Pages

KAPIPI TV

Friday, May 27, 2016

UBA TANZANIA CELEBRATES AFRICA DAY 2016

MD and CEO Mr. Peter Makau
MD/CEO Mr. Peter Makau, (centre in white) poses for a group photo with HO staff members.
Like other in African countries and the rest of the world, UBA Tanzania celebrated Africa day, Wednesday, May 25, 2016.
Africa Day is designated to celebrate the uniqueness of the African continent and its people.
UBA celebrating the day across all countries where we have presence with the theme “Africa Rising”, as a demonstration of UBA’s optimism about the huge potential and resources the continent has been blessed with.
The deep understanding of the businesses and trends in Africa has led UBA to being the leading pan-African Bank on the continent with operations in 19 countries. UBA not only provides finance to critical sectors of the African economy, but also drives financial access and inclusion among millions of Africans.
UBA will continuously seek to invest in critical sectors, such as power, agriculture, infrastructure, ICT etc which have the capacity to create employment for the growing population, a key requirement for the continent to achieve its huge socio- economic potentials.
UBA celebrates the day with pride.
Mr. Peter Makau
MD/CEO Mr. Peter Makau, breaks the Kola nut and takes a sip, looking on are Mr. Chris Byaruhanga COO, Ms. Josephine Lukoma, Head Marketing & Corporate relations, and Charles Silayo Relationship Officer Pugu Branch.
UBA Tanzania Staff members take a group photo at the Pugu branch
Staff members take a group photo at the Pugu branch.
UBA Tanzania City Centre branch staff members pause for a group photo during the celebrations of Africa Day
City Centre branch staff members pause for a group photo during the celebrations of Africa Day.
UBA Tanzania Kariakoo Branch staff member being creative with their pose in the group photo during the celebrations
Kariakoo Branch staff member being creative with their pose in the group photo during the celebrations.
Clients at Pugu Branch were also part of the celebrations
Clients at Pugu Branch were also part of the celebrations.
????????????????????????????????????
Adam Mwaipyana Team Member branch Support talks to the media about the day and what it means for UBA staff member and UBA customers as a whole.
Omar Msangi
It was the Birthday of the Head of Retail Banking, Omar Msangi as well, he cut the cake to celebrate his birthday with UBA staff members.
Josephine Lukoma
The Head MCC, Josephine Lukoma takes on the dance floor with the traditional dance troupe.
DSC_0220
The traditional dance troupe as it entertains the staff members on Africa Day.
Bahati Msuya,
The female winner of the best dressed completion Bahati Msuya, Team Member Domestic operations.
Paul Mpanda
The Male winner of the best dressed competition Mr. Paul Mpanda, Chief Security Officer.
 

Thursday, May 26, 2016

KATIBU MKUU KIONGOZI AFANYA ZIARA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA KINONDONI MWANANYAMALA DAR ES SALAAM LEO

Katibu Tawala wa Mkoa wa Dar es Salaam, Theresia Mmbando (kushoto), akitoa taarifa fupi kabla ya kumribisha Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi (katikati), wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni ya Mwananyamala Dar es Salaam leo mchana. Kutoka kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wazee na Watoto, Michael John, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Salum Ali Hapi.
Viongozi mbalimbali wakimsikiliza Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Kijazi.
Mkutano ukiendelea.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Makani ya Pentekosti (MMPT), Askofu Saldonie Sinde (katikati), akimkabidhi Katibu Mkuu magodoro 50 yaliyotolewa na Umoja wa Makanisa hayo kwa ajili ya kusaidia hispitali hiyo.



Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Kijazi (katikati), akienda kutembelea hospitali hiyo. Kushoto ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Grace Magembe.



Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi (kulia), akiwajulia hali wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kinondoni ya Mwananyamala alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja katika hospitali hiyo.
Katibu Mkuu Kiongozi akizungumza na viongozi mbalimbali katika ziara hiyo.
Hapa Katibu Mkuu Kiongozi akisikiliza malalamiko kutoka kwa wananchi waliofika katika hospitali hiyo kupata huduma (hawapo pichani)

MAMIA WAJITOKEZA KUMUAGA MWANAHABARI MAKONGORO OGING' KUZIKWA MKOANI MARA KESHO KUTWA.

