Pages

KAPIPI TV

Tuesday, August 30, 2016

MKURUGENZI WA FULLSHANGWEBLOG AKABIDHIWA TAARIFA YA UCHAGUZI MKUU 2015

1
Bw . Mohamed Seif Ofisa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa niaba ya Mkurugenzi wa Tume hiyo akikabidhi kwa Bw. John Bukuku Mkurugenzi wa Mtandao wa Fullshangweblog Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2015, Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye mgahawa wa Mokka City Mtaa wa Samora jijini Dar es salaam.
2
Bw. John Bukuku Mkurugenzi wa Mtandao wa Fullshangweblog Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2015 mara baada ya kukabidhiwa rasmi.
3
Bw. John Bukuku Mkurugenzi wa Mtandao wa Fullshangweblog Taarifa ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kuhusu Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2015

MAHOJIANO NA PROF.JULIUS NYANG'ORO KATIKA KIPINDI CHA JUKWAA LANGU

Profesa Julius Nyang'oro ni Mwalimu, mtaalam wa sayansi ya siasa na mwanasheria.
Amekuwa mwalimu tangu mwaka 1977 nchini Tanzania na hapa nchini Marekani.

Ni mwandishi wa vitabu zaidi ya 14, vingi vikiigusia Tanzania kwa namna moja ama nyingine. Moja ya vitabu alivyoandika, na ambavyo vilimtambulisha zaidi kwa jamii ya waTanznia, ni kumhusu Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete. Ambapo ameandika vitabu viwili kumhusu.

Prof Nyang'oro alikuwa mkarimu sana kuungana nasi kwenye kipindi cha JUKWAA LANGU Jumatatu ya Agosti 29, 2016 kuzungumzia mambo mbalimbali kuihusu Tanzania akiwa mwandishi, mwalimu, mtaalamu wa mausala ya siasa na mwanasheria
KARIBU

RC SINGIDA AKABIDHI MADAWATI 630 KWA WAKURUGENZI WA WILAYA NA MANISPAA

Na Mathias Canal, Singida


Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri za Mkoa wa Singida wamekabidhiwa jumla ya madawati 90 kwa kila Halmashauri ili kuondoa adha waliyokuwa wanakumbana nayo wanafunzi wa shule za msingi na sekondari Mkoani humo ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kampeni ya kuchangia madawati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli alipowaagiza wakuu wa mikoa yote nchini wakati akiwaapisha Ikulu, jijini Dar es Salaam Machi 15, 2016.




Wakurugenzi hao wametakiwa kuyachukua haraka madawati hayo na kuyapeleka Katika shule zenye kadhia hiyo ikiwa ni ishara ya kuamsha taswira ya elimu kwa wanafunzi mchini kuondokana na mateso ya kukaa chini wakiwa darasani.


 Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Singida Mhandisi Mathew J. Mtigumwe wakati wa makabidhiano hayo katika Ukumbi wa Ofisi za Mkoa huo huku akisifu wadau na Taasisi mbalimbali kujitolea kuunga mkono uchangiaji wa madawati ambao awali ulianza kwa ngazi ya Halmashauri kabla ya kuhusisha taasisi mbalimba sambamba na wadau wa maendeleo Mkoani humo.
Mtigumwe amesema kuwa Hali ya Madawati katika Mkoa ilikuwa chini ya asilimia 40% lakini chini ya uongozi wake kwa kushirikiana na wadau 67 wa Maendeleo wameweza kuchangia jumla ya shilingi milioni 42,626,500 hivyo kufanikisha lengo la utengenezaji wa madawati kufikia asilimia 98% ambapo hata hivyo upungufu Mkubwa ulikuwa zaidi katika Halmashauri za Singida na Manyoni.

WATANZANIA WARAHISISHIWA UPATIKANAJI WA HUDUMA ZA TEKNOLOJIA


Pamoja na kuwepo kwa maendeleo ya kasi katika nyanja mbalimbali lakini sekta ya teknolojia inabaki kuwa moja ya njia ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa mafanikio hayo kwa kurahisisha kazi nyingi kufanyika kwa haraka.

Kwa kutambua hilo, kampuni inayohusika na utoaji wa huduma zinazohusiana na teknolojia ya EnGenius imeingia katika makubaliano na kampuni ya usambazaji wa vifaa vya kiteknolojia ya Red Dot ili iweze kusambaziwa vifaa na huduma mbalimbali ambazo zinafanywa na Red Dot katika nchi za Afrika Mashariki.
Mkuu wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao akizungumzia kazi ambazo wanazifanya na mipango ya kutoa bidhaa bora kwa nchi za Afrika Mashariki.

Kampuni ya EnGenius ambayo inatoa huduma kama za internet wireless, radio frequency (RF) technology na kusambaza bidhaa mbalimbali kama kompyuta imesema kuwa imefanya maamuzi ya kuingi katika makubaliano na Red Dot ikiamini kuwa ni moja ya njia sahihi ambayo itawawezesha kuwafikia wateja kwa karibu zaidi.

Akizungumzia makubaliano hayo, Mkuu wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao alisema kampuni ao kwa sasa inahitaji kujitanua katika nchi za Afrika Mashariki kama Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia hivyo wameungana na Red Dot ili waweze kukuza biashara yao zaidi.

"Tumeingia makubaliano na moja ya wasambazaji wakubwa wa Red Dot na tunaamini watatusaidia EnGenius kufikia malengo yetu ya kuwa wauzaji wakubwa wa bidhaa za kiteknolojia kwa Afrika Mashariki, tunafahamu kuwa ni wasambazaji wakubwa na atatusaidia kukuza biashara yetu," alisema Hsiao.


Na Rabi Hume, modewjiblog.com
Mkurugenzi Mtendaji wa Red Dot Distribution akielezea jinsi ambavyo wamejipanga kufanya kazi na EnGenius. (Picha zote na Na Rabi Hume, modewjiblog.com)

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Red Dot Distribution, Munir Bharwani alisema kuwa ni ushirikiano mzuri ambao wameanza kuufanya na EnGenious na wana mipango mingi kuhakikisha malengo ambayo yamewekwa yanafikiwa.

"Tuna taraji mafanikio makubwa, Red Dot ni kampuni ya kitanzania ambayo inafanya kazi katika nchi za Afrika Mashariki kwahiyo tunatazamia ushirikiano huu utakuwa na faida," alisema Bharwani.
Meneja Mkuu wa Red Dot Distribution Tanzania, Rajesh Adiani akifungua halfa ya uzinduzi wa makubaliano kati ya Red Dot na EnGenius kwa kuelezea shughuli ambazo wanazifanya.
Mkurugenzi wa Mauzo na Masoko wa EnGenius, Alishan Zaidi akilelezea huduma ambazo wanazitoa za kiteknolojia na usambazaji wa vifaa vya kiteknolojia kama kompyuta na kamera za usalama.
Mkurugenzi Mtendaji wa Red Dot Distribution, Munir Bharwani na Mkuu wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao wakipongezana baada ya kuingia rasmi katika makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja.

Baadhi ya wageni waalikwa wakiangalia bidhaa ambazo zinatolewa na EnGenius.
Baadhi ya wageni waaliakwa waliohudhuria halfa ya makubaliano ya Red Dot Distribution na EnGenius.

Wednesday, August 17, 2016

BLACKFOX MODELS AFRICA WAFANIKISHA ZOEZI YA KUSAJILI VIJANA WA ARUSHA

Jumapili ilikuwa siku ya furaha kwa wanamitindo wa Arusha, kwani timu ya Blackfox Models ilitua jijini humo kusajili vijana wenye fani hiyo.

Zoezi hili lilifanyika katika hoteli ya Tulia Boutique Hotel and SPA iliyopo Sakina.
Miss Aj Mynah, alisema " nimefurahi sana kwa sisi kufanikisha jambo hili, kwani, lengo letu kubwa ni kuendeleza vipaji vya vijana hawa hasa kwenye uanamitindo na hata kwenye mambo ya Arts Vililevile.

Tumeona Arusha ina vipaji vingi sana, na tumekuta kijana mmoja utakuta ana kipaji cha kuimba, uanamitindo, acrobatics na hata kucheza. Kwakweli tumefurahishwa na tutafanya vilivyo kuhakikisha tunakuza vipaji hivi - alisema AJ.
Blackfox wamesajili vijana 12 kutoka Arusha, na wameahidi kutembea kwenye miji mingine kusajili.

Blackfox Models Africa, ni Agency ambayo inajihusisha kwenye kusajili vijana na kuwapa mazoezi kwenye uanamitindo, pia kuwatafutia kazi za kwenye uanamitindo nchini. Ofisi yao iko Karibu na ubalozi wa Marekani. Kwa wale vijana ambao wanataka kuingia Blackfox wanaweza kwenda kwenye tovuti yao www .blackfoxmodelsafrica.com< /div>

KAIMU KAMISHNA MSAIDIZI WA SHIRIKA LA MAENDELEO YA PETROLI KUTOKA WIZARA YA NISHATI NA MADINI ATUA TANGA KUANGALIA ENEO LITAKAPOJENGWA GATI KWA AJILI YA KUSHUSHIA MAFUTA GHAFI


 Greda likisafisha eneo ambalo linatarajiwa kujengwa gati kwa ajili ya kushushia mafuta ghafi
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kulia akiwa na viongozi kutoka Wizara ya Nishati na Madini walipotembelea sehemu  ambayo litajengwa gati mpya eneo la Chongoleani jijini Tanga kushushia mafuta ghafi kulia ni Kaimu Kamishna Msaidizi wa Petroli kutoka Wizara ya Nishati na Madini ,Mwanamani Kidaya kushoto ni Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika

Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa pili kutoka kushoto akisisitiza jambo wakati walipotembelea eneo la Chongoleani ambapo kutajengwa gati ya kushushia mafuta ghafi



Kaimu Kamishna Msaidizi wa Petroli kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Mwanamani Kidaya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kulitembelea eneo hilo leo
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella akizungumzia namna mkoa huo ulivyojipanga na fursa hiyo mara baada ya kulitembelea eneo hilo

Kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga,Henry Arika kulia akisisitiza jambo kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella wa tatu kutoka kushoto namna walivyojipanga kutokana na fursa hiyo
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Petroli kutoka Wizara ya Nishati na Madini,Mwanamani Kidaya kushoto akimuonyesha kiti Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martine Shigella mara baada ya kutembelea eneo hilo






Muonekano wa eneo ambalo kutajengwa gati mpya kwa ajili ya kushushia mafuta ghafi
Habari kwa hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

DC MTATURU AMALIZA MGOGORO KATI YA MWEKEZAJI NA WANANCHI


Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mang’onyi wakati wa kutatua mgogoro kati ya wananchi na muwekezaji Shanta Gold Mine
Wanachi Kijijini Mang’onyi wakisikiliza kwa makini maelezo ya Mkuu wao wa Wilaya
Baadhi ya viongozi wakisikiliza maelezo ya awali katika ufunguzi wa mkutano huo uliodumukwa zaidi ya masaa matatu
Dc Mtaturu akikemea tabia ya wanasiasa kutoa matamko ya kisiasa kwa maslahi yao binafsi huku wakiwa mbali na eneo la wawakilishi wao

MAHOJIANO NA OLYMPIAN HILAL HEMED HILAL(Live) KUTOKA BRAZIL

Photo Credits: MissiePopular.com
Katika kipindi cha JUKWAA LANGU (Jumatatu Agosti 15 2016) Mubelwa Bandio alifanya mahojiano ya moja kwa moja na Hilal Hemed Hilal. Nahodha wa Tanzania katika mchezo wa kuogelea kwenye mashindano ya Olimpiki huko Rio de Janeiro nchini Brazil.
Alikuwa mkarimu kujiunga nasi kwa njia ya Skype sambamba na kocha wake Alexander Mwaipasi
Karibu uungane nasi

"SERIKALI IPO TAYARI KUCHUKIWA NA WAVIVU"-DC MTATURU

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mirajji Jumanne Mtaturu akisisitiza jambo wakati wa kufunga mafunzo ya waendesha pikipiki.
Mkurugenzi wa Taasisi inayojihusisha na kupunguza umasikini na kutunza mazingira nchini Tanzania (APEC), Respicius Timanywa akiwashukuru washiriki wote wa mafunzo hayo
Dc Mtaturu (Kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi wa APEC Respicius Timanywa zawadi ya kuku iliyotolewa na wahitimu wa mafunzo hayo

ZADIA YATOA MKONO WA POLE KWA WAZANZIBAR KUFUATIA KIFO CHA MZEE ABOUD JUMBE


215 459 4449
zadia.org
انا لله وانا اليه راجعون
TAARIFA
Jumuiya ya Wazanzibari Nchini Marekani (ZADIA), imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mzee Aboud Jumbe Mwinyi.
Mzee Jumbe aliyewahi kuwa rais wa Zanzibar na Makamo wa Kwanza wa Rais wa Tanzania, atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika harakati za kuleta maendeleo na mabadiliko ya kisiasa visiwani Zanzibar.
Chini ya Uongozi wake, kwa mara ya kwanza Zanzibar ilipata katiba yake na hivyo kuanzishwa kwa Baraza la Wawakilishi kama chombo cha uwakilishi wa Umma na kutunga sheria.
Atakumbukwa pia kwa msimamo wake shupavu wa kupigania haki sawa ndani ya Mungano wa Tanganyika na Zanzibar khususan madai yake ya kutaka kuwa na serikali tatu.
Marehemu Jumbe alikuwa rais wa Zanzibar kuanzia mwaka 1972 kufuatia kifo cha rais wa kwanza wa Zanzinbar Marehemu Abeid Aman Karume. Alilzaimishwa kujiuzulu nyadhifa zake zote za kisiasa mwaka 1984 baada ya kutuhumiwa kuchafua hali ya hewa ya kisisasa Zanzibar. Uchafuzi ambao si chochote ila ushupavu wake wa kutetea maslahi ya Zanzibar ndani ya Muungano wa Tanzania.
Kwa mnasaba huu, ZADIA inatoa mkono wa pole kwa Wazanzibari wote kwa ujumla kwa kuondokewa na kiongozi wao mzalendo.
Aidha kono wa pole makhasusi uwafikie wanafamilia ya Marehemu, tukimwomba Mwenyezi Mungu Mtukufu awape subira katika kipindi hiki kigumu cha msiba, na kumwomba Mola Mlezi amlaze marehemu mahali pema Peponi. Amin.
Omar H Ali, Mwenyekiti, ZADIA
Agosti 14, 2016

"JESHI LA POLISI HALIPASWI KUFANYA KAZI KWA MAZOEA"-DC MTATURU

Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akizungumza na askari wa Jeshi la polisi mara baada ya ziara yake katika makao makuu ya Wilaya hiyo eneo la Ikungi.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Miraji Jumanne Mtaturu akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Kituoni hapo.
 Dc Mtaturu akikagua chumba cha mahabusu kituoni hapo
 Askari watiifu wa Jeshi la Polisi Wilayani Ikungi waliposimama kutoa heshima zao kwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi alipotembelea katika ofisi yao (Picha zote na Mathias Canal)

MFUKO KICHOCHEO WA SAGCOT WASAINI MAKUBALIANO NA SHIRIKA LA BOTHAR KUTOKA NCHINI IRELAND


Katibu Mtendaji wa Mfuko Kichocheo wa SAGCO Bwa. John J. Kyaruzi akisaini makubaliano hayo na Mwasisi wa Shirika la Bothar Bwa. Peter Ireton huku wakishuhudiwa na Dkt. Bernard Muyeya (kulia) Mkurugenzi wa Huduma za Nje ya Nchi wa Bothar na Bwa. Abdallah S. Msambachi ( kushoto) Mratibu wa Biashara wa Mfuko wa SAGCOT. 
Ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa kuongeza tija na uzalishaji kwa wafugaji wa ng’ombe wa maziwa mkoani Njombe, Iringa na Mbeya, Mfuko Kichocheo wa SAGCOT yaani SAGCOT CATALYTIC TRUST FUND tarehe 12 Agosti 2016 umesaini makubaliano na Shirika la Bothar kutoka nchini Ireland ambalo linajihusisha na kutoa misaada mbalimbali inayolenga kutoa fursa kwa familia zenye kipato cha chini kuweza kuboresha maisha yao kupitia uwekezaji wa shughuli zinazowaletea kipato hususani kaya zinazojishughulisha na ufugaji.

Katika makubaliano hayo jumla ya Ng’ombe wa kisasa 630 wanatarajiwa kuingizwa nchini katika kipindi cha miaka mitatu. Ng’ombe hao watagawiwa kwa wafugaji walioandaliwa chini ya miradi inayotekelezwa na Mfuko huo, Aidha wafugaji watahakikishiwa masoko pamoja na huduma mbalimbali za mifugo kupitia wataaalamu wa Halmashauri husika.

Katibu Mtendaji wa Mfuko Kichocheo wa SAGCOT Bwa. John. J. Kyaruzi ( kushoto) akisaini makubaliano na Muasisi wa Bothar Bwa. Peter Ireton .
Bwa. John. J. Kyaruzi na Bwa. Peter Ireton wakibadilishana hati za makubaliano.
Mkurugenzi wa huduma za nje ya Nchi wa Bothar,Dkt Bernard Muyeya akitoa maelezo kwa wajumbe namna shirika hilo linavyotoa huduma zake.
--

WAZIRI NAPE AFUNGA MASHINDANO YA GOFU YA WAZI YA TANZANIA JIJINI ARUSHA,WAKENYA WATAMBA


Richard Owiti kutoka nchini Kenya akionesha kombe lake la ushindi mara baada kushika nafasi ya kwanza kwa wachezaji wa ridhaa,kwenye mashindano ya Gofu ya Wazi ya Tanzania yaliyoanza kufanyika juzi ijumaa katika viwanja vya Kili Golf-USA River jijini Arusha na kuhitimishwa jana jioni,ambapo Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye (wa pili kulia).Kushoto ni Mwenyekiti wa chama cha Gofu Tanzania (TGU),Joseph Tango wakishuhudia kwa pamoja.


Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye akimkabidhi vifaa vya mchezo huo wa Gofu mshindi wa kwanza wa wachezaji wa ridhaa katika Mashindano ya Gofu ya wazi ya Tanzania,Richard Owit kutoka nchini Kenya,yaliofungwa jana jioni katika viwanja vya Kili Golf-USA River jijini Arusha,pichani kushoto ni Mwenyekiti wa chama cha Gofu Tanzania (TGU),Joseph Tango. Mashindano hayo yaliyokuwa na msisimko mkubwa yalishirikisha washiriki wapatao zaidi ya 150 kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Tanzania,Kenya na Unganda.
Mshindi wa kwanza kwa wachezaji wa kulipwa wa mchezo huo wa Gofu kutoka nchini Kenya,Jacob Okelo akikabidhiwa mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni sita,kwenye hafla fupi ya kuhitimisha mashindano hayo ya Gofu ya Wazi ya Tanzania ,yaliyoanza kufanyika juzi ijumaa katika viwanja vya USA River na kuhitimishwa jana jioni,ambapo Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye.
Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi milioni moja Afisa Maendeleo ya jamii na Uhusiano,Justine Kesi ikiwa ni sehemu ya kiasi cha fedha kilichotolewa na Wadhamini waliodhamnini mashindano hayo ya Gofu kwa ajili ya kuchangia maendeleo ya huduma za jamii mbalimbali kwa vijiji vinavyozunguka viwanja vya Kili Golf,jijini Arusha.

Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye akizungumza mbele ya wageni waalikwa mbalimbali jana jioni wakati wa kufunga mashindano ya Gofu ya Wazi ya Tanzania yaliyoanza kufanyika juzi ijumaa katika viwanja vya Kili Golf- USA River  jijini Arusha na kuhitimishwa jana jioni,ambapo wageni waalikwa wakiwemo wachezaji wa kulipwa na ridhaa wa mchezo huo walishiriki.PICHA NA MICHUZI JR-ARUSHA
Baadhi ya wageni waalikwa waliofika kushuhidia hitmisho la mashindano hayo ya gofu,wakifuatilia hotuba fupi iliyokuwa ikisomwa na Waziri Nape

Baadhi ya wageni waalikwa waliofika kushuhidia hitmisho la mashindano hayo ya gofu,wakifuatilia hotuba fupi iliyokuwa ikisomwa na Waziri Nape

Wazir Nape (wanne kulia) akiwa na wadau mbalimbali wa mchezo huo wa Gofu hapo jana kabla ya kuhitimisha mashindano hayo
Baadhi ya Wadau nao walikuwepo kufuatilia kuhitimishwa kwa mashindano hayo ya Gofu jana jioni jijini Arusha

Waziri Nape pia alikutana na wadau ambao walidhamini mashindano hayo ya Gofu

Waziri wa Habari ,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mh Nape Nnauye akimsikiliza Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA),Mh Godbless Lema,kwenye viwanja vya Kiligolf,USA-River jijini Arusha,ambapo Mh Nape alikuwa mgeni rasmi katika kuhitimisha mashindano hayo ya Gofu ya Wazi ya Tanzania.Pichani kulia ni Diwani wa kata ya Maroroni,Mh.Bryason Issangya (CHADEMA)
Waziri Nape (wanne kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wadau wa Gofu kwenye viwanja vya Kiligolf jijini Arusha,kutoka kulia ni Makamu Mwenyekiti wa chama cha Gofu Tanzania,Chris Martin,Mkurugenzi wa viwanja vya Gofu (KiliGolf),Jerome Bruins,Mmoja wa wasimamizi waku wa kampuni ya Group Six International LTD,Janson Huang,na kushoto kwa Waziri ni Mke wa Mbunge wa Arumeru Mashariki,Mh Joshua Nassari,Mh Joshua Nassari,Mwenyekiti wa chama cha Gofu Tanzania (TGU),Joseph Tango pamoja na Diwani wa kata ya Maroroni,Mh.Bryason Issangya (CHADEMA)
Waziri Nape akishiriki kucheza mchezo wa Gofu

Waziri Nape akipata maelezo mafupi kuhusiana na uwanja huo wenye viwango vyote kimataifa cha Kiligolf.
Waziri Nape akifurahia jambo na Mhe Nassri,kulia ni Mke wa Mh Nassari


Waziri Nape pia alipata wasaa wa kutembelea mashimo ya mchezo huo wa Gofu yapatayo 18 ndani ya uwanja wa Kili Gofu,uliopo USA River jijini Arusha.