Pages

KAPIPI TV

Sunday, April 26, 2015

JESHI LA POLISI KIGOMA LAWAMANI LEO

 Na Magreth Magosso,Kigoma
 
CHAMA Cha Waganga wa Tiba za asili na mbadala Mkoa wa Kigoma ,umelitaka Jeshi la Polisi mkoani humo, washirikishe uongozi wa mitaa na kiongozi wa chama cha tiba asilia katika operesheni ya kamatakamata waganga wapiga ramli chonganishi  kwa kuwa, baadhi ya Askari polisi hujinufaisha na sakata la mauwaji ya albino kwa kuvamia kaya za waganga  na kuomba fedha kiasi cha sh.200,000 ili wachiwe huru.
 
Hayo yalibainika kigoma Ujiji wakati wanachama wa chama hicho,kilichoketi  kujadili njia mbadala ya kuepuka tiba hizo na uhusishwaji wa mauwaji ya vikongwe na walemavu wa ngozi (Albinism) na kulaani vitendo vya  udhalilishaji wa kijinsia unaofanywa na baadhi ya waganga washirikina ,ambapo  kuwaingilia kimwili wateja kwa madai ni tiba ilihali  mwenyezi mungu ameweka miti na matunda katika kuboresha afya za watu.
 
Akielezea hilo Mwenyekiti  wa chama (ATME) Abdallah Joseph Mkazi wa Ujiji alisema kitendo cha baadhi ya askari polisi  kwa nyakati tofauti wamekuwa kero kwa waganga wa tiba hizo,kwani huwavizia katika nyumba na kuwabana kwa maswali yasiyo na mashiko sanjari na kuomba fedha ili wamwache huru.
 
Alisema ili jamii itofautishe baina ya waganga wa tiba asilia na mbadala na waganga washirikina hawana budi kuanza ujenzi wa Kliniki bora nay a kisasa ambayo itatoa huduma kwa walengwa kwa mujibu wa sheria na taratibu za kitiba bila kuingilia uhai wa mtu na atakayekaidi kujiunga na vyma mtambukwa vya kijadi atakuwa na lake.
 
“hakuna tiba inayoruhusu udhalilishaji kwa  wateja kuwa ni dhambi kubwa kwa mungu kwa mujibu wa vitabu vya mungu(Qur`an na Biblia) na ni ukiukwaji wa haki za binadamu na kukiri hakuna tiba ya kuingiliana  kimwili baina ya mteja na mganga” alibainisha Joseph.
 
Alitaka kitendo cha uogeshaji utupu kwa wateja katika njia panda na utupaji wa  madawa hovyo njiani umepitwa na wakati na kinachangia kushusha thamani ya tiba asili na kuongeza uchafuzi wa mazingira na kudai mkakati walionao  chama cha  (ATME) Tawi la hapa ni ujenzi wa kliniki ya kisasa , ili kuepuka kero ya mauwaji hayo.
 
Akifafanua hilo Mjumbe wa dawa asilia na utunzaji wa mazingira kanda mgharibi Gregori Kassian ambaye ni Mkazi wa wilaya ya Kibondo kigoma alisema kuna mchakato maalum wa kitaifa wa kuwaelimisha waganga  wafuate sheria na taratibu za  tiba ziwe za uwazi na wajiunge katika   vyama ili kuwabaini waganga feki wanaoharibu umuhimu wao katika jamii.
 
Alisema ili kukabiliana na aibu ya utupaji wa madawa katika njia panda wameanzisha ulinzi shirikishi miongoni mwao ili kubaini wanaohusika na tiba za udhalilishaji wa kijinsia kwa tija ya kulinda watu wenye ulemavu wa ngozi.Wakatihuohuo  Sadick Kimwaga  alitaka watakaobainika kuchangia mauwaji ya vikongwe na albino wahukumiwe kwa mujibu wa sheria.
 
Akifunga kikao hicho Mwenyekiti wa Serikali wa Mtaa wa Rusimbi Pia Katibu wa chama cha walemavu kigoma Bakari Songoro  alisema wapo tayari kutoa ushirikiano katika maboresho ya tiba hizo na kukiri kigoma Ujiji inaongoza kwa tiba za njia panda ,ambazo hulazimisha mteja aoge na atupe dawa njia panda, ambapo madawa hayo uchanganywa na nyembe,pini,sindano ni hatari kwa watoto.

No comments: