Tuesday, May 28, 2013
TATHMINI YA MIKUTANO YA CHADEMA NA CCM MKOANI TABORA...!!!!
Monday, May 27, 2013
KATIBU MKUU WA CCM ABDULRAHMAN KINANA AWASILI IRINGA KWA ZIARA YA SIKU SABA

Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi,
Nape Nnauye wakisalimia baadhi ya viongozi, baada ya kuwasili Uwanja wa
Ndege wa Iringa asubuhi hii, kwa ajili ya kuanza ziara ya siku saba,
mkoani Njombe. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Joyce
Msambatavangu

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa na viongozi wa mkoa wa Iringa. Nyuma ni Nape Nape naye akiwa na wenyeji

Kinana akisaini kitabu cha wageni Uwanja wa Ndege wa Iringa baada ya kuwasili uwanjani hapo asubuhi hii. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa, Joyce Msavatavangu
PICHA NA:BASHIR NKOROMO
KIKONGWE ANUSURIKA KUUAWA KWA KUTUHUMIWA MCHAWI -TABORA MWANZAROAD
OMBAOMBA ANAYEDAI HANA MKONO MMOJA APATA KIPIGO!!!
"Amefanya utapeli kwa muda mrefu,watu wamemgundua na kumuaibisha vibaya"
Omba omba tapeli anayejifanya hana mikono akikamatwa na wananchi baada ya kukimbia
Hapa akibanwa kuonyesha mikono yake yote miwili
Wananchi eneo la Miyomboni wakiwa wamembana omba omba huyu tapeli kuonyesha mikono yake yote
'' Huwa unasema wewe ni mlemavu huna mkono mmoja hii nini ....nyosha juu watu waone utapeli wako"
Hapa ni kipigo kikiendelea
Tapeli huyo akitaka kujinasua kutoka mikono ya wananchi wenye hasira kali
Hapa baada ya kupata upenyo akivaa nguo zake
Hapa akiwa ameachiwa na kuanza kutimua mbio
Baada ya kuchezea kichapo tapeli huyo sasa anajaribu kuficha aibu
OMBA OMBA ALIYEIGIZA MLEMAVU WA MIGUU NA MIKONO AKIWA KATIKA KAZI ZAKE ZA KUOMBAOMBA
Huyu ni omba omba anayeigiza kutokuwa
na mkono mmoja na mguu akiwa ameka eneo la M.R akisubiri kuomba
chochote kutoka kwa wapita njia leo
Hapa akisubiri msaada kutoka kwa wasamaria wema leo
Hapa akitimua mbio kukwepa kamera ya mtandao huu leo
AMA Kweli mwisho wa utapeli ni aibu
kubwa na wahenga walinena kuwa ukistaajabu ya mussa utayaona ya
filauni leo kwa wakazi wa Miyomboni mjini Iringa wamepata kushuhudia
kituko cha mwaka baada ya watu waliochoka kuvumilia vitendo vya
kitapeli vinavyofanywa mzee mmoha ambae amekuwa akiigiza ni mlemavu
asiye na mguu mmoja na mkono mmoja.
Tapeli huyo mbali ya kuumbuliwa kwa
kutakiwa kuonyesha miguu yake yote pamoja na mikono yake yote
bado amepata kuchezea kichapo kiasi cha kunusurika kuuwawa na
wananchi hao wenye hasira kali.
Tukio la mzee huyo kubainika kama ni tapeli kwa mara ya kwanza mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com na www.matukiodaima.com ndio ulipata kufichua siri hiyo ya omba omba huyo kuwa si omba omba kutokana na kumnasa akijiweka mfano wa mlemavu .
