Hatimaye Mhe Freeman Aikael Mbowe
Amechaguliwa Tena kuwa mwenyekiti wa Chadema Taifa kwa kupata kura 789
sawa na asilimia 97.3 ya kura zote. Aliyeshinda nafasi ya Makamu
mwenyekiti Bara ni Profesa Abdallah Safari kwa kupata kura 775 sawa a
asillimia 95 na nafasi ya Makamu mwenyekiti Zanzibar ameshinda Mh Saidi
Issa Mohamedi kwa kupata kura 645 sawa na asilimia 79.
Monday, September 15, 2014
KINANA ASONONESHWA NA MIKOROSHO YA WAKULIMA ILIVYOKAUKA KWA UGONJWA USIOJULIKANA WILAYANI MKURANGA, AAHIDI KUSAIDIA WAKULIMA WAFIDIWE
Katibu
Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akionyeshwa mikorosho iliyokauka katika
mashamba ya wakulima wa zao hilo katika kijiji cha Magawa katika wilaya
ya Mkuranga mkoa wa Pwani, alipokagua adhari za mikorosho hiyo Sepetemba
14, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama
na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua
katika mkoa huo. Baada ya kushuhudia madhara hayo Kinana amesononeshwa
na kuahidi kulifikisha tatizo hilo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili
serikali itazame njia ya kuwafidia wakulima ili kunusuru hali za maisha
yao.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akikagua mikorosho iliyokauka
katika mashamba ya wakulima wa zao hilo katika kijiji cha Magawa katika
wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani, alipokagua adhari za mikorosho hiyo
Sepetemba 14, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani
ya Chama na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za
kuzitatua katika mkoa huo. Baada ya kushuhudia madhara hayo Kinana
amesononeshwa na kuahidi kulifikisha tatizo hilo kwa Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda ili serikali itazame njia ya kuwafidia wakulima ili
kunusuru hali za maisha yao.Kinana akisalimiana na wananchi alipowasili katika wilaya ya Rufiji, Septemba 14, 2014, wakati akiendelea na ziara yake katika mkoa wa Pwani. Kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambaye ameambatana naye katika ziara hiyo.
Kinana akimsalimia Mbunge wa rufiji alipowasilikatika wilaya hiyo
Kinana akimsalimia Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurudin Babu alipowasili katika wilaya hiyo, leo Septemba 14, 2014.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimsalimia Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurudin Babu alipowasilina Kinana katika wilaya hiyo.
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Rufiji wakiwakwenye kikao chao na Kinana, wilayani humo leo, Septemba 14, 2014.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Rufiji, leo Septemba 14,2014.
Katibu Mkuu wa CCM, Kinana, akifungua Ofisi ya mafundi seremala Mbuyuni wilayani Rufiji, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo.
Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia Wananchi katika mkutano wa Kinana uliofanyika katika mji mdogo wa Utete, wilayani Rufiji, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo.Nape amewataka wananchi kuendelea kuwa na Imani na CCM akisema ndicho chama chenye uwezo wa kutatua kero zao na ndicho chenye uhakika wa kuwa nao kwa muda mrefu kwa sababu kinaendelea kuimarika wakati vile vya upinzani vikizidi kufa.
Katibu Mkuu wa NEC, Kinana akihutubia Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji mdogo wa Utete, wilayani Rufiji, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo.Kinana amesema, CCM itaendelea kusikiliza kero za wananchi na kushirikiana nao kupata njia za kuzitatua katika njia iliyo sahihi.
Wanachama wapya wa CCM wakila kiapo baada ya kukabidhiwa kadi zao za uanachama na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, katika mkutanowa hadhara uliofanyika leo, Septemba 14, 2014 katika mji mdogo wa Utete, wilayani Rufiji mkoa wa Pwani. Jumla ya wanachama wapya 180 walipewa kadi. Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog
JENGO LA GHOROFA MOJA LINAPANGISHWA MKOANI DODOMA, LIPO KATIKATI YA MJI.KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA 0787 970 072
Muonekano wa Jengo hilo ambalo lipo Katikati ya Mji wa Dodoma, lenye Ghorofa moja linakodishwa tunapenda kuwakaribisha Mtu binafsi, makampuni, shirika au taasisi ambayo inataka kufungua ofisi au imekuwa ikihitaji jengo kwaajili ya Ofisi sasa Jengo Zuri tu lenye huduma zote muhimu lipo na Nafasi pia Zipo Karibu Kwa Mawasiliano Zaidi
Piga namba hii 0787 970 072
Korido Kama inavyoonekana
Vyumba vyake ni Vikubwa na Unaweza kufanya Ofisi kama inavyoonekana kwenye picha.
Sehemu ya Kupandia Kwenda kwenye ghorofa ya Kwanza
NI Jengo la Ghorofa 1 ambalo hapo awali lilikuwa ni hotel lakini kwasasa linapagishwa kwaajili ya Makampuni, Maofisi na Mashirika mbalimbali au Watu binafsi ambao wanahitaji Ofisi Mkoani Dodoma, Jengo Hilo linapatikana Mkoani Dodoma na Lipo Katikakati ya Mjini Kabisa huku likiwa na Huduma Zote Muhimu za Kijamii.
Kama Kampuni, Shirika, au Taasisi inataka kupanga au Mtu Binafsi basi asisite kuwasiliana na Sisi kupitia namba hii 0787 970 072
NDUGU ABDULRAHMAN KINANA KATIBU MKUU WA CCM AENDELEA NA ZIARA RUFIJI
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Juma
Abeid Diwani wa Kata ya Magawa wilayani Mkuranga wakati alipotembelea
shamba la Mikorosho lenye hekari 1000 ambapo mikorosho inayokaribia elfu
20 imeharibika vibaya baada ya kupata ugonjwa unaonyausha mikorosho
hiyo , Diwani huyo amesema wananchi wa kata hiyo wako katika hali mbaya
kwakuwa zaidi ya miaka minne sasa hawajavuna chochote na maisha yao
yanazidi kuwa mabaya, Katibu Mkuu Kinana yuko katika ziara ya mikoa ya
Pwani, Tanga na Iringa akikagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM
ya mwaka 2010 na kuhimiza wananchi kushiriki katika shughuli za
maendeleo, Katika ziara hiyo Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa
NEC Siasa, Itikadi na Uenezi.PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-
Juma Abeid Diwani wa Kata ya Magawa wilayani Mkuranga akimuongoza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati akikagua shamba hilo leo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyeshwa na Mwenyekiti wa CCM
Mkoa wa Pwani Mwishehe Mlao jinsi mikorosho hiyo ilivyoharibika kutokana
na kukumbwa na ugonjwa huo, kushoto ni Juma Abeid Diwani wa kata ya
Mgama
Juma Abeid Diwani wa kata ya Mgama akitoa maelezo yake mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani
Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa, Itikadi na Uenezi
akisalimiana na baadhi ya watendaji wa Wilaya ya Rufiji wakati Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipowasili katika mji wa Ikwiriri
kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurdin Babu.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Mh. Nurdin Babu.
Wajumbe wa Harmashauri kuu ya Wilaya wakiwa katika kikao cha ndani kilichofanyika kwenye ukumbi wa FDC mjini Ikwiriri
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Wajumbe wa Harmashauri kuu ya Wilaya.kilichofanyika kwenye ukumbi wa FDC mjini Ikwiriri
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi kwenye ofisi ya mafundi seremala mjini Utete.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
akipokea zawadi ya viti kutoka kwa kikundi cha vijana Maseremala mjini
Utete kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa , Itikadi na Uenezi na
wa pili kutoka kulia ni Mbunge wa jimbo la Rufiji na Waziri wa Afya na
Ustawi wa jamii Mh. Dr. Seif Rashid.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi Ofisi ya CCM wilaya ya Utete Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua jengo la ofisi ya CCM wilaya ya Utete
Mmoja
wa wapiga ngoma wa kikundi cha ngoma cha mjini Utete akipiga ngoma huku
akiwa amebeba mtoto wake mdogo na mtoto wake mwingine akiwa amekaa
pembeni.
Mkuu wa wilaya ya Rufiji Mh. Nurdin Babu akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Utete leo
Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa , Itikadi na Uenezi akiwahutubia wananchi wa Utete katika mkutano uliofanyika leo mjini humo
Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa , Itikadi na Uenezi akimuwekea
kipaza sauti mmoja wa wazee waliofika kwenye mkutano ili kumsikiliza
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na kuuliza maswali yake
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wana Utete wakati wa mkutano wa hadhara uliofnyika mjini Utete.
Baadhi ya wanachama wapya wa Chama cha Mapinduzi wakila kiapo mara baada ya kupokea kadi zao za uanachama
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa , Itikadi na Uenezi wakinyanyua mikono yao juu wakati wakila kiapo cha utii kwa chama,
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Dr. Onesmo Mambosho Mganga Mfawidhiwa wa kituo cha afya cha Nyamwage.
Sunday, September 14, 2014
WASHINDI TUZO ZA HABARI ZA TANAPA 2013 WAENDELEA KUJIFUNZA MAENEO YA UTALII AFRIKA KUSINI
Mwanahabari
Vedasto Msungu wa ITV (kushoto) na David Rwenyagira (Radio 5) walikuwa
miongoni mwa wanahabari waliofika nje ya Jengo la Mahakama Kuu ya
Pretoria ambapo ilikuwa siku muhimu ya utoaji hukumu kwa mwanariadha
Oscar Pistorius aliyeshitakiwa kwa makosa ya kumuua mpenzi wake kwa
silaha. Unayoyaona hapo nyuma ni magari maalum ya urushaji tukio hilo
moja kwa moja katika vyombo mbalimbali vya habari duniani(OB Van) na
mahema meupe ni Kambi iliyopigwa na wanahabari hao kwa ajili ya
kufuatilia tukio hilo muhimu.
Wanahabari
Vedasto Msungu na David Rwenyagira walipata nafasi ya kumhoji raia huyu
wa Afrika Kusini juu ya maoni yake kwa hukumu iliyotarajiwa kutolewa
Washindi
wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 waliweza kufika hadi katika Hifadhi ya
Taifa ya Pilanesberg ili kujionea wanyama mbalimbali. Kutoka Kushoto ni
Mtanzania Peter Masika anayeishi Johannesburg, Vedasto Msungu (ITV),
Pascal Shelutete(Meneja Mawasiliano TANAPA) na Gerald Kitabu wa The
Guardian
Wanyama aina ya Nyumbu wanaopatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Pilanesberg
Washindi wa Tuzo za TANAPA 2013 waliweza pia kufika katika Mji wa Sun City kama wanavyoonekana hapa
KINANA ZIARA YA MKURANGA
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Kata ya Kimanzichana leo wakati alipoanza Ziara yake ya mikoa ya Pwani ,Tanga na Iringa Ikiwa ni kuimarisha Chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2010 huku akihimiza wananchi kushiriki katika shughuli za kujiletea maendeleo katika maeneo yao, Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi na leo amefanya shughuli mbalimbali katika ziara hiyo. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MKURANGA -PWANI) Mbunge wa jimbo la Mkuruanga na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Adama Malima akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mkuranga wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo leo. Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi akizungumza na wananchi wa kata ya Kimanzichana wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapo. Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Mh. Mercy Silla akwahutubia wananchi wa kata ya Kimanzichana kwenye mkutano wa hadhara. Baadhi ya wananchi wakipunga mikono kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Kimanzichana. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kuwasili katika eneo la mkutano mjini Kimanzichana, kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkuranga. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika shughuli ya kufyatua matofali pamoja na wanakikundi wa kikundi cha Mkuranga Youth Development ambapo amekipa kikundi hicho mashine 2 ili kuongeza uwezo wa kikundi hicho. Mmoja wa wanakikundi wa kikundi cha Mkuranga Youth Development Bi Faraja Msani akionyesha jinsi wanavhoshiriki shughuli za kujiletea maendeleo. Wananchi wakishiriki kukusanya matofali katika shule ya sekondari ya Mwarusembe. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika shughuli ya ujenzi wa mafarasa katika shule ya sekondari ya Mwarusembe huku wananchi wakiendelea na kazi ya kukusanya matofali. Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi akishiriki ujenzi wa madarasa katika shule ya sekondari ya Mwarusembe. Baadhi ya wakuu wa wilaya za mkoa wa Pwani kutoka Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Mh. Ahmed Kipozi Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi akionyesha ripoti mbalimbali za utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM wakati wa kutano wa ndani na wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wa Pwani. Mmoja wa viongozi wa CCM wilaya ya Mkuranga Bi Agricola akiwa katika mkutano huo