Pages

KAPIPI TV

Thursday, October 8, 2015

RAIS JAKAYA KIKWETE AWEKA JIWE LA MSINGI LA JENGO LA MOROCCO SQUARE JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akifungua pazia kuashiria  uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa Jengo la Morocco Square Dar es Salaam jana. Wanaoshuhudia tukio hilo kutoka kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la  Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya CRDB, Dk.Charles Kimei, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.
 Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akisalimiana na wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakati wa hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa Jengo la Morocco Square.
 Rais Jakaya Kikwete (katikati), Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa  (NHC), Zakhia Meghji (kulia) na Waziri wa Ardhi Nyumba Maendeleo na Makazi, William Lukuvi wakipiga makofi kumpongeza Rais Kikwete katika siku yake ya kuzaliwa iliyofanyika sanjari na hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la jengo hilo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa  (NHC), Zakhia Meghji (wa pili kulia), akimkabidhi zawadi ya sherehe yake ya kuzaliwa.

 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakifungua shampeni kumpongeza Rais Kikwete katika siku yake hiyo ya kuzaliwa.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la  Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kulia), wakati wa hafla hiyo ya uwekaji wa jiwe la msingi la jengo hilo. Kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la  Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu akiteta jambo na Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki wakati wa hafla hiyo.
 Wadau mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi huo.
 Waandishi wa habari wakiwa kwenye hafla hiyo.
 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakiwa kwenye sherehe hiyo.
 Wadau mbalimbali na Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), wakiwa kwenye sherehe hiyo.
Rais Jakaya Kikkwete akiwa katika picha ya pamoja na viongozi 
wa NHC.

Na Dotto Mwaibale

RAIS Jakaya Kikwete amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa, (NHC), chini ya Mkurugenzi wake Nehemia Mchechu kwa mradi wa ujenzi wa jengo la Moroco Square ambao utagharimu sh.bilioni 150 za kitanzania hadi kukamilika kwake.

Mradi wa ujenzi huo utakamilika mwaka 2017 na jengo litakuwa na mita za mraba 110,000 na ukiwa na majengo manne.Mawili ni kwa ajili ya ofisi , moja hoteli na nyingine nyumba za makazi ya watu 100, ghorofa 20 na kiwanha cha  ambapo mawili ni kwa ajili ya ofisi, moja Hoteli na lingine ni kwa ajili ya nyumba za makazi ya watu 100 , ghorofa 20 lenye eneo la kiwanja cha ndege kwa juu yake.

Akizungumza Dar es salaam jana, wakati wa uwekaji jiwe la msingi wa ujenzi wa eneo hilo jana, Rais Kikwete alisema mradi huo ni mkubwa kuliko yote katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati na utaifikisha nchi katika hatua nyingine za kimaendeleo.

Aliongeza kuwa ni mambo mapya kuanzishwa Tanzania tofauti na siku za nyuma, hivyo alilipongeza NHC kwa kwenda na wakati. 

Rais Kikwete alisema utakapokamilika mradi wa eneo hilo la Mororco Square utakuwa na faida nyingi kama kupunguza gharama za wananchi kwenda mijini kutokana na huduma zote za kijamii kupatikana eneo hilo.

Alitoa mwito kwa NHC kufungua huduma ya Online ili watu wasipate shida wawe wanafanya kila kitu kupitia mitandao badala ya kuhangaika barabara kwenda kutafuta huduma na matokeo yake wanapoteza muda.

Alisema katika kuhakikisha huduma zinafanyika kwa urahisi inabidi ziwekwe barabara za juu ili watu wanaopita katika eneo hilo wavuke salama.

"Pale Morocco kuna njia nne, hivyo kinachotakiwa ni kuweka barabara ya juu lakini sijui kama itawezekana kutokana na kuwa namaliza muda wangu, lakini nawaahidi kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za NHC, hivyo changamoto zenu zitatatuliwa "alisema.

Kwa upande wake, Mchechu alifafanua eneo hilo litakuwa na viwanja vya michezo kwa watoto, maduka hivyo ni kitovu cha kuchangamsha mji kutokana na kuwa lipo katikati ya mji. 

Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Zakhia Meghji alisema anaamini kuwa Rais ajaye ni Dk.John Magufuli, hivyo anaamini ataendeleza mradi huo aliouacha Kikwete.

Alisema umefika wakati wa kutungwa sheria itakayowezesha wageni kununua nyumba hizo kutokana na iliyopo hairuhusu ili kupanua soko kwa wateja.

Mradi huo umefanikiwa kwa kupata mkopo wa fedha kutoka Benki ya CRDB chini ya uongozi wa Mkurugenzi Mkuu, Dk. Charles Kimei.


Wednesday, October 7, 2015

AISHA, A MOVIE WITH DIFFICULT STORY TO TELL

Aisha in agony
Aisha in agony.
By our Reporter
AISHA a movie produced locally to address the pains of turning a blind eye on issues which affects women in particular rape, was screened over the weekend at Century Cinema in Mlimani City, Dar es salaam.
It was a shocking story, coupled with dangerous moves portrayed very accurately by actress and actors on the movie.
The director Omar Chande brilliantly made his shocking story understood to the public by presenting close ups and cuts barely used in the country.
Godliver Gordian, Adarusi Walii, Florah Nicholas and, Juma Madenge managed to send home the message and in fact the audiences in a full packed house at Mlimani cinema hall were kept in suspense for a long time before realizing that all glitters are not diamonds, ex- lover revenge was so distasteful to a tune of making the full packed room very uncomfortable, aghhhh!.
Aisha, which is UZIKWASA’s Third Film tells a story of a young married pharmacist living in the city who decides to go home to visit her younger sister who is about to be wedded to the son of a local village leader.
While at home, she meets with familiar faces and attempts rekindling the past. However, when an old flame turns cold and spoke the truth she cannot engage in extramarital an ex-boyfriend who was also married got furry and decided to seek revenge.
Aisha being consollled by her brother
Aisha being counselled by her brother.
In his outrage action with a director consequences to the girl, a group of people rapped the girl in turn and left her dying. She did not die. Her little sister set out early in the morning searching for her until she found her in the beach laying there unconscious.
She cried she didn’t know what happed to her big sis and when the brother arrived the way he talked to his little sister one can start thinking what kind of a community was that, it looks like the deed was done and everyone would rather turn a blind eye, than seeking justice.
Diana Kamara, one of the audiences at the Movie, said the film made her feel very angry as it took her like a storm. She said she failed to swallow the stigma, shame and victim blame with leaders reluctance to take action against culprits.
Her girlfriend, Monica added that there should be a campaign to arose interest on common forms of violence against women .She believed that Aisha showed a way to break the silence about one of the most devastating form of violence against women, rape.
The husband listening the horrofying story
The husband listening the horrifying story.
Godliver Gordian who acted as Aisha in the movie, said she acted with passion after hearing what happened to her fellow women, to her it was a tragedy which was supposed to be exposed with compassion and clarity so as to catch audience who in turn will do something about this devastating behavior.
Godliver made me believe we have actress she worked hard and in a way managed to make people shout no in the theatre while rape scene was being screened.
The trauma from rape and injustice it was just like love being betrayed everywhere and even the husband who declared her love showed no interest in it, after listening to the tell of rape done to her spouse by a bunch of thugs. He left her in a hurry not to come back; she wanted it she got it, what a stigma!
Godliver (Aisha) talking to one of her new fan after Aisha screening
Godliver (Aisha) talking to one of her new fan after Aisha screening.
To her next of kins it was another betrayal. Her Brother for reasons known best to him failed to reason with her sister to seek justice and he was forced to try it by his wife when she told her point blank: If Ramadhan is the culprit what are you waiting for? Until your daughter and I being rapped?
Yes, it was like a question directed to the audiences, what are they waiting for.
Director of the film Omar Chande giving a hand to Adarus Walii who acted as Ramadhan, Aisha ex boyfriend
Director of the film Omar Chande giving a hand to Adarus Walii who acted as Ramadhan, Aisha ex boyfriend.
Director of the film Omar chande possing for a picture with executive director of the film
Director of the film Omar Chande posing for a picture with executive director of the film, Vera Pieroth.
Godliver taking selfie
Godliver taking selfie.
The director of the movies Omar Chande said it took him three weeks to do the film which is dedicated to women who have gone through the same sufferings as Aisha.
Although the story is very difficult to tell, the actors and actress who went almost 21 days of training, managed to produce a movie which unfolds itself. That is From confidant and cheerful life to the most challenging life when confidence destroys peace, love and harmony.
Executive producer of the movie Vera Pieroth spoke about the need of the community to break the silence and start helping women by ensuring their safety and dignity.
Different people after the screening of Aisha at Mliman Century
Different people after the screening of Aisha at Mliman Century.
Godliver Gordian who acted as Aisha
Godliver Gordian who acted as Aisha.
Invited guests after the show.
Ramadhan and his henchmen after being surrounded by the village
Ramadhan and his henchmen after being surrounded by the village.
The gang after doing their dirty job
The gang after doing their dirty job.
Preparations for the wedding day
Preparations for the wedding day.
Aisha and ramadhan remembering their old goodtimes
Aisha and ramadhan remembering their old goodtimes.

WIZARA YA UJENZI YAELEZEA MAFANIKIO YAKE KWA KIPINDI CHA MIAKA 10


Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Ujenzi, Segolena Francis (kulia), akizungumza na wanahabari Dar es Salaam leo asubuhi wakati akimkaribisha  Mkurugenzi wa Barabara wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Ven Ndyamkama (kushoto), kuzungumza na waandishi wa habari  kuhusu mafanikio ya serikali katika sekta ya ujenzi kwa kipindi cha  miaka 10 kuanzia mwaka 2005 hadi 2015.

Mkurugenzi wa Barabara wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Ven Ndyamkama (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo mchana, kuhusu mafanikio ya serikali katika sekta ya ujenzi kwa kipindi cha  miaka 10 kuanzia mwaka 2005 hadi 2015. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa wizara hiyo, Segolena Francis.
Hapa mkutano ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale


WIZARA ya Ujenzi imesema itashirikiana na Sekta Binafsi (PPP) kuhakikisha kuwa baadhi ya miradi ya barabara inajengwa na sekta hiyo ili kukamilisha miundombinu ya usafiri nchini.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Barabara katika Wizara hiyo Mhandisi Ven Ndyamukama wakati akizungumza na waandishi wa habari leo katika Ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam.

Alisema mfano wa mradi wa ushirikiano wa Serikali na PPP ni barabara ya Dar es Salaam hadi Chalinze ambayo itakuwa na njia sita unatarajiwa kuanza hivi karibuni.

Alisema lengo la Serikali kushirikiana na sekta binafsi ni kuhakikisha kuwa miradi mingi inakamilika kwa wakati ambapo kwa kipindi cha miaka 10 ya Serikali ya awamu ya nne wamekamilisha ujenzi wa kilometa 5,568 za lami zilizogharimu sh. bilioni 4,090 kati kilometa 17,762 ambazo zilitarajiwa kujengwa.

"Tumejipanga kushirikiana na sekta binafsi katika utekelezaji wa miradi mingi hapa nchini lakini kwa kuanza ni huu wa Dar es Salaam hadi Chalinze unaotarajiwa kuanza hivi karibuni," alisema.


Pia alisema kilometa 3,873 zinaendelea kujengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya jumla ya sh.bilioni 4,533 na barabara zenye urefu wa kilometa 4,965 zimefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa gharama ya shilingi bilioni 29.257 ambapo Serikali inatafuta fedha za ujenzi wa lami.

UNESCO KUENDELEZA UTAMADUNI WA KUZISAIDIA REDIO JAMII

IMG_4940
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Utawala na Fedha), Bw. Liberat Mfumukeko alipowasili katika chumba maalum cha wageni kabla ya kuelekea kwenye ufunguzi wa kongamano la siku tatu la Mtandao wa Redio za Jamii katika nchi za Afrika Mashariki (EACOMNET) linalolenga kujadili namna ya kuziwezesha redio hizo kujiendesha katika mipango endelevu kwa kuwa na mipango sahihi ya kifedha bila kutegemea fedha kutoka kwa wafadhili ili ziweze kutoa mchango unaokusudiwa kwa wananchi linaloendelea katika makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Na Modewjiblog team, Arusha
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), limeonyesha nia yake ya kuendeleza utamaduni wa kuzisaidia redio za jamii nchini Tanzania kwa lengo la kuwawezesha Watanzania walio wengi kupata elimu na hatimae kujinasua katika umaskini.

Akizungumza katika ufunguzi wa kongamano la Mtandao wa Redio za Jamii katika nchi za Afrika Mashariki (EACOMNET) linalofanyika makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC) mjini Arusha, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi mkazi wa UNESCO Zulmira Rodrigues alisema kwamba watu zaidi ya milioni 16 wengi wao wakiwa pembezoni mwa Tanzania wanategemea redio za jamii katika kuelimishwa masuala mbalimbali ya ustawi wa jamii jambo ambalo shirika lake linawajibika kwa redio hizo kwa kutoa misaada mbalimbali ili ziweze kujitegemea na kutoa huduma zake kikamilifu.
Alisema anaamini kwamba kwa miaka kadhaa ijayo redio za jamii zitakuwa chanzo cha maarifa kwa watu wengi nchini Tanzania kutokana na uasilia wake na kwa kuyatumikia maeneo ambayo kimawasiliano ni vigumu kufikika, na wakati huo huo vyombo vikuu vya mawasiliano kushindwa kukidhi mahitaji ya wanajamii jambo linalosababisha ukosefu wa kupata habari muhimu na kuzorotesha maendeleo katika jamii husika.
IMG_4942
Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Utawala na Fedha), Bw. Liberat Mfumukeko akisalimiana na Mwenyekiti wa Radio za Jamii kutoka UNESCO India, Prof. Vinod Pavarala katika chumba maalum cha wageni katika makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha.
Zulmira amezihimiza redio hizo kutoa huduma zinazostahili kwa jamii za kupasha, kuelimisha na kuburudisha, pamoja na kujiwekea mikakati wa kudumu ya kuhamasisha rasilimali fedha zitakazosaidia kuboresha huduma za redio na kuboresha mfumo wa mawasiliano kati kituo cha redio na wanajamii.
Miongoni mwa maboresho yatakayoendelezwa na Unesco ni kusaidia uhakiki wa ubora wa matangazo, vipindi vyenye kuzingatia maadili na ushirikishwaji wa makundi yote wakiwemo wanawake ,vijana ,watu wenye ulemavu na Albinism katika mchakato wa demokrasia, amani na maendeleo .
Kongamano hilo la siku tatu pamoja na mambo mengine linalenga kujadili namna ya kuziwezesha redio hizo kujiendesha katika mipango endelevu kwa kuwa na mipango sahihi ya kifedha bila kutegemea misaada kutoka kwa wafadhili ili ziweze kutoa mchango unaokusudiwa kwa wananchi.
Kwa niaba ya mtandao wa redio jamii ukanda wa Afrika Mashariki, mwenyekiti wa Mtandao wa redio za Jamii Tanzania, COMNETA Joseph Sekiku aliishukuru Unesco kwa kuziwezesha redio za jamii kutoka nchi za Afrika Mashariki kukutana kwa lengo kushirikiana na kupeana maarifa kuhusu uendeshaji wa redio hizo na zitakavyoweza kutekeleza kwa ubora malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu na UNESCO India kwa kuleta maarifa mapya kuhusu uendeshaji wa redio za jamii.
IMG_4980
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues (kulia) akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Utawala na Fedha), Bw. Liberat Mfumukeko katika chumba maalum cha wageni kabla ya kuelekea kwenye ufunguzi wa kongamano la siku tatu la Mtandao wa Redio za Jamii katika nchi za Afrika Mashariki (EACOMNET) linalofanyika makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha.
Nchi zilizoshiriki katika kongamano hilo ni Burundi, Kenya, Rwanda na Uganda chini ya mwamvuli wa Mtandao wa Redio za jamii Afrika mashariki (EACOMNET), ukiwa na redio wanachama 50 zenye uwezo wa kuwafikia wasikilizaji milioni 35 kati ya watu milioni 120 waliomo katika nchi hizo.
Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Utawala na Fedha), Liberat Mfumukeko ameelezea kufurahishwa kwake kufanyika kwa kongamano hilo ambalo litasaidia redio jamii kupata maarifa zaidi na elimu kuhusu mtengamano wa Afrika Mashariki na kuufanikisha.
Alisema Jumuiya ya Afrika Mashariki inaelewa umuhimu wa vyombo vya habari hasa vya jamii kutokana na kazi yake kwa kuzingatia juhudi utekelezaji wake wa kuhamasisha jamii kuendeleza mtengamano wa Afrika Mashariki.
IMG_5030
Mwenyekiti wa Mtandao wa redio za Jamii Tanzania, (COMNETA), Joseph Sekiku akizungumza kwa niaba ya mtandao wa redio jamii ukanda wa Afrika Mashariki (EACOMNET) kabla ya kumkaribisha Prof. Vinod Pavarala.
IMG_5097
Mwenyekiti wa Radio za Jamii kutoka UNESCO India, Prof. Vinod Pavarala akieleza dhumuni na lengo la kongamano hilo kwa washiriki. Kulia ni Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la UNESCO nchini, Zulmira Rodrigues.
IMG_5199
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Utawala na Fedha), Bw. Liberat Mfumukeko kufungua rasmi kongamano hilo linaloendelea jijini Arusha.
IMG_5266
Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Utawala na Fedha), Bw. Liberat Mfumukeko akifungua rasmi kongamano la siku tatu la Mtandao wa Redio za Jamii katika nchi za Afrika Mashariki (EACOMNET) linalolenga kujadili namna ya kuziwezesha redio hizo kujiendesha katika mipango endelevu kwa kuwa na mipango sahihi ya kifedha bila kutegemea fedha kutoka kwa wafadhili ili ziweze kutoa mchango unaokusudiwa kwa wananchi linaloendelea katika makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha.
IMG_5151
Mwenyekiti wa Radio za Jamii kutoka UNESCO, Prof. Vinod Pavarala akimkabidhi Ofisa Miradi katika kitengo cha Mawasiliano, Habari na Tehama UNESCO, Bw. Al Amin Yusuph zawadi kwa heshima ya ukumbusho wa India.
IMG_5155
Ofisa Miradi katika kitengo cha Mawasiliano, Habari na Tehama UNESCO, Bw. Al Amin Yusuph akitoa shukrani zake kwa Prof. Vinod baada ya kupokea zawadi.
IMG_5060
Ofisa miradi mpya katika kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizilege akijitambulisha kwa hadhira ya washiriki wa kongamano.
IMG_5010
Sehemu ya washiriki katika kongamano hilo.
IMG_5382
Mhadhiri wa Chuo cha Uandishi wa Habari cha Hyderabad India, Dkt. Kanchan Malik akiongoza kikundi kazi kilichojumuisha washiriki kutoka Rwanda na Uganda.
IMG_5360
Mwenyekiti vyombo vya Habari Jamii kutoka UNESCO India, Prof. Vinod (aliyeipa mgongo camera) akiongoza kikundi kazi kinachojumuisha washiriki kutoka Burundi na Tanzania.
IMG_5281
Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akifurahi jambo na Mjumbe wa bodi udhamini ya Mtandao wa Radio Jamii Tanzania (COMNETA), Balozi Mstaafu, Christopher Liundi nje ya chumba cha mikutano makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha.
IMG_5296
Mjumbe wa bodi udhamini ya Mtandao wa Radio Jamii Tanzania (COMNETA), Balozi Mstaafu, Christopher Liundi (kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu mpya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Utawala na Fedha), Bw. Liberat Mfumukeko wakati wakielekea kwenye zoezi la picha ya pamoja.
IMG_5307
Picha ya pamoja baada ya ufunguzi wa kongamano hilo.
IMG_5309
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akiwapungia kama ishara ya kuagana na washiriki wa kongamano hilo wakati akiondoka makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) jijini Arusha kuanza safari ya kuelekea uwanja wa ndege tayari kurejea Dar es Salaam.

UBA TANZANIA CELEBRATES THE EVERYDAY HEROES: CUSTOMER SERVICE WEEK


Customers and the MD cut the cake to celebrate the Customer Service Week 5-9 October 2015.(All photos by Geofrey Adroph).
Customers toast their glasses in celebration of the Customer Service Week 5–9 October 2015
A cross section of UBA staff with customer of the Bank during the celebration of the Customer Service Week 5 – 9 October 2015.
The Managing Director Mr. Demola Ogunfeyimi addressing UBA staff and Customers at the UBA banking hall at PUGU road during the Customer Service Week celebration.
Mr. Demola Ogunfeyimi the MD of UBA Tanzania hands over gifts to Customers in celebration of the Customer Service Week 5–9 October 2015
Mr. Demola Ogunfeyimi the MD of UBA Tanzania hands over gifts to Customers in celebration of the Customer Service Week 5–9 October 2015
A cross section of UBA staff during the celebration of the Customer Service Week 5 – 9 October 2015.
“I have been banking with UBA since its inception in Tanzania in 2009 and I can say your services are great. I have been receiving first class service, in that manner I have been able to recommend UBA to other businessmen in my circle and I will continue to refer them so they can receive what I am getting from here which excellent customer service” Commented one happy Customers. UBA Tanzania recognizes this year’s theme as a powerful message for our service teams and entire organization to celebrate during this Customer Service Week. “In celebration of our everyday heroes, we invite all our customers to celebrate with us during this Customer Service Week, October 5-9, 2015” mentioned Queen Odunga the Head of Service Quality. “Since UBA started in 2009 we had a very small customer base, but now we have managed to open more that 5000 accounts, sold more than 7000 Visa prepaid cards and enrolled a big number of clients on our other E-banking products, i.e. the U-Direct corporate and U-mobile which helps a customer to access financial convenience on their mobile phones or computers wherever they may be, in Tanzania and the rest of the world. This is reason enough for UBA Tanzania to celebrate this Customer service week” Said Madam Flavia Kiyanga the Head of Domestic Operation. This year’s Customer Service Week theme is “Everyday Heroes” The theme recognizes that every day, frontline customer service professionals are heroes in their customer’s eyes.