Pages

KAPIPI TV

Wednesday, September 17, 2014

TFDA YAFUNGIA MACHINJIO YA MANISPAA KIGOMA



Na Magreth Magosso Kigoma


Mamlaka  ya  Chakula  Dawa na Vipodozi (TFDA ) imezifungia machinjio ya nyama zilizopo katika Manispaa ya Kigoma-Ujiji mkoani hapa   kwa sababu ya kukithiri kwa uchafu sanjari na kukosa vigezo bora na taratibu za afya ili kuepusha  hatari  ya  kuenea kwa magonjwa ya mlipuko hasa ugonjwa wa Kimeta.


Akithibitisha hilo Mkuu wa idara mifugo na  uvuvi  Dr.John Shauri  alisema wamalaka ilifika hapo mwaka 2005 na iligundua madhaifu bora ya kuendelea kutoa huduma hiyo kwa jamii kutokana na machinjia yote yalikuwa chini ya kiwango cha sheria ya mwaka 2003.


“shida hazina vyoo,maji na shimo la kutupia mizoga ambapo kitaalamu ni kosa aha tumeboresha haraka machinjio ya kibirizi juzi kwa kuweka nyavu ili mbwa wasirukie nyama na kuhatarisha afya za walaji machinjio ya ujiji hatari ugonjwa wa kimeta hauepukiki sakafu mashimo maji yanatwama ,mizoga inatupwa hovyo  ” alibainisha Dkt.Shauri .


Msimamizi wa machinjio ya Kibirizi Lucas Bandiliki  alisema kuwa alikuja mtalaamu wa TFDA na kukagua eneo la machinjio na kutoa amri yafanyike marekebisho haraka kabla hazijachinjwa ng’ombe.


“nimeona nyavu leo asubuhi, mwenzangu alisema alikuwepo mganga wa manispaa  usiku wa kuamkia leo akiwa na mafundi  wakiweka nyavu ,ilikuwa usiku ,sisi tunafuata magizo kutoka kwa wakubwa” alisema Badilika.


Jamboleo likafanya mahojiano na mfanyabiashara wa kuuza na kusamabaza nyama  Laini Ramadhani  na Rama Yahaya  wakiri machinjio haina maji na hulazimika  kubeba nyama kichwani na kuziosha  mwalo wa Forodhani  na  kufungwa  kwa  Machinjio ya Ujiji  inawapa gharama kubwa katika utoaji wa huduma husika.



Kwa upande  wa Mwenyekiti  Nuru Sadiki na Diwani wa kata ya Kitongoni Kassim Zaid kwa nyakati tofauti walisema wanaunga mkono kufungwa kwa machinjio hiyo kutokana na kukosa sifa za usafi,kwa kuwa haina choo , maji hivyo inaweza kusababisha magonjwa kutoka kwenye  nyama .


 Walisema mapungufu yanachangiwa na hujuma na ushindani wa kisiasa hali inayochaochea  kudorora huduma za jamii kwa wakati,ambapo kikao cha DCC ,desemba,2008 ilipangiwa bajeti ya milioni 142 kwa ajili ya kuboresha  machinjio ya kisasa na bajeti ya mwaka 2013/14 ilitengwa milioni 140 halikutekelezwa na kushauri  wasimamie kuboresha  adha za jamii waache siasa kwenye tija.



Akijibia hilo   Meya wa Manispaa, Bakari Beji  alisema mapungufu  ni makubwa katika machinjio ya ujiji ikiwemo mashimo, kutokuwa na uzio na shimo la kuhifadhi damu  ilibidi  yafungiwe mpaka yatakapokarabatiwa.


Alisema kuwa mwaka jana walitenga shilling 1200,000/= ili kukalabati machinjio lakini pesa hazikupatikana na kwa mwaka huu walitenga shilingi 2500,000/= kwa lengo hilohilo lakini   pesa za miradi hazijafika na  zikifika zitatumika ipasavyo.


Aidha  Manispaa ina  maeneo ya  mawili ya Ujiji na  ya kibirizi ila iliyofungwa ni ile ya Ujiji kutokana na kuwa na mapungufu mengi ambayo yanahatarisha afya za walaji wa nyama hapa mkoani.

No comments: