Pages

KAPIPI TV

Saturday, October 25, 2014

KAMPUNI YA KARIATI YAKABIDHI WAKULIMA MATREKTA MANNE LEO, JIJINI DAR ES SALAAM


Kampuni ya Kariati Matracktor Diwani wa Kata ya Kwadelo, Kondoa mkoani Dodoma, Omary Kariati, leo imekabidhi matrekta manne kwa wakulima wa wilaya ya Kondoa (matrekta matatu) na Mbarali (trekta moja), katika hafla iliyofanyika leo asubuhi, kwenye Ofisi za Kariati Matrektor, Kinondoni, Dar es Salaam. Zinazofuatia ni picha za hafla hiyo. Picha/Maelezo na Bashir Nkoromo
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kariati Matractor, Omary Kariati akimkabidhi fungua za trekta Mwakilishi wa wkulima wa Kondoa, Karoli Lubuva, katika hafla ya makabidhiano hayo, iliyofanyika leo.
Kariati akikata uatepe kuzindua makabidhiano ya trekta hizo
 Kariati akiwapa maelezo kuhusu trekta husika kabla ya kuzikabidhi kwa wawakilishi wa wakulima hao leo
Kariati akilijaribu moja ya matrekta hayo akiwa na mwakilishi wa wakulima kutoka Kondoa Karoli Lubuva.

NAIBU WAZIRI ELIMU NA MAFUNZO JENISTA MHAGAMA ANENA - KIGOMA

JENISTA MHAGAMA -KIGOMANa Magreth Magosso,Kigoma

Naibu Waziri wa  Elimu  na  Ufundi Jenista Muhagama ashauri Uongozi wa  shule ya Sekondari ya Mwilamvya ifungue kitengo cha ushauri nasaha shuleni hapo, ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa maadili  kwa wanafunzi husika.
 
Kauli hiyo imetokana na risala iliyosomwa jana na Mkuu wa shule Emmanuel  King  katika mahafali ya Darasa la saba na kidato cha Nnne yaliyofanyika  shuleni hapo ambayo ipo katika  kata ya murusi wilayani Kasulu Mkoa wa Kigoma.
 
Akifafanua hilo kwa niaba ya Naibu  husika,Mkaguzi wa shule Kanda magharibi Adriani Mlelwa alisema   utandawazi ni chanzo cha madili kwenda mlama , shida ipo katika mapokeo huku ashauri wafungue kitengo hicho,  ili kudhibiti maadili  na nidhamu kwa wanafunzi.
 
“mawasiliano ni muhimu , wekeni taratibu,kanuni na sheria itasaidia kudhibiti wanafunzi kumiliki simu za mkononi holela,mnaweza mkawa na simu moja ambayo mzazi ataongea na kijana  ” alisema Mlelwa.
Ampongeza mtendaji wa shule Elias Maliyatabu kwa kitendo cha kutumia rasilimali mali na akili katika kuwekeza  elimu mkoani kigoma , ni mtendaji wa kwanza wa hapo mwenye tija ya kufuta ujinga kwa wakazi husika.

Wigo mpana wa kushirikisha  na ushawishi kwa wadau ni chachu ya kuboresha  vitendea kazi  hasa mabara ya kisasa  ni moja ya sifa ya wanafunzi kufuta  alama ya sifuri katika  mtihani wa taifa na kanda  tangu ianzishwe  2005.

Akijibia hilo Mkurugenzi Maliyatabu alisema mafaniko yanatokana na wazazi ambao wanaufahamu  wa tija ya elimu kwa mtoto ,ambapo ni urithi bora wa kushinda adui ujinga na umaskini siku za usoni.
Baadhi ya wanafunzi wahitimu Elimina Segenya na Inocent Batholomeo kwa nyakati tofauti walisema umiliki wa simu kwa wanafunzi chanzo cha kukosa umakini katika masomo.

Waomba wazazi wasiwape simu vijana na kutaka uongozi wa shule uweke utaratibu wa kuweka  watoa huduma ya chakula  zaidi ya mmoja  ili kuboresha uwajibikaji.

Pia Zaidi ya Milioni  Tatu zimetumika katika  ununuzi wa ng`ombe jike moja la maziwa na dume,vitenge doti 10,debe moja la dagaa wa hapa na Lita 20 mafuta ya mawese.

Friday, October 24, 2014

PROF.TIBAIJUKA:MAGONJWA YA MLIPUKO YATEKELEZWE KIMATAIFA


Picha-na-3

Na Anita Jonas-MAELEZO
Umoja wa Mataifa umeshauri  kuchukua  hatua za haraka kwa magongwa ya mlipuko yanayotokea Afrika kama Ebola kwani yanadhiri uchumi wa mataifa husika.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka wakati wa Maadhimisho ya Miaka 69 ya Umoja wa Kimataifa leo Jijini Dar es Salaam.

Prof. Tibaijuka alisema kuwa Umoja wa Mataifa wanatakiwa kuchukua tahadhari ya milipuko ya magonjwa hatarishi na kuyachukulia kama ni magonjwa ya Kidunia kwani yanaathiri mifumo yote ya kimaendeleo.

“Mataifa yaliyoendelea yasingepuuzia mlipuko wa  ugonjwa wa Ebola ulipojitokeza  Afrika  hali  isingekuwa  hatarishi kama ilivyo sasa, hivyo ni rai yangu kwa Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na mataifa husika kuchukua  tahadhari wakati wote ”Alisema Prof. Tibaijuka.

Aidha, Prof. Tibaijuka alisema kuwa kutokana na tatizo la mabadiliko ya tabia nchi kuwa tishio miongoni mwa wengi duniani, wahisani wa maendeleo hawanabudi kusaidia Mataifa mengine ikiwamo utekelezaji wa Mfuko wa Kijani wa Hali ya hewa.

Akizungumzia kuhusu hatua ya Rais Dkt. Jakaya Kikwete kutoa uraia kwa wakimbizi 162,000 kutoka Burundi, Prof. Tibaijuka alisema kuwa Tanzania imeonyesha ulimwengu kuwa suala la mapambano dhidi ya ukimbizi linaweza kufanyiwa kazi na kuwafanya wakimbizi kuishi maisha kama binadamu wengine.

Naye Mratibu muwakilishi wa makazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Bw. Alvaro Rodriguez alisema kuwa shirika hilo kwa kushirikiana na serikali na wadau wengine,  wamepanga kusaidia na kuboresha miundombinu ya kiusalama ili kuendeleza amani Duniani kwani bila amani maendeleo ni vigumu kupatikana.

Pia Bw. Rodriguez aliipongeza Tanzania katika kutekeleza Malengo ya Millenia katika sekta ya afya kwa ambapo asilimia 96 ya vituo vyote vya afya nchini vinatoa huduma ya afya ya uzazi kwa mama na mtoto.

Sherehe hizo zimebebwa na kauli mbiu ya “Leave no One Behind” ikiwa na mlengo wa kuleta maendeleo yenye usawa duniani.

UBORESHAJI WA DAFTARI LA MPIGA KURA KUANZA KATIKATI YA NOVEMBA 2014


IMG_8833
Makamu Mwenyekiti wa  Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC), pia  na Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Hamid   Mahamoud Hamid(kushoto)  akitoa ufafanuzi baada kusoma taarifa kuhusu kuanza kwa shughuli za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dares Salaam kwenye ukumbi wa mikutano wa NEC.Kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi Julias Malaba.
…………………………………………………………..
Na Magreth Kinabo,Maelezo
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) imesema kwamba  zoezi la majaribio ya  Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linatarajia kuanza rasmi katikati mwa mwezi  Novemba mwaka huu.
 
Aidha  NEC imefafanu kwamba zoezi hilo, litafanyika kwa kutumia mfumo mpya wa ‘Biometric Voter Registration’(BVR) katika majimbo matatu ya uchaguzi ambayo ni Kawe katika Manispaa ya Kinondoni, Kilombero, Halimashauri ya Mji wa Kilombero na Mlele, Halimashauri ya Mlele, ambapo vituo vya uandikishaji vimewekwa katika kata zilizomo katika majimbo husika.
 
Hayo yalisemwa  na Makamu Mwenyekiti wa NEC  pia  na Jaji  Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Hamid   Mahamoud  Hamid,wakati  akisoma taarifa kuhusu kuanza kwa shughuli za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura  katika  mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dares Salaam.
 
“Tume tayari imekwishapokea baadhi ya vifaa muhimu vya uandikishaji zikiwemo fomu za unadikishaji, hivyo kinachosubiriwa ni kupokea BVR kits 250 zinazotarajiwa kupokelewa wakati wowote kuanzia leo. Zoezi la Uandikishaji litakapoanza, vituo vitafunguliwa kuanzia saa 2:00 asubuhi na kufungwa saa 12:00 jioni, vyama vya siasa vinaruhusiwa  kuweka mawakala wao katika kituo ili kushuhudia jinsi uandikishaji utakavyokuwa unafanyika,” alisema  Hamid.
 
 Makamu Mwenyekiti huyo alisema baada ya zoezi hilo kukamilika zoezi hilo litaanza katika maeneo mengine.
 
“ Tunatarajia Uboreshaji  wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utafanyika kwa wakati mmoja katika mikoa yote nchini isipokuwa mkoa wa Dares Salaam na Zanzibar.Uandikishaji katika mikao ya Dares Salaam na Zanzibar utafanyika baada ya uandikishaji katika mikoa yote utakapokamilika.Muda wa uandikishaji  utakuwa ni siku saba katika kila kituo,” alisema.
Aliongeza kwamba uandikishaji katika mikoa yote umepangwa kufanyika kuanzia mwanzoni mwa mwezi Januari, mwaka huu hadi katikati ya   Februari mwaka huu, wakati katika mikoa ya Dares Salaam na Zanzibar utafanyika mwishoni mwa mwezi Februari mwaka huu.
 
 Alisema uandikishaji katika mikoa yote utafanyika katika awamu nne kwenye kila halimashauri ili kutoa fursa ya kuhamisha vifaa vya uandikishaji   kutoka eneo moja kwenda eneo lingine.
 
“Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura utahusisha  wapiga kura wote wapya na wa zamani. Wapiga kura wa zamani yaani wale ambao walikuwa wamejiandikisha katika Daftari la Zamani, watatakiwa kwenda katika vituo vya kujiandikisha vilivyoko karibu na maeneo wanayoishi ili kuchukuliwa taarifa zao hasa alama za vidole, picha na saini zao kuiongizwa katika mfumo Biometric Voter Registration na hatimaye watapewa vitambulisho vipya.” Alisisitiza.
 
Alisema wapiga kura ambao watakuwa na kadi zao za kupiga kura za zamani watatakiwa kwenda na kadi zao katika kituo cha kujiandikisha ili kurahisisha zoezi la kuhamisha taarifa zao za awali katika mfumo mpya wa BVR.
 
Aidha alifafanua kwamba  kwa wapiga kura waliopoteza kadi au wale ambao kadi zao zimeharibika watatakiwa kwenta kituoni ili kujiandikisha na kupewa kadi mpya.
 
 Hamid alisema kwa wapiga kura wenye vitambulisho vya taifa Dares Salaam na Zanzibar watakuja na kadi zao ambazo ni taarifa zao zitasomwa na vifaa maalum ili kupunguza muda utakaotumika katika zoezi hilo, pia watapewa kadi mpya ya mpiga kura.
 
 Alisema kwa wapiga kura wanaoishi na ulemavu na wale ambao hawajui kusoma na kuandika wanaruhusiwa kwenda kituoni na mtu mmoja katika familia wanayemuamini ili kusaidia katika uandikishaji.
 
“Uboreshaji huu unahusisha pia kuandikisha wapiga kura wote waliotimiza umri wa miaka 18 au zaidi na wale ambao ifikapo siku ya upigaji  kura ya maoni na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 watakuwa wametimiza umri wa miaka 18. Pia wale wote ambao kwa sababu mbalimbali hawakuwahi kujiandikisha katika Daftari la  Kudumu  la Wapiga Kura katika mazoezi yote uandikishaji yaliyopita,” alisisitiza.
 
Hivyo jumla ya watu wenye umri wa miaka 18 na zaidi wapatao milioni 23.09 wanatarajiwa kujiandikisha.
 
Hamid aliongeza kwamba mpiga kura atakayejiandikisha katika daftari hilo la sasa pekee na kupewa kadi ndiye atakayeruhusiwa kupiga kura.
 
“Wakati wa uandikishaji, kipaumbele kitatolewa  kwa watu wanaoishi na ulemavu, wazee, wagonjwa wakinamama wajawazito na wenye watoto wachanga. Hivyo hawatalazimika kusimama kwenye mstari.
 
Naye Mkurugenzi wa Uchaguzi kutoka  NEC, Julias Malaba alisema tayari kiasi cha fedha cha Sh. bilioni 15 zimeshatolewa kwa ajili ya zoezi hilo.Huku Makamu Mwenyekiti wa NEC  akisema bajeti halisi litafafanuliwa baadae.
 
Kwa upande wake, Sisti  Cariah ambaye ni Mkuu wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na Naibu Katibu NEC, alisema daftari hilo litakamilika  Aprili 14,mwaka huu na litawekwa  wazi   kwa muda wa siku tano katika maeneo husika  ili kumwezesha kila mtu aliyejiandikisha  aende  kukagua na kujiridhisha kwa taarifa zake zimeandikwa  kwa usahihi.
 
 Tume hiyo inatoa wito kwa wananchi wote wenye sifa za kujiandikisha kujitokeza kwa wingi katika vituo vyote vya uandikishaji kwa ajili ya kujiandikisha katika daftari hilo.
Akizungumzia  kuhusu mfumo wa BVR alisema unasaidia kupunguza ujiandikisha mara mbili na kuwa na taarifa sahihi.

UKARABATI NA UPANUZI WA UWANJA WA NDEGE WA MPANDA WAKAMILIKA


??????????????????????????????? Meneja wa Uwanja wa ndege wa Mpanda,  Mkoa wa Katavi Seneti Lyatuu akiwaonesha timu ya ukaguzi wa miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mpanda. Nyuma yake (mwenye suti nyeusi) ni Mhandisi Caroline Mntambo kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndenge Tanzania, Makao Makuu, Dar es Salaam. ??????????????????????????????? Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda  Bw.  Seneti Lyatuu akifafanua jambo wakati timu ya ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango walipotembelea kiwanja hicho. ??????????????????????????????? Timu ya ukaguzi ikitazama barabara ya kutua na kurukia ndege katika uwanja wa ndege wa Mpanda ??????????????????????????????? Barabara ya kutua na kurukia ndege katika uwanja wa ndege wa Mpanda, mkoani Katavi ???????????????????????????????Mhandisi Caroline Mntambo (mwenye suti nyeusi) akifafanua jambo kwa timu ya wakaguzi kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango. Uwanja wa ndege wa Mpanda umekarabatiwa na kupanuliwa hivyo , kuwa  katika hali nzuri kwa matumizi ya ndege zote za binafsi na biashara
PICHA NA JOYCE MKINGA
………………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu, Mpanda
Serikali imekamilisha ukarabati na upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mpanda, mkoa wa Katavi na hivyo kuufanya uwe wa kiwango kizuri tayari kwa kutumika kwa ndege za binafsi na biashara.

Meneja wa Uwanja wa Ndege wa Mpanda, Bw Seneti Lyatuu alisema uwanja huo umeboreshwa na hivyo, unaweza kutumika kutua na kuruka ndege za kiwango cha kati na hata zile ndege kubwa zinaweza kutua kwa dharura.

Aliiambia timu ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kutoa Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango iliyotembelea uwanja huo mwishoni mwa wiki kuwa uwanja huo umeongeza idadi ya wasafiri mara dufu kutokana na ukarabati na upanuzi uliofanyika.

Meneja wa Uwanja huo alisema idadi ya abiria imeongezeka kutoka abiria 285 mwaka 2009 hadi 2,390 mwaka 2013/14.

Bw. Lyatuu alisema kuwa uwanja huo umekarabatiwa na barabara ya kuruka na kutua ndege imerefushwa kwa kiwango cha lami kutoka urefu wa mita 1,500 na upana wa mita 30 hadi kufikia urefu wa mita 1,820 na upana wa mita 30.

Alisema maeneo mengine yaliyokarabatiwa ni pamoja na kujenga uzio na mifereji ya kupitishia maji ya mvua.

“Kwa sasa kiwanja kipo vizuri na ndege za aina zote zinaweza kutua hapa uwanjani hivyo, tunawakaribishwa wadau wote kuutumia uwanja huu” alisema Bw Lyatuu.

Eng. Caroline Mntambo kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Makao Makuu Dar es Salaam alisema kuwa tayari wamealika mashirika ya ndege yanayofanya biashara hapa nchini kuanzisha safari katika uwanja huo. Mashirika hayo ni pamoja na ATC, Precision Air, Fast jet   nk.

Eng Mntambo alisema kwa sasa shirika la ndege la Auric Air tayari limeanzisha safari za kwenda Mpanda ambapo linasafirisha abiria kutoka Dar- Mpanda – Mwanza mara tatu kwa wiki.

Alisema ndege zingine zinazotua uwanjani hapo kwa sasa ni pamoja na za UNHCR, ndege za kukodi na ndege za serikali.

IDADI YA WAJASILIAMALI YAONGEZEKA TABORA

Baadhi ya wakazi wa Tabora mjini wakionekana katika hali ya utafutaji wa riziki.
Na Mwandishi wetu Tabora mjini.
Kumekuwa na dalili za waziwazi kuwa idadi ya wajasiliamali imeendelea kuongezeka Tabora mjini hali inayotokana na kuongezeka kwa watu wanaofanya shughuli mbalimbali za kutafuta riziki zao ikiringanishwa na miaka mitatu iliyopita.

Ushahidi wa kuongezeka kwa makundi ya wajasiliamali ni pale inapodhihirika kuwa watu wengi wanaonekana kufanya shughuli zao binafsi za kuwaongezea kipato huku ikibainika kuwa kumekuwepo mzunguuko wa pesa kila kona na kuwafanya watu kuwa katika hekaheka za mara kwa mara za utafutaji.

Biashara ndogondogo zinaendelea kushamili,huku ikionesha kuwa idadi kubwa ya wanawake wamekuwa wakijishughulisha kuliko idadi ya wanaume.

Ongezeko na huduma za taasisi za kifedha kama mabenki ambazo zimeonesha hali ya kutoa mikopo kwa wajasiliamali na kuwafanya waongeze juhudi katika kujitafutia riziki zao.

Serikali ya mkoa wa Tabora imeacha milango wazi kwa wajasiliamali kuendesha shughuli zao bila kubughudhiwa na mtu yeyote.  


TAJI LA MISS TANZANIA 2014 KUUNDIWA TUME!!!

 Mshindi wa taji la Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu huenda akavuliwa taji hilo kama serikali kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Baraza lake la Sanaa la Taifa ambalo ndio watoaji vibali vya mashindano hayo na kusimamia dhima na maudhui ya shindano hilo pamoja na kusimamia maadili yake itaingilia kati moja kwa moja suala hilo kwa kuunda tume maalum ya kulichunguza na kutafuta ukweli halisi wa umri wa mrembo huyo na kutoa mapendekezo ya ama Sitti avuliwe taji hilo na kuvikwa Mshindi wa pili, Lillian Kamazima (pichani kulia) ama vinginevyo. Kushoto ni Jihhan Dimachk aliyeshika nafasi ya tatu.
 
Shindano la Miss Tanzania 2014 lilifanyika katika ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam Oktoba 11,  na Sitti Mtemvu kuvikwa taji hilo na kuanza utata wa umri wake halisi licha ya kuanika hadharani cheti chake cha kuzaliwa ambacho wadau wa sanaa ya urembo kukitilia shaka na kushindwa kuoanisha na pasi yake ya kusafiria na leseni ya udereva iliyotolewa nchini Marekani. http://mrokim.blogspot.com/2014/10/taji-la-miss-tanzania-2014-kuundiwa-tume.html

KAMATI YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA MAZINGIRA YATEMBELEA ENEO LA TANGANYIKA PAKERS AMBAKO NHC INATEKELEZA MRADI WA NYUMBA WA KAWE CITY

SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFAKaimu Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Felix Maagi akiiongoza Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira wakati ilipotembelea eneo la mradi wa nyumba ambao unatarajiwa kuanza katika uwanja wa kulenga shabaha wa jeshi la wananchi Kunduchi, baada ya makubaliano kati ya jeshi la wananchi na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC). Kamati hiyo ikiongozwa na mwenyekiti wake na jimbo la Kahama Mbunge Mh. James Lembeli na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka ilitembelea eneo hilo ili kujiridhisha na kujionea hali halisi na kupata maelezo ya kina kabla ya kuanza kutekelezwa kwa mradi huo. Kulia ni Mjube wa Kamati hiyo Mh. Hamud Jumaa na Mbunge wa jimbo la Kibaha Vijijini, kulia ni James Lembeli Mbunge wa Kahama na Mwenyekiti wa kamati hiyo.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM) 2Isaack Peter Mkurugenzi wa Ubunifu Shirika la Nyumba la Taifa NHC akielekeza jambo wakati alipokuwa akionyesha eneo hilo kwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka na wajumbe wa kamati hiyo wakati alipotembelea eneo hilo huku Kunduchi. 3Mjumbe wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Mazingira na Maliasili Mh. Hery Shekifu akifafania jambo huku Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mh. James Lembeli wakimsikililiza 4Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mh. James Lembeli akizungumza jambo wakati kamati hiyo ilipotembelea eneo la kulenga shabaha la jeshi Kunduchi, kulia ni Mama Zakhia Megji Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa Shirika la Nyumba NHC na kushoto ni Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka 5Baadhi ya watendaji na maofisa wa Shirika la Nyumba la Taifa NHC wakiwa katika picha ya pamoja kwenye uwanja wa Kulenga Shabaha wa jeshi Kunduchi ambao kwa sasa matumizi yake yanabadilisha na kuwa mradi wa nyumba za Shirika la Nyumba la NHC. 7Baadhi ya wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi , Maliasili na Mazingira wakishuka kwenye gari mara baada ya kuwasili katika eneo la Tanganyika Pakers ambapo mradi wa Kawe City unatarajiwa kuazishwa na shirika hilo la NHC. 8Huu ndiyo uwanja wa Kulenga Shabaha wa jeshi Kunduchi mahali ambapo sasa panaanzishwa mradi wa nyumba za NHC. 9Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka akishuka kwenye gari mara baada ya kuwasili katika eneo la Tanganyika Pakers Kawe jijini Dar es salaam. 10Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira na mbunge wa Kahama Mh. James Lembeli akishuka kwenye gari katika eneo la Tanganyika Pakers mahali ambapo patatekelezwa mradi wa Kawe City unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa NHC. 12Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka akizungumza na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mh. James Lembeli katikati ni mjumbe wa kamati hiyo na Mbunge wa jimbo la Lushoto Mh. Hery Shekifu 13Isaack Peter Mkurugenzi wa Ubunifu Shirika la Nyumba la Taifa NHC akendelea kutoa maelezo kwa kamati hiyo wakati ilipotembelea katika eneo la Tanganyika Pakers Kawe. 14Wajumbe wa kamati hiyo wakipata maelezo kabla ya kuanza ziara yao leo katika makao makuu ya shirika la Nyumba la Taifa NHC Upanga jijini Dar es salaam. 15Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mh. James Lembeli akizungumza wakati kamati hiyo ilipokuwa ikipata maelezo ya awali kabla ya kutembelea maeneo yatakapotekelezwa miradi hiyo mikubwa ya makazi , Kushoto ni Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Mh. Profesa Anna Tibaijuka na kutoka kulia ni Mh. Mary Mwanjelwa mjumbe wa kamati hiyo na mbunge wa viti maalum Mbeya mjini na Mh. Abdulkarim Shah Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo na na Mbunge wa Mafia. 17Kutoka kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Nyumba la NHC Mh. Zakhia Megji, Bw. Felix Maagi Kaimu Mkurugenzi wa NHC na Mbunge wa jimbo la Ubungo na mjumbe wa kamati hiyo Mh. John Mnyika ambaye naonekana akitoa mchango wake wakati wa wajumbe hao walipokuwa wakipata taarifa ya awali..

Thursday, October 23, 2014

PRESIDENT KIKWETE OPENS TANZANIA-CHINA BUSINESS FORUM IN BEIJING


D92A6612President Dr.Jakaya Mrisho Kikwete pose for a group photograph with Tanzania and Chinese delegates who attended the Tanzania and China Business and Investment Forum that was held at Diaoyutai State Guest House in Beijing this morning. President Kikwete who officiated at the opening of the forum, is in working visit in China at the invitation of the Chinese President Xi Jinping.(photo by Freddy Maro)

WAZIRI UMMY MWALIMU ATAKA HALMASHAURI YA KINONDONI KUSIMAMIA SHERIA ZA MAZINGIRA

WAZIRI UMMY MWALIMUMkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty(kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu wakati wa ziara ya kujifunza masuala ya usimamizi wa taka zinazozalishwa katika halmashauri hiyo.
2Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu wakati wa ziara ya kujifunza masuala ya usimamizi wa taka zinazozalishwa katika halmashauri hiyo.Kulia ni wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na watendaji wa halmashauri hiyo.
3Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu, akizungumza na watendaji wa kata za manispaa ya Kinondoni(hawapo pichani) wakati wa ziara hiyo.Kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty.
4Badhi ya watendaji wa kata mbalimbali za manispaa ya Kinondoni wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu, wakati alipotembelea kujifunza masuala ya usimamizi wa taka zinazozalishwa katika halmashauri hiyo.
5Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu (katikati) akiongozwa na Mwenyekiti wa soko la Tandale, Sultan Kiumbo kuingia kwenye ofisi ya soko hilo, wakati alitembelea kujifunza changamoto za mazingira zinazolikabili soko hilo.
6Mwenyekiti wa soko la Tandale, Sultan Kiumbo, akmueleza jambo Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu, wakati alipotembelea soko hilo kujifunza changamoto za mazingira.
7 Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu, akisalimiana na mama lishe katika soko la Tandale jijini Dar es Salaam, wakati alipotembelea soko hilo kujifunza changamoto za mazingira.
8Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu, akizugumza na muuza mbogamboga kujua jinis anavyoshughulikia taka anazozalisha kwenye soko la Tandale jijini Dar es Salaam, wakati alipotembelea soko hilo kujifunza changamoto za mazingira.
9Mwenyekiti wa soko la Tandale, Sultan Kiumbo, akimuonesha Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Ummy Mwalimu, mabaki ya matunda yalitupwa, wakati alipotembelea soko hilo kujifunza changamoto za mazingira.
Picha zote na Hussein Makame-MAELEZO

MKE WA RAIS MAMA SALMA KIKWETE NA MATUKIO YA PICHA KATIKA ZIARA YA RAIS DR. JAKAYA KIKWETE NCHINI CHINA

1Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea ua kutoka kwa mfanyakazi wa Hoteli ya Diaoyutai iliyoko Beijing mara baada ya kuwasili hotelini hapo. Mama Salma ameambatana na mumewe Rais Dkt. Jakaya Kikwete ambaye amewasili nchini China tarehe 21.10.2014 kwa ziara ya kiserikali. 2Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiwapungia wafanyakazi wa Hoteli ya Diaoyutai ya mjini Beijing mara baada ya kuwasili nchini China kwa ziara ya kikazi tarehe 21.10.2014. 3Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwa pamoja na Bwana Yang Hua, Mmoja wa viongozi wakuu wa China National Offshore Oil Corporation (CNOOC), wakisikiliza kwa makini maelezo yaliyokuwa yakitolewa na Mwenyekiti wa Shirika hilo Bwana Wang Yilin kwa Rais Dkt. Jakaya Kikwete alipotembelea makao makuu ya Shirika hilo yaliyoko Beijing nchini China tarehe 22.10.2014. Shirika hilo hujishughulisha na utafiti wa mafuta na gesi baharini, uchimbaji na uuzaji wa maliasili hizo. 4Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mwenyekiti wa China National Offshore Oil Corporation Bwana Wang Yilin wakizindua rasmi mtambo mpya wa utafutaji wa mafuta na gesi baharini, Uzinduzi huo ulifanyika kwenye Makao Makuu ya Shirika hilo huko Beijing tarehe 22.10.2014. 5Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiongoza ujumbe wa Tanzania unaozuru nchini China wakiangalia vifaa mbalimbali vinavyotumiwa na Shirika la  CNOOC la China katika kazi ya utafutaji wa mafuta na gesi baharini wakati walipotembelea Makao Makuu ya Shirika hilo huko Beijing tarehe 22.10.2014. 6Rais Dkt. Jakaya Kikwete akishirikiana na Mkewe Mama Salma Kikwete na Professa Li Songshan (kushoto kwa Rais Kikwete), Mwanzilishi wa Kijiji cha Sanaa cha Afrika kuondoa kitambaa ikiwa ni ishara ya kufungua rasmi kijiji hicho kilichopo katika wilaya ya Songzhuang nchini China tarehe 22.10.2014. 7 8 Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiangalia baadhi ya ngoma za asili ya Afrika zilizokuwa zikipingwa na vijana wa kichina mara baada ya ufunguzi rasmi wa kituo cha sanaa za Afrika huko Songzhuang tarehe 22.10.2014. 9Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiandika kumbukumbu yake katika kitambaa maalum mara baada ya kuzindua rasmi Kijiji cha sanaa za Afrika. Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anaonekana wa kwanza kushoto akifuatiwa na Professa Li Singshan. Kulia kwa Rais Kikwete ni Dkt. Han Rong, Mke wa Professa Li na Mwanzilishi mwenza wa Kijiji hicho na wa kwanza kushoto ni Bwana Joseph Kahama. 10Rais Dkt. Jakaya Kikwete akiandika kumbukumbu yake katika kitambaa maalum mara baada ya kuzindua rasmi Kijiji cha sanaa za Afrika. Mke wa Rais Mama Salma Kikwete anaonekana wa kwanza kushoto akifuatiwa na Professa Li Singshan. Kulia kwa Rais Kikwete ni Dkt. Han Rong, Mke wa Professa Li na Mwanzilishi mwenza wa Kijiji hicho na wa kwanza kushoto ni Bwana Joseph Kahama. 11Waanzilishi wa Kijiji cha Sanaa za Afrika Professa Li Songshan na Mke wake Dkt. Han Rong wakimkabidhi zawadi ya picha Rais Dkt. Jakaya Kikwete na Mke wake mara baada ya ufunguzi rasmi wa kijiji hicho tarehe 22.10.2014.
PICHA NA JOHN  LUKUWI.