 Picha ya Mwanahabari Makongoro Oging'  enzi za uhai wake.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Global Publishers alikokuwa akifanyia kazi Makongoro Oging', Eric Shigongo akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Oging' wakati wa kuagwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ilala ya Amana Dar es Salaam mchana wa leo.
 Mmiliki wa Blog ya Michuzi, Issa Michuzi akitoa heshima za mwisho  kwa mwili wa marehemu.
 Mhariri wa Habari wa Gazeti la Champion, Salehe Ali akitoa heshima za mwisho kwa marehemu.
 Waombolezaji wakiwa na huzuni wakati wa kuaga mwili wa mpendwa wao Makongoro.
 Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha ITV. Samu Mahela akitoa heshima za mwisho.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri wa Habari Tanzania (TEF), Absalom Kibanda akiwa kwenye shughuli hiyo ya kumuaga Makongoro Oging'
 Ndugu yake na Makongoro Oging' akilia wakati wa kumuaga mpendwa wake Makongoro.
 Ndugu jamaa na marafiki wakiwa kwenye uagaji wa mpendwa wao.
 Uagaji ukiendelea.
 Mtoto wa marehemu akimuaga baba yake 'hakika ni huzuni kubwa'
 Mjane wa marehemu akiwa hajiwezi baada ya kumuaga mume wake.
 Mhariri wa habari wa gazeti la Uwazi alilokuwa akiandikia marehemu Oging' Elvan Stambuli akilia kwa uchungu wakati wa kumuaga Makongoro.
 Baba mlezi wa Makongoro Oging ambaye alimsomesha, akizungumza na wanahabari.
Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Makongoro kulipeleka kwenye gari kabla ya kuanza kwa safari ya kwenda mkoani Mara.
Jeneza likiingizwa kwenye gari tayari kwa safari.

TIGO YAMDHAMINI MWANAMUZIKI BEN POL KUBURUDISHA TAMASHA LA NYAMA CHOMA

 Mkuu wa Kitengo cha Burudani na Digitali wa Tigo, Paulina Shao (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo kuhusu tamasha la nyama choma litakalofanyika  Viwanja vya Leaders kesho kutwa Jumamosi Mei 28, 2016 jijini Dar es Salaam, ambapo mwanamuziki Ben Pol atatoa burudani kwa udhamini wa kampuni ya Tigo. Kulia ni Mratibu Mkuu wa Tamasha hilo, Carol Ndosi na katikati ni mwanamuziki Ben Pol.
 Mratibu Mkuu wa Tamasha hilo, Carol Ndosi (kulia), akizungumza katika mkutano huo.
 Mwanamuziki, Ben Pol (katikati), akizungumza katika mkutano huo.
 Mtaalamu wa Kidigitali, Samira Baamar (kushoto), akichangia jambo kwenye mkutano huo.
Wanahabari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.


Na Dotto Mwaibale

Kampuni inayooongoza kwa maisha ya kidijitali Tigo Tanzania leo imekubali kumdhamini mwanamuziki nguli na mtunzi wa nyimbo za muziki, Bernard Michael Paul Mnyang'anga, maarufu kama ‘Ben Pol’ kuburudisha katika tamasha la mwaka huu la Nyama Choma.

 Tamasha hilo ambalo linafanyika kwa mwaka wa tano sasa ni moja ya tamasha maarufu linalovutia watu wengi kutoka maeneo yote ya Dar es Salaam litafanyika kwenye viwanja vya Leaders Jumamosi Mei 28, 2016. 
 Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Mkuu wa Tigo wa masuala ya Dijitali Paulina Shao  alisema kuwa  kumuunga mkono Ben Pol kunaonesha  kuendelea kujikita kwa Tigo katika  kuwekeza katika kusaidia  sekta ya muziki ya ndani kwa kuhakikisha  wasanii  wanawezeshwa  kufikia viwango vya juu katika kazi zao.

“Kama kampuni ya maisha ya kidijitali, Tigo inatambua  mchango muhimu wa wasanii wa Tanzania  wanaoutoa katika sekta ya burudani. 

Hii ndio maana  tumewekeza kwa kiwango kikubwa  kuwasaidia wasanii  hususani wanamuziki  wa ndani katika kuhakikisha wanafahamika katika masoko ndani ya nchi, kikanda na kimataifa kwa kutumia majukwaa ya kidijitali yanayokuwepo na kushiriki  matukio mbalimbali  na hivyo kuongeza  mauzo ya  muziki wao  pamoja na nembo zao,” alisema Shao.

Aidha akiishukuru Tigo kwa uungwaji mkono huo, Ben Pol  aliisifu Tigo kwa juhudi  inazofanya bila kuchoka  katika kukuza  ukuaji wa  sekta ya muziki wa ndani  kupitia Jukwaa la Muziki  la Tigo.

“Ninaishukuru sana Tigo  kwa uungwaji mkono ambao ni muendelezo wa mtiririko wa  programu ambazo imezianzisha  ili kuinua maisha ya wasanii wachanga wa Tanzania,” alisema Ben Pol na kutoa changamoto kwa wasanii wanaoibukia kuwa wasione aibu  kuomba msaada  kutoka kwa mashirika kama Tigo.

Nguli huyo wa muziki wa Bongo Flava  kwa hivi sasa anatamba na  kibao ‘MoyoMashine’ ambayo aliitoka hivi karibuni.

Ben Pol ni miongoni mwa wasanii  wanaonufaika na jukwaa la Muziki la Tigo  ambalo lilianzishwa mwaka 2015 likiwa na lengo la  kuiunga mkono sekta ya muziki Tanzania  kwa kuwasaidia wasanii wa ndani  kupata kipato zaidi kutokana na mauzo ya  kazi zao  na kuwawezesha kufahamika katika masoko ya kimataifa  kupitia majukwaa hayo ya kidijitali  kama vile Music portal na Deezer, ambayo ni majukwaa ya kimataifa yaliyo kwenye mtandao yakiwa na  nyimbo kutoka sehemu mbalimbali  duniani  zaidi ya  milioni 36.


ESRF YAFANYA WARSHA KUJADILI MPANGO WA MAENDELEO ENDELEVU (SDG)

Na Rabi Hume, Modewjiblog
Katika kusaidia kukamilika kwa Mpango wa Maendeleo Endelevu ambao unataraji kumalizika 2030, Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF) imefanya warsha ambayo imekutanisha wadau mbalimbali ili kuona ni jinsi gani wanaweza kubadilishana mawazo ili kufanikisha mpango huo nchini.

Mgeni rasmi katika warsha hiyo alikuwa ni Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha ambaye wakati akifungua warsha hiyo alisema kuwa mpango huo ni muhiu wa nchi yetu kwa sababu unakwenda kubadili maisha ya kila Mtanzania ili kuondokana na umaskini na kuwa katika maisha bora kama jinsi malengo 17 ya mpango huo yanavyojieleza.

Mo Dewji Blog ilipata nafasi ya kuhudhuria mkutano huo na kukuandalia habaroi picha jinsi warsha hivyo ilivyofanyika katika ukumbi wa ESRF.
DSC_2311
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida akitoa neno la ufunguzi katika warsa iliyoandaliwa na ESRF ili kuzungumzia Mpango wa Mendeleo Endelevu (SDG). (Picha zote na Rabi Hume, Modewjiblog)
DSC_2313
DSC_2330
Baadhi ya washiriki waliohudhuria warsha hiyo wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii, Dkt. Tausi Kida wakati akifungua warsha hiyo.
DSC_2341
Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Awa Dabo akitoa neno kwa niaba ya UNDP ambao ndiyo wasimamizi wa mpango huo. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida na Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha
DSC_2354
Mgeni rasmi katika warsha hiyo, Mkurugenzi wa Kupunguza Umaskini na Kuinua Uchumi kutoka Wizara ya Fedha, Anna Mwasha akifungua warsha hiyo iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Kijamii (ESRF).
DSC_2367
DSC_2384
Washiriki wakiendelea kufatilia kinachoendelea katika warsha hiyo.
DSC_2478
Stephen Chacha kutoka Shirika la Beyond 2015 for Africa akizungumza jinsi Mpango wa SDG unaweza kufanyika nchini.
DSC_2481
DSC_2521
Mmoja wa washiriki, Dkt. Kitila Mkumbo akichangia mada zilizokuwa zikijadiliwa.
DSC_2457
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja.