Pages

KAPIPI TV

Sunday, December 21, 2014

UEFA GOO NIGHT CLUB KUZINDULIWA MKESHA WA KRISMAS

3Kiwanja kipya cha maraha Uefa Goo Night Club kinatarajiwa kuzinduliwa mkesha wa sikukuu ya Krismas jijini Dar es salaam Kiwanja hiki ni cha Kisasa kiko maeneo ya Ukonga Mombasa Barabara ya kuelekea Moshi Baa Karibu na njia panda ya Mahitamita 200 kutoka barabara kuu iendayo Pugu, siku ya mkesha wa Krismas burudani kibao zimeandaliwa na na kiko katika hatua za mwisho mwisho kukamilisha kila kitu ili kuwapa burudani wateja wake ikiwa ni pamoja na Ligi mbalimbali za ulaya, muziki wa kisasa kama vile Bongofleva na muziki wa zamani na vyakula mbalimbali vitapatikana
 
UEFA GOO NIGHT 2Hizi ni baadhi ya picha zinazoonyesha jengo kwa nje na maendeleo ya kukamilisha ujenzi kwa ndani kwenye klabu hiyo ambao umefikia asilimia 99 kabla ya kufunguliwa mkesha wa Krismas.7 6 5 4

WAIMBAJI WA TAMASHA LA KRISMAS MKOANI MBEYA WAELEZEA MAANDALIZI YAO

 
1Mwimbaji wa muziki wa injili Tumaini Njole akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za kampuni ya Msama Promotion ambayo inaandaa Tamasha la Pasaka litakalofanyika sikukuu ya Krismas tarehe 25/12/2014 mkoani Mbeya wakati alipozungumzia maadalizi ya tamasha hilo na jinsi alivyojipanga kukonga mioyo ya mashabiki wa nyimbo za injili mkoani Mbeya , Tamasha hilo linatarajiwa kuanza muda wa Saa nane mchana viingilio vikiwa ni shilingi 5000 kwa watu wazima na watoto shilingi 2000, Katika tamasha hilo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Fredrick Sumaye na waimbaji wengine watakaotumbuiza ni Faraja Ntaboba, Upendo Nkone, Upendo Kirahilo, Rose Muhando, Bony Mwaiteje Edson Mwasabwite, Ambwene Mwasongwe na wengine wengi, Pia matamasha mengine yanatarajiwa kufanyika mkoani Iringa tarehe 26/12/2014 na Songea tarehe 28/12/2014, Katika Picha kushoto ni Mwimbaji Joshua Mlelwa.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM) 2Mwimbaji wa muziki wa Injili Edson Mwasabwite akifafanua jambo wakati wa mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam , Kushoto ni mwimbaji Joshua Mlelwa na katikati ni Mwimbaji Tumaini Njole 3Mwimbaji Joshua Mlelwa akielezea maandalizi yake wakati wa Tamasha la Pasaka litakalofanyika mkoani Mbeya wakati wa Sikukuu ya Krismas kulia ni Mwimbaji Tumaini Njole.

Saturday, December 20, 2014

AJALI YAUA WATU WAWILI,YAJERUHI 25-BARABARA YA KIGWA, TABORA

Baadhi ya wauguzi hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tabora Kitete wakiwapatia huduma za matibabu watu waliojeruhiwa katika ajali ya gari huko barabara ya Kigwa-Nyahua,...Imeelezwa kuwa watu hao ambao ni wafanyakazi wa moja ya kampuni ya wachina inayojenga barabara ya kutoka Kigwa kuelekea Nyahua ambapo magari mawili yakiwa yamewabeba wafanyakazi hao kuwapeleka eneo la kazi yalikuwa yakifuatana kwa mwendo wa kasi hatimaye gari kugonga jingine kwa nyuma....Watu wawili wamefariki na wengine 25 kujeruhiwa vibaya ambao wamelazwa katika hospitali hiyo huku hali zao zikiwa si za kuridhisha.(Picha na Mrisho Juma 0783 626771)


Friday, December 19, 2014

FEDHA ZAPORWA ENEO LA MSIKITINI ZANZIBAR,NI EURO 1000 NA SHILINGI MILIONI TANO ZA KITANZANIA

Umati mkubwa wa wananchi wakistaajabu tukio hilo la wizi wa fedha eneo la msikitini.


 Na Haroub Hamisi -Zanzibar
Watu wasiofahamika wamevunja kioo cha gari na kuiba pesa Euro 1000 na shilingi milioni tano za kitanzania.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari kutoka eneo la tukio mwenye gari  hilo aina ya Landcruiser  lenye nambari za usajili Z 977 BM alifika na kuliegesha na kisha kuingia Msikitini kusali sala ya Ijumaa katika Msikiti wa eneo la Mlandege mjini Zanzibar.

Aidha baada ya kuegeshwa gari hilo lilitokea gari jingine nyuma yake ambalo mtu mmoja alishuka akiwa na Panga mkononi na kuanza kugonga kioo cha gari hiyo na kufanikiwa kufungua mlango na kutoa mkoba uliokuwa umehifadhiwa kiasi hicho kikubwa cha fedha na kutoweka nacho kusikojulikana.

Hata hivyo imeelezwa kuwa askari wa Jeshi la polisi walifika eneo la tukio kwa lengo la kufuatilia sakata hilo la uporaji.





SERIKALI YAZINDUA RASMI USAMBAZAJI TAKWIMU ZA PATO LA TAIFA, PATO LA MWANACHI LAONGEZEKA

unnamedWaziri wa Fedha Mh. Saada Mkuya Salum (katikati) akizindua rasmi Takwimu za Pato la Taifa zilizorekebishwa kwa mwaka wa kizio wa 2007 leo jijini Dar es salaam. unnamed1 Waziri wa Fedha Mh. Saada Mkuya Salum (kulia) akimkabidhi Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servicius Likwelile chapisho la lenye Takwimu za Pato la Taifa zilizorekebishwa kwa mwaka wa kizio wa 2007 wakati wa uzinduzi wa usambazaji wa takwimu hizo leo jijini Dar es salaam. unnamed2Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa(Kushoto) akitoa ufafanuzi wa kazi ya kurekebisha takwimu za Pato la Taifa iliyofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu iliyotumia tafiti za taifa zilizofanyika kwa kipindi cha mwaka 2001 hadi 2007.Kulia ni Waziri wa Fedha Mh. Saada Salum Mkuya. unnamed3Baadhi ya viongozi na wageni waliohudhuria uzinduzi wa usambazaji wa Takwimu za Pato la Taifa zilizorekebishwa kwa mwaka wa kizio wa 2007 wakimsikiliza Meneja wa Takwimu za Pato la Taifa, Bw. Daniel Masolwa wakati akiwasilisha mada kuhusu Pato la Taifa leo jijini Dar es salaam.
....................................................................................................
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
. Dar es salaam.
Serikali imesema kuwa Pato la Taifa kwa mwaka 2007 limeongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 26.8 ikilinganishwa na trilioni 20.9 za mwaka 2001, ambapo wastani wa pato la mwananchi mmoja mmoja limeongezeka kutoka shilingi milioni1,186,200/= mwaka 2001 hadi shilingi milioni 1, 561,050/= mwaka 2013.

Akizindua usambazaji wa takwimu hizo leo jijini Dar es salaam, Waziri wa Fedha Mh. Saada Mkuya Salum ameeleza kuwa matokeo hayo ni sawa na ongezeko la ukubwa wa Pato la Taifa kwa asilimia 27.8.

Amesema ongezeko hilo ni matokeo ya juhudi za Serikali kuweka mazingira mazuri na kutengeneza fursa za kuwawezesha wananchi kufanya kazi za kujiajiri na hatimaye kupata kipato halali kwa kazi wanazofanya.

Mh. Mkuya amesema kuwa kukua kwa uchumi wa Tanzania kumechangiwa na kujumuishwa kwa shughuli mbalimbali zikiwemo Sayansi na Teknolojia ambako kumetoa fursa kwa wananchi kujiongezea kipato hususan matumizi ya simu za kiganjani ambazo zimerahisisha mawasiliano na utafutaji wa masoko ya bidhaa ndani na nje ya nchi.

Amezitaja shughuli nyingine kuwa ni ukamilishaji wa miamala mbalimbali ya kibenki na mikopo ambazo zimekuzwa na sekta ya mawasiliano , kuongeza ajira na kupunguza muda wa kusubiri huduma za malipo katika maeneo mbalimbali nchini.

Aidha, amefafanua kuwa kuongezeka kwa thamani ya Pato la Taifa kunaiongezea Serikali uwezo kimapato kupitia kodi na kuiwezesha kugharamia ujenzi wa miundombinu na utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi.

“Serikali imeendelea kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji safi na salama, utafiti wa mapato na matumizi ya Kaya Binafsi ya mwaka 2012 unaonyesha asilimia 60 ya kaya zote nchini zinapata maji safi na salama hasa hususan maeneo ya mijini,zaidi ya asilimia 20 ya kaya zote nchini zinatumia nishati umeme haya ni mafanikio makubwa ya matokeo ya ukuaji wa uchumi nchini” Amesisitiza Mh. Mkuya.

Akizungumzia mchango wa Sekta Binafsi katika kukua kwa pato la taifa nchini amesema kuwa ajira zipatazo laki nne kati ya laki sita katika sekta iliyo rasmi zimepatikana.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa akizungumza wakati wa uzinduzi huo amesema kuwa kazi ya kurekebisha takwimu za Pato la Taifa imetumia Tafiti za Taifa zilizofanyika kwa kipindi cha mwaka 2001 hadi 2007.

Amezitaja tafiti hizo kuwa ni pamoja na utafiti wa mapato na matumizi ya Kaya wa mwaka 2007, Sensa ya Kilimo iliyofanyika mwaka 2008 na Takwimu nyingine za utawala kutoka katika Wizara na Idara za Serikali.

Aidha, amefafanua kuwa ukokotoaji wa takwimu hizo umefuata mfumo wa Umoja wa Mataifa wa kutayarisha takwimu za Pato la Taifa wa mwaka 1993 na 2008 kwa lengo la kuhakikisha kuwa takwimu hizo zinalinganishwa na takwimu nyingine duniani.