Kutokana na kufichuliwa kwa siri hiyo
ya kujiigiza kuwa ni omba omba mlemavu wananchi wamekuwa wakimtimua
kila kona anayokaa tapeli huyo na kumtimua mbio kabla ya leo wananchi
hao kuamua kumkimbiza kutoka eneo la Hazina Ndogo hadi miyomboni na
kuanza kumpa kichapo hadi alipoamua kuonyesha viungo vyote kuwa si
mlemavu
Tapeli huyo mbali ya kujifanya ni
mlemavu wa viungo wakati mwingine huwa anajifanya ni mtu asiyeongea
(bubu) asiye na viungo kama mikono na miguu ila wakati mwingine
akijifanya ni hana mguu mmoja na kuwaomba watu fedha za matibabu .
Hata hivyo baada ya mmoja kati ya
wananchi kufika eneo hilo alionyesha kufichua mbinu hiyo chafu ya
mzee huyo kujifanya ni mlemavu wakati asubuhi alikutana maeneo akiwa
mzima wa afya njema na katika kumhoji zaidi ndipo kamera ya mtandao
huu ilipoamua kufanya kazi yake ya kunasa kituko hicho na ndipo
mzee huyo alipoanza kuongea kwa sauti vizuri tofauti na alivyokuwa
akijifanya kuwa hawezi kuongea kabisa (bubu)
Wakati mabishano yakiendelea eneo hilo
ghafla mzee huyo alisimama kwa miguu yake yote miwili pamoja na
awali kujifanya ni mlemavu asiye na mguu mmoja ila baada ya watu
kutaka apigwe picha ndipo mzee huyo alipoanza kutimua mbio huku
ulemavu aliokuwa nao akiusahau hapo kutokana na kichapo alichokipata
na kuumizwa vibaya usoni .
Hata hivyo inasemekana mzee huyo
amekuwa akiadhibuwa katika maeneo mbali mbali kutokana na mbinu yake
ya kufuru anayoifanya kuwa ni mlemavu wakati si mlemavu na kuwa ni
heri kuomba kama mtu mwenye matatizo ya kiuchumi kuliko kuwaigiza
walemavu na kuwa iwapo atarudia na kukutwa akifanya hivyo watamvunja
kweli mkono ili kuwa mlemavu walisema wananchi hao ambao hata hivyo
mtandao huu uliwaomba kufanya hivyo .
Aidha anadaiwa chanzo cha kichapo
cha leo kwa mzee huyo tapeli ni mmoja kati ya mpenzi wake ambae
alikuwa amemsusa na kuhamia kwa mpenzi mwingine kuueleza umma kuwa
huyo ni tapeli na yeye ni mpenzi wake ambae anamtambua kuwa na miguu
yote,mikono na si bubu kama anavyoigiza jambo lililopelekea wananchi
kufanya udadisi .
Kabla kufukuzwa na kuchezea kichapo
tapeli huyo alifukuzwa eneo ambalo alikuwa amekaa barabara eneo la
Santona na kutoka kuondoka haraka na mmoja kati ya vijana wanaofanya
kazi ya kusafisha na kushona viatu na kupuuza na ndipo mtiti ulipoanza.
Baadhi ya wananchi wameuomba uongozi
wa Manispaa ya Iringa kuwabana omba omba hao ambao wamekuwa
wakidanganya watu kuwa wao ni walemavu kumbe ni wazima na kutaka
kuwepo kwa utaratibu maalum wa watu kuomba misaada.
MAAFISA WA JESHI LA MAGEREZA KUPATIWA MAFUNZO

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Kamishna Jenerali Evaristus Shikongo akiijaribu moja ya silaha inayotumika kwa ajili ya kutuliza ghasia wakati wowote inapotokea ndani na nje ya gereza

Askari wa Kikosi Maalum cha Kutuliza Ghasia Magerezani, wakimuonesha mbinu za kupambana na adui pasipo kutumia silaha Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia,

Mkuu wa Chuo cha Maafisa Magereza Ukonga, ACP Mbaraka Semwanza akitoa taarifa fupi ya chuo hicho kwa Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Kamishna Jenerali Evaristus Shikongo (katikati). Kushoto aliyekaa ni Kamishna wa Sheria na Utawala wa Jeshi la Magereza, Dk Juma Malewa, kulia ni Kamishna wa Fedha na Utawala, Gaston Sanga, anayefuata ni Kamishna wa Rasilimali Watu, Fedha na Utawala wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Clementine Feris. Picha na Felix Mwagara.

Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, Kamishna Jenerali John Minja (kushoto) na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini Namibia, Kamishna Jenerali Evaristus Shikongo wakionyesha taarifa ya makubaliano waliyosaini.
Sunday, May 26, 2013
MKUTANO WA CCM TABORA,CHADEMA WACHEZEA KICHAPO,KEJELI NA ZOMEAZOMEA VYATAWALA!!
![]() |
| Katibu wa CCM mkoa wa Tabora Bw.Idd Ame akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara ambapo katibu huyo alikuwa akinadi Sera za CCM. |
![]() |
| Mmoja kati ya makada wa CCM wilaya ya Tabora mjini alikuwa akisikiliza kwa makini hotuba za baadhi ya viongozi wa CCM katika mkutano huo wa hadhara. |
![]() |
| Mjumbe wa NEC Bw.John Mchele naye alipata fursa ya kuzungumza na wananchi ambapo aliwataka kutokihama CCM kutokana na baadhi ya kauli za wanasiasa wanao kikejeli na kukichafua chama hicho. |
Na (mwandishi wetu).
VIONGOZI WA CCM TABORA WAZOMEWA MKUTANONI.
CHAMA mapinduzi (CCM),na baadhi ya viongozi wake,kwa mara ya kwanza
jana walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kukumbwa na
“zomeazomea”toka kwa wanannchi kwenye mkutano wa hadhara.
Tukio la kuzomewa kwa viongozi wa wilaya na mkoa lilijiri kwenye
mkutano wa hadhara ambao ulifanyika kwenye viwanja vya stendi ya
mabasi zamani ambapo CCM ilikuwa ikifanya mkutano wake.
Mkutano huo wa hadhara unafanyika baada ya CHADEMA ikiongozwa na naibu
katibu mkuu wake,Zitto Kabwe, kufanya mkutano eneo hilo na kutamka
wabunge wa CCM Tabora hawawatendei haki wapigakura wao na CHADEMA
watapiga kambi Tabora kuwatetea wananchi kwenye haki zao.
Hatua hiyo iliwafanya CCM nao kuja na badhi ya viongozi akiwemo mbunge
wa jimbo la Tabora mjini Aden Rage kujibu mapigo.
Dalili za zomeazomea zilianza mapema kwani baadhi ya wananchi walianza
vicheko na kejeli kwa viongozi wa CCM huku wengine wakisikika na
kutamka hawataki majigambo,matusi bali wanataka barabara za lami
Tabora-Nzega,Tabora-Urambo na ile ya Itigi-Tabora na wengine 'Peoples
Power'.
Wakati katibu wa CCM mkoa wa Tabora Idd Ame,akimwaga sera
zake,wananchi wachache waliokusanyika kwenye mkutano huo walianza
kuzomea kila katibu huyo alipokuwa akikikejeli chama demokrasia na
maendeleo,(CHADEMA).
“Ndugu zangu wananchi hebu angalieni mnavyodanganywa hivi hawa CHADEMA
wanajigamba kujenga barabara wakati wao siyo watoaji wa fedha na
kwamba fedha zinatolewa na serikali ya CCM siyo hao CHADEMA wanafiki
waongo.”alisema Ame.
Wakati katibu huyo akiendelea ma sera zake huku akikejeli na kufikia
kutamka mtu anakuja anaacha jimbo lake Kigoma kuja Tabora kuwafundisha
siasa huu ni ‘upumbavu’ kabisa.
Baada ya katibu huyo kutamka maneno hayo ndipo wananchi walipoanza
kuzomea kwa nguvu na kudai wanantaka sera za siyo matuzi huku wengine
wakisema nyie CCM waongo siku zote mlikuwa wapi kuja kufanya mikutano
hadi CHADEMA waje.
Aidha zomea zomea ilizidi ambapo katibu wa CCM mkoa wa
Tabora,alipoendelea kutamka kuwa endeleeni na huo ujinga wenu hapa
tutaumizana hapa hali ambayo ilizidisha hasira za wananchi huku nao
wakijibu mapigo kuwa sawa tu tuumizane tumechoka na ahadi zenu za
uongo.
“Hapa tuko kamili endeleeni kuzomea tu……..tutaumizana kwelikweli hapa
msifikiri hatuwezi na tutawashitaki viongozi wa CHADEMA Tabora kwa
kutufanyia fujo kwenye mkutano wetu.”
Wakati katibu huyo akitamka hayo,mjumbe wa NEC John Mchele alitoka
jukwaani na kwenda kumnong`oneza katibu huyo aachane na hayo amwage
sera tu.
Baada ya hapo ndipo ilizuka fujo kubwa huku Green Gurd wa CCM
wakitembeza mkong`oto kwa baadhi ya wananchi ambao walikuwa
wakionyesha ishara ya vema ikiwa ni alama ya CHADEMA na tafrani hiyo
ilidumu kwa dakika 20 hivi na ndipo askari polisi walipoongezwa na
mkutano kuendelea.
Baada ya vurugu kutulia huku wananchi wengine wakiondoka, mbunge
Tabora mjini Aden Rage alipopanda jukwaani ni kuongea na
wananchi,ambapo alitoa sh milioni 68 kwa kata kumi za manispaa hiyo,na
kila kata ilikabidhiwa hundi yake kwa ajili ya miradi ikiwemo ujenzi
wa vyoo,umaliziaji nyumba za walimu na madarasa.
Aidha mbunge huyo alikabidhi chama wanedesha bodaboda pikipiki mbili
na kutoa ahadi ya kuendelea kuchangia misaada.
Katika hatua nyingine mwenyekiti wa CCM tabora mjini Moshi Abdurahaman
Nkonkota alilaani jeshi la polisi kuwa hawataki kulinda mikutano ya
CCM hadi wanafanyiwa vurugu.
Tutalipeleka lalamiko hili ngazi za juu kuwa askari polisi huwa
hawafiki kwenye mikutano ya CCM.” Alisema.
VIONGOZI WA CCM TABORA WAZOMEWA MKUTANONI.
CHAMA mapinduzi (CCM),na baadhi ya viongozi wake,kwa mara ya kwanza
jana walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kukumbwa na
“zomeazomea”toka kwa wanannchi kwenye mkutano wa hadhara.
Tukio la kuzomewa kwa viongozi wa wilaya na mkoa lilijiri kwenye
mkutano wa hadhara ambao ulifanyika kwenye viwanja vya stendi ya
mabasi zamani ambapo CCM ilikuwa ikifanya mkutano wake.
Mkutano huo wa hadhara unafanyika baada ya CHADEMA ikiongozwa na naibu
katibu mkuu wake,Zitto Kabwe, kufanya mkutano eneo hilo na kutamka
wabunge wa CCM Tabora hawawatendei haki wapigakura wao na CHADEMA
watapiga kambi Tabora kuwatetea wananchi kwenye haki zao.
Hatua hiyo iliwafanya CCM nao kuja na badhi ya viongozi akiwemo mbunge
wa jimbo la Tabora mjini Aden Rage kujibu mapigo.
Dalili za zomeazomea zilianza mapema kwani baadhi ya wananchi walianza
vicheko na kejeli kwa viongozi wa CCM huku wengine wakisikika na
kutamka hawataki majigambo,matusi bali wanataka barabara za lami
Tabora-Nzega,Tabora-Urambo na ile ya Itigi-Tabora na wengine 'Peoples
Power'.
Wakati katibu wa CCM mkoa wa Tabora Idd Ame,akimwaga sera
zake,wananchi wachache waliokusanyika kwenye mkutano huo walianza
kuzomea kila katibu huyo alipokuwa akikikejeli chama demokrasia na
maendeleo,(CHADEMA).
“Ndugu zangu wananchi hebu angalieni mnavyodanganywa hivi hawa CHADEMA
wanajigamba kujenga barabara wakati wao siyo watoaji wa fedha na
kwamba fedha zinatolewa na serikali ya CCM siyo hao CHADEMA wanafiki
waongo.”alisema Ame.
Wakati katibu huyo akiendelea ma sera zake huku akikejeli na kufikia
kutamka mtu anakuja anaacha jimbo lake Kigoma kuja Tabora kuwafundisha
siasa huu ni ‘upumbavu’ kabisa.
Baada ya katibu huyo kutamka maneno hayo ndipo wananchi walipoanza
kuzomea kwa nguvu na kudai wanantaka sera za siyo matuzi huku wengine
wakisema nyie CCM waongo siku zote mlikuwa wapi kuja kufanya mikutano
hadi CHADEMA waje.
Aidha zomea zomea ilizidi ambapo katibu wa CCM mkoa wa
Tabora,alipoendelea kutamka kuwa endeleeni na huo ujinga wenu hapa
tutaumizana hapa hali ambayo ilizidisha hasira za wananchi huku nao
wakijibu mapigo kuwa sawa tu tuumizane tumechoka na ahadi zenu za
uongo.
“Hapa tuko kamili endeleeni kuzomea tu……..tutaumizana kwelikweli hapa
msifikiri hatuwezi na tutawashitaki viongozi wa CHADEMA Tabora kwa
kutufanyia fujo kwenye mkutano wetu.”
Wakati katibu huyo akitamka hayo,mjumbe wa NEC John Mchele alitoka
jukwaani na kwenda kumnong`oneza katibu huyo aachane na hayo amwage
sera tu.
Baada ya hapo ndipo ilizuka fujo kubwa huku Green Gurd wa CCM
wakitembeza mkong`oto kwa baadhi ya wananchi ambao walikuwa
wakionyesha ishara ya vema ikiwa ni alama ya CHADEMA na tafrani hiyo
ilidumu kwa dakika 20 hivi na ndipo askari polisi walipoongezwa na
mkutano kuendelea.
Baada ya vurugu kutulia huku wananchi wengine wakiondoka, mbunge
Tabora mjini Aden Rage alipopanda jukwaani ni kuongea na
wananchi,ambapo alitoa sh milioni 68 kwa kata kumi za manispaa hiyo,na
kila kata ilikabidhiwa hundi yake kwa ajili ya miradi ikiwemo ujenzi
wa vyoo,umaliziaji nyumba za walimu na madarasa.
Aidha mbunge huyo alikabidhi chama wanedesha bodaboda pikipiki mbili
na kutoa ahadi ya kuendelea kuchangia misaada.
Katika hatua nyingine mwenyekiti wa CCM tabora mjini Moshi Abdurahaman
Nkonkota alilaani jeshi la polisi kuwa hawataki kulinda mikutano ya
CCM hadi wanafanyiwa vurugu.
Tutalipeleka lalamiko hili ngazi za juu kuwa askari polisi huwa
hawafiki kwenye mikutano ya CCM.” Alisema.
WAREMBO WA SHINDANO LA REDD'S MISS TABORA WATEMBELEA TABORA REST HOUSE
Warembo wakipozi na mdhamini wa shindano la REDD'S MISS TABORA 2013 Bw.Humud Nassor mmiliki wa TABORA REST HOUSE na kampuni la SUPER SONIC.
Nyumba hizi waweza pumzika na familia, rafiki, pia kwa wale wafanyao kazi za maofisi. Panakidhi haja zote za nyumbani. NYUMBA ZINAPATIKANA UZUNGUNI
Warembo wakiwasili eneo hilo la nyumba za kupumzikia (TABORA REST HOUSE)
Warembo wakizunguka kuangalia mahadhi mbalimbali ya makazi hayo waliyokaribishwa kwaajili ya kuweka kambi
wakipozi ndani ya nyumba hizo za kupumzikia
wakikatiza toka upande mmoja wa nyumba hadi mwingine
kuna mazingira mazuri ya kuvutia ambapo ukiwepo huwezi boreka
warembo wakibembea
moja ya kivutio maji yakitiririka kwa namna ya pekee
Mmiliki wa Tabora Rest House Bw. Humud Nassor
---------------------------------------------------------------------------------
SHINDANO LIKIWA LIMEBAKIZA SIKU CHACHE KUFANYIKA HAPO TAREHE 31 MAY, 2013 KATIKA UKUMBI WA FRANKMAN PALACE.
HUKU MSANII MKALI OMMY DIMPOZI KWA POZI KUSHUSHA MVUA YA BURUDANI NA KIPAZA SAUTI KUBURUZWA VILIVYO NA MKALI WA VICHEKESHO BAMBO a.k.a KISHTOBE.
---------------------------------------------------------------------------------
JIPATIE TIKETI YAKO MAPEMA KATIKA MAENEO YAFUATAYO
BAGENZI NETWORK TRADERS 0754-416724, ALOY SON 0715-103054, GAMALO PUB, CLUB ROYAL ENTERTAINMENTS 0754-666620/ 0713666624
---------------------------------------------------------------------------------
(PICHA: www.aloyson.com)
Wednesday, May 22, 2013
VURUGU MTWARA:-JENGO LA CCM LACHOMWA!!!

Habari zilizotufikia muda huu
zinaripoti kwamba hali sio nzuri huko Mtwara, kwa ufupi hali ni tete na
hakuna amani, mabomu ya machozi yanarindima muda huu na huduma zote za
kijamii zimefunngwa hakuna usafiri, masoko, maduka na bar zote
zimefungwa, daladala, Taxi na Bodaboda hazifanyi kazi. Kwa ujumla
kinachoendelea ni mapambano makali kati ya Jeshi la polisi na wananchi
wenye hasira wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato wa gesi ilihali
nchi ikiwa haina sera inayosimamia nishati hiyo.
Kufuatia Kambi ya Upinzani kuukataa mpango wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara Mpaka Dar es salaam ilihali Waziri wa Nishati akisoma hotuba yake.
HALI NI TETE MTWARA LEO TANGU ASUBUHI,SAKATA LA GESI...!!!!
leo ntwara tangu asubuhi kila huduma imefungwa watu wapo kimakundi makundi wanasikiliza bunge hasa bajeti ya wizara ya nishati na madini,ni magari ya ffu tu ndio yapo barabarani nayo hupata wakati mgumu kupita kwasababu ya mawe na magogo yaliyowekwa na vijana,baadhi ya watu kadhaa wamechukuliwa na askari eti kwakuwa walipita jirani na gari yao,askari wengi waliokuja si wa hapa ntwara wengi wametoka Masasi na Lindi.
Kauli mbiu ya huku kwa sasa - "gesi haitoki hata kwa bomba la peni"
MORE UPDATES
MATAIRI KILA KONA YA MJI YAMECHOMWA BARABARANI POLISI NA ZIMA MOTO NDIO WANAKAZI YA KUZIMA NA KUFUKUZA RAIA
TAYARI NYUMBA KADHAA ZA WATUMISHI WA SERIKARI ZIMETIWA KIBERITI MAENEO YA SHANGANI
MMOJA WA WAMILIKI WA JAMII FORUMS APATA AJALI MBAYA NZEGA
Msemaji wa Jamiiforums, Mike Mushi, amesema hali ya Maxence kwa sasa si mbaya sana na walikimbizwa katika hospitali ya Rufani ya Bugando kwa matibabu na uchunguzi zaidi.
Pamoja na Maxence alikuwapo ndugu yake mmoja ambaye naye amejeruhiwa vibaya na wote wamekimbizwa Bugando. Maxence na mwenzake walikua njiani kuelekea mkoani Kagera na gari walilokua wakisafiria (pichani) limeharibika vibaya.
Mwenyezi Mungu awawekee wepesi wa kupata nafuu haraka.












