamia ya wataalamu katika masuala ya utalii ambao huwasiliana na wateja wetu. Ofisi zetu zinapatikana katika miji na nchi zifuatazo Lagos (Naijeria), Accra (Ghana), Dakar (Senegali), Abidjan (Ivory Coast), Algiers (Algeria), Douala (Cameroon), Kampala (Uganda), Dar Es Salaam (Tanzania), Nairobi (Kenya), Addis Ababa (Ethiopia), Porto (Ureno) na Paris (Ufaransa).

Kabla ya mwezi Juni mwaka 2016, Jumia Travel ilikuwa ikijulikana kama Jovago. Ilianzishwa mwaka 2013 na Jumia ambayo inaendeshwa kwa kushirikiana na MTN, Rocket Internet, Millicom, Orange na Axas kama washirika wao katika masuala ya kifedha. 

Tuesday, October 4, 2016

MRADI WA GREEN VOICES UMEONYESHA MAFANIKIO, UTAWAKOMBOA WANAWAKE TANZANIA


Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, akisalimiana na maofisa wa ulinzi na usalama mara baada ya kuwasili katika bandari ya Nansio, Ukerewe hivi karibuni kuzindua mradi wa kilimo cha viazi lishe unaofadhiliwa na taasisi yake ya inayoshughulikia maendeleo ya Wanawake wa Afrika.
Mama Getrude Mongella (waliosimama katikati mwenye blauzi nyekundu) akifafanua jambo kwa Mkamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, wakati walipotembelea mradi wa kilimo cha viazi lishe wilayani Ukerewe. Kushoto kwa Mama Mongella ni Bi. Leocadia Vedastus, ambaye ni mshiriki kiongozi wa mradi huo.
Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania na Rais wa Taasisi ya Women for Africa Foundation, Mama Maria Tereza Fernandez de la Vega, akiangalia bidhaa zilizo mbele yake ambazo zinatokana na viazi lishe katika kuongeza mnyororo wa thamani. Hii ni wakati alipokwenda kuuzindua mradi huo wilayani Ukerewe katika Mkoa wa Mwanza.

MRATIBU wa mradi wa akinamama wapambanao na mazingira wa Green Voices, Alicia Cebada, amesema kwamba wamefarijika na mradi huo kwa kuwa umeonyesha mafanikio makubwa nchini Tanzania.

WAFADHILI WAFURAHISHWA NA UKAUSHAJI WA MBOGA MBOGA WA WANAWAKE MOROGORO



Mkurugenzi wa mawasiliano wa taasisi ya Mfuko wa Wanawake Afrika, Anna Salado (kulia), akipakua mboga zilizopikwa kiasili na kuungwa kwa nazi wakati yeye na ujumbe wake walipotembelea mradi wa ukaushaji wa mboga na matunda wa wanawake wa Kata ya Mzinga mkoani Morogoro hivi karibuni. Kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro, Milikieli Mansweat Mahiku.

Mratibu wa mradi wa Green Voices kutoka taasisi ya Mfuko wa Wanawake Afrika ya Hispania, Alicia Cebada, akiwa ameshikilia pakiti ya kisamvu kilichokaushwa na kufungashwa huku akiwapongeza wanawake wa kikundi cha Mzinga katika Kata ya Mzinga, Manispaa ya Morogoro kwamba wamefanya kazi nzuri sana. Mwenye fulana nyeupe ni Bi. Esther Muffui, mshiriki kiongozi wa mradi huo.

SIYO tu mapishi ya asili ya kisamvu kikavu kilichoungwa kwa nazi, lakini mafanikio makubwa katika ukaushaji na usindikaji wa mboga na matunda katika mradi wa wanawake wa Kata ya Mzinga, Manispaa ya Morogoro yamewavutia wahisani wa taasisi ya Women for Africa Foundation kutoka Hispania.
Hali hiyo imewafanya wanawake hao wawe katika nafasi kubwa zaidi ya kusonga mbele ikiwa wafadhili hao watatoa tena fedha katika awamu ya pili ya mradi wa Green Voices unaotekelezwa nchini Tanzania.