KAJALA AKUNWA NA KUMWAGA MAHELA KWA WAIMBAJI WA SKYLIGHT BAND WANAOTOA BURUDANI KILA IJUMAA THAI VILLAGE,MASAKI

DSC_0028
Meneja wa Skylight Band Aneth Kushaba AK47 akitoa burudani kwa mashabiki wa bendi hiyo Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village huku akipewa sapoti na Digna Mbepera.
DSC_0030
Digna Mbepera na Bela Kombo wakimpa back up Aneth Kushaba AK47 kwenye show zao za kila Ijumaa ndani ya viunga vya Thai Village Masaki jijini Dar.
DSC_0071
Majembe ya Skylight Band yakionyesha manjonjo yao jukwaani Ijumaa iliyopita ndani ya kiota cha Thai Village Masaki.
DSC_0082
Aneth Kushaba na Sam Mapenzi wakiwapa raha mashabiki wao huku Digna Mbepera na Bella Kombo.
DSC_0092
Sam Mapenzi na Aneth Kushaba AK47 wakifanya yao jukwaani.
DSC_0147
Pichani juu na chini ni mashabiki wa Skylight Band wakiserebuka mdogo mdogo.
DSC_0149
DSC_0158
Birthday girl nae hakubaki nyuma aliunga tela na kuburudika na Skylight Band.
DSC_0279
Msanii wa bongo movie Kajala akitembeza manoti ya wekundu wa msimbazi kwa waimbaji wa Skylight Band Ijumaa iliyopita alipokunwa na uimbaji wao.
DSC_0280
Kajala akizichomoa tu kwenye pochi lake.
DSC_0281
Joniko Flower akisubiria zamu yake.
DSC_0282
Joniko Flower akipokea manoti yake kutoka kwa Msanii wa bongo movie Kajala.
DSC_0283
Na kwa wale wasanii waliokuwa back stage pia walibahatika kujizolea manoti kutoka kwa Kajala.
DSC_0298
Wapenzi wa Skylight Band wakishuhudia tukio hilo.
DSC_0306
Twende kazi... na burudani iendeleeee..!
DSC_0326
Mashabiki nao wakajibu mapigo.
DSC_0340
Sam Mapenzi akitunzwa na shabiki wake.
DSC_0343
DSC_0160
Sam Mapenzi akiwapa raha mashabiki wa Skylight Band, Ijumaa iliyopita huku Joniko Flower na Sony Masamba wakimpa sapoti.
DSC_0164
Mashabiki wakiendelea kula raha..!
DSC_0345
DSC_0170
Birthday girl na mabeste zake wakicheza mdogo mdogo.
DSC_0189
Mguu wa kushoto mbele wa kulia nyuma...... mashabiki wakiondoka ma-style ya Skylight Band.
DSC_0115
Hashim Donode na Bela Kombo wakiburudisha mashabiki wa Skylight Band huku wakipewa back up na Aneth Kushaba pamoja na Digna Mbepera.
DSC_0121
nakupenda pia pia aha...Nakupenda pia...You make me wanna say....Nakupenda pia pia ahaa.....Vijana wakiwa kwenye hisia kali jukwaani.
DSC_0196
Majembe ya Skylight Band yakisebeneka jukwaani huku yakijaribu kuwafundisha mashabiki wao.
DSC_0198
Mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Joniko Flower akiwachezesha ligwaride la sebene majembe ya Skylight Band Ijumaa iliyopita ndani ya Thai Village .
DSC_0146
Mtaalamu wa kupiga kinanda Danny akifanya yake huku akipata Ukodak.
DSC_0044
Mmoja wa mashabiki wa Skylight Band alikuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa ndani ya kiota cha Thai Village Masaki huku bendi hiyo ikimpa zawadi ya kumwimbia wimbo maalum wa sherehe hizo kumpongeza.
DSC_0045
Birthday girl akiendelea na zozezi la kulisha vipande vya cake shosti zake.
DSC_0048
DSC_0053
Birthday girl akiteta jambo na mchumba wake Lota Mollel.
DSC_0054
Mahaba niuweeeeeeee! Birthday girl akipata kiss kutoka kwa mchumba wake Lota Mollel.
DSC_0056
Birthday girl akiendelea kukata cake kwa ajili ya kuwalisha ndugu, jamaa na marafiki waliojumuika naye.
DSC_0058
Birthday gilr na mchumba wake wakilishana cake kimahaba zaidi....!
DSC_0207
Emma Beyz na Danny Kinanda.
DSC_0223
Wadau wakipata Ukodak.
DSC_0356
Mdau Iddi Baka na Blogger King Kif wakishow love mbele ya camera yetu.
DSC_0226
Warembo wa ukweli na wenye viwango na ubora wanapatikana Skylight Band pekee hakunaga kwingine.
DSC_0239
DSC_0358
Nyomi la mashabiki wa Skylight Band likiwa limeshona Ijumaa iliyopita ndani ya Thai Village.