Pages

KAPIPI TV

Monday, September 15, 2014

MH FREEMAN AIKAEL MBOWE ASHINDA NAFASI YA MWENYEKITI CHADEMA TAIFA

Hatimaye Mhe Freeman Aikael Mbowe Amechaguliwa Tena kuwa mwenyekiti wa Chadema Taifa kwa kupata kura 789 sawa na asilimia 97.3 ya kura zote. Aliyeshinda nafasi ya Makamu mwenyekiti Bara ni Profesa Abdallah Safari kwa kupata kura 775 sawa a asillimia 95 na nafasi ya Makamu mwenyekiti Zanzibar ameshinda Mh Saidi Issa Mohamedi kwa kupata kura 645 sawa na asilimia 79.

KINANA ASONONESHWA NA MIKOROSHO YA WAKULIMA ILIVYOKAUKA KWA UGONJWA USIOJULIKANA WILAYANI MKURANGA, AAHIDI KUSAIDIA WAKULIMA WAFIDIWE

Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akionyeshwa mikorosho iliyokauka katika mashamba ya wakulima wa zao hilo katika kijiji cha Magawa katika wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani, alipokagua adhari za mikorosho hiyo Sepetemba 14, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama  na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo. Baada ya kushuhudia madhara hayo Kinana amesononeshwa na kuahidi kulifikisha tatizo hilo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili serikali itazame njia ya kuwafidia wakulima ili kunusuru hali za maisha yao.

 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akikagua mikorosho iliyokauka katika mashamba ya wakulima wa zao hilo katika kijiji cha Magawa katika wilaya ya Mkuranga mkoa wa Pwani, alipokagua adhari za mikorosho hiyo Sepetemba 14, 2014, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama  na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo. Baada ya kushuhudia madhara hayo Kinana amesononeshwa na kuahidi kulifikisha tatizo hilo kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ili serikali itazame njia ya kuwafidia wakulima ili kunusuru hali za maisha yao.
 Kinana akisalimiana na wananchi alipowasili katika wilaya ya Rufiji, Septemba 14, 2014, wakati akiendelea na ziara yake katika mkoa wa Pwani. Kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambaye ameambatana naye katika ziara hiyo.
 Kinana akimsalimia Mbunge wa rufiji alipowasilikatika wilaya hiyo
 Kinana akimsalimia Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurudin Babu alipowasili katika wilaya hiyo, leo Septemba 14, 2014.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akimsalimia Mkuu wa Wilaya ya Rufiji Nurudin Babu alipowasilina Kinana katika wilaya hiyo.
 Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Rufiji wakiwakwenye kikao chao na Kinana, wilayani humo leo, Septemba 14, 2014.
 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Rufiji, leo Septemba 14,2014.
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana, akifungua Ofisi ya mafundi seremala Mbuyuni wilayani Rufiji, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama  na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia Wananchi katika mkutano wa Kinana uliofanyika katika mji mdogo wa Utete, wilayani Rufiji, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama  na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo.Nape amewataka wananchi kuendelea kuwa na Imani na CCM akisema ndicho chama chenye uwezo wa kutatua kero zao na ndicho chenye uhakika wa kuwa nao kwa muda mrefu kwa sababu kinaendelea kuimarika wakati vile vya upinzani vikizidi kufa.
  Katibu Mkuu wa NEC, Kinana akihutubia Wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji mdogo wa Utete, wilayani Rufiji, akiwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya Chama  na kusikiliza kero za wananchi na kujadiliana nao njia za kuzitatua katika mkoa huo.Kinana amesema, CCM itaendelea kusikiliza kero za wananchi na kushirikiana nao kupata njia za kuzitatua katika njia iliyo sahihi.
Wanachama wapya wa CCM wakila kiapo baada ya kukabidhiwa kadi zao za uanachama na Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana, katika mkutanowa hadhara uliofanyika leo, Septemba 14, 2014 katika mji mdogo wa Utete, wilayani Rufiji mkoa wa Pwani. Jumla ya wanachama wapya 180 walipewa kadi. Picha zote na Bashir Nkoromo-theNkoromo Blog

JENGO LA GHOROFA MOJA LINAPANGISHWA MKOANI DODOMA, LIPO KATIKATI YA MJI.KWA MAWASILIANO ZAIDI PIGA 0787 970 072

Muonekano wa Jengo hilo ambalo lipo Katikati ya Mji wa Dodoma, lenye Ghorofa moja linakodishwa tunapenda kuwakaribisha Mtu binafsi, makampuni, shirika au taasisi ambayo inataka kufungua ofisi au imekuwa ikihitaji jengo kwaajili ya Ofisi sasa Jengo Zuri tu lenye huduma zote muhimu lipo na Nafasi pia Zipo Karibu Kwa Mawasiliano Zaidi 
Piga namba hii 0787 970 072
 Korido Kama inavyoonekana 
 Vyumba vyake ni Vikubwa na Unaweza kufanya Ofisi kama inavyoonekana kwenye picha.
 Sehemu ya Kupandia Kwenda kwenye ghorofa ya Kwanza
NI Jengo la Ghorofa 1 ambalo hapo awali lilikuwa ni hotel lakini kwasasa linapagishwa kwaajili ya Makampuni, Maofisi na Mashirika mbalimbali au Watu binafsi ambao wanahitaji Ofisi Mkoani Dodoma, Jengo Hilo linapatikana Mkoani Dodoma na Lipo Katikakati ya Mjini Kabisa huku likiwa na Huduma Zote Muhimu za Kijamii.
Kama Kampuni, Shirika, au Taasisi inataka kupanga au Mtu Binafsi basi asisite kuwasiliana na Sisi kupitia namba hii 0787 970 072

NDUGU ABDULRAHMAN KINANA KATIBU MKUU WA CCM AENDELEA NA ZIARA RUFIJI

Sunday, September 14, 2014

WASHINDI TUZO ZA HABARI ZA TANAPA 2013 WAENDELEA KUJIFUNZA MAENEO YA UTALII AFRIKA KUSINI

1Mwanahabari Vedasto Msungu wa ITV (kushoto) na David Rwenyagira (Radio 5) walikuwa miongoni mwa wanahabari waliofika nje ya Jengo la Mahakama Kuu ya Pretoria ambapo ilikuwa siku muhimu ya utoaji hukumu kwa mwanariadha Oscar Pistorius aliyeshitakiwa kwa makosa ya kumuua mpenzi wake kwa silaha. Unayoyaona hapo nyuma ni magari maalum ya urushaji tukio hilo moja kwa moja katika vyombo mbalimbali vya habari duniani(OB Van) na mahema meupe ni Kambi iliyopigwa na wanahabari hao kwa ajili ya kufuatilia tukio hilo muhimu.
2Wanahabari Vedasto Msungu na David Rwenyagira walipata nafasi ya kumhoji raia huyu wa Afrika Kusini juu ya maoni yake kwa hukumu iliyotarajiwa kutolewa 3Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 waliweza kufika hadi katika Hifadhi ya Taifa ya Pilanesberg ili kujionea wanyama mbalimbali. Kutoka Kushoto ni Mtanzania Peter Masika anayeishi Johannesburg, Vedasto Msungu (ITV), Pascal Shelutete(Meneja Mawasiliano TANAPA) na Gerald Kitabu wa The Guardian 4Wanyama aina ya Nyumbu wanaopatikana katika Hifadhi ya Taifa ya Pilanesberg 5Washindi wa Tuzo za TANAPA 2013 waliweza pia kufika katika Mji wa Sun City kama wanavyoonekana hapa

KINANA ZIARA YA MKURANGA

1Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Kata ya Kimanzichana leo wakati alipoanza Ziara yake ya mikoa ya Pwani ,Tanga na Iringa Ikiwa ni kuimarisha Chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Mwaka 2010 huku akihimiza wananchi kushiriki katika shughuli za kujiletea maendeleo katika maeneo yao, Katibu Mkuu Abdulrahman Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi na leo amefanya shughuli mbalimbali katika ziara hiyo. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MKURANGA -PWANI) 2Mbunge wa jimbo la Mkuruanga na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Adama Malima akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mkuranga wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo leo. 3Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi akizungumza na wananchi wa kata ya Kimanzichana wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapo. 4Mkuu wa wilaya ya Mkuranga Mh. Mercy Silla akwahutubia wananchi wa kata ya Kimanzichana kwenye mkutano wa hadhara. 5Baadhi ya wananchi wakipunga mikono kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Kimanzichana. 6Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwapungia mkono wananchi mara baada ya kuwasili katika eneo la mkutano mjini Kimanzichana, kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkuranga. 8Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika shughuli ya kufyatua matofali pamoja na wanakikundi wa kikundi cha Mkuranga Youth Development ambapo amekipa kikundi hicho mashine 2 ili kuongeza uwezo wa kikundi hicho. 9Mmoja wa wanakikundi wa kikundi cha Mkuranga Youth Development Bi Faraja Msani akionyesha jinsi wanavhoshiriki shughuli za kujiletea maendeleo. 10Wananchi wakishiriki kukusanya matofali katika shule ya sekondari ya Mwarusembe. 11 12Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika shughuli ya ujenzi wa mafarasa katika shule ya sekondari ya Mwarusembe huku wananchi wakiendelea na kazi ya kukusanya matofali. 13Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi akishiriki ujenzi wa madarasa katika shule ya sekondari ya Mwarusembe. 15Baadhi ya wakuu wa wilaya za mkoa wa Pwani kutoka Katikati ni Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Mh. Ahmed Kipozi 16Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi akionyesha ripoti mbalimbali za utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM wakati wa kutano wa ndani na wajumbe wa kamati ya siasa ya mkoa wa Pwani. 17Mmoja wa viongozi wa CCM wilaya ya Mkuranga Bi Agricola akiwa katika mkutano huo