NHC YAKABIDHI MARARASA SHULE YA MSINGI SAKU WILAYA YA TEMEKE

1
Meya wa Halmashauri ya Temeke Abdallah Chaurembo akikata utepe kama ishara ya uzinduzi wa madarasa ya shule ya msingi Saku wilayani Temeke wakati wa makabidhiano yaliyofanyika shuleni hapo jana, Madarasa hayo yamejengwa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC kwa gharama ya shilingi milioni 32 , makabidhiano hayo yamefanyika shuleni hapo mwishoni mwa wiki kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Nassib Mmbaga , Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari na Mkuu wa wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaviva.
2
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akifungua mlango mara baada ya makabidhiano hayo kulia ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke Bw. Nassib Mmbaga na kushoto ni Meya wa Halmashauri ya Temeke Abdallah Chaurembo.
3
Haya ndiyo madarasa yaliyojengwa na Shirika la Nyumba NHC kwa gharama ya shilingi Milioni 32 katika shule ya msingi Saku.
5
Baadhi ya wanafunzi wakikokotoa hesabu walizopewa na Mh. Meya wa Manispaa ya Temeke Halmashauri ya wilaya ya Mh. Temeke Abdallah Chaurembo.
6
Mh. Meya wa Halmashauri ya wilaya ya Temeke Abdallah Chaurembo akiwafundisha hesabu wanafunzi wa darasa la sita katika shule ya ya msingi Saku.
7
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akipiga picha ya pamoja na wafanyakazi wenzake mara baada ya makabidhiano ya madarasa hayo.
8
Mh. Meya wa Manispaa ya Temeke Halmashauri ya wilaya ya Mh. Temeke Abdallah Chaurembo akikabidhi vitabu kwa mwanafunzi Leokadia Projestus wa darasa la sita shule ya msingi Saku katikati ni Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari
9
Mkuu wa wilaya ya Temeke Mh. Felix Lyaviva. akizungumza na wanafunzi.
10 11
mwanafunzi Leokadia Projestus wa darasa la sita shule ya msingi Saku akitoa hotuba kwa niaba ya wanafuzni wenzake.
12
Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Shirika la Nyumba NHC Susan Omari akizungumza neno katika makabidhiano hayo.
13
Wanafunzi wakiimba kwaya wakati wa makabidhiano hao

Friday, September 23, 2016

WANAFUNZI KISARAWE NA TABORA KUNUFAINIKA NA MSAADA WA MADAWATI KUPITIA KAMPENI YA SIMAMA KAA INAYOFANYWA NA DR.AMON MKONGA FOUNDATION

Stella Pius Afisa Mawasiliano wa Kampuni ya simu za mkononi ya Halotel(Kulia) akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo kuhusu kampeni ya Madawati mkoani Tabora , katikati ni Mwenyekiti wa Dr. Amon Foundation Bw. Amon Mkoga na kushoto ni Ngo Duy Truong Meneja Masoko Halotel
Mwenyekiti wa Dr. Amon Foundation Bw. Amon Mkoga katikati ,  Ngo Duy Truong Meneja Masoko Halotel, Kushoto na Stella Pius  Meneja Mawasiliano wa Halotel wakionyesha kwa waandishi wa habari mfano wa Madawati ambayo watakuwa wanayagawa kupitia kampeni ya Simama Kaa Desk  itakayofanyika mkoani Tabora na Pwani.
 
Mwenyekiti wa Dr. Amon Foundation Bw. Amon Mkoga  ametoa mchango wa madawati  katika kampeni ya uchangiaji madawati  kwa udhamini wa mtandao wa simu za mkononi wa Halotel hii leo katika ukumbi wa Idara ya Habari  Maelezo jijini Dar-es-Salaam.
 
Akizungumza na waandishi wa habari Amon Mkoga amesema kuwa ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. John Pombe Magufuli ,wameandaa kampeni ya “Simama Kaa Desk” Kampeni.,  itakayosaidia kupunguza uhaba wa madawati ikidhaminiwa na Kampuni ya Simu ya  Halotel.
 
“Lengo kubwa la kampeni hii ya “Simma Kaa Desk”   ni kuchangia na kupunguza upungufu  wa madawati katika shule za msingi na sekondari  ili kumuunga mkono rais wa  Tanzania Dk. John Pombe Magufuli, Kampeni hiyo  itaanzia katika mkoa wa Tabora na Pwani tukiwa pamoja na Kampuni ya Halotel.”
 
