Pages

KAPIPI TV

Wednesday, July 27, 2016

DC MUHEZA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA HOSPITALI YA TEULE MUHEZA,AWATAKA WAFANYAKAZI KUACHA KUFANYA KAZI KWA MAZOEA


MKUU wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto akipofanya ziara ya kuitembelea hospitali ya Teule kuangalia changamoto zinazoikabili kulia ni Mganga Mfawizi wa Hospitali hiyo,Malahiyo Rajabu katikati ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza

Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo aliyekaa kulia kuzungumza na watumishi wa Hospitali Teule ya Muheza

 Mganga Mfawizi wa Hospitali Teule ya Muheza Malahiyo Rajabu akizungumza jambo kwa Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye hayupo pichani wakati alipofanya ziara ya kuitembelea hospitali hiyo
 Mganga Mfawizi wa Hospitali Teule ya Muheza Malahiyo Rajabu kulia akitoa ufafunuzi kwa Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat Mhandisi Mwanasha Tumbo kushoto katikati ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza wakati mkuu huyo wa wilaya alipofanya ziara kwenye hospitali hiyo
kulia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Mhandisi,Hajat Mwanasha Tumbo akisisitiza jambo kwa DMO wa wilaya ya Muheza wa pili kutoka kushoto Dkt Elias Mayala wakati alipofanya ziara ya kuitembelea hospitali Teule ya Muheza


Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo aliyevaa hijabu akiwa na baadhi ya watumishi wa Hospitali ya Teule ya Muheza wakati alipofanya ziara kulia ni Mganga Mfawizi wa Hospitali hiyo Malahiyo Rajabu na anayefuata ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza

Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo wa pili kutoka kulia aliyevaa hijabu akipata maelezo kutoka kwa mhudumu wa zama katika hospitali Teule ya Muheza kushoto mara baada ya kufanya ziara ya kuitembelea anayefuatia ni Katibu Tawala wa wilaya ya Muheza


Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Teule Muheza Mkoani Tanga,Malahiyo Rajabu kushoto akitoa ufafanuzi kwa Mkuu wa wilaya ya Muheza,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kabla ya kuingia kwenye chumba cha maabara wakati alipofanya ziara ya kuitembelea hospitali hiyo

Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo katikati akitembea hospitali ya Teule wilayani humo kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo,Malahiyo Rajabu kushoto ni DMO wa wilaya ya Muheza,Daktari Elius Mayala


Kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali Teule ya Muheza,Malahiyo Rajabu akimueleza jambo Mkuu wa wilaya ya Muheza Mkoani Tanga,Hajat,Mhandisi Mwanasha Tumbo kuhusua namna wanavyofanya kazi kwenye maeneo mbalimbali ambaye alifanya ziara ya kushtukiza ya kuitembelea hospitali hiyo Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.

WATEJA WAFURAHIA MICHUANO YA ICC INAYOONEKANA KUPITIA STARTIMES


 Meneja Mauzo wa StarTimes Tanzania, Bw. David Kisaka akizungumza na timu ya StarTimes na maveterani wa uwanja wa Mwembe Yanga – Temeke kabla ya mchezo wa kirafiki uwanjani hapo. StarTimes iliweka kambi uwanjani hapo ikiwa ni uzinduzi wa michuano ya ICC mwaka 2016 iliyokwishaanza kutimua vumbi Julai 22 wiki iliyopita ambapo ilidhamiria kuonyesha mchuano mkali wa ‘Manchester Derby’ uliopaswa kuchezwa jijini Beijing, China lakini kwa bahati mbaya ukaahirisha kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya na hivyo wateja wakapewa kutazama marudiano ya mchezo baina ya Manchester United na Borrusia Dortmund ambapo Dortmund waliibamiza United kwa magoli 4 - 1.
 Baadhi ya wateja na mashabiki wa soka waliojitokeza kutazama mchezo wa  ‘Manchester Derby’ uliopaswa kuchezwa jijini Beijing, China lakini kwa bahati mbaya ukaahirisha kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya na hivyo wateja wakapewa kutazama marudiano ya mchezo baina ya Manchester United na Borrusia Dortmund ambapo Dortmund waliibamiza United kwa magoli 4 - 1.

Mmoja wa wateja waliofika katika viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke, akipata maelekezo juu ya huduma za StarTimes kutoka kwa mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo.

Na Dotto Mwaibale

Wateja wa StarTimes na watanzania kwa ujumla wameipongeza kampuni inayouza na kusambaza visimbuzi vya matangazo ya dijitali, Starimes, kwa kuwaletea michuano ya kombe la mabingwa kimataifa au ICC mwaka 2016 moja kwa moja kupitia chaneli yake ya ST WORLD FOOTBALL.

Hayo yalisemwa na wateja mbalimbali waliohudhuria tamasha la uzinduzi wa michuano hiyo iliyoanza katika viwanja vya Temeke, Mwembe Yanga.

Katika tamasha hilo StarTimes walitinga viwanjani hapo na timu kamili ya wafanyakazi wake wa vitengo mbalimbali ambapo pia walifunga luninga uwanjani ili kuonyesha moja kwa moja mtanange wa watani wa jadi kutoka jiji la Manchester unaojulikana kama ‘Manchester Derby’ uliopangwa kufanyika jijini Beijing China lakini kutokana na hali ya hewa mbaya ikabidi uahirishwe.

Akizungumza katika viwanja hivyo Meneja Mauzo wa StarTimes Tanzania, Bw. David Kisaka alibainisha kuwa, “Siku ya leo tumefika viwanjani hapa kwa lengo kubwa la kutaka kuwapa fursa wateja wetu kujionea uhondo wa michuano ya ICC inayonekana moja kwa moja kwenye visimbuzi vyetu. Michuano hii inayofanyika katika nchi ya Marekani, Ulaya, Australia na China inazishirikisha timu kubwa duniani kama vile Real Madrid, Barcelona, Manchester United na City, Juventus, Chelsea, Liverpool na nyiginezo.”

“Michuano hiyo imekwishaanza tangu Ijumaa ya wiki iliyoishia ambapo tumekwishashuhudia tayari timu kama Manchester United, Borussia Dortmund, Celtic, Leicester City, Inter Milan na PSG zimekwishatinga uwanjani. Siku ya leo tumekuja hapa kwa lengo la kuonyesha Manchester Derby lakini tunasikikita kuwa mchezo huo umeahirishwa kutokana na hali ya hewa mbaya kulikumba jiji la Beijing ambamo mchezo huo ulipangwa kuchezwa. Lakini badala yake tunaonyesha mchezo wa marudio baina ya Manchester United na Borussia Dortmund.” Aliongezea Bw. Kisaka

Meneja huyo wa Mauzo alimalizia kwa kusema, “Ningependa kuchukua fursa hii kwa kuwashukuru wateja wetu kwa kuendelea kufurahiamichuano hii mikubwa zaidi ambayo ni ya awali au maandalizi kabla ya ligi kuu mbalimbali kuanza mwishoni mwa mwezi wa Agosti. 

StarTimes pia tunaonyesha ligi hizo ambapo wateja watafurahia mechi zote za ligi za Bundesliga na Serie A kupitia chaneli zetu za michezo za SPORT ARENA, SPORTS FOCUS, WORLD FOOTBALL, SPORT LIFE NA SPORT PREMIUM na bila kusahau ligi za Ufaransa na Ubelgiji kupita chaneli ya FOX SPORTS. 

Ili kufaidi michuano hii ya ICC mwaka 2016 wateja itawabidi kulipia malipo kiduchu ya kifurushi cha Mambo kwa shilingi 12,000/- tu na kuweza kutazama mechi zote moja kwa moja ambazo zitarajiwa kuisha Agosti 13.”

Michuano ya ICC mwaka 2016 imekwishaanza Julai 22 ambapo mechi ya kwanza iliyofungua pazia ilikuwa ni kati ya Machester United na Borrusia Dortmund ambapo Dortmund iliibamiza United kwa mabao 4 – 1. Michezo mingine iliyokwishachezwa ni pamoja na PSG kuitandika 3 -1 Inter Milan na Leicester City kuwashinda Celtic kwa mikwaju 6 – 5 ya penati baada ya kutoshana nguvu kwa kufungana magoli 1 – 1 ndani ya dakika 90.


Siku ya leo Jumanne kutakuwa na mechi nyingine ambapo mabingwa wa Italia, Juventus watashuka dimbani kuwakabili timu ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza katika mishale ya saa 7 mchana kwa muda wa hapa nyumbani Tanzania kupitia chaneli ya WORLD FOOTBALL ndani ya ya StarTimes pekee.

KAMPUNI YA MGODI WA GEITA GOLD MINING (GGM) YAFANIKISHA ZOEZI LA KUKUSANYA PESA KWA AJILI YA UKIMWI

Mkuu wa wilaya ya Moshi Kipi Warioba akiongozana na kundi la wapanda mlima Kilimanjaro kutoka kampuni ya Mgodi ya Geita Gold Mining (GGM) waliopanda kwa lengo la kuchangisha fedha za kusaidia taasisi mbalimbali zinazo shughulika na mapambano dhidi ya Ukimwi.
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Geita Gold Mining (GGM)  ,Simon Shayo akizungumza wakati wa hafla fupi ya mapokezi ya kundi la wapanda mlima wakiwemo wafanyakazi wa mgodi huo waliopanda kwa leongo la kuchangisha fedha  za kusaidia taasisi mbalimbali zinazo shughulika na mapambano dhidi ya Ukimwi.
  Kiongozi wa kundi la wafanyakazi wa kampuuni ya Mgodi ya Geita Gold Mining ,Kelvin Yasiwa akizungumza kwa niaba ya wenzake mara baada ya kuwasili wakitokea katika kilele cha Uhuru ,Mlima  Kilimanjaro.
Balozi wa Tume ya kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) Msanii Mrisho Mpoto akizungumza mara baada ya kurejea salama kutoka katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Kipi Warioba akikabidhi cheti kwa mtoto Lucy Mashauri(15)baada ya kufanikiwa kufika katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
  Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Kipi Warioba akikabidhi cheti kwa mtoto Jacob Musa (16) baada ya kufanikiwa kufika katika kilele cha Mlima Kilimanjaro.
Balozi wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi nchini (TACAIDS) Msanii Mrisho Mpoto akifurahia baada ya kukabidhiwa cheti kwa kufanikiwa kufika katika moja ya vilele vya Mlima Kilimanjaro,kilele cha Stela .
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba akikabidhi vyeti kwa washiriki wengine wa changamoto hiyo ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa ajili ya kuchangisha fedha za kusaidia taasisi mbalimbali zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya Ukimwi.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba aliyekua mgeni rasmi katika hafla hiyo Kipi Warioba akizungumza mara baada ya kuwapokea wapandaji wa Mlima Kilimanjaro kutoka kampuni ya Mgodi ya Geita Gold Mining.
Washiriki wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengoo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia taasisi mablimbali zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya Ukimwi wakifungua "champagne" kuonesha furaha mara baada ya kurejea salama kutoka katika kilele cha Mlima Kilimannjaro.
Washiriki wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia taasisi mbalimbali zinazojihusisha na mapambano dhidi ya Ukimwi wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi wa hafla ya mapokezi yao,Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,Kipi Warioba.
Watoto Yatima ambao ndio pekee walioshiriki katika changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro na kufika Kileleni wakiwa katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi,Mkuu wa wilaya ya Moshi,Kipi Warioba pamoja na viongozi wengine akiwemo Makamu wa Raisi wa kampuni ya Mgodi wa Geita Gold Mining,(GGM).
Makamu wa Rais wa Kampuni ya Mgodi wa Geita Gold Mining (GGM) Simon Shayo akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya mapokezi ya washiriki wa changamoto ya kupanda Mlima Kilimanjaro kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya mapambano dhidi ya Ukimwi.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.

TANAPA YAIONGEZEA NGUVU TIMU YA TAIFA YA RIADHA INAYOJIANDAA NA MASHINDA YA OLYMPIK

Meneja Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Pascal Shelutete akitoa neno la ukaribisho kwa wanahabari na wageni wengine katika hafla fupi ya kukabidhi hundi kwa wanariadha wanaounda timu ya taifa, inayojiandaa na mashindano ya Olimpiki yatakayoafanyika mwezi Agosti  nchini Brazil.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi,akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi hundi ya Shilingi Milioni tano kwa wanariadha wanaounda timu ya taifa inayojiandaa na mashindano ya Olimpiki.
Mkurugenzi Mkuu  wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni tano kwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda timu ya taifa wakijiandaa na mashindano ya Olimpiki. 
Mkurugenzi Mkuu  wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi akikabidhi "Track Suit "maalumu zenye maandishi na nembo yanayotangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini kwa Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka kwa ajili ya kusaidia wanariadha wanaounda timu ya taifa wanaojiandaa na mashindano ya Olimpiki
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Anthony Mtaka akizungumza mara baada ya kukabidhiwa hundi pamoja na mavazi maalumu kwa ajili ya wanariadha hao .
Baadhi ya viongozi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) waliohudhuria hafla hiyo.kutoka kushoto Mkurugenzi wa Utalii na Masoko,Ibtahim Musa,Meneja Utalii Johnson Manase na Mhifadhi Vitalis Uruka.
Wanariadha watakaoiwakilisha nchi katika mashindano ya Olimpiki katika jiji la Reo De Jeneiro nchini Brazil wakiwa katika mavazi maalumu yanaotangaza vivutio vilivyoko nchini.
Mkufunzi wa Wanariadha wanaojiandaa na mashindano ya Olyimpiki ,Francis John akizungumzia matarajio yake juu ya vijana hao.
Mmoja wa Wanariadha hao,Alphonce Felix Simbu akizungumza mara baada ya kupoke msaada kutoka  TANAPA.
Baadhi ya Wanahabari na wageni wengine waliofika katika ofisi za Makao Makuu ya Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kushuhudia makabidhiano hayo.
Mwanariadha Said Makuka atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Sara Ramadhan ,mwanadada pekee atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Alphonce Felix atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Mwanariadha Fabian Joseph atakayepeperusha bendera ya Tanzania katika michuano ya Olyimpiki nchini Brazil.
Wanariadha wanne watakao iwakilisha Tanzania katika Michuano ya Olyimpiki nchini Brazil wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Allan Kijazi pamoja na Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) Antony Mtaka ,wengine kutoka kulia ni Mkufunzi wa wanariadha hao,Francis John na anyefuatia ni Mkurugenzi wa Utalii na Masokowa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Ibrahim Musa.

Na Dixon Busagaga wa Michuzi Blog,Kanda ya Kaskazini.

SHIRIKA la Hifadhi za Taifa (TANAPA) limetangaza  kutumia fursa ya mashindano ya Olyimpiki yanayotarajia kuanza mwezi ujao katika jiji la Rio de Janeiro nchini Brazili kutangaza vivutio vya utalii kupitia wanariadha wa Tanzania.

Hadi sasa ni wanariadha wanne ,wakiume watatu na wa kike mmoja ndio waliofuzu kushiriki mashindano hayo na tayari wako kambini katika hosteli za Chuo cha Misitu cha FITI zilizoko West Kilimanjaro wilayani Siha.

Akiongea mjini Arusha wakati akikabidhi msaada wa fedha na vifaa kwa ajili ya wanariadha hao Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA,Allan Kijazi amesema wameamua kutumia fursa hiyo pia kusaidia wanariadha hao wanaoiwakilisha nchi katika mashindano hayo ili waweze kurejea na medali.

Akishukuru kwa msaada huo Rais wa Shirikisho la Riadha nchini ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu AnthonY Mtaka amesema fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kuwakatia bima ya Afya mwaka mmoja wanariadha hao pamoja na familia zao ili wanapokua nchini Brazili wasiwe na mawazo mengi kuhusiana na familia zao walizoziacha hapa nchini.

Naye mmoja wa wanariadha waliofuzu kushiriki mashindano hayo Alphonce Felix pamoja na mkufunzi wa timu hiyo ya Riadha Francis John wameushukuru uongozi wa Riadha kwa kuiwezesha timu hiyo kukaa kambini kwa miezi saba na kuahidi safari hii timu hiyo haiendi kushiriki bali kupambania medali.

Wanariadha waliopo katika timu hiyo ya taifa wanaotarajiwa kwenda Brazili ni mwanamke pekee Sara Ramadhani, Fabiani Joseph, Saidi Makuka na Alfonce Felix .