Aidha afisa mawasiliano wa Halotel Stella Pius amesema kuwa Halotel itakuwa pamoja na Dr Mkoga Foundation kuhakikisha kwamba watakuwa bega kwa bega ili kuwasilisha mchango wa madawati katika elimu.
 
“Ikiwa ni pamoja na kuunga mkono uchangiaji wa madawati Haloteli tutahakikisha katika kampeni hii ya Simama Kaa Desk kampeni,  tunawakilisha mchango wetu tukishirikiana na Dr Amoni Foundation kupitia kampeni hii ambapo  tunaamini kuwa ni njia pekee ya kupunguza uhaba wa madawati mashuleni.”
 
Licha ya hayo pia kutakuwa na burudani ya mziki wakati wa kukabidhi madawati hayo ambayo italetwa na  kundi la muziki wa kizazi kipya la Mabaga Fresh la jijini Dar es salaam.
 

AMON MKOGA
MANAGING DIRECTOR
CHIEF PROMOTIONS
P.O BOX 78566
MOBILE 0755 638 004/0784 772628/0655 638 004
EMAIL dramontz2002@yahoo.com
WEBSITE www.chiefpromotions.or.tz
WEBSITE www.mtemimilambofestival.blogspot.com
DAR ES SALAAM
TANZANIA

MTAA WA MASAKI JIJINI DAR ES SALAAM WAANZISHA TOVUTI YAKE KWA AJILI YA MAENDELEO

 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita (kulia), akizungumza katika na waandishi wa habari katika hafla ya uzinduzi wa Tovuti ya mtaa huo iliyofanyika Hoteli ya Best Western Plus Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta. 
 Mwenyekiti wa Mtaa wa Serikali ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam, Kimweri Mhita, akitoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya tovuti hiyo.
 Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (katikati), akikata utepe kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kionondoni, aliyekuwa mgeni rasmi, kuashiria uzinduzi rasmi wa tovuti hiyo. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta, Mwenyekiti wa mtaa huo, Kimweri Mhita, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Masaki, Richard Mwakyulu na Mjumbe wa Kamati ya Mtaa huo, Rose Mkisi.
 Mkutano na wanahabari ukiendelea kabla ya uzinduzi huo.
 Wajumbe wa kamati ya mtaa huo wakishiriki kwenye uzinduzi huo.
 Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo,  Peter Mkongereze akizungumza kwenye hafla hiyo.
 Diwani wa Kata ya Msasani, Benjamin Sitta (kulia), akizungumza katika hafla hiyo.
 Mmoja wa waendeshaji wa tovuti hiyo, Benjamin Chaula (kulia), akielezea jinsi itakavyokuwa ikifanya kazi.Kushoto ni Norbert Baranyikwa.
 Makofi yakipigwa baada ya uzinduzi wa tovuti hiyo.
Katibu Tarafa ya Magomeni, Fullgence Sakafu (kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.


Na Dotto Mwaibale

SERIKALI ya Mtaa wa Masaki jijini Dar es Salaam imezindua tovuti yake ili kurahisisha mawasiliano na shughuli za maendeleo kwa wananchi.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa tovuti hiyo Dar es Salaam leo asubuhi Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Masaki, Kimweri Mhita alisema tovuti hiyo imeanzishwa kwa lengo la  kuwasiliana na kuwashirikisha katika shughuli za maendeleo raia wa kigeni wanaoishi katika mtaa huo.

"Kutokana na jiografia ya eneo letu kulikuwa na changamoto kuwa ya kuwashirikisha wenzetu katika masuala mbalimbali kutokana na kutokuwa na mawasiliano tukaona tuanzishe tovuti yetu itakayosaidia kuondoa changamoto hiyo" alisema Mhita.

Alisema kupitia tovuti hiyo itasaidia kuwatambua wafanyabiashara waliopo katika mtaa huo ambao wameanza kujisajili pamoja na wananchi.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni ambaye alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, Katibu Tarafa wa Kata ya Magomeni, Fullgence Sakafu alisema kuanzishwa kwa tovuti hiyo katika wilaya hoyo wilaya hiyo mtaa huo umeonesha njia hivyo akaomba mitaa mingine kuiga mfano huo.


Alisema tovuti hiyo itasaidia kuweka wazi mipango ya maendeleo katika mtaa huo pamoja na kuhimizana kwenye kampeni ya kufanya usafi inayoendeshwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuwa.